Kama ningepata nafasi ya kuishauri Serikali kuhusu shule zake za mjini basi haya ndio mawazo yangu

Kama ningepata nafasi ya kuishauri Serikali kuhusu shule zake za mjini basi haya ndio mawazo yangu

instagramer

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2024
Posts
215
Reaction score
492
Habari Wadau Wa Jukwaa Hili...

Kuweka kumbukumbu sawa, Mimi ni mmoja wa vijana wa kitanzania niliyesoma katika shule za Serikali kuanzia elimu ya msingi, sekondari mpaka chuo, hivyo mawazo nitakayotoa hapa yasiyafsirike kupinga shule za Serikali.

Kwa muda mrefu nimekua nikiwaza namna ya kufikisha ushauri wangu huu kwa Serikali. Kwa kuzingatia mahitaji na ukuaji wa Jiji letu la Dar es salaam Kiuchumi.

Hivi Serikali yetu Haioni umuhimu kwa Sasa wa kubomoa shule zake zote za msingi na hata sekondari ambazo zipo katikati ya Jiji??? Hizo shule nyingi zimekua kongwe na za kizamani Sana, na siamini kama zinaachwa kwa ajili ya kutunza historia.

Serikali izivunje ili maeneo hayo yajengwe maghorofa ya Kisasa kwa ajili ya shughuli za kibiashara. Kwa maana wakati shule hizi zinajengwa miaka ya zamani, basi maeneo hayo walikaa watu wa kipato Cha chini au Cha kawaida, ambao ndio wanufaika wa shule hizo. Ila watu hao kwa Sasa wapo nje ya Jiji na sio katikati tena kama zamani. Mfano, shule ya msingi Mtendeni, zamani wanafunzi walikua ni wakazi wa Kariakoo ambao kwa Sasa wanaoishi maeneo hayo asilimia kubwa ni matajiri ambao watoto wao Wanasoma shule zenye ma'bus.

Hivyo kwa mfano huo wa Mtendeni Pekee, unaweza Kuta wanafunzi wake wanatoka maeneo ya mbali kabisa ambapo wanakumbana na changamoto ya usafiri na suluba za hapa na Pale wakati huko huko walipo Kikwete alishapeleka shule nyingi tu za kata.

Je kwa mawazo haya, Serikali Haioni umuhimu wa kuvunja shule zote hizo na kubadili matumizi ya ardhi????

CC: Waziri wa elimu
Waziri wa ardhi
Spika wa Bunge
 
Majengo yabomolewe na yajengwe madarasa ,ofisi nyumba za walimu za maghorofa ili kuendanda na usasa na kupunguza matumizi makubwa ya ardhi
Tunahitaji kutoa shule katikati ya mjini ambako kumejaa maduka na maofisi kupeleka walipo wananchi
 
Hili nalo neno kwa kweli ukiangalia shule kama ya mtendeni na nyinginezo inawezekana kabisa zaidi ya asilimia 80 ya wanafunzi wake wanatoka nje ya mji(wanapanda daladala) kuja shule kwanini shule zisiongezeke huko walipo

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Hili nalo neno kwa kweli ukiangalia shule kama ya mtendeni na nyinginezo inawezekana kabisa zaidi ya asilimia 80 ya wanafunzi wake wanatoka nje ya mji(wanapanda daladala) kuja shule kwanini shule zisiongezeke huko walipo

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
Ndio Hilo wazo langu Mimi.... Sioni umuhimu wa shule kuendelea kubaki maeneo ambayo wanufaika hawaishi...
 
mimi ningeishauli serikali iwape ruhusa wafanya biashara wa ma bus ya daladala asubui na jioni wapakie wanafunzi tu mchana wapige route zao kama kawaida mabasi kadhaa yangesajiliwa kwa hiyo huduma na serikali ingewaondolea kodi kwenye magari yao.

wanafunzi wanapata tabu sana kwenye usafiri unakuta mtoto mdogo anaangaika usafiri duu mtu unajiuliza kweli mpaka karne hii tunaishi ivi kweli
 
Back
Top Bottom