Kama nitakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kama nitakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mzee mbona unataka kutulazimisha kuamini vitu Ambazo siyo.....
Yaani ikiambiwa useme Russia, china ni nchi za kijamaa. Utataja Duh!!! Aibu kubwa sana...
Mkuu sitaki porojo nataka ushaidi wa SERA za nchi hizo ili tujue kama ni za kijamaa au kibepari.
 
Naona porojo zimekua nyingi.Mimi ninachohitaji ni SERA.Ujamaa ni mfumo mpana ndio maana kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa historia utaona katika sera ujamaa kila nchi ilikua na siasa ya namna yake mfano Tanganyika ni ujamaa na kujitegemea, harambee-kenya,humanism -Zambia n.k

Ukweli ni kwamba sisi Waafrika tulishindwa kupanga kimakati ya kimaendeleo kupitia ujamaa.Ndio maana Tanzania ujamaa ulikufa tangu enzi za Mwinyi japokua katiba inasema ujamaa ila hii nchi inaongozwa kibepari.

China na Russia ni nchi zilizopitia masaibu ya ujamaa na hatimaye zikafikia malengo yake ya kimkakati ya kimaendeleo kupitia ujamaa.

Tatizo hapa hamjui ujamaa ni nini.Ujamaa sio constant kama ubepari bali ujamaa unajidhihirisha kulingana na sera za serikali husika katika kufikisha mahitaji ya wananchi wake huku wananchi wakinufaika zaidi kupitia hizo huduma.

Ushaidi ni huu kuhusu kitengo cha afya cha Urusi na China,angalia ni kwa asilimia ngapi wananchi wanapata matibabu bure alafu linganisha na Marekani ambayo huduma za afya ni most expensive na japokua Kuna hospitali za serikali,ni lazima kulipia.Vilevile linganisha na Tanzania kama matibabu ni bure,je kuna huduma bora?Kuna vifaa?Lakini angalia hospitali binafsi zinavyotoa huduma bora kuizidi serikali.Ndio ujue Tanzania hakuna ujamaa.

Vilevile pitia historia katika kitengo hiko cha afya kwa nchi zote mbili utaona kua wakati USSR inakufa baada ya muda kidogo Urusi ilipokea privatization policy katika kitengo cha afya.Je hiyo policy ilidumu?Kwa nini haikudumu?Kwa nini mpaka sasa mwaka 2022 hapo Urusi kuna hospitali binafsi(ambazo ni chache) lakini serikali bado inatoa huduma nzuri za kiafya ambazo ni bure na bora .Ndio utajua hujui Ujamaa ni nini.

Vilevile angalia na China na katika kitengo cha afya.NDIPO UTAKAPOGUNDUA UJAMAA UNANGUVU YA KUMSAIDIA MWANANCHI MASIKINI TATIZO NI SISI WAAFRIKA TUSIO NA AKILI NA MAARIFA YA KUBUNI MIFUMO CHINI YA UJAMAA.USISINGIZIE UJAMAA WAKATI HAUNA AKILI YA KULETA MAENDELEO.HUKO CHINA NA URUSI KUNA TAASISI BINAFSI LAKINI WANUFAIKA WAKUBWA NI WANANCHI WENYEWE LAKINI SISI HUKU TUNANYONYWA KILA KUKICHA KUPITIA UBEPARI.KWANZA NINYI NYOTE MNAOSEMA TANZANIA INAONGOZWA KWA SERA YA UJAMAA NI WAJINGA TU,HAMJUI UJAMAA NI NINI.SIKATAI KATIBA INASEMA NCHI IPO CHINI YA UJAMAA,JE UNAFUATWA?ACHENI KUA KICHWA CHA MWENDAWAZIMU.
 

Attachments

Wewe una miaka 17 tu, haya mambo yako juu ya uwezo wako, jikite na shule kwanza kwa sasa ukifikisha miaka 22 ndio urudi hapa
 
Mawazo ya kizamani kabisa haya! Ujamaa ulishindwa dunia na mbinguni! Leo hii bado tu unatamani kuwa Rais chini ya mfumo mfu wa Ujamaa!

Ujamaa ni mfumo wa kinafiki wa kuwanufaisha viongozi wachache, huku wananchi walio wengi wakiishi maisha ya kutaabika.

Ningekuunga mkono kama ungeifuta ccm baada ya kuwa Rais! na hivyo kuruhusu uwanja sawa wa watu kufanya demokrasia. Maana matatizo yote ndani ya nchi hii; kuanzia ya kijamii, kiuchumi na pia kisiasa! Chanzo ni ccm na sera zake mbovu.
Mleta uzi ni mtoto wa miaka 17
 
Mleta uzi ni mtoto wa miaka 17
Mkuu umri sio kipimo cha akili ya mtu.Kuna wazee hawana busara na kuna vijana wana hekima.Miaka ni namba tu,Marekani mtu akifikisha 16 tayari mkubwa hapa Tanzania mpaka 18,sababu nini?Akili au kujitambua hakuendani na miaka as long as nishabalehe na nina uwezo wa kumtungisha mwanamke mimba ubongo umetanuka kwa kufiria mambo ya msingi.
 
Wewe una miaka 17 tu, haya mambo yako juu ya uwezo wako, jikite na shule kwanza kwa sasa ukifikisha miaka 22 ndio urudi hapa
Ndio nyie ambao mkiwa viongozi hamtaki kushauriwa na vijana mkidhani vijana hawana wanachojua.Alisikika ... akimuambia Furaha,mjomba wake"wewe kijana niletee mambo kuhusu ukemia nitakuelekeza lakini haya mambo ya siasa..."
 
Mkuu kuna kitu kimoja unashindwa kuelewa Sera zote ujamaa au ubeapari ni nzuri-issue kubwa ni ngoma inachezwa kipindi kipi?.

Kumbuka kabla USA hajawa superpower Russia ndio alikuwa superpower,sasa ulitaka USA baada ya kiwa super power aendelee na sera ya Ujamaa ambayo ilikuwa ya mtangulizi wake (USSR)??,it is obviously lazima aanzishe mfumo wake wa uchumi na utawala.

Ndio maana walikaa chini na kuanzisha mifimo hiyo ili kuhakikisha wanaendelea kuwepo katika nafasi hiyo.

Maono yako yanawezekana kama Tanzania ingekuwa Taifa kubwa kama Urusi au China na upo next kuchukua nafasi ya USA kama superpower wa Dunia.

Kwa Nchi kama yetu ambayo Mifumo ya uchumi na siasa,ya magharibi tupo katika makwapa huwezi kuchomoka ukiwa peke yako.

Njia pekee ya kuondokana na mfumo huo ungewezekana kama Africa nzima ingeungana na kuwa Tiafa mmoja-Nyerere alilona hilo na ndio alijaribu kulipigania mpaka anakufa halikuwezekana,sababu kubwa ni kqamba hao western kwa njia yoyote wanahakikidha hilo haliyokei.

Kama unataka kutekeleza hayo maono yako,anza kwanza na kuiunganisha Afrika yote.
 
Mkuu kuna kitu kimoja unashindwa kuelewa Sera zote ujamaa au ubeapari ni nzuri-issue kubwa ni ngoma inachezwa kipindi kipi?.

Kumbuka kabla USA hajawa superpower Russia ndio alikuwa superpower,sasa ulitaka USA baada ya kiwa super power aendelee na sera ya Ujamaa ambayo ilikuwa ya mtangulizi wake (USSR)??,it is obviously lazima aanzishe mfumo wake wa uchumi na utawala.

Ndio maana walikaa chini na kuanzisha mifimo hiyo ili kuhakikisha wanaendelea kuwepo katika nafasi hiyo.

Maono yako yanawezekana kama Tanzania ingekuwa Taifa kubwa kama Urusi au China na upo next kuchukua nafasi ya USA kama superpower wa Dunia.

Kwa Nchi kama yetu ambayo Mifumo ya uchumi na siasa,ya magharibi tupo katika makwapa huwezi kuchomoka ukiwa peke yako.

Njia pekee ya kuondokana na mfumo huo ungewezekana kama Africa nzima ingeungana na kuwa Tiafa mmoja-Nyerere alilona hilo na ndio alijaribu kulipigania mpaka anakufa halikuwezekana,sababu kubwa ni kqamba hao western kwa njia yoyote wanahakikidha hilo haliyokei.

Kama unataka kutekeleza hayo maono yako,anza kwanza na kuiunganisha Afrika yote.
Umeongea kwa utimamu mkuu.Hoja nzuri 👏🏽.
 
Urusi na China sio nchi za kijamaa, Korea Kaskazini ni nchi ya ujamaa uchwara ambayo Kiduku na kikundi chake kidogo wanatumia mkono wa chuma kunyonya jasho la raia watawaliwa waliobaki mafukara na skelton tupu.
Cuba
 
Mkuu ushaidi wangu ni huu:China inatoa matibabu bure kwa wazee. Je Marekani inatoa?

Urusi imewajengea watu wasio na malazi(homeless), lockers za kuweka mizigo yao. Je homeless people wa Marekani hawalali juu ya mifuko ya rambo yenye mizigo yao?

Marekani usipokua na uwezo wa kifedha you are nothing ila China usipokua na uwezo wa kifedha utatafutiwa karama yoyote ile hata ya kujenga fly overs za Tanzania, kutengeneza saa za 1000/= na kuzitupia Afrika.

Mkuu toa ushaidi wako unaosadifu huo ubepari(nadhani unaelewa maana ya ubepari).
Sijawahi kufika na wala sijui lolote lakini nasikia marekani kuna hadi chakula cha bure kwa wasiojiweza. Kama hilo wanalifanya, wataacha huduma ya afya kwa wazee kweli?!!! Halafu vp kuhusu hili la maeneo maalumu ya kutunza wazee?!!!!!
 
Naomba ushaidi? Kuna Uzi pia hapa JF una haya maudhui. Sijawahi elewa kwa nini masikio yenu yapo sensitive kumsikiliza Mmarekani. Kwanza naomba ushaidi alafu niambie China inaongozwa na chama gani, je kuna vyama vingapi, na sera zao ni zipi? Sasa tuone hizo sera ni za kijamaa au kibepari. Vilevile toa ushaidi kwamba sera za urusi ni za kibepari.

Vilevile nitajie rank ya North Korea kiuchumi duniani? Nanitolee ushaidi wa picha unaoonyesha umasikini wa nchi hiyo.Kama umetanguliza sikio kabla ya jicho basi hakuna unachojua maana utaishia kusema: mara kuna mtu alitoroka akahojiwa UN...., mara wanawake wananyanyaswa, maneno kibao pasipo ushaidi wa picha ni ubatili
Nje ya mada, kwanini wachina wengi wanakimbilia ulaya na marekani?!!!!
 
Sijawahi kufika na wala sijui lolote lakini nasikia marekani kuna hadi chakula cha bure kwa wasiojiweza. Kama hilo wanalifanya, wataacha huduma ya afya kwa wazee kweli?!!! Halafu vp kuhusu hili la maeneo maalumu ya kutunza wazee?!!!!!
Fuatilia.
 
Habari zenu wana JF. Moja kwa moja kwenye mada;

Kulingana na maono yangu kuhusiana na suala la maendeleo katika jamii ya watu wa Tanzania, naona asilimia kubwa ya watu wamesahau kitu ambacho waasisi wetu wa taifa walikua wamekiacha kama kifaa cha kuleta maendeleo. Mnamo mwaka 1967 kulikuwa na azimio la Arusha kuhusiana na siasa ya ujamaa na kujitegemea.

Siasa ya ujamaa na kujitegemea ililenga serikali kutumikia wananchi wake na watu katika jamii kusaidiana.Kila mtu kuweza kubuni fursa zitakazo tatua changamoto za kijamii.

Ni dhahiri kwamba waasisi wa taifa walikua na maono mazuri lakini walishindwa kubuni njia sahihi na nzuri za kuleta maendeleo. Hata sasa tunajua ya kuwa Mtanzania anaweza akatoa wazo zuri kwelikweli ambalo litatatua changamoto za kijamii, lakini hawawezeshwi kufikia ndoto zao.

Swali la msingi Watanzania wenzangu: Katika miaka 60 ya uhuru je Tanzania inafanya siasa ya ujamaa na kujitegemea au imebadilisha mlengo na kuingia katika siasa ya ubepari pasipo kuwa na azimio lolote lile?

Kama nitakua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania;

Nitakuwa moja ya viongozi wanaopinga siasa ya vyama vingi. Siasa ya vyama vingi ni siasa ya kibepari. Ili Tanzania iweze kuendelea ni lazima wote tuwe na malengo sawa na sawia.Nitavunja vyama vyote vya siasa(kuanzia kile nitakachokitumikia mpaka vile vya upinzani). Chama kipya cha taifa kitaundwa ambacho kitachukua viongozi na sio watawala. Yoyote yule aliye Mtanzania na mzalendo atajiunga pasipo kuangalia chama chake alichokitumikia hapo kabla. Nia ya kufanya hivyo ni kuwa na malengo sawa ya kimaendeleo hivyo kuhamasisha shauri na sio kupakaziana mabaya.

Mnamo mwaka 1944, Bretton Woods Institutions:IMF,WB ziliundwa nchini Marekani kwa lengo la kusaidia nchi za Ulaya kujijenga kiuchumi baada ya vita vya pili vya dunia. Lakini mnamo mwaka 1980 mlengo ulibadilika na kuhamia Afrika kwa kile walichokiita mpango wa kuondoa umasikini bara la Afrika.Ukoloni mambo-leo ukazaliwa na kuota mizizi katika ardhi ya bara la Afrika.

Zile SAP's ndizo chanzo kikuu cha ukoloni mambo-leo.Natumaini mnazijua SAP's pamoja na kanuni(principles) zake.

Leo hii watu wanaiita Marekani, mama wa demokrasia ilhali hiyo demokrasi yao imeleta mashoga(kwa misingi ya mtu kufanya chochote anachokitaka*Sisi Watanzania hatuna tamaduni hii na hatuwezi ikubali), imeshindwa kufuta ubaguzi wa rangi, maandamano ambayo jeshi la polisi limetumia nguvu ilhali watu wanasema ukweli, watu kuvamia bunge, masikini kukosa malazi(homeless) n.k.


Ukweli ni huu:wakati utafika Tanzania kuwa na demokrasia yake ambayo itaendana na mahitaji ya watu wake.Je panaweza kuwa na demokrasia ilhali chama cha siasa ni kimoja?Jibu langu ni ndiyo.Hili taifa kwa sasa halina enzi kuu(sovereignty) kwa sababu kuna viongozi ambao ni vibaraka wa nchi za kibepari na hutumia siasa ya vyama vingi kama chaka la kuficha maovu yao.

Siasa ya ujamaa na kujitegemea ndiyo siasa pekee itakayoleta elimu bure,matibabu bure,uwajibikaji,uzalendo,ubunifu,uwezeshaji,umoja,upendo,amani,maisha yenye kipato kizuri kwa kila Mtanzania.Ila kama tutaendelea kwa njia hii ya kutegemea uwekezaji kutoka nje(ubepari) mafarakano kati ya mkulima na mwekezaji,mfugaji na mwekezaji,mchimba madini na mwekezaji hajataisha na nchi haitokuja kuendelea.

Kwa nini nchi haitokuja kuendelea?Jibu:kwa sababu wawekezaji wa nje ni lazima wachukue asilimia kubwa katika magawio ilo kupata faida.Sasa kumbuka wakati wao wanachukua faida kujenga nchi zao vilevile sisi tunapata faida lakini yenye hasara,kwa nini?Jibu:Kwa sababu sisi hatuna wawekezaji wakubwa katika nchi za kigeni hususani Ulaya na Marekani hivyo hatuchukui faida kutoka kwao.Wakati sisi tunapiga hatua moja wale wanapiga hatua mia moja.Sasa tutawafikia lini?Au kwenye ndoto?Hii nchi inavyoendeshwa kuelekea maendeleo ni kana kwamba nchi nyingine zimelala!!

Kama nitakua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.....
Rubbish,kama unataka ujamaa mbona hauufanyi hapo mtaani kwako?

Kwani kuwa mjamaa kunahitaji hadi uwe Rais? Acha kukariri makaratasi wewe kiazi..

Walioasisi ujamaa uliwashinda,walipiga kama akina Nyerere uliwashinda ndio uje kuweza wewe maskini wa huko nanjilinji?

Ujamaa ni Imani kama Imani zingine na lazima uishi hivyo wala haotegemei hadi uwe Rais.
 
Rubbish,kama unataka ujamaa mbona hauufanyi hapo mtaani kwako?

Kwani kuwa mjamaa kunahitaji hadi uwe Rais? Acha kukariri makaratasi wewe kiazi..

Walioasisi ujamaa uliwashinda,walipiga kama akina Nyerere uliwashinda ndio uje kuweza wewe maskini wa huko nanjilinji?

Ujamaa ni Imani kama Imani zingine na lazima uishi hivyo wala haotegemei hadi uwe Rais.
Ukiandika kama great thinker nitakujibu.
 
Nitakuwa moja ya viongozi wanaopinga siasa ya vyama vingi. Siasa ya vyama vingi ni siasa ya kibepari. Ili Tanzania iweze kuendelea ni lazima wote tuwe na malengo sawa na sawia.Nitavunja vyama vyote vya siasa(kuanzia kile nitakachokitumikia mpaka vile vya upinzani)
Mvua zimeanza, nenda kaoteshe mahindi upate tiba ya kuwalisha wanao na kuwasomesha!
Achana na hadithi zako za abunuwasi, hata M.kiti wa kitongoji sio rahisi wewe kupata!
 
Habari zenu wana JF. Moja kwa moja kwenye mada;

Kulingana na maono yangu kuhusiana na suala la maendeleo katika jamii ya watu wa Tanzania, naona asilimia kubwa ya watu wamesahau kitu ambacho waasisi wetu wa taifa walikua wamekiacha kama kifaa cha kuleta maendeleo. Mnamo mwaka 1967 kulikuwa na azimio la Arusha kuhusiana na siasa ya ujamaa na kujitegemea.

Siasa ya ujamaa na kujitegemea ililenga serikali kutumikia wananchi wake na watu katika jamii kusaidiana.Kila mtu kuweza kubuni fursa zitakazo tatua changamoto za kijamii.

Ni dhahiri kwamba waasisi wa taifa walikua na maono mazuri lakini walishindwa kubuni njia sahihi na nzuri za kuleta maendeleo. Hata sasa tunajua ya kuwa Mtanzania anaweza akatoa wazo zuri kwelikweli ambalo litatatua changamoto za kijamii, lakini hawawezeshwi kufikia ndoto zao.

Swali la msingi Watanzania wenzangu: Katika miaka 60 ya uhuru je Tanzania inafanya siasa ya ujamaa na kujitegemea au imebadilisha mlengo na kuingia katika siasa ya ubepari pasipo kuwa na azimio lolote lile?

Kama nitakua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania;

Nitakuwa moja ya viongozi wanaopinga siasa ya vyama vingi. Siasa ya vyama vingi ni siasa ya kibepari. Ili Tanzania iweze kuendelea ni lazima wote tuwe na malengo sawa na sawia.Nitavunja vyama vyote vya siasa(kuanzia kile nitakachokitumikia mpaka vile vya upinzani). Chama kipya cha taifa kitaundwa ambacho kitachukua viongozi na sio watawala. Yoyote yule aliye Mtanzania na mzalendo atajiunga pasipo kuangalia chama chake alichokitumikia hapo kabla. Nia ya kufanya hivyo ni kuwa na malengo sawa ya kimaendeleo hivyo kuhamasisha shauri na sio kupakaziana mabaya.

Mnamo mwaka 1944, Bretton Woods Institutions:IMF,WB ziliundwa nchini Marekani kwa lengo la kusaidia nchi za Ulaya kujijenga kiuchumi baada ya vita vya pili vya dunia. Lakini mnamo mwaka 1980 mlengo ulibadilika na kuhamia Afrika kwa kile walichokiita mpango wa kuondoa umasikini bara la Afrika.Ukoloni mambo-leo ukazaliwa na kuota mizizi katika ardhi ya bara la Afrika.

Zile SAP's ndizo chanzo kikuu cha ukoloni mambo-leo.Natumaini mnazijua SAP's pamoja na kanuni(principles) zake.

Leo hii watu wanaiita Marekani, mama wa demokrasia ilhali hiyo demokrasi yao imeleta mashoga(kwa misingi ya mtu kufanya chochote anachokitaka*Sisi Watanzania hatuna tamaduni hii na hatuwezi ikubali), imeshindwa kufuta ubaguzi wa rangi, maandamano ambayo jeshi la polisi limetumia nguvu ilhali watu wanasema ukweli, watu kuvamia bunge, masikini kukosa malazi(homeless) n.k.


Ukweli ni huu:wakati utafika Tanzania kuwa na demokrasia yake ambayo itaendana na mahitaji ya watu wake.Je panaweza kuwa na demokrasia ilhali chama cha siasa ni kimoja?Jibu langu ni ndiyo.Hili taifa kwa sasa halina enzi kuu(sovereignty) kwa sababu kuna viongozi ambao ni vibaraka wa nchi za kibepari na hutumia siasa ya vyama vingi kama chaka la kuficha maovu yao.

Siasa ya ujamaa na kujitegemea ndiyo siasa pekee itakayoleta elimu bure,matibabu bure,uwajibikaji,uzalendo,ubunifu,uwezeshaji,umoja,upendo,amani,maisha yenye kipato kizuri kwa kila Mtanzania.Ila kama tutaendelea kwa njia hii ya kutegemea uwekezaji kutoka nje(ubepari) mafarakano kati ya mkulima na mwekezaji,mfugaji na mwekezaji,mchimba madini na mwekezaji hajataisha na nchi haitokuja kuendelea.

Kwa nini nchi haitokuja kuendelea?Jibu:kwa sababu wawekezaji wa nje ni lazima wachukue asilimia kubwa katika magawio ilo kupata faida.Sasa kumbuka wakati wao wanachukua faida kujenga nchi zao vilevile sisi tunapata faida lakini yenye hasara,kwa nini?Jibu:Kwa sababu sisi hatuna wawekezaji wakubwa katika nchi za kigeni hususani Ulaya na Marekani hivyo hatuchukui faida kutoka kwao.Wakati sisi tunapiga hatua moja wale wanapiga hatua mia moja.Sasa tutawafikia lini?Au kwenye ndoto?Hii nchi inavyoendeshwa kuelekea maendeleo ni kana kwamba nchi nyingine zimelala!!

Kama nitakua Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.....
Njoo upime wazo lako kwenye Game hii ya president simulator

Game hii ina Kupa Fursa ya kuendesha inch
 
Back
Top Bottom