Kama nyani alibadilika akawa binadamu ni kwanini nyani na sokwe wa sasa hawabadiliki tena kuwa binadamu?

Kama nyani alibadilika akawa binadamu ni kwanini nyani na sokwe wa sasa hawabadiliki tena kuwa binadamu?

1. Kiumbe gani hicho ambacho binadamu alitokana nacho?
Zamani tuliambiwa ni jamii ya sokwe, karibuni tumeambiwa ni mijusi wa kale. Kuna facts hapo au fix tu?

2. Mabadiliko gani hayo ambayo hayakupangwa tena ya mabilioni ya miaka ikawaje yakazaa kiumbe kikamilifu, tena ukamilifu uliosanifika?

3. Ni vipi hizo mutation na recombination zikazaa perfect species kimaumbile kama binadamu alivyo? Yaani Mutation na Recombination zitengeneze vitu vizuri na vilivyokamilika tu!?

Ukitazama aina za viumbe wote utagundua wana utofautiano wa kimantiki, wana maumbile ya kipekee na usanifu wa hali ya juu mnoo. Hakuna Mutation, Recombination au Natural selection inayoweza kutengeneza species universe ya namna hiyo.
1. Australopithecus
2. Mabadiliko madogo madogo ndani ya vinasaba
3. Natural selection; Viumbe wenye vigezo vinavyowawezesha kuishi wanabaki hai na kuendeleza vinasaba vyao kwenye vizazi vijavyo.

Usanifu upo, lakini kuhusu usanifu huo kuwa wa hali ya juu sidhani ni kweli. Magonjwa, Mchakato mzima wa kuzaliana ulivyo mgumu, uzee na kifo vinnathibitisha hilo.
 
Wewe unafikiri origin of life ni nini na mwanadamu ametoka wapi/chanzo chake ni nini?
Kisanyansi tulibadilika vinasaba kutoka kwa great ape ambapo aligawanyika katika makundi manne. Yaani tulitokana na uzao wa mageuzi ya nyani, na hivyo ndivyo inavyofundishwa na walimu wa history hadi huko mashuleni vizazi na vizazi... Sasa swali bado lina rudi pale pale kama ni hivyo kwanini hawa nyani wa sasa hivi hawabadiliki kua binadamu na kwanini sisi binadamu haturudii kwenye asili yetu ya unyani ( apes), tena na chipanzee tulichoreshwa kabisa?
 
Babu yao ndo huyo ape

babu yetu ndo huyo ape ambapo inaonyesha sisi tomedevelop kutoka kwa Kizazi cha nyani wa kubwa, sasa kama ndo hivyo ni kwanini nyani wa sasa hivi na wao wasidevelop wakawa binadamu. Au sisi binadamu tusirudie kizazi cha asili cha babu yetu great ape. ?
Kwanza kwa nini wa develop kuwa binadamu?

Kwani evolution lengo lake ni viumbe wote wawe binadamu?
 
Kwanza kwa nini wa develop kuwa binadamu?

Kwani evolution lengo lake ni viumbe wote wawe binadamu?
Hata hayo maswali ndo mimi na jiuliza, na kama endapo evolution ilikua labda sio wote tuwe binadamu ni kwanini ndugu zetu nyani tuwaache / wasibadilike?
 
Ndugu zangu.

1: Tukiachana na maswala ya kidini, historia inatuambia binadamu wa kwanza alikua ni nyani / sokwe /chipanze, sasa kama kweli binadamu tulikua ni manyani ni kwanini nyani / sokwe tunaowaona sasa hivi hawabadiliki kua binadamu na wala hawakatiki tena mikia na kua na mwili na utashi wa binadamu kama historia ilivyokua huko awali?

2: Je, kama kweli tulikua nyani na tukabadilika kua binadamu ni kwanini sahivi haiwezekani tena binadamu kubadikika na kurudia kua nyani kama wanasayansi wanavyodai?
Nyani na sokwe walibadilika na kuwa Binadamu kwa Muda Usiopungua Miaka Milioni ..
kwa sasa hawawezi Kwa sababu hakuna Nyani anayeishi Miaka zaidi ya Milioni kwa Sasa
 
Nyani na sokwe walibadilika na kuwa Binadamu kwa Muda Usiopungua Miaka Milioni ..
kwa sasa hawawezi Kwa sababu hakuna Nyani anayeishi Miaka zaidi ya Milioni kwa Sasa
Hiyo miaka milioni inahesabiwaje? Mwaka namba 1 ilikuwa lini na mwaka 999,999 ilikuwa lini?
 
Hata hayo maswali ndo mimi na jiuliza, na kama endapo evolution ilikua labda sio wote tuwe binadamu ni kwanini ndugu zetu nyani tuwaache / wasibadilike?

Kwanza kabisa hatukuwaacha nyani ambao hawakubadilika.

Watu wengi wanafanya makosa ya kufikiri kuwa evolution inasema zamani tulikuwa sawa na hawa nyani wa sasa, sisi tumebadilika wao hawajabadilika.

Hivyo si evolution inavyosema. Wote tumebadilika. Ila tulikuwa na a common ancestor ambaye alikuwa more ape like, maana yake sisi tumebadilika zaidi.

Kwa mujibu wa evolution.

Evolution inakwenda kwa natural selection. Kuna mazingira fulani yanafanya species fulani zife, nyingine ziendelee kuwapo, nyingine zibadilike.

Kwa mfano, kwenye mazingira ya misitu, wanyama wanaofanana na misitu ile wanaweza kupata advantage ya kuwa camouflaged wakaendelea kuwapo, na wasio na rangi ya hiyo misitu kuwindwa kirahisi na kutoweka, matokeo yake baada ya vizazi vingi wanyama wenye rangi isiyo na advantage ya camouflage watatoweka na wale wanaofanana na msitu wataongezeka na kuwa ndiyo watawala.

Kitu kingine ambacho ni kigumu kuelewa ni kuwa, kwa mujibu wa theory ya evolution, evolution inatokea katika mamilioni na malaki ya miaka, mabadiliko madogo madogo yanalimbikizana na kusababisha mabadiliko makubwa.

Sasa watu wengi wanaohoji evolution wanahoji kama vike wanataka kuona mabadiliko katika umri wao, miaka 30, miaka 50.

Ukitaka kuona evolution katika muda nfupi usiangakie wanyama wakubwa kama sokwe, nyani au watu. Ukitaka kuangalia evolution katika muda nfupi angalia vidudu kama bacteria, virus.

Angalia kitu kinaitwa anti-biotic resistance na jinsi bacteria wanavyojenga resistance dhidi ya dawa.

Unajua kwa nini hospitali hawatumii tetracycline tena? Unajua kwa nini madawa ya zamani ya malaria hayatibu tena malaria inabidi tutumie madawa mapya?

Hiyo ni evolution. Vidudu vimejipanga kuweza kujikinga na dawa, vime evolve.

Ukitaka kuelewa evolution usiangakie nyani na watu, angalia jinsi bactwria na microorganism nyingine zinavyojenga resistance dhidi ya dawa, na kwa nini tunahitaji dawa mpya, kwa nini zamani magonjwa kama gono yalikuwa yanatibiwa na tetracycline lakini siku hizi kuna gononsugu halisikii dawa.

Vidudu vya gono vimefanya evolution.
 
hapa unaangaliwa uwezo wa akili za mtu mweusi.sasa wewe kama unaangalia manyoya na mkia shaulizako.

na ukumbuke hii ni kwa watu weusi tu.wazungu hawahusiki kwenye ushahidi huu.
 
Kwanza kabisa hatukuwaacha nyani ambao hawakubadilika.

Watu wengi wanafanya makosa ya kufikiri kuwa evolution inasema zamani tulikuwa sawa na hawa nyani wa sasa, sisi tumebadilika wao hawajabadilika.

Hivyo si evolution inavyosema. Wote tumebadilika. Ila tulikuwa na a common ancestor ambaye alikuwa more ape like, maana yake sisi tumebadilika zaidi.

Kwa mujibu wa evolution.

Evolution inakwenda kwa natural selection. Kuna mazingira fulani yanafanya species fulani zife, nyingine ziendelee kuwapo, nyingine zibadilike.

Kwa mfano, kwenye mazingira ya misitu, wanyama wanaofanana na misitu ile wanaweza kupata advantage ya kuwa camouflaged wakaendelea kuwapo, na wasio na rangi ya hiyo misitu kuwindwa kirahisi na kutoweka, matokeo yake baada ya vizazi vingi wanyama wenye rangi isiyo na advantage ya camouflage watatoweka na wale wanaofanana na msitu wataongezeka na kuwa ndiyo watawala.

Kitu kingine ambacho ni kigumu kuelewa ni kuwa, kwa mujibu wa theory ya evolution, evolution inatokea katika mamilioni na malaki ya miaka, mabadiliko madogo madogo yanalimbikizana na kusababisha mabadiliko makubwa.

Sasa watu wengi wanaohoji evolution wanahoji kama vike wanataka kuona mabadiliko katika umri wao, miaka 30, miaka 50.

Ukitaka kuona evolution katika muda nfupi usiangakie wanyama wakubwa kama sokwe, nyani au watu. Ukitaka kuangalia evolution katika muda nfupi angalia vidudu kama bacteria, virus.

Angalia kitu kinaitwa anti-biotic resistance na jinsi bacteria wanavyojenga resistance dhidi ya dawa.

Unajua kwa nini hospitali hawatumii tetracycline tena? Unajua kwa nini madawa ya zamani ya malaria hayatibu tena malaria inabidi tutumie madawa mapya?

Hiyo ni evolution. Vidudu vimejipanga kuweza kujikinga na dawa, vime evolve.

Ukitaka kuelewa evolution usiangakie nyani na watu, angalia jinsi bactwria na microorganism nyingine zinavyojenga resistance dhidi ya dawa, na kwa nini tunahitaji dawa mpya, kwa nini zamani magonjwa kama gono yalikuwa yanatibiwa na tetracycline lakini siku hizi kuna gononsugu halisikii dawa.

Vidudu vya gono vimefanya evolution.
Samahani Kidogo Mkuu..
Hebu nipe Tofauti ya Mutation na Evolution..
Maana Katika maongezi yako ya Chini Paragraph ya Tano kutokea Chini Umeelzea Mutation badala ya Evolutiion
 
Ndugu zangu.

1: Tukiachana na maswala ya kidini, historia inatuambia binadamu wa kwanza alikua ni nyani / sokwe /chipanze, sasa kama kweli binadamu tulikua ni manyani ni kwanini nyani / sokwe tunaowaona sasa hivi hawabadiliki kua binadamu na wala hawakatiki tena mikia na kua na mwili na utashi wa binadamu kama historia ilivyokua huko awali?

2: Je, kama kweli tulikua nyani na tukabadilika kua binadamu ni kwanini sahivi haiwezekani tena binadamu kubadikika na kurudia kua nyani kama wanasayansi wanavyodai?
Siku moja binadàmu wanatoka msituni wanakuja kusema, sijui kwa kitumia lugha gani, kwamba wálikuwa sokwe na wamebadilika kuwa binadàmu na wanatafuta vitambulisho vya taifa!
Serious kabisa!
 
Hapa tunazungumzia evolution ya mawe?
Lengo la theory ya evolution si kuelezea maisha yalivyoanza, lengo la evolution ni kuelezea maisha yaanavyobadilika baada ya kuanza, jinsi species zinavyobadilika muda unavyoenda kuendana na natural selection.

Somo la jinsi maisha yalivyoanza ni somo la abiogenesis, si somo la evolution.
 
Ndugu zangu.

1: Tukiachana na maswala ya kidini, historia inatuambia binadamu wa kwanza alikua ni nyani / sokwe /chipanze, sasa kama kweli binadamu tulikua ni manyani ni kwanini nyani / sokwe tunaowaona sasa hivi hawabadiliki kua binadamu na wala hawakatiki tena mikia na kua na mwili na utashi wa binadamu kama historia ilivyokua huko awali?

2: Je, kama kweli tulikua nyani na tukabadilika kua binadamu ni kwanini sahivi haiwezekani tena binadamu kubadikika na kurudia kua nyani kama wanasayansi wanavyodai?
Baada ya uchaguzi ijao nyani watakuwa binaadamu na watu watageuka binaadamu tujiandae kusipatwe na mshituko.
 
Back
Top Bottom