Kama Rais Samia ana nia ya kukomesha mara moja watu kutekwa na kuuawa, atoe tamko hili

Kama Rais Samia ana nia ya kukomesha mara moja watu kutekwa na kuuawa, atoe tamko hili

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Inahitaji tamko moja tu kwa Raisi Samia kukomesha uteaji na uuaji wa raisa wa Tanzania. Anachotakiwa kufanya ni kutoa tamko hili kama Amiri Jeshi Mkuu;

"Kwa kipindi hiki tukitafuta suluhisho la kudumu kokomesha utekaji na uuaji, ieleweke wazi kwa raia na wakazi wote hapa Tanzania kwamba kuanzia sasa hakuna chombo chochote cha usalama nchini, zaidi ya Jeshi la Polisi, ambacho kina mamlaka ya kukamata watu (kufanya arrest). Na ukamataji wowote utakaofanywa na Polisi, ni lazima ufanyike askari wa polisi wakiwa na uniform zao na vitambulisho, na wakitumia magari yenye utambulisho wa alama za polisi na pamoja na registration number.

Na ni jukumu la vyombo vingine vyote vya usalama, kutia ndani Usalama wa Taifa TISS na Takukuru, kama wana sababu za kumkamata au kufanya arrest ya mtu yeyote ndani ya Tanzania, watafanya hivyo kwa kupitia na kuwatumia Jeshi la Polisi, na Polisi watamkamata huyo mtu kwa utaratibu niliousema hapo juu.

Hivyo basi, na iwe wazi kwa raia wote wa Tanzania kwamba ukamataji wowote wa mtu ndani ya Tanzania, awe raia au mgeni, ukifanyika nje ya utaratibu huu, huo si ukamataji halali, na Jeshi la Polisi na raia wote kwa ujumla wanakuwa na wajibu wa kuzuia ukamataji huo usifanyike, kutia ndani kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi"


Sasa, kama ni kweli Raisi Samia ana nia na yeye binafsi au serikali yake haihusiki, au chama chake CCM hakinufaiki na utekaji huu na mauaji yanayofanyika, hili tamko litakomesha huu utekaji mara moja. Swali ni kwamba, je huu utekaji hauna baraka za serikali, au chama cha CCM? Kama una hizo baraka, basi tusitarajie kama Raisi Samia atatoa tamko hili, kwa sababu atakuwa anajua kinachoendelea na menginne yote anayosema kuhusu utekaji yanakuwa ni maigizo tu.
 
Hawezi kwa sababu ana uhusika kwenye hili.

  1. kuiweka TISS chini yake
  2. Kuwapa mamlaka ya kisheria ya kuarest
  3. Kuwapa kinga ya kisheria endapo wataua
  4. Alishasema utekaji ni drama kwa wanaotekwa
  5. Alishasema yeye ni chura kiziwi. Imekuwaje akasikia uchungu wa haya mauaji?
 
Hawezi kwa sababu anahusika
Ndio maana nikasema la sivyo anajua kinachoendelea. Nimetumia diplomasia tu kusema hivyo ili asione nampa ushauri huku nikimtuhumu!

Na kama hawezi kutoa agizo kama hili atueleze kwa nini hawezi kufanya hivyo, akijua tamko hili litakomesha utekaji mara moja!
 
Hawezi kwa sababu ana uhusika kwenye hili.

  1. kuiweka TISS chini yake
  2. Kuwapa mamlaka ya kisheria ya kuarest
  3. Kuwapa kinga ya kisheria endapo wataua
  4. Alishasema utekaji ni drama kwa wanaotekwa
  5. Alishasema yeye ni chura kiziwi. Imekuwaje akasikia uchungu wa haya mauaji?
Kwa hiyo kuna uwezekano haya yote yanafanywa na TISS? Kama ni wao, hivi hao TISS ni raia wa Tanzania kweli?

Ila ninachokumbuka, wakati wa Raisi Mwinyi, ilisemekana TISS walimchinja kama kuku mwanafunzi mmoja wa uhandisi pale Chuo Kikuu, Hall 2. Sasa ilileta mtafaruku kwa sababu ndani ya TISS walianza kulaumiana, ikawa watu wa TISS wa Nyerere, ambao walionekana ni watu wa kutoka Tanzania bara, wakawa wanasema waliofanya kitendo kile ni watu wa TISS walioletwa na Mwinyi, hasa kutoka Zanzibar. Watu wa TISS-Mwinyi wakawa wanasema watu wa TISS-Nyerere ndio walikuwa wanashirikiana na Mzee Punch na kutoa siri za Ikulu. Ikawa wazi kuna mtafaruku kati ya TISS iliyoonekana ni ya Nyerere, na TISS iliyoonekana ni ya Mwinyi. Hali ilipofikia hapa ilibidi UDSM ifungwe mwaka mzima. Wengi hawakujua sababu halisi za kukifunga chuo. Muulize James Mbatia anaweza kukusimulia!

Labda sasa pia kumeanza kuwa na mtafaruku wa namna hii ndani ya TISS - kumezuka TISS ya mama!
 
Polisi pekee ndo wanamamlaka ya kwanza ya kukamata, japokua kisheria hata raia anaruhusiwa kukamata muhalifu lakini baada ya kumkamata tu anatakiwa amfikishe kituo cha polisi, na baada ya hapo mtuhumiwa anayo haki ya kuwajulisha ndugu zake, vinginevyo yeyote atakaekukamata na baada ya kukukamata asipokupeleka kwenye chombo chenye mamlaka ya kukuhifadhi ambacho ni kituo cha polisi mtu huyo atahesabika kuwa ameteka.
 
Polisi pekee ndo wanamamlaka ya kwanza ya kukamata, japokua kisheria hata raia anaruhusiwa kukamata muhalifu lakini baada ya kumkamata tu anatakiwa amfikishe kituo cha polisi, na baada ya hapo mtuhumiwa anayo haki ya kuwajulisha ndugu zake, vinginevyo yeyote atakaekukamata na baada ya kukukamata asipokupeleka kwenye chombo chenye mamlaka ya kukuhifadhi ambacho ni kituo cha polisi mtu huyo atahesabika kuwa ameteka.
Ndio maana nikasema kwa sasa, Polisi peke yake wapewe hayo mamlaka wakati athari za sheria za ukamataji zikiangaliwa upya
 
Inahitaji tamko moja tu kwa Raisi Samia kukomesha uteaji na uuaji wa raisa wa Tanzania. Anachotakiwa kufanya ni kutoa tamko hili kama Amiri Jeshi Mkuu;

"Kwa kipindi hiki tukitafuta suluhisho la kudumu kokomesha utekaji na uuaji, ieleweke wazi kwa raia na wakazi wote hapa Tanzania kwamba kuanzia sasa hakuna chombo chochote cha usalama nchini, zaidi ya Jeshi la Polisi, ambacho kina mamlaka ya kukamata watu (kufanya arrest). Na ukamataji wowote utakaofanywa na Polisi, ni lazima ufanyike askari wa polisi wakiwa na uniform zao na vitambulisho, na wakitumia magari yenye utambulisho wa alama za polisi na pamoja na registration number.

Na ni jukumu la vyombo vingine vyote vya usalama, kutia ndani Usalama wa Taifa TISS, Takukuru na vyombo vingine, kama wana sababu za kumkamata au kufanya arrest ya mtu yeyote ndani ya Tanzania, watafanya hivyo kwa kupitia na kuwatumia Jeshi la Polisi , na Polisi watamkamata huyo mtu kwa utaratibu niliousema hapo juu.


Hivyo basi, na iwe wazi kwa raia wote wa Tanzania kwamba ukamataji wowote wa mtu ndani ya Tanzania, awe raia au mgeni , ukifanyika nje ya utaratibu huu, huo si ukamataji halali, na Jeshi la Polisi na raia wote kwa ujumla wanakuwa na wajibu wa kuzuia ukamataji huo usifanyike, kutia ndani kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi"

Sasa, kama ni kweli Raisi Samia ana nia na yeye binafsi au serikali yake haihusiki, au chama chake CCM hakinufaiki na utekaji huu na mauaji yanayofanyika, hili tamko litakomesha huu utekaji mara moja. Swali ni kwamba, je huu utekaji hauna baraka za serikali, au chama cha CCM? Kama una hizo baraka, basi tusitarajie kama Raisi Samia atatoa tamko hili, kwa sababu atakuwa anajua kinachoendelea na menginne yote anayosema kuhusu utekaji yanakuwa ni maigizo tu
Tamko halisaidii...ile sheria ya kikatili iliyopitishwa fasta fasta ifutwe🚮
 
Tunatoa angalizo mapema wasije wakatuletea wafungwa kutoka DRC au Uganda wakafanya cover up kwamba ndiyo wanahusika na mauaji ya Ali Kibao.

Waliomuua Ali Kibao ni "wasiojulikana" na pia kuna sheria ya kuwalinda hao watu sasa sijui watafanyaje hapo kuweza kuwashitaki.
 
Tunatoa angalizo mapema wasije wakatuletea wafungwa kutoka DRC au Uganda wakafanya cover up kwamba ndiyo wanahusika na mauaji ya Ali Kibao.

Waliomuua Ali Kibao ni "wasiojulikana" na pia kuna sheria ya kuwalinda hao watu sasa sijui watafanyaje hapo kuweza kuwashitaki.
Hivi yule taxi driver aliyeshirikiana na foreigners kumteka Mo kesi yake iliishaje?
 
Hivi yule taxi driver aliyeshirikiana na foreigners kumteka Mo kesi yake iliishaje?
Hakuwepo mtu wa namna hiyo, walifanya hivyo kutuliza hasira za wananchi. Hata hili la sasa watakuambia tumekamata watu tunawahoji nk, ili kutuliza hasira tu, halafu wanasubiri mechi ya Liverpool na Arsenal ije ili watu waanze kuongelea mpira badala ya utekaji!
 
Hawezi kwa sababu ana uhusika kwenye hili.

  1. kuiweka TISS chini yake
  2. Kuwapa mamlaka ya kisheria ya kuarest
  3. Kuwapa kinga ya kisheria endapo wataua
  4. Alishasema utekaji ni drama kwa wanaotekwa
  5. Alishasema yeye ni chura kiziwi. Imekuwaje akasikia uchungu wa haya mauaji?
Aisee..
Hatarii..
 
Hawezi kwa sababu ana uhusika kwenye hili.

  1. kuiweka TISS chini yake
  2. Kuwapa mamlaka ya kisheria ya kuarest
  3. Kuwapa kinga ya kisheria endapo wataua
  4. Alishasema utekaji ni drama kwa wanaotekwa
  5. Alishasema yeye ni chura kiziwi. Imekuwaje akasikia uchungu wa haya mauaji?
Hatima yake itakuwa kama ya Jiwe.
 
Back
Top Bottom