Kama Serikali ya Tanzania haina dini, Mungu anayetajwa katika wimbo wa taifa ni yupi?

Kama Serikali ya Tanzania haina dini, Mungu anayetajwa katika wimbo wa taifa ni yupi?

ngoshwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2009
Posts
4,131
Reaction score
937
Hivi iki kiapo cha uaminifu kwa viongozi wetu wakiwa wameshikilia vitabu vya dini zao mikononi au kutamka maneno yanayofaa kuchukuliwa kama "kiapo cha uamninifu" kina maana yeyote kwetu au ni mambo ya mapokeo na ambayo yamejaa kwa waliotoa dhamana?

Ikiwa ukiapa kanisani kwa kushika/ kuiinua juu Msaafu au Biblia na badae ukatenda dhambi ya kushindwa kutekeleza yale uliyoapa, unapaswa kumrejea Mungu na kumwaomba huruma zake, na ikiwa kwa Serikali viongozi wanaapa kwa kushika Vitabu vya Dini na Katiba ya Nchi mbele ya Watanzania, inakuwaje mtu akitenda uovu unaokiuka kiapo cha uaminifu aishie kusema "nimejihudhuru / nimeachia ngazi" tu na kama alikuwa Waziri basi ataendelea na nafsi yake ya ubunge ambao pia una kiapo cha uaminifu kwa mujibu wa Katiba?

Je, ikiwa kiongozi amevunja kiapo cha uaminifu na ameendelea kuwepo ndani ya mmoja ya mihimili ya Serikali , kuna sababu yeyote ya kuwa na kiapo cha uaminifu ikiwa kiutendaji ioanekana kama hakiheshimiwi kabisa?

Ikiwa kukiri kosa ni pamoja na kusema "najihudhuru/naachia ngazi" ikimaanisha kushindwa kuendelea na dhamana ile uliyopewa aua umehusika moja kwa moja na tuhuma zinazodaiwa dhidi yako au watendaji waliochini yako, Je, ipo haja tena ya mtu ambaye alikiri kushindwa kutekeleza kiapo cha uaminifu kwa kwa staili ya "kujihudhuru wadhifa fulani" kuendelea kupewa madaraka mengine Serikalini pasipo kutakiwa kuapa upya kiapo cha uaminifu au hata kufikishwa mbele ya Mahakama ili ikamsafishe kwa dhambi ambazo anatuhumiwa nazo?

Ikiwa kiongozi aliyekula kiapo cha uaminifu na kwa makusudi au kwa kutokujali anashindwa kutimiza wajibu chini ya kiapo kwa kutowachukulia hatua stahiki wale ambao wanatuhumiwa kwa ufisadi na oovu wa kurejesha nyuma maendeleo ya nchi, Je, tuna haja ya kuendelea kuwa na hiki kiapo cha uaminifu katika taratibu zetu.?

Na ikiwa kiongozi anaweza kuthibutu kudanganya mali zake chini ya kiapo cha uaminifu, ipo sababu yeyote ya kukiamini "kiapo cha uaminifu?" au tubadili sheria zetu ili kama mtu aliwahi kukiuka kiapo cha uaminifu asiruhusiwe tena kushika wazifa wowote wa kisherikali au kisiasa?


KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA YA MWAKA 1977

Ibara ya 42(5) Kila Rais mteule na kila mtu atakayeshikilia kiti cha Rais, kabla ya kushika madaraka ya Rais, ataapa mbele ya Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, kiapo cha uaminifu na kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

Ibara ya 49. Makamu wa Rais, kabla ya kushika madaraka yake ataapishwa mbele ya Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, kiapo cha uaminifu na pia kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

Ibara ya 51.-(1) Kutakuwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano atakayeteuliwa na Rais kwa kufuata masharti ya ibara hii na ambaye kabla ya kushika madaraka yake ataapa mbele ya Rais kwa kiapo kinachohusika na kiti cha Waziri Mkuu kitakachowekwa na Bunge.

Iabra ya 56. Waziri au Naibu Waziri hatashika madaraka yake ila mpaka awe ameapa kwanza mbele ya Rais kiapo cha uaminifu na pia kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

Iabara ya 68. Kila Mbunge atatakiwa kuapishwa katika Bunge kiapo cha uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za Bunge; lakini Mbunge aweza kushiriki katika uchaguzi wa Spika hata kabla hajaapishwa.

Ibara ya 84 (9) Mtu yeyote ambaye si Mbunge atakayechaguliwa kuwa Spika, atatakiwa, kabla ya kuanza kutekeleza madaraka yake, kuapishwa katika Bunge kiapo cha uaminifu.

Ibara ya 103 (2) Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kabla ya kushika madaraka yake ataapa mbele ya Jaji Mkuu wa Zanizibar kiapo cha kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano, na kiapo kingine chochote kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar kinachohusika na utendaji wa kazi yake, kisha atashika na kutekeleza madaraka hayo kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii na Katiba ya Zanzibar, 1984.

Iabra ya 111. Jaji wa Mahakama Kuu hatashika madaraka yake ila mpaka awe ameapishwa kwanza kiapo cha uaminifu na pia kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungw na Bunge.

Iabara ya 121. Jaji wa Mahakama ya Rufani hatashika madaraka yake ila mpaka awe ameapishwa kiapo cha uaminifu na kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

Tafsiri:

Iabra ya 151.-(1) "kiapo" maana yake itabidi ifahamike kwa maana ya kawaida ya
neno hilo na ni pamoja na tamko rasmi la namna yoyote linaloruhusiwa kisheria kutumiwa badala ya kiapo;

"kiapo cha uaminifu" maana yake ni kiapo cha kuwa mwaminifu kwa nchi na kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
 
ngoshwe,

Kiapo kwa viongozi wetu hakina uzito unaostahili wala maana yoyote kwao wao.

Ingawa si mfano mzuri sana lakini kinachotokea katika uapaji huu usio na tija ni sawa na mwanamume ama mwanamke wa kikristo anapofunga ndoa kuahidi kumpenda mkewe hadi kifo kiwatenganishe lakini baada ya muda ndoa hiyo inasambaratika!
 
Excellent! hakuna haja ya kuapa(swering, vows, oaths), simply wenye dini wengi hawa wasio viongozi tu ni wasanii, watanzania wengi sio wafuataji wa dini hizi, dini zimekuwa utamaduni tu na sio reality. That goes even kwa viongozi, vile vitabu vya dini havina nguvu zozote zile kwa wahusika, mbaya zaidi mnaposeam serikali haina dini!

Kama apa ya viongozi ni (vows); Basi muapaji wa dini husika ni yule anayejua fika kuhusu hiyo dini, anamwamini Mungu vilivyo, ingekuwa hivyo hao waapaji wangekuwa wanapata madhara fulani kwa kutosimamia viapo vyao. Hali kadhalika kwa wanandoa ambao seriously wanamwabudu Mungu, wakati wanaapa(vows) walijua value ya viapo vyao, then wengi hupata matatizo wanapovunja viapo vyao. Kama haumwamini Mungu, hauko kisawa swa then kiapo hakina matatizo na wewe! so kwa wasanii wanandoa ambao wanadhani kuapa kanisani kunasaidia hakuna maana yoyote kama muhusika hajuo lolote kuhusu dini! the same applies kwa viongozi. Maana uhusiano wa mtu na Mungu haukai kwenye vitabu bali moyoni na kiapo kina nguvu sana aana unatamka! ila kama hauna uhusioan na huyu unayemwapia, then hakuna kinachotokea!. Kuapa kwa viongozi kunaweza kuangu

we need to find another solution, maana aliyekosea kutimiza kiapo, ataishia kuomba msamaha kwa Mungu! then serikali haitakiwi kuwa hivyo.

Asante Ngoswe for this insight, is completely meaningless kuwa na viapo, waapaji, wasimamia,viapo, na hakuna kinachofanyika wakikosea! aha! ha! ha! tuliingizwa mjini. Kumbe EL, Chenge wanaweza tu kuomba msamaha!

KAMA apa yao hii ni (oaths au swering); Ukija in bible point of viewI i hairuhusu swering/oaths. Matthew 5:33-37). Ukifuata agano la kale linaruhusu oaths, ila hutakiwi kuvunja, agano letu la sasa Yesu anasema hata kuapa hutakiwi kabisa. SO kinachoendelea kwa viongozi wetu ni usanii kwa kwenda mbele!
 
Excellent! hakuna haja ya kuapa(swering, vows, oaths), simply wenye dini wengi hawa wasio viongozi tu ni wasanii, watanzania wengi sio wafuataji wa dini hizi, dini zimekuwa utamaduni tu na sio reality. That goes even kwa viongozi, vile vitabu vya dini havina nguvu zozote zile kwa wahusika, mbaya zaidi mnaposeam serikali haina dini!

Kama apa ya viongozi ni (vows); Basi muapaji wa dini husika ni yule anayejua fika kuhusu hiyo dini, anamwamini Mungu vilivyo, ingekuwa hivyo hao waapaji wangekuwa wanapata madhara fulani kwa kutosimamia viapo vyao. Hali kadhalika kwa wanandoa ambao seriously wanamwabudu Mungu, wakati wanaapa(vows) walijua value ya viapo vyao, then wengi hupata matatizo wanapovunja viapo vyao. Kama haumwamini Mungu, hauko kisawa swa then kiapo hakina matatizo na wewe! so kwa wasanii wanandoa ambao wanadhani kuapa kanisani kunasaidia hakuna maana yoyote kama muhusika hajuo lolote kuhusu dini! the same applies kwa viongozi. Maana uhusiano wa mtu na Mungu haukai kwenye vitabu bali moyoni na kiapo kina nguvu sana aana unatamka! ila kama hauna uhusioan na huyu unayemwapia, then hakuna kinachotokea!. Kuapa kwa viongozi kunaweza kuangu

we need to find another solution, maana aliyekosea kutimiza kiapo, ataishia kuomba msamaha kwa Mungu! then serikali haitakiwi kuwa hivyo.

Asante Ngoswe for this insight, is completely meaningless kuwa na viapo, waapaji, wasimamia,viapo, na hakuna kinachofanyika wakikosea! aha! ha! ha! tuliingizwa mjini. Kumbe EL, Chenge wanaweza tu kuomba msamaha!

KAMA apa yao hii ni (oaths au swering); Ukija in bible point of viewI i hairuhusu swering/oaths. Matthew 5:33-37). Ukifuata agano la kale linaruhusu oaths, ila hutakiwi kuvunja, agano letu la sasa Yesu anasema hata kuapa hutakiwi kabisa. SO kinachoendelea kwa viongozi wetu ni usanii kwa kwenda mbele!

Ngoshwe, Kiapo kwa viongozi wetu hakina uzito unaostahili wala maana yoyote kwao wao. Ingawa si mfano mzuri sana lakini kinachotokea katika uapaji huu usio na tija ni sawa na mwanamume ama mwanamke wa kikristo anapofunga ndoa kuahidi kumpenda mkewe hadi kifo kiwatenganishe lakini baada ya muda ndoa hiyo inasambaratika!



Nakubalina kabisa!

Kinacho nisikitisha zaidi ni pale unapokuta mtu anapofunga nadhiri na "agano la kishetani" kule Mlingotinio na kwingineko ili aendelee kuishi katika nyazifa. Hapo daima anakuwa akiheshimu hilo agano hata pale inapobidi kutoa roho ya mwingine nk, ataitoa. Kuna ushuhuda wa kutosha kabisa kuwa wapo waheshimiwa wanatembea na "waganga wa Kienyeji" kama msaidizi wake popote aendapo (Guru) na mganga ndio nguzo yake muhimu kuliko Serikali wala wapiga kura wake...

Kwa hivi viapo vya kiserikali hakuna shaka kabisa kuwa haviheshimiki kwa kuwa havina madhara yoyote ukikiuka. Hivyo havina maana yeyote zaidi ya kutudanganya na kupoteza akili sisi wapiga kura tukabakia tukiona waapaji wataheshimu mamlaka ya Mungu na Serikali yao ambayo Mungu amaiweka.
 
Wana JF,

Naomba tushauriane inakuwaje wakati wa kuapishwa viongozi tunaona serikali ikiwaapisha kwa kutumia vitabu vya dini wakati Serikali yenyewe haina dini wala imani yoyote ya kidini?

Labda kiapo hiki ni cha uongo ndio maana hata walioapa kwa vitabu hivyo wanafanya maovu lakini hawadhuriki.

Tupendekeze wakati wa kuapishwa waalikwe vion gozi wakuu wa dini waje na vitabu ambavyo vimeswaliwa na kuombewa ili wawaapishe waumini wao ambao wanakabidhiwa dhamana ya kuongoza nchi na watu wake.

Mnasemaje wana JF hoja hii imekaaje? tujadili.
 
Labda kuwe na viapo viwili na vyote iwe lazima kutimizwa.

Kiapo cha kwanza kiwe kiapo cha dini kinachoongozwa na kiongozi wa dini ya Mhusika wakitumia kitabu husika,

Na cha pili kiwe kiapo secular kinachoongozwa na jaji mkuu akitumia katiba.

Hiki kinachofanyika sasa hivi ni usanii mtupu usiokuwa na maana, Mfano kitendo cha Jaji Mkuu wa dini fulani kumwapisha Rais ambae ni wa dini tofauti na yeye tayari kunaleta walakini fulani katika kiapo.

Kama serikali imeamua kutambua umuhimu wa dini ya mtu katika kiapo, NI lazima itengeneze mazingira ya kufanya kiapo hiki kiwe na maana kwa yule anaeapa, kwa kutambua tofauti zilizomo katika imani hizi na kuheshimu tofauti hizi.

Ni kichekesho na utani kwa Mwislamu kumuapisha Mkristo and vice versa kwa sababu hawana common belief.
 
serikali haina dini ila raia wake wana dini. Hata uchawi ni hivyo hivyo, serikali haiamini uchawi ila kiongozi mmoja mmoja anakwenda kwa mganga au ana shiriki uchawi na mwingine anaahidiwa ulinzi na mnajimu wakati kuna pesa wa wananchi za kuwalipa ma-body guards.
 
Serikali kwa muda mrefu imekua ijigamba kuwa haina dini? Cha kushangaza kuna matangazo ya dini hurushwa kila siku kupitia vyombo vya habari vya Taifa. Ie. TBC! Je, hii imekaaje?
 
serikali haina dini ila wananchi ndio wenye dini na tbc uwa inaonyesha vipind vya waislam na wakristo pia bila kubagua.
 
Nijuavyo serikali haina dini kweli ila inatambua watu wake wanadini na serikali inaliheshimu Hilo.ka hili la kurusha matangazo ya dini sioni Kama ni makosa kwani ni kuwapa wananchi wake nafasi ya kuona na kushirikiana ktk imani zetu.
 
Dini sio ukristo na uislam tu! Kwa hiyo kurusha matangazo ya hizo dini mbili huoni tayari inafanya 'bias'? Na kwa ambao hawana dini je?
 
Serikali kwa muda mrefu imekua ijigamba kuwa haina dini? Cha kushangaza kuna matangazo ya dini hurushwa kila siku kupitia vyombo vya habari vya Taifa. Ie. TBC! Je, hii imekaaje?

...ndiyo! Isipokuwa viongozi wake, kama rais wetu na taasisi mbalimbali, kama hile iliyoanzisha ......Banking
 
Serikali kwa muda mrefu imekua ijigamba kuwa haina dini? JCha kushangaza kuna matangazo ya dini huushwa kila siku kupitia vyombo vya habari vya Taifa. Ie. TBC! Je, hii imekaaje?
kbla hujaleta uzi ungejiuliza kwanza ni dini zotehurushwa na iyo chanel au ni moja alafu rudi tupe jibu tukufafanulie yaweza kuwa umekurupuka tu
 
Tunazugwa tuu hapo. Kuna dini inafuatwa ila kinachofanyika ni siri.
 
Sababu wanaoimba wimbo huo na wanaoishi Nchi ya Tanzania ndiyo wenye dini,hivyo ni haki kumtaja Mungu wanayemuamini.

Nadhani waislamu wanamini Mungu,wakristu vile vile na wapagani nao wanamaini miungu yao.Sioni kama kuna shida japo namna ya kuabudu na kuamini ni tofauti.
 
Serikali ya Tz haina dini, tunapoimba wimbo wa taifa tunamtaja Mungu yupi? Inanipa shida sana kuelewa kwenye hii issue. Tafadhari kama kuna mtu anaelewa the reason behind.

Kusema Serikali haina dini ni kutokujuwa maana ya neno "dini".

Hilo lililetwa na Nyerere, huku anahubiri serikali haina dini, huku anawajaza Wagalatia wenzake kila sehemu na kuwapa kipaumbele cha elimu.

Msome Sivalon anachambuwa hilo.

Unafik mtupu.
 
Serikali ya Tz haina dini, tunapoimba wimbo wa taifa tunamtaja Mungu yupi? Inanipa shida sana kuelewa kwenye hii issue. Tafadhari kama kuna mtu anaelewa the reason behind.

Haina dini ndiyo, lakini ina Mungu. Haina dini maanake haifungamani na dhehebu lolote. Ila ina Mungu, na wimbo wake wa taifa unashuhudia hilo.
 
Back
Top Bottom