Onghwise , ujue serikali ina wajibu na maisha ya kila siku ya mwananchi. Kwani wameapa kulinda na kusimamia ustawi wa taifa letu. Sasa wanaposhauriwa kufuata taaluma ya jambo husika, halafu unasikia kiongozi mkuu anasema tusitishwe !!. Unabaki unashangaa. Hapo unalaumuJe wapinzani ?! Tuwe wakweli
Leo hii Dar na Zanzibari ilitakiwa ziwe zimeshafungiwa ili ugonjwa uwe controlled huko. Lakini kinyume chake ndege, mabasi na hata treni zinasomba na kuendelea kuuguza nchi nzima. Hapa unawalaumuJe wapinzani ?!. Kikwetu wanasema ukiona giza toka ukojoe nje sio ndani kwa kuhofia giza. Maana yake hutakiwi kuendelea kutukuza madhaifu ya serikali kisa tu uoga. Mwisho ugonjwa huu utamalizwa na taaluma si siasa za nani ni shujaa. Waulize wa Germany, China na sasa Rwanda wamefaulu vipi kupunguza maambukizi . Hebu tuache ushabiki wa kumuunga mtu hata kama anafanya mambo ya hovyo.
Odhis *