#COVID19 Kama Taifa limekubali chanjo ndio maslahi ya Taifa, Viongozi wote wanakuwa Bind na A Collective Responsibility Clause. Must support, Shut up or quit!

Inawezekana Gwajima kawakera wengi lakini kwangu nashukuru amesema maana tunaijua nchi yetu, tatizo la umeme lilitumika tukapigwa! Hata hii issue ya Uviko ni vizuri maswali ya msingi yajibiwe kitaalam.

Zipo taarifa nyingi za waliochanjwa huko nje kuwa ni waathirika wa hili wimbi jipya la uviko, je kinga imesaidia nini?

What if hao wanaochanjwa ndio wanakuja kuambukiza zaidi (hapa wataalam wafafanue).

Baadhi ya chanjo zilisitishwa huko zinakotoka je tumejirithisha ni salama kwa utafiti upi? Wasiwasi isiwe tumetumia maelekezo ya hao manufacturers kuamua badala ya kufanya utafiti hadi wa components za chanjo hizo. Kamati iliyotushauri ilifanya kazi siku chache tu!

Matokeo ya matumizi ya hizi chanjo si lazima iwe ni mwezi au wiki, madhara yanaweza kutokea hata miaka 10 au zaidi ijayo!

Huu ugonjwa kuanzia kuibuka kwake hadi suluhisho lake yamejaa utata mwingi sana, tunapaswa kwenda kiutata hivyo hivyo badala ya wimbo wa twende na dunia! Hoja za hao wazungu wangetaka kutumaliza wangeshafanya hivyo ni mfu maana ni sawa usahau kufunga mlango hadi asubuhi alafu sababu hukuibiwa basi uamue kuishi daima bila kufunga mlango!

Mwisho, Mch Gwajima staili yake ya kujenga hoja Inawezekana kuleta ukakasi na kama alivyosema Mh January Makamba mjadala juu ya usalama wa chanjo ni muhimu lakini si kuhamasisha kinyume ili maoni yako tu yachukuliwe.

Hata mimi binafsi ningetamani swala ya usalama wa chanjo lijadiliwe na wataalamu kwa uwazi baada ya kufanyika utafiti wa kina ikiwemo hizo components za chanjo. Ndio maana baadhi ya mataifa wametengeneza chanjo zao kwa usalama wao.

Swala la chanjo hata kama ni hiari haiondoi wajibu wa serikali tunayoiamini kuweka mazingira ya kuaminika juu ya swala hili. Chanjo na facts zake plus conspiracy inayoizunguka inahitaji kujibu maswali ambayo ni mjadala dunia nzima.
 
Swala la chanjo ikitokea bahati mbaya kuna makosa hatuwezi kurevise. Tunaweza kuunga mkono bajeti, sheria n.k maana haina matokeo ya kudumu! Chanjo ina matokeo ya kudumu ikitokea kuna makosa. Tujadiliane badala ya kutafuta nidhamu tu na kuacha la msingi.

Hapa Tanzania mpaka sasa si madaktari wala yeyote anayejadili usalama wa hizi chanjo kutokana na tafiti. Tuna chuo kikongwe kama Muhimbili wako kimya! Taasisi mbalimbali wako kimya.

Rais aliyepita alituonya juu ya hizi chanjo, kwanini tusimuamini aliyepita tuamini sasa? Kama tayari kuna contradictions kwanini taasisi zetu zije na hoja za kitafiti kabla hatujaanza kudunga watu wetu?

Tumepata chanjo ni vizuri ila nashauri zitumike kitafiti zaidi na si kama tiba ili tuweze kutengeneza zetu au kujiandaa na matokeo yake maana hata hao manufacturers wanakiri hawajui madhara mengine yanayoweza kutokea.
 
Ufunuo wa Yohana 13:16
Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao;

Ufunuo wa Yohana 13:17
tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.

Ufunuo wa Yohana 13:18
Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita.
 
Gwajima ni boya mmoja tu...hukatazwi kutoa maoni lkn siyo kwa style ile.
Sidhani kama watu wote wanaamin jamaa ni askofu kweli kimaadili lkn watu hao wamenyamaza kama wameshindwa kuongea.
Yeye mwenye kuweza kuongea hajui namna nzuri ya kuongea ndo maana leo mtu kama mimi nathubutu kumwita jamaa ni mpumbav,atafute namna nzuri ya kuongea na waumini wake juu ya chanjo na si kuidhihaki serikali na rais
 
Gwajima hana kosa.
Yeye ni mbunge nayeye ni raia anahaki ya kutowa mawazo yake ikiwa sawa na serikali au kinyume.
Wanaotaka watasikiliza wasopenda waya puuze.

Nchi zilizo endelea wamebadilisha chanjo mara chungunzima baada ya kugunduwa zina matatizo. Tunauhakika gani hizo zitakazo letwa ni new batch au zile batch zilizo na matatizo.
Tanzania hatuna wataalamu , hata kama tunao basi rahisi kununuliwa.
Mpaka hii leo hizi chanjo bado zinaleta madhara lakini watu hupelekwa hospitali na kufanyiwa uchunguzi na kutibiwa.
Jee kwetu tunaoutaalamu au vifaa au nyenzo za kumchukuwa mtanzania aliye chanja na kumwahisha hospital kama chanjo imeleta matatizo?
 
Kwangu Gwaji boy ni wa kusaidiwa. Siaamini kama ni mzima. Kama yeye ni mzima basi wafuasi wake watakuwa ndiyo wenye matatizo.

Huyu bwana alifufua mtu mchana kweupe tena mbele ya wafuasi wake, wakamuamini.

Huyu bwana alikufa halafu akajifufua na kutoa ushahidi mbele ya wafuasi wake, wakamuamini.

Huyu bwana aliahidi amepata pesa za kuleta train ya kuwabeba wafuasi wake, Wakaamini.

Huyu bwana alisema mbele ya wafuasi wake Corona haitafika Tanzania, wakamuamini.

Huyu bwana alidai mbele ya wafuasi wake kuwa anaponya corona na hakuna atakayekufa kwa corona, wakamuamini.

Huyu bwana sasa anadaia watakaochanja watanzania corona watakufa, Wamemuamini.

Yaani uongo wote huo kama bado kuna watu bado wanamsikiliza wanamuamini, tena in numbers basi wao ndiyo wenye matatizo. Diallo alishasema ....... sasa sisi tuchanganye na zetu!!
 
Unaanza kumendea teuzi? Kazana.
Alihoji Bungeni hawajatoa majibu unataka afanye Nini? Au unafiki Kama wewe.
 
Gwajima acha kuhubiri matukio ila neno la Mungu
 
Naunga mkono hoja hoja, hili mimi pia nililizungumzia...
katika muktadha mbili
1. A Collective Responsibility Clauses

2. Insubordination


P
 
Wewe umelipwa kuja kutudanganya hatutaki sumu zenyu muacheni Gwajima aongee
Gwajima scientists?????Gwaji boy kilaza tu mtihani wa form four alirudia mara tano kupata credits tatu😆😄😁🤣😳
 
i salute you. a henaho wayomba geete paasi
 
Ni kweli Insubordination sio jambo zuri but it depends on circumstances.
Kwa kesi ya Gwaji kwa kuwa ilishasemekana chanjo ni hiyari basi angeacha ibaki hivyo bila ya kuleta mtafaruku kama inavyochukuliwa kwa sasa. Hapa angeepuka malumbano. Unless otherwise kuna jambo analolijua linalompelekea kuendelea kufanya anavyofanya kama mtu anayejitoa muhanga.
 
Umeharibu mwishoni baada ya kumtaja jiwe kuwa alikuondolea hofu. Mengine uko sahihi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…