Kama Taifa nashauri tukubaliane kwa kauli moja kwamba majadiliano ya katiba mpya yaanze rasmi baada ya uchaguzi mkuu 2025

Kama Taifa nashauri tukubaliane kwa kauli moja kwamba majadiliano ya katiba mpya yaanze rasmi baada ya uchaguzi mkuu 2025

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Kutokana majukumu ya maandalizi mazito ya kazi za kikatiba kitaifa, kwa mfano ya uchaguzi wa serikali za mitaa nchini nzima, pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka ujao 2025..

Mambo haya muhimu kwa taifa, yanahitaji muda mwingi wa kutosha kijipanga na kuyaandaa, yanahitaji umakini, utulivu, uangalifu na weledi mkubwa sana wa kusheria na kikanuni ili yafanyike kwa ufanisi, lakini pia yanahitaji fedha na rasilimali watu wa kutosha kusimamia utekelezaji wake, ili kuepuka utata na malalalamiko yasio na tija baadae....

Ni busara kama Taifa la wastaarabu, wenye kuheshimiana kulingana na mila, desturi na utamaduni wa kitanzania, lakini pia kama Taifa linaloongozwa katika misingi ya kisheria, kikatiba, uwajibikaji, uwazi, usawa, haki, utawala bora, utangamano wa kidugu, amani na utulivu wa nchi yetu,

Kwa maoni yangu, kama hamtojali ndugu wananchi na waTanzania wenzangu,

Nashauri na kuwarai nyote kama Taifa, tuipe nafasi na muda wa kutosha serikali hii sikivu sana ya wananchi, na tuiache na kuipa fursa tulivu, ifanye maandalizi haya mazito na ya msingi sana kwa kipindi hiki, ili kwa wakati muafaka haya yanayoendelea kuhusu chaguzi yatakapotamatika, tuanze sasa mchakato wa katiba mpya tukiwa huru, wamoja na wenye nia, muda wa kutosha, dhamira na uelekeo moja kwa mustakabali mwema wa umoja, mshikamano na amani ya MAMA TANZANIA :pulpTRAVOLTA:

nawatakia nyote mapumziko mema ya wiki enda...

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE WOTE AIMEN..
 
Kwa jinsi tulivyoichoka ccm, hata huo uchaguzi tumeupuuza, na hicho kitendo Cha kulazimisha kuandika katiba kwa mtazamo wa kiccm, msitegemee katiba hiyo kukubalika na kizazi hiki.
zingatia ushauri wangu muhumu sana, inaweza kua msaada kwako baadae,

mengine ni uamuzi wa wananchi,
wenyewe wataamua kwa wakati muafaka kadiri watakavyoona inafaa na sio kwasababu wewe ati wewe binafsi unachukia nini na unapenda nini. ni muhimu hilo ukabaki nalo moyoni mwako binafsi tu:pulpTRAVOLTA:
 
zingatia ushauri wangu muhumu sana, inaweza kua msaada kwako baadae,

mengine ni uamuzi wa wananchi,
wenyewe wataamua kwa wakati muafaka kadiri watakavyoona inafaa na sio kwasababu wewe ati wewe binafsi unachukia nini na unapenda nini. ni muhimu hilo ukabaki nalo moyoni mwako binafsi tu:pulpTRAVOLTA:
Wananchi gani wanaaamua hapa? Hapa kwetu viongozi majizi wa ccm ndio wanaamua na kushurutisha wananchi kufuata watakacho. Kama ingekuwa ni wananchi wanaamua, leo hii tungekuwa na katiba mpya kupitia rasimu ya Warioba.
 
zingatia ushauri wangu muhumu sana, inaweza kua msaada kwako baadae,

mengine ni uamuzi wa wananchi,
wenyewe wataamua kwa wakati muafaka kadiri watakavyoona inafaa na sio kwasababu wewe ati wewe binafsi unachukia nini na unapenda nini. ni muhimu hilo ukabaki nalo moyoni mwako binafsi tu:pulpTRAVOLTA:
Michango ya watu humu pia ni maoni ya baadhi ya wananchi , unaweza ukalinganisha maoni ya humu ukajua picha halisi ya maoni ya wananchi kwa asilimia kubwa 🐒 .
 
Kutokana majukumu ya maandalizi mazito ya kazi za kikatiba kitaifa, kwa mfano ya uchaguzi wa serikali za mitaa nchini nzima, pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka ujao 2025..

Mambo haya muhimu kwa taifa, yanahitaji muda mwingi wa kutosha kijipanga na kuyaandaa, yanahitaji umakini, utulivu, uangalifu na weledi mkubwa sana wa kusheria na kikanuni ili yafanyike kwa ufanisi, lakini pia yanahitaji fedha na rasilimali watu wa kutosha kusimamia utekelezaji wake, ili kuepuka utata na malalalamiko yasio na tija baadae....

Ni busara kama Taifa la wastaarabu, wenye kuheshimiana kulingana na mila, desturi na utamaduni wa kitanzania, lakini pia kama Taifa linaloongozwa katika misingi ya kisheria, kikatiba, uwajibikaji, uwazi, usawa, haki, utawala bora, utangamano wa kidugu, amani na utulivu wa nchi yetu,

Kwa maoni yangu, kama hamtojali ndugu wananchi na waTanzania wenzangu,

Nashauri na kuwarai nyote kama Taifa, tuipe nafasi na muda wa kutosha serikali hii sikivu sana ya wananchi, na tuiache na kuipa fursa tulivu, ifanye maandalizi haya mazito na ya msingi sana kwa kipindi hiki, ili kwa wakati muafaka haya yanayoendelea kuhusu chaguzi yatakapotamatika, tuanze sasa mchakato wa katiba mpya tukiwa huru, wamoja na wenye nia, muda wa kutosha, dhamira na uelekeo moja kwa mustakabali mwema wa umoja, mshikamano na amani ya MAMA TANZANIA :pulpTRAVOLTA:

nawatakia nyote mapumziko mema ya wiki enda...

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE WOTE AIMEN..

Katiba mpya ni muhimu sana kwa sasa ili tusiendelee na hili giza la sasa. Kama ni lazima aheri tuusukume uchaguzi hata kwa mwaka mmoja au miwili mbele, lakini tusiendelee na mifumo hii ya giza isiyo na tija kwa Taifa.

Ni vema tukapata katiba bora mpya ya wananchi itakayolinda mamlaka ya mwananchi kuliko hii katiba iliyoandakuwa na watawala kwaajili ya kumgandamiza mwananchi.
 
zingatia ushauri wangu muhumu sana, inaweza kua msaada kwako baadae,

mengine ni uamuzi wa wananchi,
wenyewe wataamua kwa wakati muafaka kadiri watakavyoona inafaa na sio kwasababu wewe ati wewe binafsi unachukia nini na unapenda nini. ni muhimu hilo ukabaki nalo moyoni mwako binafsi tu:pulpTRAVOLTA:
Wananchi wa Tanzania hawajawahi kuandaa katiba ya nchi. Katiba tuliyo nayo sasa iliandaluwa na watawala kwa lengo la kumtawala mwananchi.
 
Michango ya watu humu pia ni maoni ya baadhi ya wananchi , unaweza ukalinganisha maoni ya humu ukajua picha halisi ya maoni ya wananchi kwa asilimia kubwa 🐒 .
si kweli hata kudogo,
huwez kua na IDs zaidi ya tano pekeyako kisha ukaja hapa ukasema ni maoni ya wananchi hali ya kua ni yako mwenyewe......

kama wa kubeba maoni na mitazamo ya wananchi wenye vyama na wasio na vyama, basi ni mimi ambae niko nao bega kwa bega physically and mentally field all the time, japo nipo hapa jukwaani kuona tu nini inaendelea duniani....

nadhani madhara ya hiyo mchezo yalishajitokeza huko nyuma hususan kwenye chaguzi kwamba fulani anakubalika sana, atashinda au ameshinda kumbe field wananchi hata hawamjui wala hawamfahamu :pedroP:
 
Wananchi wa Tanzania hawajawahi kuandaa katiba ya nchi. Katiba tuliyo nayo sasa iliandaluwa na watawala kwa lengo la kumtawala mwananchi.
ni muhimu sana ushauri wangu ukachukuliwa kwa uzito na umuhimu mkubwa na wa kipekee sana,
kwani baada ya uchaguzi mkuu wa kikatiba, wananchi watapata fursa na muda mzuri sana kuandaa katiba yao kwaajili ya mustakabali na uelekeo mpya wa nchi yao Tanzania:pulpTRAVOLTA:
 
si kweli hata kudogo,
huwez kua na IDs zaidi ya tano pekeyako kisha ukaja hapa ukasema ni maoni ya wananchi hali ya kua ni yako mwenyewe......

kama wa kubeba maoni na mitazamo ya wananchi wenye vyama na wasio na vyama, basi ni mimi ambae niko nao bega kwa bega physically and mentally field all the time, japo nipo hapa jukwaani kuona tu nini inaendelea duniani....

nadhani madhara ya hiyo mchezo yalishajitokeza huko nyuma hususan kwenye chaguzi kwamba fulani anakubalika sana, atashinda au ameshinda kumbe field wananchi hata hawamjui wala hawamfahamu :pedroP:
Kwel kila kitu unakijua mkuu hongera sana mheshimiwa.
 
Katiba Mpya inaweza isichukue hata zaidi ya mwezi kupatikana kama kuna dhamira njema!
Kwa kuwa hakuna dhamira njema ya Watawala hata baada ya 2025 hakutawepo na mchakato wa kupata Katiba Mpya!
 
Katiba mpya ni muhimu sana kwa sasa ili tusiendelee na hili giza la sasa. Kama ni lazima aheri tuusukume uchaguzi hata kwa mwaka mmoja au miwili mbele, lakini tusiendelee na mifumo hii ya giza isiyo na tija kwa Taifa.

Ni vema tukapata katiba bora mpya ya wananchi itakayolinda mamlaka ya mwananchi kuliko hii katiba iliyoandakuwa na watawala kwaajili ya kumgandamiza mwananchi.
nadhani ni afadhali tukawa makini sana, watulivu, wastahimilivu na wenye subra kwebye jambo hili muhimu, kuliko kujaribu kuisigina katiba iliyoko kwa nanmna yoyote ile na tukasababisha mgogoro mpya na hasa ukizingatia nchi yetu ni ya siasa za vyama vingi...

chama hiki kitasema sawa, kingine kitasema hapana, mwanaharakati mwingine atajiona bora zaid ya mwingine, atasema aah hivi vyama vingine vidogo vidogo tuvipuuze, wengune watasema aah, hivi vyama vingine ni matawi ya chama tawala.

si hivyo tu, na huenda mahakamani pakawa na kesi za kikatiba lukuki kuliko kipindi kingine chochote huko nyuma Tabzania...

nadhani busara ituelekeze kuvumilia tu,
kisha baada ya uchaguzi mkuu, tuanze kazi hiyoo muhimu sana, ambayo inaweza kuchukua zaidi ya mpaka miaka mi3 :pulpTRAVOLTA:
 
Hata tukianza mwaka 2030.maana Watanzania ukiwasikiliza vizuri huku mitaani shida yao na kiu yao na mahitaji yao wala siyo habari za katiba.watanzania wanahitaji kuona yake afanyayo Rais Samia yanaendelea.mambo hayo ni kama vile uboreshwaji wa huduma za afya,elimu,usambazaji wa maji safi na salama,ajira kwa vijana, upatikanaji wa pembejeo hususani mbolea kwa wakati kwa wakulima pamoja na bei nzuri kwa mazao yao.

Wanasiasa walioshindwa kuwashawishi wananchi kwa hoja ndio wanahisi katiba itawasaidia kupata madaraka ya ubunge na udiwani.

Watanzania wanahitaji sera nzuri na wezeshi pamoja na uhakika wa kupata milo mitatu mezani pao.
 
Wananchi gani wanaaamua hapa? Hapa kwetu viongozi majizi wa ccm ndio wanaamua na kushurutisha wananchi kufuata watakacho. Kama ingekuwa ni wananchi wanaamua, leo hii tungekuwa na katiba mpya kupitia rasimu ya Warioba.
wananchi wazalendo wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania muungwana....

hapo kwenu wap? na huyo warioba ni nani miongoni mwa wananchi wenye nchi yao? si nae ni mwananchi tu kama walivyo wengine...

maamuzi ya wananchi yanafanyika field kwa nanamna mbalimbali ikiwa ni pamoja na kwenye uchaguzi katika box la kura...
ukiweka imani na matumaini yako kwa kujidanganya kwa mihemko na ghadhabu za eti ndio maoni na mitazamo ya wananchi mitandaoni, utapata tabu sana kisaikolojia, field mambo ni tofauti sana gentleman :pulpTRAVOLTA:

nachelea kusisitiza rai yangu kwa waTanzania wenzangu wote wenye mapenzi mema na MAMA TANZANIA..
tuipe fursa na nafasi serikali tebdelee na ikamilishe maandalizi ya chaguzi za kikatiba zilizopo mbele yetu, na baada ya hapo 2026 mchakato wa katiba mpya uanze rasmi:pulpTRAVOLTA:
 
CCM acheni Janja Janja, hakuna cha hadi uchaguzi,2025.. Rasimu ya Warioba ipo tayari ni UAMUZI tu!
nadhani mimi natoa rai na wito wa katiba mpya ya wananchi kuanza mchakato mapema baada ya uchaguzi mkuu...,

hiyo rasimu yako wewe na huyo sijui nani unayemtaja, mnaweza kutafuta namna yenu binafsi mkamalizana wenyewe hukohuko, ila katiba ya wanachi na waTanzania wote nashauri tuitafute kuanzia baada ya uchaguzi mkuu2025:pulpTRAVOLTA:
 
Back
Top Bottom