Black Opal
JF-Expert Member
- Jan 22, 2023
- 233
- 298
Wabari wakuu,
Nimekuja kwenu na swali la kusindikiza 77.
Ikitokea umempa kazi fundi, inaweza kuwa kukujengea kibaraza nyumbani, kukushonea nguo, kutengeneza kabati, kurekebisha gari lako nk halafu fundi akazingua, tuseme kazi ilikuwa ya wiki mbili, siku ya kukabidhi fundi hajafanya chochote, ndio kwanza ameshika kitambaa alipokuona, au lile kabati ulilotaka akutengenezee ndio anakwambia sasa mbao ndio inaenda kutafutwa!
Tuseme ukweli wakuu, kingeeleweka wapo? Ungemuelewa huyo fundi? Kwa watu wenye roho ndogo wanarusha matusi na ngumi juu, na kwa wale wastaarbu kidogo au wenye mili midogo, wanaojua wakirusha ngumi atapigwa, wanachukua hela yao wanaenda kwa fundi mwingine.
Na tena wanakuwa vinara wa kusambaza taarifa kuwa fundi yule hakuna kitu, ni bure kabisa, usithubutu kumpa kazi yako. Fundi yule kama kazi zilikuwa zinamiminika na umaarufu unashuka, asipojirekebisha na kigenge anafunga, anahama kabisa kwenda ambako hajulikani akaanze upya.
Sasa kama tunaweza kuwakomalia mafundi wanaoharibu kazi tunazowapa, kwanini tunashindwa kuwakomalia viongozi tunaowapa dhamana ya kusimamia mali za umma kwa niaba yetu? Mtu anaiba miaka nenda rudi bado tunashupaza shingo kila wakati kuwachangua muda unapofika na kutetea ujinga wanapofanya ubadhirifu kwa kuwa machawa!
Ina maana hatuna uchungu kabisa na Tanzania yetu kiasi hicho? Tanzania ambayo iko moja tu, sio kwamba kuna nyingine kwamba hii ikiharibika basi kuna nyingine tutahamia huko?
Kwanini hatusimami kidete kuhakikisha mafundi hawa wabovu wanaoharibu Tanzania yetu hawapati tena nafasi ya kufanya uharibifu? Kwanini hatuwapi nafasi mafundi wanaofanya kazi kwa weledi, ambao akifanya kitu wewe mwenyewe unajisikia fahari popote unapokuwa?
Karibuni kwa mjadala wakuu.
Nimekuja kwenu na swali la kusindikiza 77.
Ikitokea umempa kazi fundi, inaweza kuwa kukujengea kibaraza nyumbani, kukushonea nguo, kutengeneza kabati, kurekebisha gari lako nk halafu fundi akazingua, tuseme kazi ilikuwa ya wiki mbili, siku ya kukabidhi fundi hajafanya chochote, ndio kwanza ameshika kitambaa alipokuona, au lile kabati ulilotaka akutengenezee ndio anakwambia sasa mbao ndio inaenda kutafutwa!
Tuseme ukweli wakuu, kingeeleweka wapo? Ungemuelewa huyo fundi? Kwa watu wenye roho ndogo wanarusha matusi na ngumi juu, na kwa wale wastaarbu kidogo au wenye mili midogo, wanaojua wakirusha ngumi atapigwa, wanachukua hela yao wanaenda kwa fundi mwingine.
Na tena wanakuwa vinara wa kusambaza taarifa kuwa fundi yule hakuna kitu, ni bure kabisa, usithubutu kumpa kazi yako. Fundi yule kama kazi zilikuwa zinamiminika na umaarufu unashuka, asipojirekebisha na kigenge anafunga, anahama kabisa kwenda ambako hajulikani akaanze upya.
Sasa kama tunaweza kuwakomalia mafundi wanaoharibu kazi tunazowapa, kwanini tunashindwa kuwakomalia viongozi tunaowapa dhamana ya kusimamia mali za umma kwa niaba yetu? Mtu anaiba miaka nenda rudi bado tunashupaza shingo kila wakati kuwachangua muda unapofika na kutetea ujinga wanapofanya ubadhirifu kwa kuwa machawa!
Ina maana hatuna uchungu kabisa na Tanzania yetu kiasi hicho? Tanzania ambayo iko moja tu, sio kwamba kuna nyingine kwamba hii ikiharibika basi kuna nyingine tutahamia huko?
Kwanini hatusimami kidete kuhakikisha mafundi hawa wabovu wanaoharibu Tanzania yetu hawapati tena nafasi ya kufanya uharibifu? Kwanini hatuwapi nafasi mafundi wanaofanya kazi kwa weledi, ambao akifanya kitu wewe mwenyewe unajisikia fahari popote unapokuwa?
Karibuni kwa mjadala wakuu.