Kama tungeuza sana bidhaa nje ya nchi tungepata dola nyingi sana, sarafu yetu ingeimarika kuliko ya Kenya

Kama tungeuza sana bidhaa nje ya nchi tungepata dola nyingi sana, sarafu yetu ingeimarika kuliko ya Kenya

Leo nitaandika kama shairi tu labda nitaeleweka.

Sijasomea uchumi kokote
Nimewaza mwenyewe tu juu ya sarafu yetu
Sarafu yetu inaporomoka.
Hatuuzi nje.
Hatupati dolla nyingi.
Matokeo yake dolla inakosekana sokoni.
Matokeo yake ili tuipate dolla inabidi tutumie shillingi nyingi.
Matokeo yake ya mwisho ni nini?
JIBU: SARAFU YETU INAPOROMOKA JAMANI HADI HURUMA.
Jana Tsh 2580 ilikua ni sawa na DOLLA 1.

What do you expect ndugu zangu.

Ukitoa kitu chako kwa wingi maana yake hakina thamani.

Hakuna balance nzuri kati ya dolla na shilling yetu.
Wew binafs unauza nn nje. ?
 
Uzuri umesema huelewi uchumi, ningekunanga hapa. Sababu ya dollar kuwa 2500+ si hiyo uliyosema. 😂😂😂.
Wewe mzuri kuandika. Ila ningekushauri vipo vitu unatakiwa kujifunza sio kuandika moja kwa moja. Kama lile swala la siku ile kuhusu TAN oil na leo hili la dollar. Jifunze zaidi
Acha maneno matupu weka fact mwenzio hajui sasa mfundishe sio unaleta story …au ndio umemaliza form six au chuo?😂😂😂😂😂
 
Unaposoma maandiko jifunze na kusoma psychology za waandishi usije ukadhani sijui kinachotokea TANOIL niliandika vile makusudi ili nifikishe ujumbe wa kile nilicholenga. Na najua niliandika kwenye sentensi moja kile ulichotaka niandike ila hukukiona.

Hapa nilipo sasa nafanya hiyo biashara ya fedha za kigeni. Fluctuations naiona kila siku sokoni. Lakini pia nafanya biashara ya kuimport. Uchumi najifunzia kwenye biashara sio darasani.

Nikisema thamani ya shillingi inashuka mimi naiona kabisa sokoni ninapo badilisha Tsh kwenda fedha ya kigeni Na sababu naiona hadharani. Sasa wewe subiri BOT wakueleze au waziri wa fedha akueleze.
Hao ndio aina ya watu wanao kariri madaftari!
 
Tulikua hatununui chochote nje
Export ilikuwa kuwa kubwa kuliko awamu yeyote tanzania ...... kulikuwa na viwanda hai vingi vikiwa chini ya serikali ...mwaka 1982 vilianza kuyumba.... sera za ujamaa zikaanza kuyumba pia kutokana na chief financier ambaye alikuwa SOVIET UNION sasa russia kuanza kupata misukosuko ya ndani ....tukaanza kukosa pesa za kufinance viwanda vya kijamaa

China wakati huo alikuwa nae anatusapoti ila nae akaingia kwenye mabadiliko makubwa mwaka huo huo kwenda mixed economy

So jibu kubwa ni Export ilikuwa kubwa kuliko import
 
Export ilikuwa kuwa kubwa kuliko awamu yeyote tanzania ...... kulikuwa na viwanda hai vingi vikiwa chini ya serikali ...mwaka 1982 vilianza kuyumba.... sera za ujamaa zikaanza kuyumba pia kutokana na chief financier ambaye alikuwa SOVIET UNION sasa russia kuanza kupata misukosuko ya ndani ....tukaanza kukosa pesa za kufinance viwanda vya kijamaa

China wakati huo alikuwa nae anatusapoti ila nae akaingia kwenye mabadiliko makubwa mwaka huo huo kwenda mixed economy

So jibu kubwa ni Export ilikuwa kubwa kuliko import
Safi sana mkuu kila kitu kipo wazi. Ukweli lazima usemwe. Wewe huwezi ukawa mtu wa shopping tu hata kwenye familia lazima uchumi wako uyumbe tu. Fanya shopping wakati huohuo zalisha nawewe uza. Lakini ni vizuri zaidi uuze kuliko kununua.
 
Back
Top Bottom