Kama ulishawahi kunywa chai ya kuunguza Sukari tukutane hapa

Kama ulishawahi kunywa chai ya kuunguza Sukari tukutane hapa

Kwa wale wenzangu na mimi tuliowahi kunywa chai ya kuunguza sukari kama majani ya chai tukutane hapa.

Chai ile ilikuwa inatengenezwa kwa kuchukua Sukari unaiweka kwenye sufuria iliyopo motoni baada ya hapo sukari itayeyuka na kuungua kidogo alafu unachukua maji unaweka basi kitu kinakuwa Cheusi kama umeweka majani ya chai na ilikuwa tamu tu.

Kama ulishawahi kunywa hiyo chai kweli udogoni mwako au ata sasa hivi basi utakuwa umepitia maisha halisi ya mtanzania.



Tuambie hapa kama wewe ulishawahi kuinywa na inakukumbusha wapi kipindi hicho.!?

.
Mpaka sukari guru niliisha kunywa chai yake mkuu.
 
hiyo sometimes ukibugi unaharibu sufuria ipo ile unachukua karatasi ((gazet n.k sio nylon) unafunga sukari then unachoma ikishaanza kuungua kama inatoa povu hivi inwekwa kwenye maji ya moto... Ila harufu yake ndio ya kipuuzi kweli yaan ila hamna namna ilibidi iwe ili life lisonge
 
Chai sio rangi.
Chai ni majani ya chai.
Ukiunguza sukari unapata rangi inayofanana na ile inayopatikana ukiweka majan ya chai, basi tunajidanganya ni chai!

Aisee kama uliwah kunywa chai ya kuunguza sukari wewe ni MUHENGA !
Chai ni rangi, mimi nyumbani tulishasahau hata bei ya majani. Unaweka mchaichai, hiliki, unaponda karafuu, tangawizi. Unapata chai maridadi kabisa.
 
Ndio, ilikuwa sukari inaunguzwa inapatikana chai maridadi sana
kisha unapaka sabuni mwilini yaani mbadala wa mafuta
safari ya shule inaanza. Mimi mara moja moja huwa nafanya mpaka leo
Duh! Unakumbushia mhenga!
 
Harufu yake aaargh, huwa sio nzuri...mi nilikuwa naikata kwa kutilia limao. Enzi za chuo.
 
Nilikua natafuta uzi wa green tea nikakutana na huu. Dah. Haya maisha haya ngoja nikae tu kimya.
 
Nkikumbuka hayo maisha sometime huwa machozi yanantoka tu.
Juzi kati majani ya chai yalikuwa yameisha ofisini kwetu so nkawaambia wale wafanyakaz wenzangu masista duu "chomeni sukari fasta tupate chai njaa znatuuma" huwezi amini hawajui kitu kuhusu hii sayansi....
Mama zetu walifanya kazi sana.

Ilikua ikikosekana sukari ya kuchoma basi utanywewa uji wa chumvi mradi siku ipite na mkono uende kinywani [emoji848][emoji3526][emoji3526][emoji17][emoji17]. Tulikotoka ni mbali sana, Mungu katuvusha katika mengi
 
Back
Top Bottom