Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Chukua weed (bangi) Choma humo ndani
Usemacho ckupingi Mimi mwenyewe hapa kuna uchawi nimefanyiwa sijui nimetupiwa jini sielewi
Nakumbuka kuna Banda niliwahi kupanga uswahilini, basi katka Ile nyumba nilikua naishi na mama wa kiha ambaye alikua na watoto watatu

Asa cjui kitu gani nilichomkosea Yule mama nakuanza kunitesa nakumbuka kuna siku mjuu wake aliingia ndani kwangu na sikua na mazoa na Yule mtoto basi alipokua mle ndani akaanza kuchezea vitu mara anachukua sabuni anamwaga, bodysray anairusha juu , mafuta anayamwaga nukimkataza anakua mkali kweli mwishiwe nikamuita mama yake akaja kumchukua

Cku nyingine aliingia ndani na kupanda kitandani kwangu then akawa anatambaa kama nyoka pale kitandani kwangu na akawa amekakamaa sana

Basi siku zilivyenda nikawa nikilala pale kitandani naota mambo ya ajabu sana haitoshi kuna kitu nakihisi kinatambaa nikikiangalia sikioni

Ikafika kipindi nikilala pale kitandani mchana naongea peke yangu yaani yanajirudia matukio kibao ambayo niliyasahau na nakua na hasira sana yakutaka kwenda kulipiza kisasi

Inshort mpaka muda huu hilo tatizo linanisumbua mkuu nashindwa nilitatue VP cjui.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shetani na mawakala zake wana operate kwenye ulimwengu wa giza / Roho ambao sisi binadam wa kawaida hatuna uwezo huo . Na shetani ni mjanja na ana akili sana .

Kama umeamua kupambana na shetani , hakikisha una imani dhabiti iliyonyooka, don’t understimate the devil [emoji49]. Usifikiri unaweza kumchallenge shetani kipumbavu, remember shetani Ana uwezo wa kiungu, Ana Uwezo kama Mungu .

Inshort Shetani pia ni mungu, ingawa kazi zake nyingi ni uharibifu, lakin Shetani pia kuna mambo mengi tu mazuri anayafanya kama Mungu , kuponya watu , kuwapa watu utajiri na Mali , shetani Ana uwezo wa kufanya yale Mungu anayoyafanya so wewe binadamu wa kawaida usifikiri unaweza kupambana nae au kum oppose kirahis kama wengi wanavyofikiria.

If you can’t fight them , join them .

Mimi sio mpinga kristo , na wala sina nia ya kuingiza watu kuzimu,

the truth is , the best coffee is always DARK and BITTER .

Hata hao wachungaji mnaokimbilia kuombewa na kuponywa na kuchukua miujiza, wanaenda kuchukua nguvu kwa Mkuu wa ulimwengu huu ( lucifer)

Tena wanaenda kujinadi kabisa kanisan na kulitaja jina la Yesu bila aibu yeyote , na kupitia hilo hilo jina, watu wanaponywa. That’s how the devil operates .


Warumi




Sent from my iPhone using JamiiForums
Duuh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeajiriwa lakin mambo yangu hayaendi mpaka Leo, unakopa mkopo wanakukata alafu inafikia kipindi unaambiwa makato hayaendi benk husika, unarudi nyumbani migogoro isiyoisha yaan n tabu tu, nishasema nikija kumfaham mbaya wangu ntamfanyia mbaya sana

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna watu wanajua kutesa binadamu wenzao, halafu unakuta wengine wamekuzidi kila kitu , ila hawataki kabisa mambo yako yawe mazuri, Sijui hyu uchawi wa aina gan


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Usemacho ckupingi Mimi mwenyewe hapa kuna uchawi nimefanyiwa sijui nimetupiwa jini sielewi
Nakumbuka kuna Banda niliwahi kupanga uswahilini, basi katka Ile nyumba nilikua naishi na mama wa kiha ambaye alikua na watoto watatu

Asa cjui kitu gani nilichomkosea Yule mama nakuanza kunitesa nakumbuka kuna siku mjuu wake aliingia ndani kwangu na sikua na mazoa na Yule mtoto basi alipokua mle ndani akaanza kuchezea vitu mara anachukua sabuni anamwaga, bodysray anairusha juu , mafuta anayamwaga nukimkataza anakua mkali kweli mwishiwe nikamuita mama yake akaja kumchukua

Cku nyingine aliingia ndani na kupanda kitandani kwangu then akawa anatambaa kama nyoka pale kitandani kwangu na akawa amekakamaa sana

Basi siku zilivyenda nikawa nikilala pale kitandani naota mambo ya ajabu sana haitoshi kuna kitu nakihisi kinatambaa nikikiangalia sikioni

Ikafika kipindi nikilala pale kitandani mchana naongea peke yangu yaani yanajirudia matukio kibao ambayo niliyasahau na nakua na hasira sana yakutaka kwenda kulipiza kisasi

Inshort mpaka muda huu hilo tatizo linanisumbua mkuu nashindwa nilitatue VP cjui.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli, ukiwa na imani Kali sana , na usiwe na dhambi , ila ushirikina una nguvu sana

Usichukulie poa nguvu za giza , Mimi nimejionea nyie mnasikia tu kwa watu[emoji16]


Sent from my iPhone using JamiiForums
Ndoto za ajabu naota mara chache sana kwa mwaka.
Wiki iliyopita niliota ndoto ya ajabu sana! Niliota nipo kwenye hekalu la kuabudu, ndani ya hilo hekalu walikuwemo watu wawili tu mimi ni watatu wao. Mmoja amesimama kwa mbali na mwili wake una mawimbi mawimbi. Mwengine alikuwepo karibu yangu.
Aliye karibu yangu alikuwa ananikaribia pembeni yake kulikuwa na kivuli kizito na chenye umbile tofauti na la kwake. Akakivua kile kivuli kwenye mwili wake kama mtu anavyovua nguo halafu akielekezea kije kwangu.

Kile kivuli kilinivaa mwili mzima! Mwili wangu niliusikia tofauti ya mwili wote ambao sikuwahi kuusikia. Halafu kikawa kinanivaa kuniingia mwilini huku nahisi maumivu, na kikanivaa mwili mzima!

Licha ya mapungufu yangu mengi ila najifahamu na Mungu ndiye anayejua zaidi. Mtume anasema Uislam una twariqah 360, yeyote atakayepita moja ya hizo twariqah yupo salama. Mi ni sunni, ni mtu wa twariqah! Nafuata twariqah ya Sheikh Abdul Qadir Al Jeilan. Ambayo hiyo twariqah ni moja ya 360. Huyu Abdul Qadir Al Jeilan ni kiongozi wa Mawalii(sage) wote. Atakayeifuata twariqah yake aliyeipitia yeye (twariqah ni njia) anasema ukiwa na shida uwe magharibi au mashriki ya Dunia au Kas au Kus ukimuita kwa kutaja jina lake tu atakusaidia.

Kwenye hiyo ndoto nikalikumbuka jina lake. Nikalitaja jina lake kama alivyosema atakusaidia, kilichotokea nikashindwa kutamka jina nikawa kama mwenye kigugumizi. Huku kivuli kikawa kimenivaa, mwili unaniuma nikawa nachoka nakihisi kabisa kinaingia mwilini. Nikataja jina lake kwa kumaanisha, sauti mdomoni hainitoki nikamtaja kwa moyo. Kile kivuli kikaanza kunitoka.

Maumivu ambayo niliyasikia yaliniumiza. Navuliwa kitu ambacho kinaniumiza ni kizito lakini ni kile kivuli kilichonivaa! Kilinitoka chote mwilini nikawa nahisi maumivu na nikawa nahema sana ila bado nipo kwenye ndoto. Aliyenitupia hicho kivuli kumuangalia yupo nje ya hekalu amesimama huku ananingalia. Lakini kile kivuli kilichonitoka kikawa kipo mbele yangu kimesimama kikamfuata aliyenitupia. Yule mwengine ambaye mwili wake una mawimbi mawimbi mda wote alikuwa amesimama tu! Kisha akawa ni mwenye kuondoka. Lakini bado mimi nilikuwa nahema sana huku nimeinama chini. Kwa ghafla akasimama na akanifuata huku akiniangalia.

Nikashtuka kutoka usingizini mwili ukawa unauma. Nikawa na wasiwasi nililala vibaya kuhusu haya maumivu ya mwili ama laa!
 
Uzuri uliishinda vita
Ndoto za ajabu naota mara chache sana kwa mwaka.
Wiki iliyopita niliota ndoto ya ajabu sana! Niliota nipo kwenye hekalu la kuabudu, ndani ya hilo hekalu walikuwemo watu wawili tu mimi ni watatu wao. Mmoja amesimama kwa mbali na mwili wake una mawimbi mawimbi. Mwengine alikuwepo karibu yangu.
Aliye karibu yangu alikuwa ananikaribia pembeni yake kulikuwa na kivuli kizito na chenye umbile tofauti na la kwake. Akakivua kile kivuli kwenye mwili wake kama mtu anavyovua nguo halafu akielekezea kije kwangu.

Kile kivuli kilinivaa mwili mzima! Mwili wangu niliusikia tofauti ya mwili wote ambao sikuwahi kuusikia. Halafu kikawa kinanivaa kuniingia mwilini huku nahisi maumivu, na kikanivaa mwili mzima!

Licha ya mapungufu yangu mengi ila najifahamu na Mungu ndiye anayejua zaidi. Mtume anasema Uislam una twariqah 360, yeyote atakayepita moja ya hizo twariqah yupo salama. Mi ni sunni, ni mtu wa twariqah! Nafuata twariqah ya Sheikh Abdul Qadir Al Jeilan. Ambayo hiyo twariqah ni moja ya 360. Huyu Abdul Qadir Al Jeilan ni kiongozi wa Mawalii(sage) wote. Atakayeifuata twariqah yake aliyeipitia yeye (twariqah ni njia) anasema ukiwa na shida uwe magharibi au mashriki ya Dunia au Kas au Kus ukimuita kwa kutaja jina lake tu atakusaidia.

Kwenye hiyo ndoto nikalikumbuka jina lake. Nikalitaja jina lake kama alivyosema atakusaidia, kilichotokea nikashindwa kutamka jina nikawa kama mwenye kigugumizi. Huku kivuli kikawa kimenivaa, mwili unaniuma nikawa nachoka nakihisi kabisa kinaingia mwilini. Nikataja jina lake kwa kumaanisha, sauti mdomoni hainitoki nikamtaja kwa moyo. Kile kivuli kikaanza kunitoka.

Maumivu ambayo niliyasikia yaliniumiza. Navuliwa kitu ambacho kinaniumiza ni kizito lakini ni kile kivuli kilichonivaa! Kilinitoka chote mwilini nikawa nahisi maumivu na nikawa nahema sana ila bado nipo kwenye ndoto. Aliyenitupia hicho kivuli kumuangalia yupo nje ya hekalu amesimama huku ananingalia. Lakini kile kivuli kilichonitoka kikawa kipo mbele yangu kimesimama kikamfuata aliyenitupia. Yule mwengine ambaye mwili wake una mawimbi mawimbi mda wote alikuwa amesimama tu! Kisha akawa ni mwenye kuondoka. Lakini bado mimi nilikuwa nahema sana huku nimeinama chini. Kwa ghafla akasimama na akanifuata huku akiniangalia.

Nikashtuka kutoka usingizini mwili ukawa unauma. Nikawa na wasiwasi nililala vibaya kuhusu haya maumivu ya mwili ama laa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waganga wanatumia details kama nguo za ndan , kucha, nywele, majina kamili na wengine hupiga ramli na kupata info zote za kitu au mtu anayemtaka.

Miaka kadhaa iliyopita niliwahi kwenda Tanga kwa mara ya kwanza kufanya ushirikina, nilienda tu kwa kuwa Rafiki yangu alishaenda pia akafanikiwa mambo yake.

Kutokana na tatizo langu kuwa kubwa kiasi , mganga aliniambia natakiwa kufanya kafara ya mbuzi , Bahati nzuri nilikua na vijisenti, nitatoa kafara , nikafanyiwa visomo pamoja na mambo mengine mengi ya kishirikina

Kwa kweli nilikua Naona mambo ya ajabu kwa kuwa ushirikina nilikua nauona kwenye movie tu .

Basi baada ya kutoka Tanga nikarudi home , ndan Ya siku Tatu tu , haja yangu ile ile niliyoitaka ikaja kwa njia ya ajabu mno, nakumbuka usiku wa ile siku sikulala kabisa , nikawa nawaza kumbe uchawi upo ?

Basi toka miaka hiyo had leo maisha yangu ni ushirikina tu na sijawahi kujuta kwa kweli wala kutapeliwa, labda kwa kuwa mtu aliyenipeleka huko ni mshirikina sana na ameenda sehem nyingi so anajua mganga yupi mzuri.

Ila kitu kimoja ukishaingia kwenye ulimwengu wa giza, roho ya kibinadamu inakutoka, mtu akikuudhi kidogo tu unaweza hat kumdhuru au kumtoa roho kwa ushirikina

Ogopa sana kugombana na watu hovyo, wengine wana nguvu za kiroho , unajikuta unagombana nao, wao wanaenda kukumaliza kwenye ulimwengu wa roho , tena hawakuumizi wala nini, wanakuacha uishi ila kwenye ulimwengu wa roho wameshakuua, hat ufanye nini huwez kufanikiwa.





Sent from my iPhone using JamiiForums
[emoji849][emoji849][emoji849] hii noma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kutokana na hii Hali. Napenda kujua mchawi na mganga.je ni halali kwenda kwa mganga sababu unahisi mauzauza au kuchzewa kichawi?na je ni uchawi kweli unaweza kumfanya mtu awe chizi?tusaidiane kwa hili kwani sikuwa napenda kuamini kuwa ushirikina upo. Pili waubiri wengi wa Sasa hutupelekea kuamini uchawi upo na kulogwa kupo

Sent using Jamii Forums mobile app
Haya mambo ni masuala ya imani tena imani inayohusisha mtu mmoja mmoja. Na huwezi jua undani kama hayajakukuta.
Mchawi na baadhi ya waganga wanashirikiana. Kuna waganga hula rushwa kwa wachawi ili waachiwe mtu wanaemtaka,lakini pia wapo waganga wanaosaidia na wanakuwa kweli wamejaaliwa karama hiyo na wanakuwa hawali rushwa.
Si lazima kwenda kwa mganga kwa kuwa tuu unahisi mauzauza, unaweza zungumza na Mungu kwa njia ya sala tuu a ukapata uponyaji japo hapa inategemeana saana na imani yako iko kiwango gani. Hata kwa waganga pia haswa wale wanaotu miti kutibu.
Uchawi ama mchawi anaweza kukufanya ama kukutupia baya lolote analoweza kukunuia ww, binafsi almanusura niwe kichaa yaani nilikuwa hatua za mwisho kabisaa dah sitasahau maishani mwangu natembea kwa mguu mbezi kariakoo nenda irudi.
Wahubiri wengi wa kisasa hawakosei kuhusu wachawi kwani hata vitabu vitakatifu vimeeleza wazi kuhusu hili ila wameenda mbali zaidi wanatumia kujinufaisha na hapo ndipo wanapokosea sasa.
 
Haya mambo ni masuala ya imani tena imani inayohusisha mtu mmoja mmoja. Na huwezi jua undani kama hayajakukuta.
Mchawi na baadhi ya waganga wanashirikiana. Kuna waganga hula rushwa kwa wachawi ili waachiwe mtu wanaemtaka,lakini pia wapo waganga wanaosaidia na wanakuwa kweli wamejaaliwa karama hiyo na wanakuwa hawali rushwa.
Si lazima kwenda kwa mganga kwa kuwa tuu unahisi mauzauza, unaweza zungumza na Mungu kwa njia ya sala tuu a ukapata uponyaji japo hapa inategemeana saana na imani yako iko kiwango gani. Hata kwa waganga pia haswa wale wanaotu miti kutibu.
Uchawi ama mchawi anaweza kukufanya ama kukutupia baya lolote analoweza kukunuia ww, binafsi almanusura niwe kichaa yaani nilikuwa hatua za mwisho kabisaa dah sitasahau maishani mwangu natembea kwa mguu mbezi kariakoo nenda irudi.
Wahubiri wengi wa kisasa hawakosei kuhusu wachawi kwani hata vitabu vitakatifu vimeeleza wazi kuhusu hili ila wameenda mbali zaidi wanatumia kujinufaisha na hapo ndipo wanapokosea sasa.
Duuh mkuu pole sana na ahsante kwa ufafanuzi pia uliponaje huo uchizi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom