Yule mwamba jooohs akisimulia lazima ucheke anajua kupangilia sana visa na mikasa 😁Dadeki. Ahh apaaa mtuu unawaza bora mngewachia majambazi wale maisha tu coz madhara ni makubwa kuliko faida. Ilaaa ao maskari wameniacha hoi.
Akhakha polisi walipatikana makofi Mpaka wamepoteanaa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mngewauwa polisi WA watu haha.
Hii storii angeisimulia jooow mzee waa ooooky inaendeleaaa nafikirii mbavu zngepasuka maana si kwa usimuliaji ule.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nilirudi na kuungana na familia huku tumeshaanza kutawaliwa na hali ya hofu lakini haikuwa hofu kubwa sana sababu naweza kukiri kwenda kwa mganga ile ndo ilikuwa mara yetu ya kwanza toka nizaliwe hivyo tulikwenda lakini hatukua tunaamini sana kwenye uwepo wa uchawi japo kwa sasa kidogo tulikuwa tumeanza kuingiwa na imani kuwa mambo tuliyoyasikia kwa yaliyowapata wenzetu wakiotufanyia ule ushenzi sasa na sisi tutayapata soon kivitendo.
Tulikaa macho mpaka usiku wa saa 5 tukiwa tunasoma sana dua mpka tunalia kabisa, then kila mmoja akaingia kwake kulala,naweza kusema kuwa lile dude ni kama lilikuwa linatusikiliza tumalize kuomba dua then tukiingia ndani lianze kazi yake, ile tumejifunika tu shuka tukasikia kishindo kikubwa mno juu ya bati.
Hakuna aliyeongea zaidi ya kila mtu kujifunika shuka yake zaidi palikuwa kimya,basi kishindo kilidumu zaidi ya masaa matatu mazima then ikafata sauti ya ngombe kupika kelele ndani ya dakika tano tu tukasikia kimya.mpka asubuhi ilivyofika asubuhi tukatoka nje,tukakuta uwani kote kumejaa nyama tupu za ngombe hakukuwa na ngombe hata mmoja mzima kati ya wale waliobakia,nyumba yetu ilikuwa ina fens hvyo ile kufungua tu geti,tukakuta majirani kibao wako getini wanauliza kulikoni.
Hapa nikiri mzee alijaribu kuficha akasema tu kuwa mtaani kuna mtu anamfanyia husuda na anamfanyia ushenzi ote huo mzee alilalamika sana,kisha majirani wakatusaidia kusafisha pale uani zile damu pamoja na zika zile nyama wakati huo pia polisi walikuja wakachukua vielelezo,na tukaenda polisi pia kutoa taarifa,wakasema watafatilia huyo mshenzi aliofanya huo ushenzi na ndani ya saa 48 watakuwa walishampata.
Mzee alirejea jioni kutoka polisi akalakiwa na majirani na pole kutoka kila sehemu,ulivyofika usiku hatukuwa hata na hamu ya kula ulinunuliwa tu mkate na chai lakini hata nusu haikufika,naweza kusema mungu tulimsahau maana hakuna aliyeomba dua tena ote tulilala barazani,
mzee alivyotoka polisi mda ule mkuu wa kituo alioanga team yake bila kumwambia mzee kuwa watafanya kitu gani,basi aliteua askari wake watano ilivyofika usiku wa saa tano wakaja mpka nyumbani na gari yao wakawa umbali kama wa mita 10 au 20 wanaiangalia nyumba yetu kwa mbali huku wengine wanaizunguka kwa mbali,sasa wakiwa wanaizunguka wakamuona mtu mweusi tiii,anakimbia juu ya bati kuanzia mwanzo wa bati mpka mwisho wa bati akiwa juu,
walivyomuona wale wa kwenye gari wakachukua silaha zao then kwa pamoja wakazunguka nyumba kumuwinda,baada ya muda wakawa wanaskia kuku kama vile wanachinjwa wao target yao kubwa ilikuwa wanasubiria atoke tu nje ya geti wamkamate mchezo uishie hapo,na kweli baada ya mda aliruka ukuta,ile anatua tu chini wakamuweka chini ya ulinzi lakini mdomoni alikuwa na damu nyingi sana ya kuku aliofyonza damu,lakini hakusimama akawa anakimbia wakapiga risasi moja juu lakini hakusimama kuna askari mwengine alisogea na yeye akampiga ya mgongo,baada ya kupigwa ya mgongo aligeuka na kuwarudia kwa uoga wakawa wanapiga risasi nyingine nyingi lakini linawafata tu,askari mmoja alipigwa kofi kali sana mpka akazimia,yule wa pili aliyekuwa anakuja akampiga risasi mgongoni akawa anakimbilia gari kule walipo wenzake,walivyomuona anakuja wakawasha gari na lenyewe likarukia ile gari na kuanza kuwachapa makofi walipiga sana risasi kulipiga na nyingine kwenda hovyo kwa hasira lilitoboa toboa mpka mataili ya magari kisha likapotelea kwenye shamba lililokuwa mbele yetu,
Wakati yote yanatokea sisi tulikuwa tuko barazani,tulivyosikia kelele za juu ya bati tulijua ni lile dubwana na hata tulivyokuwa tunasikia kelele za kuku tukawa tunaelewa nini kinaendelea lakini tuliingiwa na butwaa zaidi baada ya kusikia risasi maana ilikuwa ni kitu kigeni na kwa wakati huo ilikuwa ukisikia basi unajua ni majambazi ambao walikjwaga wengi ni majambazi kutoka burundi,
Ghafla tukawa tunasikia tunagongewa hodi na majirani ambao kwa sauti tuliwajua,ile tumetoka nje tukakuta geti limetobolewa tobolewa na risasi mbele tunaiona difenda ya polisi imegonga mti wa umeme,lakini tyre zikiwa zimechanwa chanwa,ndani walikuwepo polisi wawili hawana fahamu lakini wanatoka damu,na mbele kuna mwengine amelala chini lakini mguu umeparuliwa tukamsikia mwengine nyuma ya ukuta ndo anazinduka lakini kama amechanganyikiwa.
mzee alitoka haraka akawasha gari akawapakia tukaingia mimi broo na wale askari gari ikawashwa wakati huo tunawakimbiza hospitali kuna askari mmoja hakuonekana kati ya wale watano,hivyo wale majeruhi wakaomba wananchi wamtafute mwenzao na pia wakatoe taarifa kituoni kule ujiji sisi hao tukawasha gari tukaondoka
Tumetembea na gari mpka sehemu moja inaitwa buzeba zeba kwa mbele kuna sehemu moja inaitwa bimala kuna bohari kubwa ya dawa ya msd sijui kama ipo mpka leo kwa mbele kuna mwembe mkubwa kwa mbele tukamuona nyoka mrefu sana anavuka bara bara ikabidi mzee asimamishe gari apite cha ajabu yule nyoka alivyotuona alisimama kichwa kikiwa kwenye kichaka,yule askari ambaye ndo alikuwa mzima aliyekuwa amezimia akawa anabishana na mzee,mzee anataka kumsubiri mpka apite yeye anataka mzee amkanyage
mwisho wa ubishi mzee akamwachia sterlimg aendeshe yeye basi akawasha tena gari akairudisha nyuma then akatoka spidi kali mno akamkanyaga yule nyoka,tuliona nyuma baada ya kumkanyaga kama aliruka juu kisha kwa mbali tukaona kama kwenye lami kwa pembeni kwenye majani kama kuna kitu kinatukimbiza kwa kasi mno lakini kwa spidi tuliyokuwa nayo hatukujali sana ila tuliskia tu gari kama imegonga kama tuseme jiwe then ikawa sawa,
baada kama ya dakika tano tukawa tumefika hospitali ya maweni wagonjwa wakashushwa,wakaenda kutibiwa,baada ya mda mkuu wa kituo akawa alishafika pale na baadhi ya askari sasa yule askari ambae alikuwa anaendesha gari yetu akaomba funguo ili achukue radio call yake mzee akampa funguo,alivyofika ile anafungua tu mlango tukasikia ukelel mkali mno mamaaa nyokaaaa,kufika pale tunakuta ndo nyoka analallizia mkia porini, tukamfunga kitambaa lile eneo tukamuwahisha haraka hospitali.
kuona hivyo mkuu wa kituo akapaniki akawa anamfata mzee amwelezee kulikoni wakati huo mzee alikuwa kama amedata fulani,basi gari zikawashwa mpka nyumbani tulivyofika pale tulikuta askari wengine ambao walifika mda mrefu,mkuu wa kituo alivyofika pale akawa anaendelea kuulizia askari wake mmoja kama alishapatikana ninachokumbuka alipatikana na wala hakuwa mbali na pale bali alikuwa ameingia kwenye shimo la taka akiwa amejifunika na gunia la mkaa juu akiwa na silaha yake mkononi,na aliyegundua yumo mle ni mzee jirani yetu ndo alienda kumwaga maji ya kahawa sasa kwenye kumwaga akaona kiatu kukivuta hivi akashangaa kuna mtu ndo akampliz na kumtoa presha akaja nae mpka pale nyumbani ambapi mtaa mzima ulihamia hapo.
Baada ya kupatikana ndo akaingizwa ndani na baadhi ya wazee pamoja na askari wengine akaelezea mwanzo mpka mwisho walichokutana nacho,hapo mzee nae akaelezea mwanzo mwsho wakafikia muafaka baba na sisi ote pamoja na baadhi ya wazee twende kwa mzee juma njemba japo alikuwa hayupo lakini walikuwa wanataka kuongea na mkewe
Tukafika tukamkuta yule mama anatwanga unga wa muhogo kwenye kinu,hapa nikiri wazi yule mama na familia yake walikuwa wanaishi maisha duni mno lakini walikuwa wanaheshimiwa mno nasema mno nimiwa namaanisha hata askari walivyoingia mle ndani walikuwa wanamsalimia yani mpka ile adabu unaona hii sasa huyu anaweza kupiga hata magoti,tulikaribishwa vizuri.
mama yule aliwaeleza kosa tulilolifanya na mtihani wa mzee kwenda DRC,kumtibu kuna mteja wake,lakini kuna kauli ambayo aliitoa kuwa kama dubwana hilo halijarudishwa/kudhibitiwa basi litatuua sisi sote na likitumaliza sisi litahama kwa yoyote maana chakula chake ni damu
basi baada ya kile kikao ikaamuliwa kuwa siku hiyo hiyo familia nzima twende huko huko congo nakumbuka kulikuwa kunaitwa kalemi wenyeji mtanisahihisha na kwenda ilikuwa ni kwa njia ya boti na mwenyeji ambae ilibidi atupeleke alikuwa ni mjukuu wa mganga maana ndo alikuwa anakujua kipindi hicho nakumbuka simu zilimuwa siyo sana na barua pia zilikuwa zinatumika,na safari tuliianza ote nakumbuka tulipewa askari wawili wenye silaha na hatukuwa na pasport wala chochote zaidi tu ya barua kutoka polisi
naomba niweke nukta hapa then ntamalizia baadae hasa kwenye kunusurika kutekwa na majambazi ya burundi na kuponene a chupu chupu kuliwa nyama na jinsi tulivyolimaliza lile dubwana
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa sisi wakuria huwa tunaenda kimya kununua sime jipya,au shoka kisha unaandika kimemo au kiujumbe maskani "mimi ni mwanaume,siwezi kuishi kwa hofu kama panya,teknolojia yao imenishinda natumia yetu".Kesho Magazetini Mwl Mwita Waitara Nyaronyo anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kumtenganisha kichwa na kiwiliwili jirani yake[emoji2][emoji23].NA HATUTAACHA SIME/SHOKA TECHNOLOGY KAMA MAMBO YENYEWE NDIO HAYO[emoji34]
Hii picha ni mama mmoja huko sengerema maeneo ya Kome kisiwani,nyumbani kwa Mh.Charles Tizeba,mama huyu alikuwa ni mshirikina,siku ya tukio mama aliondoka na kumwacha mmewe akiwa amelala ,bahati mbaya alienda kufanya shiriki kwenye mji uliokuwa umezindikwa hivyo alifia kwenye huo mji,
Huku nyumbani Mme wake hakuwa na taarifa ,aliendelea kuuchapa usingizi hadi saa mbili asubuhi alipoamshwa na kelele za wanazengo wakimjulisha kuwa mke wake kakamwa Sehemu na huenda anekufa
Chakushangaza ,yeye usiku wote alijua kuwa kalala na mkewe,wana nzengo wakati wanamwasha Mme wa mama huyo walishangaa kuona fisi anatoka na kukimbia,na kumwacha jamaa akishangaa,maana yeye alijua kuwa kalala na mtuView attachment 1418350
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu yangu mtu anakutumia dude kama hilo linaua ng'ombe,haliogopi risasi😃...mpaka askari anajificha jalalani na bunduki heheheheh huyo sio wa kucheka nae aisee
Stori matata sana. Tatizo mkuu unachukua miezi kuja kuendeleza kisa.wengi walinitafuta na kutaka kuwaelezea ni kipi hasa kilitokea hasa baada ya kupata vitu vyetu na wapo walonibeza mpka nikafikia hatua ya kuwaonyesha evidence. Mtanisamehe kwa kuwa siyo mzuri sana kwenye uandishi
NAMALIZIA,
Nakumbuka baada ya kuchukua vitu vyetu vyote pale polisi na vingine vilikuwa siyo vyetu but tulipewa vyote na nahisi polisi walitupa vile sababu,baada ya kupata vile vitu vyetu pamoja na zile fedha kuna baadhi walitaka kuchukua lakini kuna mambo yalitokea hivyo wakaone vile vitu vilikuwa siyo vya kawaida hivyo walitupigia sana simu nakumbuka simu ilikuwa inapigwa kila baada ya dakika tano,na la mwisho nakumbuka hata ticket ya treni hatukukata bali tulipanda treni bure second class(ni chumba ndani ya behewa mnakaa na kunakuwa na vitanda)
Nakumbuka tuliingia jioni ilikuwa mida ya saa jioni nakumbuka wakati huo kupata ticket ilikuwa ni ngumu mno,tulivyofika tu Stesheni tukapokelewa na polisi kisha msafara ukaanza mpka polisi ambapo tukakutana na mkuu wa pale nakumbuka tulikuta vitu vingi sana lakini tulichoambiwa ni chukueni kila kilicho chenu, tulikuta mpka hizo fedha tukasema zetu wakatupa bila kuuliza na kingine cha ajabu siku ya pili asubuhi tukapewa escort na polisi gari mbili moja mbele moja nyuma mpka tunaingia kigoma mjini.
wakati tupo njiani mzee alijaribu kumuuliza askari mmoja tuliyekuwa nae ndani ya gari inakuwaje mbona mnatufanyia yote haya haliyakuwa mlipaswa kutukabidhi na kutuacha tuondoke? jamaa ndo akatoa mkasa mzima.
kuwa siku moja baada ya lile tukio kutokea walipata simu,kuwa kuna watu wanaohisiwa majambazi wameuliwa na wanyama,kila mtu akawa anasema la kwake wengine simba,wengine chui,basi baada ya kupata hyo case wakaamua wawapigie watu wa maliasili ili waende kwa pamoja lakini cha ajabu ni kwamba baada ya kufika eneo la tukio,wakakuta miili imetapakaa sehemu yote ya porini mingine ikiwa haina mikono, miguu nk,lakini kitu cha ajabu waliwakuta wakiwa na silaha zaidi ya 15,lakini haikutumika silaha risasi hata moja.
wale majambazi pale lilipotokea tukio lile kulikuwa jirani kabisa na kambi yao ambapo ndipo walipokuwa wanaficha mali zote baada ya kuibia watu kwenye mabasi hvyo mali zilikuwa za kutosha pale hivyo ilikuwa unaweza kichukulia hvyo unaweza kupata picha kama binadam unaweza kufanya nini?
basi kuna baadhi wali...............,sasa kuna mambo yaliwatokea mazito sitapenda kuyasema kwaiyo kilichotokea ili usalama na uzima uwepo ilibidi wenyewe tukabidhiwe mizigo yetu yote na sharti la mwsho ni kwamba ni lazma tufikishwe kigoma mjini salama la sivyo .............,
Tulivyokifka kigoma ujiji ile gari ya mbele ilisimama nakumbuka ni zile difenda 110 nyeupe akashuka askari na wengine ote wakashuka kisha akatuambia jamani sisi safari yetu ndo imeishia hapa muende salama tukaagana pale lakini walikuwa wanatushangaa sana na hofu za wazi wazi na sisi tuliliona hilo sababu tulikuwa tumeshaambiwa nini kilichotokea.
Tukawasha gari mpka sokoni ambapo tulinunua mbuzi mzuri pamoja na zawadi zingine baba akasema lazima kituo cha kwanza twende kwa mzee juma njemba kumpa zawadi zake na shukrani zake,tulivyofika tukamkuta ameenda sokoni basi alivyofika akatuambia kuwa kila mlichopewa ni cha kwenu basi tukampa yule mbuzi japo hela na zawadi nyingine aligoma kupokea ila furaha ikapotea alipotuambia kuwa kile kiumbe ni cha kwenu na nyinyi ndo mtatumika kama mlivyotumika kukileta.
Ninachokumbuka ni mzee aliingia kwenye mfuko uliokuwa na zile fedha zote akampa yule mzee ili hilo swala alishughulikie yeye mwenyewe,mzee aligoma kata kata nachokumbuka ni chozi tu lilinitoka hasa baada ya kuambiwa kuwa kile kiumbe kama kitaendelea kuwepo bila kurudishwa kilipotokea basi kitaturudia wenyewe tukiisha kitaingia kwenye ukoo mzima kitamaliza na hata mkoa mzima.
Basi tukaambiwa kuwa ili kile kiumbe kiweze kurudishwa ni wahusika wakuu tutoe zawadi ya damu yah damu,tukauliza dawa gani mganga akatuambia kila mmoja anatakiwa atoe damu yake kidogo,lakini damu hiyo apatikane mbuzi au kondoo au ngombe then kila mmoja atoe damu hiyo kwa atavyojua yeye then hyo damu ichanganywe na apakwe mnyama huyo mwili mzima then mganga atatupatia maelezo nini cha kufanya,
Basi siku hyo mzee aliomba hilo swala tulifanye kesho,maana kwa leo ni ngumu ukizingatia tumechelewa na safari ndefu mganga akakubali ila ajasema hakikisheni mnafanya haraka sana kwani mwenye uwezo wa kukirudisha hicho kiumbe ni mimi na nyinyi mlioingia kwenye hilo agano maana anayeijua kesho ni mungu,sisi hao tukaondoka.
Tumefika zetu nyumbani ilikuwa ni kama kinisherehe kidogo bimkubwa alikuwa amepika msosi wa kutosha nakumbuka ilikuwa pilau mbuzi na vinywaji maana waliitwa mpka watoto wa mtaani kula siku hiyo ikapita.
siku ya pili ilivyofika nikamkumbushia broo kuhusu kwenda kumaliza ile kazi kwa mganga bro akanambia kausha na mimi nae nkasema ngoja nikaushe kwani mambo yameshakwisha, ilivyofika usiku ndo bimkubwa akatukumbusha jana mlinambia kuwa leo mnatakuwa kwenda kumaliza ile kazi mbona hamjaenda?kumbe mzee nae alikuwa anakumbuka ila akajikausha kimya kuambiwa ndo akajifanya kuzinduka,akamwambia mama bwana e hayo sisi tumeshayamaliza tutaenda hata week ijayo,bimkubwa aliongea sana ila ote tukamuona kama anapiga kelele tu.
nakumbuka tulikaa sana kwa raha nadhani unaweza kujua 7m ilikuwa inathamani gani miaka hyo,kwani mzee akitupa kila mtu laki 1 nilikuwa don mtaani naweza kwenda dukani nikanunua creti zima la soda dah ujana huu.
Kasheshe ilianza siku ya tatu,tumetoka kule mida kama ya saa 3 usiku,tunaingia zetu kulala ghafla ikapiga radi ambayo sikuwahi kuiskia toka siku ile mpka leo,baada ya kama dakika 5 tukasikia kishindo kikubwa sana juu ya bati ghafla ikawa kama mtu anakimbia juu ya bati letu,hali hiyo ilidumu kama dakika 10 nzima,ikafuatia sauti ya ngombe zizini kupiga sana kelele kutokana na kutokukutana na masuala ya kishirikina nikatoka nikafungua geti ilikwenda kuona kulikoni(kunifanya shujaa)ila kabla sijatoka nje kabisa nikatoa sura sasa ile nmetoa kichwa nje nachungulia ile kurudisha kichwa ndani lilikuwa limebakia skio nje niliskia kitu kama kisu kinakata skio kwa kasi ya ajabu mnoo alafu nkaishia kuona kivuli tu.
Nilipata maumivu ambayo makali mno,mzee alitoka ndani mbio japo walikuwa wanaogopa kuangalia skio linaruka damu nikahudumiwa nikakimbizwa mawezi hospital nilishonnwa nyuzi zaidi ya 12 lakini donda lilikuwa na alama kama nmengatwa na mbwa vile au mnyama mkali.nikabaki hospitali mpka asubuhi.
asubuhi mzee akaenda kwa mganga,bahati wakamkuta mke mtu lakini cha kusikitisha ni kwamba mganga alienda Kaleni (kuna kiongozi fulani alienda kumtibu) dah mzee alipagawa ndo akaanza kumuekezea kilichotokea mke mtu akamwambia tu ukweli yani hapo mwanako ilikuwa anatolewa shingo ni mungu tu,mimi cha kufanya sina msubirini mpka mwenyewe arudi kwa maana siku 3 mpka 4 mbele. kumbuka toka watu wanipeleke hospitali mda ule mpka sasa wako kwa mganga hakuna aliyerudi nyumbani.
basi mzee akakubaliana na mke wa mganga basi wakarudi nyumbani sasa wakati wanafungua geti wakawa wanasikia harufu kali ya damu na uozo,wakawa wanafuata damu iliyokuwa imetapakaa pale uani ambayo usiku wa jana haikuonekana wakaifata mpaka zizini walichokiona kilikuwa ni gombe mmoja yani alikuwa ameraluliwa mwili ote yani kama vile mtu alikuwa na panga alafu akamkata kata vipande vipande.basi wakasafisha pale na baadhi ya vipande vikazikwa,jioni nikaruhusiwa nikarudi nyumbani.
naomba niweke nukta hapa but naahid kuimalizia tulipata mitihani mingi mpka kuamua kwenda congo kumfata mganga huko huko ambako,tulikutana na viongozi wazito mno,ambao sitopenda kuwataja lakini la mwisho ni tulivyonusurika kuliwa nyama ndio nyama tena na watu wenzetu ntawasimulia vyote na jinsi gani tulivyoponea kutoka kwenye tundu la sindano
Sent using Jamii Forums mobile app
Taarifa nusu nusu hii...Kuna watu wengi wananitumia PM kuomba namba za waganga. Ila hakuna hata mmoja ambaye nimempa, Coz nafsi yangu bado haijaridhia kumpa mtu yeyote iwe bure au kwa pesa. Halafu muwe makini sana na watu wanaowapa namba za waganga humu, mtaishiwa kutapeliwa na kupelekwa sehemu sio .
Nakumbuka kuna kipindi nilikua so desperate na waganga, nilihangaika sana yani kumpata mtu wa kunielekeza huko kwa mda mrefu. Mpaka ikabidi niombe dua hili nipate mtu sahihi kwa kunipeleka kwa waganga.
Mungu sio athumani, akaniunganisha na mtu sahihi aliyetimiza tamaa ya moyo yangu , tamaa ya kufanya ushirikina.
So ushauri wangu , watu wajaribu kutulia na kuongea na nafsi zao na kuomba, kama ni kweli ni kitu wanachokitaka kukifanya, basi watakipata tu kwa njia yeyote, wala hautahitaji nguvu. Roho zetu siku zote zinasikiliza tamaa zetu na kutupatia kile kinachostahili.
Mimi naweza kukupa namba za waganga nilioenda na bado usifanikiwe, so ni bora ukambana wewe mwenyewe kutafuta kile unachokitaka, pambana usikate tamaa.
Mimi ninachojua na nilichojifunza katika haya maisha , Watu wengi wakubwa hapa Duniani, wamefanikiwa kwa nguvu za shetani, inshort shetani ndie anayemiliki hii dunia , tutake tusitake.
Kitu kingine ambacho nilikua sikijui, kumbe kuna watu Tupo nao hapa duniani wanaenda kuongeza mda wa kuishi hapa duniani kwa nguvu za giza
Na kwa kuongezea tu , ni kweli nguvu za giza zipo , na zinatenda kazi .
Sent from my iPhone using JamiiForums
Taarifa nusu nusu hii...
Kama hili la kuongeza miaka sidhani kama ni possible,labda kama wanakuonyesha muda ambao adui angekufyeka then wanakusogeza
Warumi...Kuna watu wengi wananitumia PM kuomba namba za waganga. Ila hakuna hata mmoja ambaye nimempa, Coz nafsi yangu bado haijaridhia kumpa mtu yeyote iwe bure au kwa pesa. Halafu muwe makini sana na watu wanaowapa namba za waganga humu, mtaishiwa kutapeliwa na kupelekwa sehemu sio .
Nakumbuka kuna kipindi nilikua so desperate na waganga, nilihangaika sana yani kumpata mtu wa kunielekeza huko kwa mda mrefu. Mpaka ikabidi niombe dua hili nipate mtu sahihi kwa kunipeleka kwa waganga.
Mungu sio athumani, akaniunganisha na mtu sahihi aliyetimiza tamaa ya moyo yangu , tamaa ya kufanya ushirikina.
So ushauri wangu , watu wajaribu kutulia na kuongea na nafsi zao na kuomba, kama ni kweli ni kitu wanachokitaka kukifanya, basi watakipata tu kwa njia yeyote, wala hautahitaji nguvu. Roho zetu siku zote zinasikiliza tamaa zetu na kutupatia kile kinachostahili.
Mimi naweza kukupa namba za waganga nilioenda na bado usifanikiwe, so ni bora ukambana wewe mwenyewe kutafuta kile unachokitaka, pambana usikate tamaa.
Mimi ninachojua na nilichojifunza katika haya maisha , Watu wengi wakubwa hapa Duniani, wamefanikiwa kwa nguvu za shetani, inshort shetani ndie anayemiliki hii dunia , tutake tusitake.
Kitu kingine ambacho nilikua sikijui, kumbe kuna watu Tupo nao hapa duniani wanaenda kuongeza mda wa kuishi hapa duniani kwa nguvu za giza
Na kwa kuongezea tu , ni kweli nguvu za giza zipo , na zinatenda kazi .
Sent from my iPhone using JamiiForums
Nimesoma post nyingi ila huyu jamaa ameniumiza mbavu kwa kucheka, daahh!!Nishawahi sikia kisa kinschohusishwa na uchawi
Kuna masela wawili walienda kwa mganga ili wapate utajiri
Mganga akawapa dawa akawaambia wakaoge usiku makaburini na wakitoka mlangoni kwa mganga hawatakiwi kugeuka nyuma
Basi unaambiwa safari yao iliandamwa na misukosuko yakutisha, mara wasikie muungurumo wa simba akiwa nyuma yao na vimbwenga vingi lakini walijitahidi kukaza ili kutovunja sharti la kugeuka nyuma
Sasa ulipofika usiku majira ya saa 8 ikabidi waende makaburini kuoga ili kumalizia zoezi lao la mwisho ili wawe mamilionea
Walipofika makaburini wakavua nguo wote nakubakia uchi kisha wakapanda juu ya kaburi ili waoge
si unajua ukiwa katika ile mood flani hivi unaoga halafu umefumba na macho ili maji yasiingie machoni.
wakastukia tu paap! wameshikwa makalio kwa nyuma.
Aaah unaambiwa wote ilibidi wageuke nyuma kwa haraka huku wanakimbia na kupiga makelele
Kesho yake kijiweni wakaanza kulaumiana "aaah wewe ndiye ulizingua, we ungekausha bila kupiga mikelele mi nisingechochora kwani kushikwa tako kitu gani bwana" yani leo nisingekua nakunywa kahawa hapa ningekua nimejikoki huko kwenye hotel zinazotambulika na dunia"
Mkuu unaweza omba 400 ikawezekana?Au ongezeko lina gharama kubwa?Hiyo ya kuongeza miaka ipo
Sent from my iPhone using JamiiForums
Mkuu unaweza omba 400 ikawezekana?Au ongezeko lina gharama kubwa?
Mkuu warumi naona unaufahanu mzuri wa maeneo, ya tiba za Asili. Nina issue yangu, natamani nikupm, Ila hapa Jamvini Ni mgeni kiasi, sijaijua procedure za kuPM.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nimekucheki pm fanya km unaiangalia kidogo
Nimeajiriwa lakin mambo yangu hayaendi mpaka Leo, unakopa mkopo wanakukata alafu inafikia kipindi unaambiwa makato hayaendi benk husika, unarudi nyumbani migogoro isiyoisha yaan n tabu tu, nishasema nikija kumfaham mbaya wangu ntamfanyia mbaya sana
Sent using Jamii Forums mobile app
Yep, nimeelewa sana time hii.Acha ufala bwana ... kuna watu wanaishi kwa kutojiamini, especially the most powerful ones, wana hofu ya kuuliwa, kuugua au kufa mda wowote, so wao huenda kuomba kinga na kuwasaidia waishi maisha marefu (65-100) watu wenngi hawafikishi hii miaka,ni wachache mno, zaidi ya hapo lazima ufe tu , so nadhan utakua umeelewa kidogo.
Sent from my iPhone using JamiiForums