Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Ndo tabia za wachawi, wachawi hawapati faida yoyote wao wanataka kuona mtu anateseka tu ndo furaha yao. Hicho kisa ni cha kweli na kimetokea Ludewa mkoa wa Njombe ukiweza ulizia wenyeji wa huko watakuambia na jamaa amekuwa tegemezi wa kupewa misaada tu, miaka ya nyuma 2000's hiki kisa kiliandikwa kwenye gazeti fulani, it's a true story.
Ukiuliza NDICHELIWE GUEST aliyekuwa RCO Iringa baadaye RPC Dodoma Omary Mganga aliwahi kukimbia nje na boxer kutokana na mauzauza aliyoyaona hapo Guest lakini ni hapo hapo guest ukitaka story za hilo tukio utazipata.
 
Ukiuliza NDICHELIWE GUEST aliyekuwa RCO Iringa baadaye RPC Dodoma Omary Mganga aliwahi kukimbia nje na boxer kutokana na mauzauza aliyoyaona hapo Guest lakini ni hapo hapo guest ukitaka story za hilo tukio utazipata.
Huyu Omary Mganga alikuwa RCO Masasi, then uRPC alianzia Iringa na mwishowe akastaafia Dodoma mkuu. Baada ya kustaafu alifanya kwa mkataba TAMISEMI miaka kama miwili ndio akastaafu mazima.
 
Nipo Njombe huku!! Kuna mwanafunzi alikuwa anafanya mtihani kabla hajamaliza mkono ukaanza kuvimba ghafla hivyo ikashindikana kumalizia mtihani huo! Ikabidi tuwasiliane na Mzazi wake akasema tusimpeleke popote anakuja mwenyewe basi wakaja hapo shuleni na mchungaji baada ya maombi kama dakika 5 tu mkono ulijirudi na kuweza kuandika vizuuuuuuri! Daaa Kweli uchawi upo!! TUMWOMBE MUNGU DAIMA!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Wachungaji tuwape heshima zao ,na hizo sadaka wanahaki kuzipata tu.
 
Hapa uliongea madini... ukiona mtu anajisemesha hakuna uchawi, hakuna uchawi unaoshindakana kwa yesu sijui sheik ujue bdo hajamalza stage za maisha... tena wengne hukohuko makanisan na kwa masheikhe ndio wanachukuliwa hadi nyota zao kabsa...!!! Hii dunia ina vitu vya ajabu mno

Nna mama yangu mkubwa alipwa kipapai akaugua ukichaa na mzee mmoja kisha mipaka ya viwanja hadi anakufa alikosa tiba watu walizunguka kila sehemu makanisa yote alimaliza, visomo vyote alisomewa kwa waganga ndio ucseme....!!! Hii dunia iacheni nyie alufu kuna mtu anataka kujaribu kurogwa daaah utoto kazi sana
Mimi natumika kanisa fulani kama mjoli wa Bwana Yesu. Uchawi upo lakini hauna nguvu kama hujajiunganisha nao. Mama yako mkubwa kuombewa na kushindikana sio kwamba Mungu hana nguvu au hatendi, ila alijiunganisha na nguvu za giza hususan alipoenda kwa waganga ndio maana ulimpa uhalali Ibilisi kumuonea na hatimaye mauti. Hii ndio changamoto kubwa inayotesa wengi.
Upitapo kwenye Jaribu la kulogwa, ukienda kwa waganga ndio kwisha habari yako kwani Shetani hawezi mtoa shetani mwenzako. Unatakiwa usimame na Mungu tu tena kwa kumaanisha japo pia hii ni neema na ufunuo wa kimungu.
Pole sana ndugu yangu.
 
Uchawi upo sema tu kuamini kunakuja kama mtu ameshawahi kupitia mauzauza au laaa.

Kipindi nasoma shule ya msingi miaka hiyo nakumbuka nilikuwa nachuana na binti mmoja. Akishika namba moja mm namba mbili. Nikishika namba moja basi namba mbili.

Baada ya muda ikawa kila ukifika wakati wa mtihani naumwa napelekwa hospitali. Hali hiyo ikatokea kama mara 6 mfululizo.
Siku moja Dr wa hiyo hospitali alikuwa anafahamiana na bi mkubwa akamwambia mwanao hataki shule kila siku anaumwa yeye tu. Ndipo bi mkubwa akashtuka.

Hali ile ikaja kujirudia siku ya mitihani umefika mi naumwa bahati nzuri yule binti niliyekuwa nachuana naye akaja kuniona basi bi mkubwa akatoa la moyoni mbele yake akasema " kila mitihani unapokaribia mwanangu anaumwa sasa mwaka huu nataka nijue kinachofanya huo ugonjwa uwe unasubiri mitihani tu." Wote tukabaki kimya yule binti wala hakujibu chochote.

Toka siku hiyo miaka ikaenda sikuwahi kuumwa tena hadi Leo hii sijawahi kuumwa hata malaria namshukuru Mungu.

Lakini baada ya kumaliza Elimu ya msingi tulipangiwa shule tofauti nilikuja kusikia kumbe yule binti alikuwa na tabia ya kuchuka akili za watu. Alivyoenda sekondari alikutana na wajanja wenzie ndo ikajulikana.

Kwa sasa hivi hata sijui yuko wapi.
 
Uchawi upo sema tu kuamini kunakuja kama mtu ameshawahi kupitia mauzauza au laaa.

Kipindi nasoma shule ya msingi miaka hiyo nakumbuka nilikuwa nachuana na binti mmoja. Akishika namba moja mm namba mbili. Nikishika namba moja basi namba mbili.

Baada ya muda ikawa kila ukifika wakati wa mtihani naumwa napelekwa hospitali. Hali hiyo ikatokea kama mara 6 mfululizo.
Siku moja Dr wa hiyo hospitali alikuwa anafahamiana na bi mkubwa akamwambia mwanao hataki shule kila siku anaumwa yeye tu. Ndipo bi mkubwa akashtuka.

Hali ile ikaja kujirudia siku ya mitihani umefika mi naumwa bahati nzuri yule binti niliyekuwa nachuana naye akaja kuniona basi bi mkubwa akatoa la moyoni mbele yake akasema " kila mitihani unapokaribia mwanangu anaumwa sasa mwaka huu nataka nijue kinachofanya huo ugonjwa uwe unasubiri mitihani tu." Wote tukabaki kimya yule binti wala hakujibu chochote.

Toka siku hiyo miaka ikaenda sikuwahi kuumwa tena hadi Leo hii sijawahi kuumwa hata malaria namshukuru Mungu.

Lakini baada ya kumaliza Elimu ya msingi tulipangiwa shule tofauti nilikuja kusikia kumbe yule binti alikuwa na tabia ya kuchuka akili za watu. Alivyoenda sekondari alikutana na wajanja wenzie ndo ikajulikana.

Kwa sasa hivi hata sijui yuko wapi.
Uchawi upo sana me mwenyewe kuna Mganga aliniambia ili ufaulu mtihani nitajie jina la mwanafunzi anaefanya vizuri hapo shuleni kwenu pia unipe na namba yake ya mtihani

Aisee niliogopa pia nikaona bora nifeli tuu kuliko kupata one halafu kumbe ni akili za mwingine
 
Uchawi upo sema tu kuamini kunakuja kama mtu ameshawahi kupitia mauzauza au laaa.

Kipindi nasoma shule ya msingi miaka hiyo nakumbuka nilikuwa nachuana na binti mmoja. Akishika namba moja mm namba mbili. Nikishika namba moja basi namba mbili.

Baada ya muda ikawa kila ukifika wakati wa mtihani naumwa napelekwa hospitali. Hali hiyo ikatokea kama mara 6 mfululizo.
Siku moja Dr wa hiyo hospitali alikuwa anafahamiana na bi mkubwa akamwambia mwanao hataki shule kila siku anaumwa yeye tu. Ndipo bi mkubwa akashtuka.

Hali ile ikaja kujirudia siku ya mitihani umefika mi naumwa bahati nzuri yule binti niliyekuwa nachuana naye akaja kuniona basi bi mkubwa akatoa la moyoni mbele yake akasema " kila mitihani unapokaribia mwanangu anaumwa sasa mwaka huu nataka nijue kinachofanya huo ugonjwa uwe unasubiri mitihani tu." Wote tukabaki kimya yule binti wala hakujibu chochote.

Toka siku hiyo miaka ikaenda sikuwahi kuumwa tena hadi Leo hii sijawahi kuumwa hata malaria namshukuru Mungu.

Lakini baada ya kumaliza Elimu ya msingi tulipangiwa shule tofauti nilikuja kusikia kumbe yule binti alikuwa na tabia ya kuchuka akili za watu. Alivyoenda sekondari alikutana na wajanja wenzie ndo ikajulikana.

Kwa sasa hivi hata sijui yuko wapi.
Kisa kingine nakumbuka Maza alikuja kijijini kutokea Dar na kiukweli mama alikuwa hana maelewano mazuri na mama mkwe wake ambaye sisi tunamwita bibi

Ile nimetoka kwa bibi ili niende nikamsalimie na nipate vizawadi aisee ile nataka kumuhagi mama nilijikuta naishiwa nguvu na kujikuta napepesuka na kuanguka chini huku nikiwa nimefumba mdomo

Kumbe Bibi aliniingia mwilini mwangu na endapo ningemuhagi mama basi angekumbwa na matatizo eidha kuumwa na kufa kabisa ila inaonesha mama alikuwa na kinga kali sana.

"2006" ilikuwa
 
Kisa kingine nakumbuka Maza alikuja kijijini kutokea Dar na kiukweli mama alikuwa hana maelewano mazuri na mama mkwe wake ambaye sisi tunamwita bibi

Ile nimetoka kwa bibi ili niende nikamsalimie na nipate vizawadi aisee ile nataka kumuhagi mama nilijikuta naishiwa nguvu na kujikuta napepesuka na kuanguka chini huku nikiwa nimefumba mdomo

Kumbe Bibi aliniingia mwilini mwangu na endapo ningemuhagi mama basi angekumbwa na matatizo eidha kuumwa na kufa kabisa ila inaonesha mama alikuwa na kinga kali sana.

"2006" ilikuwa
Nyie kwenu ni walozi

Sent from my Infinix X624B using JamiiForums mobile app
 
Hii ilitokea Tanga wilaya M. Kuna mganga fulani alikua mganga akaona akatoe huduma za kiganga wilaya M akitokea wilaya K. Basi alifikia nyumba ya jamaa mmoja na kumueleza kwamba amekuja hapo kutoa huduma kama kuna mwenye tatizo lolote aje. Basi mganga akapewa chakula akala na kupewa mahali pa kulala. Muda kufika akaenda kulala na mikoba yake. Kulipokucha adibuhi mganga alijikuta yuko nyumbani kwake wilaya K na mke wake na mikoba yake
Nimecheka sana. Amekutana na wenyeji, hotatenaneee, kwaakua mbui.
 
Back
Top Bottom