Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Yuko dogo mmoja alikua anasoma B sekondary. Alikua anamchukua mke wa mtu. Mtu mwenyewe alikua nje ya nchi kimasomo. Ndugu zake msomi hawakupendezewa shemeji Yao aliwe na student. Kuna siku dogo wakapanga na bibie wakapeane penzi kwenye minazi. Enzi hizo gesti wanaingia wenye pesa zao.

Dogo alikua dent hana pesa. Basi kweli muda kufika mke akafika na mechi ikaanza bila refa. Dogo akapakua mzigo kufika kileleni utamu Ulipozidi ni kawaida mtu kufunga macho. Basi dogo wakati anafyatua risasi alimkumbatia mke wa mtu kisawasawa huku amefunga macho. Ile kumaliza na kufumbua macho akajikuta alikua anafanya mapenzi na kisiki cha mnazi na sio mtu. Dogo kutoka pale hakurudi shuleni. Alipanda basi la Dar na kuacha shule. Sidhani kama alisharudi wilaya ya B.
B sekondary, wilaya E, mkoa wa K.... Ni woga au?
 
Miaka kadhaa nyuma, bibi yangu mzaa mama, katika umri wake wa makamo, mrembo na mwenye kinywa kilichosheheni meno imara na meupeeee, aliamka asubuhi moja tusiyoisahau mpaka leo, kinywani akiwa hana jino hata moja. Alikuwa kibogoyo kabisa kama alizaliwa na kukua bila meno.

Wakati ukoo mzima tumetunduwaa kwa mshangao, jamii ilitutuliza kwa kutuambia kuwa tuwe wapole na habari ndiyo ilikuwa imekwisha hivyo. Kuwa bibi yangu eti alifanya uzembe wa kuamka na kupiga kelele akidai meno yake hayamo kinywani.

Kumbe ilimpasa, baada ya kuona kinywa chake kitupu, angerudi kimya kimya kulala. Meno yake yangerejeshwa na walioyaazima kwenda kutafunia nyama na bisi!! Ni juzi tu tumemzika bibi yetu akiwa kibogoyo kwa miaka kibao, kwani meno hakurejeshewa tena. Uchawi wa migombani Unyakyusa huu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Uwiii lazima ningelipiza tu, liwe jua iwe mvua...
 
Kaka yangu alisimulia akiwa na crew yake wametoka zao kuwinda ghafla gari ikagoma, wakaicheki kila kitu ipo fresh lakini haiwaki, wakashauriana walale kwenye gari kesho wataikagua vizuri, basi usingizini waliota kama wapo shamba wanalima, kuamka asubuhi wakashangaa miguu imejaa tope jekundu yaan wamechafuka mno gari inanuka vitunguu na ina maganda ya vitunguu kujikagua vizuri wakakuta vitunguu vinne na wao walikua wanne.

Moro hiyooo mwaka 2016.
Mchawi kawazawadia kila mtu kitunguu akamwonyeshe mkewe...
 
Biashala ina mambo mengi ndugu uchawi ktk biashala upo nakupa kisa kimoja hivi miaka ya nyuma nilifanya biashala ya duka maeneo ya kwa mkandawile huko nikawa nikiweka mtaji biashala nauza vizuri ila hela jioni siioni nikajiongeza mana pale kulikuwa na waha wanauza hao mpk basi basi nikaenda sehemu kwa mzee mmoja kule Kunduchi yy ni marehemu kwa sasa akaniangalia nyota akasema inabidi kazi yako tuifanye siku ya j5 kulingana na ulivyo ila apatikane kuku mweupe ambaye tutatoa damu yake kweli nikaacha hela ya kuku pale nikaondoka siku nimefika akafanya mambo yake na akanichanja chale kadhaa mwilini yule mzee ni mha akaniambia nakupa hii azima kaiweke dukani kwako huyo ni jini atakuwa anakujazia bidhaa pale dukani na ndio wafanyabiashala wakubwa wanamtumia akanipa na masharti kadhaa basi nakumbuka nilikimbiza pale ila nilikuja kukosea sharti moja kila kitu kikafa ila tangu hapo hakuna ninachofanya kikaenda sawa tena mpk sasa
Toa full story
 
Biashala ina mambo mengi ndugu uchawi ktk biashala upo nakupa kisa kimoja hivi miaka ya nyuma nilifanya biashala ya duka maeneo ya kwa mkandawile huko nikawa nikiweka mtaji biashala nauza vizuri ila hela jioni siioni nikajiongeza mana pale kulikuwa na waha wanauza hao mpk basi basi nikaenda sehemu kwa mzee mmoja kule Kunduchi yy ni marehemu kwa sasa akaniangalia nyota akasema inabidi kazi yako tuifanye siku ya j5 kulingana na ulivyo ila apatikane kuku mweupe ambaye tutatoa damu yake kweli nikaacha hela ya kuku pale nikaondoka siku nimefika akafanya mambo yake na akanichanja chale kadhaa mwilini yule mzee ni mha akaniambia nakupa hii azima kaiweke dukani kwako huyo ni jini atakuwa anakujazia bidhaa pale dukani na ndio wafanyabiashala wakubwa wanamtumia akanipa na masharti kadhaa basi nakumbuka nilikimbiza pale ila nilikuja kukosea sharti moja kila kitu kikafa ila tangu hapo hakuna ninachofanya kikaenda sawa tena mpk sasa
Ulikosea nn
 
Wakuu habari zenu, ni matumaini yangu kuwa hamjambo.

Leo nataka kuweka ushuhuda wangu kwa niliyoyashuhudia live juu ya nguvu za giza, kwa wasioamini nadhani uzi huu hautakuwa na thamani kwao, kama na wewe unao ushuhuda usisahau kushea nasi.

1. Ushuhuda wangu unaanzia mwaka 1992 nikiwa nafundisha shule X wilaya ya Sengerema, kuna mwalimu nilikuwa nafundisha naye kituo kimoja.

Siku hiyo kuna kamvua kalinyesha sana, baada ya kupungua mwalimu mwenzangu alimuagiza mtoto wake wa kiume aliyekuwa akisoma darasa la kwanza kwenda kuchuma maharage shambani.

Bahati mbaya mtoto akiwa shambani aligongwa/aliumwa na nyoka na kupeleka kifo, tulifanya taratibu za mazishi na kumsitiri mtoto huyo.

Cha kushangaza mwaka 2008 mtoto huyo alionekana akiwa uchi na nywele ndefu sana alikuja moja kwa moja nyumbani na kupitiliza ndani nyumbani kwao, alikuwa ameshakuwa baba mzima, nywele zilikuwa ndefu sana pamoja na mikono iliyofikia usawa wa magoti.

Watu walistaajabu sana lakini hakudumu sana alifariki baada ya kukaa uraiani kwa wiki mbili.

2. Ushuhuda wangu bado unabaki huko huko Sengerema katika kijiji cha Bubandwamhela.

Nikiwa nafundisha shule X, kuna binti kijijini aliyekuwa akisoma darasa la saba aliugua ghafla baada ya kutoka shuleni.

Wazazi wake walipompeleka hospitali daktari aliwaambia mtoto hana ugonjwa, wazazi waliamua kujiongeza na kumpeleka kwa mganga wa jadi.

Cha kushangaza kesho yake shangazi ya binti alikutwa kwa mganga akiwa uchi, huku akiweweseka na akili zimemruka, shangazi mtu alikamatwa na kupelekwa kituo cha polisi lakini kwa kuwa serikali haiamini ushirikina aliachiwa huru, lakini hadi leo hii alishakuwa chizi. Binti yeye alipona kabisa.

3. Kisa cha tatu na mwisho ni hiki kilichotokea Liwale shule ya sekondari X nikiwa na walimu wenzangu ambao tulikuwa tunasoma chuo cha SAUT-Mtwara.

Tulipangiwa field katika wilaya ya Liwale ilikuwa mwaka 2009, mwanachuo mwenzetu akiwa zamu siku hiyo alikumbana na mtoto ambaye kwao iliaminika kuwa bibi yake alikuwa mtaalamu wa mambo ya giza.

Mwanafunzi huyo alichelewa kufika shule, mwalimu alipotaka kumuadhibu aligoma, wakasumbuana sana mwisho wa siku akamuadhibu yakaisha, jioni tukiwa uwanjani tunafanya mazoezi yule mwanachuo mwenzangu alianguka na kupoteza fahamu, ikawa jumla hadi kifo.

Kama na wewe umewahi kukutana/kushuhudia live ushirikina share nasi kisa chako watu tupate ilimu.

Mungu ni mwema siku zote.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mambo ya giza yanaikumba jamii kwa kasi kikubwa ni kushikia imani za dini zetu kwa nguvu.
 
Uchawi upo tena sanaaa tu kuna tajiri mkoani njombe jina nahfadhi..
Alitoka dar kununua gari kiusalama zaid akamchukua fundi toka dar kuja nae njombe. Walifka mikumi ghafla gari ikazima hakunA kitu kinachofnya kazi milango haifunguki. Tajir akawa amejua nn kimatokea sasa atafnyaje. Hawez kutoka akaongea na simu njee ikabid ampigie mkewe amwambie apulize chungu cha tatu. Fundi akabaki anashangaa baada ya mda gari ikawaka wakaendelea na safarii yule ndie alitupa hichi kisaaa
Da
 
Supu ilibadilika Radha baada ya mbibi kuinyooshea kidole,
Aisee uchawi upo ndg zangu nilinunua supu ikiwa na Radha yake nzuri kabisa lakini baada ya kuja bb ambaye yeye mwenyewe alikuwa anauza supu jirani na pale niliponunua, akanikuta nakunywa Ile supu ghafla nikamuona kama kanyoosha kakidore kwenye Ile bakuri ya supu ghafla Radha ilipotea nikawa nakunywa kama maji, jamani nani asiyeamini uchawi.
 
Miaka ya nyuma nilienda Mafia Island kwa Babu yangu.
Basi nilienda na Redio ya kuchaji kwa kuzungusha kama unapandisha Kioo ktk Gali kubwa.yaani unapo zungusha ndio linajichaji nazani ushapata picha.
Basi ikawa nikilala Usiku naliwasha kwa sauti kubwa mwenyewe nalala.
Kumbe kuna wazee majilani walikua nawakera Usiku, Wakamwambia Babu asubuhi.
Babu akanielezea alichoambiwa na Wazee wenzake,nikaacha kuweka sauti kubwa nikapunguza sauti.
Ikapita siku kama tatu hivi nikakutana na Bibi mmoja njiani nilivyo msalimia akaitikia alafu akaniuliza wewe ndie unatupigia kelele usiku na Redio yako eee?.
Mzee nikauchuna kimya basi nikaacha kabisa kuwasha Usiku.
Ikapita siku kazaa Mzee nikajisahau nikarudia tena ujinga wangu wa kuwasha Redio tena kwa sauti kubwa nakula zangu ladha za Bongo.
Nilivyo kuja kustuka saa 9 usiku Redio imepunguzwa sauti yaani ule mziki unapigwa lakini mwimbaji kama sauti imemkauka,nikapotezea nikazima nikilala zangu.
Asubuhi nikachaji Redio yangu basi kila nikibadili Station Mtangazaji sauti imemkauka,nikaweka Kanda za kaseti vilevile .
Ikabidi niipeleke kwa fundi, fundi akaniambia Spika mbovu akaibadilisha ngoma vilevile .
Nikamfuata Babu nikamuelezea yaliyo tokea akasema wale wazee washafanya yao. Basi nikarudi zangu Dar na redio yangu na haikupona tena. Licha ya kufanya juhudi ya kuangaika kwa mafundi
 
Wakuu habari zenu, ni matumaini yangu kuwa hamjambo.

Leo nataka kuweka ushuhuda wangu kwa niliyoyashuhudia live juu ya nguvu za giza, kwa wasioamini nadhani uzi huu hautakuwa na thamani kwao, kama na wewe unao ushuhuda usisahau kushea nasi.

1. Ushuhuda wangu unaanzia mwaka 1992 nikiwa nafundisha shule X wilaya ya Sengerema, kuna mwalimu nilikuwa nafundisha naye kituo kimoja.

Siku hiyo kuna kamvua kalinyesha sana, baada ya kupungua mwalimu mwenzangu alimuagiza mtoto wake wa kiume aliyekuwa akisoma darasa la kwanza kwenda kuchuma maharage shambani.

Bahati mbaya mtoto akiwa shambani aligongwa/aliumwa na nyoka na kupeleka kifo, tulifanya taratibu za mazishi na kumsitiri mtoto huyo.

Cha kushangaza mwaka 2008 mtoto huyo alionekana akiwa uchi na nywele ndefu sana alikuja moja kwa moja nyumbani na kupitiliza ndani nyumbani kwao, alikuwa ameshakuwa baba mzima, nywele zilikuwa ndefu sana pamoja na mikono iliyofikia usawa wa magoti.

Watu walistaajabu sana lakini hakudumu sana alifariki baada ya kukaa uraiani kwa wiki mbili.

2. Ushuhuda wangu bado unabaki huko huko Sengerema katika kijiji cha Bubandwamhela.

Nikiwa nafundisha shule X, kuna binti kijijini aliyekuwa akisoma darasa la saba aliugua ghafla baada ya kutoka shuleni.

Wazazi wake walipompeleka hospitali daktari aliwaambia mtoto hana ugonjwa, wazazi waliamua kujiongeza na kumpeleka kwa mganga wa jadi.

Cha kushangaza kesho yake shangazi ya binti alikutwa kwa mganga akiwa uchi, huku akiweweseka na akili zimemruka, shangazi mtu alikamatwa na kupelekwa kituo cha polisi lakini kwa kuwa serikali haiamini ushirikina aliachiwa huru, lakini hadi leo hii alishakuwa chizi. Binti yeye alipona kabisa.

3. Kisa cha tatu na mwisho ni hiki kilichotokea Liwale shule ya sekondari X nikiwa na walimu wenzangu ambao tulikuwa tunasoma chuo cha SAUT-Mtwara.

Tulipangiwa field katika wilaya ya Liwale ilikuwa mwaka 2009, mwanachuo mwenzetu akiwa zamu siku hiyo alikumbana na mtoto ambaye kwao iliaminika kuwa bibi yake alikuwa mtaalamu wa mambo ya giza.

Mwanafunzi huyo alichelewa kufika shule, mwalimu alipotaka kumuadhibu aligoma, wakasumbuana sana mwisho wa siku akamuadhibu yakaisha, jioni tukiwa uwanjani tunafanya mazoezi yule mwanachuo mwenzangu alianguka na kupoteza fahamu, ikawa jumla hadi kifo.

Kama na wewe umewahi kukutana/kushuhudia live ushirikina share nasi kisa chako watu tupate ilimu.

Mungu ni mwema siku zote.

Sent using Jamii Forums mobile app
hapo ni hata sijakusoma mkuu!!

yaan mwaka 1992 ndio ushuhuda wako wa kwanza ukiwa unafundisha shule X

halafu ushuhuda wako wa mwisho ni mwaka 2009 ukiwa field liwale wakati huo inasoma chuo cha sauti mtwara

hoja yangu sasa, yaani ulianza kufundisha kabla haujawa mwl?
 
Back
Top Bottom