Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Hii ilimtokea Mshiakaji wangu dereva wa lori
Anatoka zake Zambia akavuka Tunduma boda, alipoona yupo Bongo akaenda kuna mahali wanalalaga madereva basi usiku mnene akasikia kama watu wanapita nje akachungulia dirishani akaona kikosi cha WANGA wanawake wako msururu, ile bado anaangalia akamuona mzee mmoja yuko kwa nyuma ndo kama anawa command, basi kufika usawa wa dirisha yule mzee akawa kama kastuka hivi akageuka upande aliko jamaa(jamaa yupo ndani) akaanza kupiga hatua akilifata dirisha, jamaa kuona hivyo akaegesha kama amelala akiskilizia nini kinafuata, Ebana yule mzee alifika akaingiza kichwa kuchungulia ndani bila kufungua dirisha huku mwili wake ukiwa nje na kichwa mpaka usawa wa mabega kaingia ndani, jamaa akakausha mzee akawacheki akaona kama wote wamelala akazepa zake.
Kubababake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimecheka mpk Bia imenipalia!
Huyo jini alikuwa bado mwanafunzi
Jirani yangu kuna siku alikuwa ananisimulia alikuwa anasafiri na broo wake usiku walikuwa kwenye gari yao. Safari ilivyokuwa inachanganya mbele wakamuona mtu kwa mbali kama anasimamisha gari. Kumuangalia vizuri kumbe ni mwanamke, halafu ni mrembo tu! Dogo akamwambia bro huyu mwanamke atakuwa jini tu haiwezekani usiku huu wote asimame njiani peke yake, tumpite tu.

Brother yake akamwambia usihofu. Akasimamisha gari. Akamwambie ndio mrembo! Yule mwanamke akamwambia naombeni lift nimekwama huu usiku naelekea eneo fulani. Brother yake akamwambia yule mwanamke ingia. Safari inachanja mbuga brother yake akaanza kumwambia yule mwanamke. Inakuaje unatusumbua unasimamisha gari wakati eneo unalotaka kwenda unaouwezo wa kufika?

Yule mwanamke akajibu sielewi unachozungumza. Brother yake akamwambia yule mwanamke, usi' panic! Sisi tuliokupa lift tunajua kwamba wewe ni jini! Ndiyo tunakuuliza kwa nini umetusumbua kusimamisha gari wakati kufika eneo unalotaka uwezo huo unao wewe kama wewe?

Yule mwanamke akawaambia simamisheni gari! Majamaa wakasimamisha. Wakasikia mlango wa siti ya nyuma unafunguliwa. Kugeuka yule mwanamke hawamuoni tena! Brother yake akasema, unatusumbua wakati uwezo wa kufika unao. Wakaendelea na safari.

Nikamuuliza sa mbona huyo jini katumia style ya zamani sana? Jamaa akanijibu, majini ni wapumbavu wapumbavu tu.
 
Hebu nisimulie hiki kisa changu...

Jumanne 23-08-2019.

Ilikuwa saa nne na nusu usiku nikiwa nimeketi sebuleni,mara gafula mzee akatoka chumbani na kuanza kunitukana matusi ya nguoni...

"Kijana gani wewe kazi kula na kujaza choo,huoni wenzio wanafanya kazi na wanategemewa na wazazi wao...ni bora ningezaa hata mbuzi ningefaidi mchuzi.."


Mara ghafula nashutuka kofi hili hapa sijakaa vizuri ngumi hii hapa,nikasimama imara na kumkazia tu macho...wadogo zangu na mama yangu wakitazama tu pasi na kusema neno.

Nikageuka taratibu na kutoka nje,chozi la uchungu likanitoka ilikuwa ni siku mbili tu toka nifukuzwe shule moja niliyokwenda kuomba ajira ya kujitolea..ati hawawezi kuajiri kiziwi!.

Nilitazama anga jeusi lililosheheni nyota nyingi,mwezi uliotoa nuru angavu nikajiuliza "Mungu upo wapi?".. Nikaingia chumbani na kuvaa viatu.. Nikatoka naenda wapi? Sijui!

Nikaambaa nisijue kama nakanyaga ardhi au ninapaa,napishana na mtu ama kisiki,ilinichukua nusu saa kuuacha mtaa wetu nikaingia mtaa wa pili,huu ulikuwa na watu wachache zaidi na nyumba zilikuwa mbalimbali kiasi.


Nikakatiza pembeni ya makaburi,nikasimama,nikayatazama na kujiuliza " kwanini nisingekuwa nimelala pale? Nipumzike!"...loooh lakini sauti nyingine ikaniambia "una uhakika ukilala pale utapumzika? Nikagutuka nikatazama huku na huko hakuna kiumbe nikaongoza njia kuliacha eneo la makaburi na kuzidi kupotelea mbali zaidi na nyumbani.


Hatimaye nikawasili sehemu pweke,barabara kubwa ya kokoto,kulia na kushoto kukiwa na msitu na vichaka vingi,kiza ni kingi kutupia macho simu yangu ni saa sita na robo usiku!

Ikafika mahali kuna njia panda na upande wa kulia kuna mti mkubwa sana aina ya mbuyu mahali pana pana joto sana bwana,pana joto kali,mapigo ya moyo yakanienda mbio " duuucha dunduncha ducha dunduncha" sasa mapigo niliyasikia hadi masikioni..

Nywele zikanisimama na vipele vya uoga vikanitoka hewa ikawa nzito na uvumilivu ukaniisha na sasa nikatimua mbio hata nilipoliacha eneo lile kwa umbali wa mita mia mbili hivi,na sasa nikaanza kutoka katika makazi ya watu.

Kufika hapa ikanipasa kujiuliza ni wapi naelekea,sikuwa napajua napoelekea kumbukumbu ya misukosuko ya kimaisha na masimango yasiyoisha zikanijia,woga wote ukabiisha donge zito la uchungu,hasira na kukata tamaa likanivaa,machozi yakanitoka,nikashika njia na kuendelea na safari,safari isiyojulikana!


Baada ya mwendo wa dakika ishirini hivi nikaingia katika barabara kubwa ya lami,nikashika uelekeo wa kushoto,ilielekea ufukweni,baada ya masaa mawili hatimaye nikawasili ufukweni,nikazitupia macho hoteli kadhaa zilizotamalaki eneo lile,nikaachana nazo na kushuka mchangani mbali kidogi na mahoteli yale,nikajikalisha kitako na kutafakari nilipotoka,nilupo na ninapoelekea,lakini mbona mbele kyna kiza kizito!


KIZAAZAA!

Hatimaye saa tisa ikawadia,nilichoka,na sasa ilikuwa ni safari ya kurudi,nikajizoa zoa na kushika njia kurudi nyumbani,bahati nzuri barabara hii ilikuwa na taa hivyo ikawa ahueni kwangu.


Baada ya mwendo wa dakika arobaini hivi nikahisi kama kwamba kulikuwa na mtu nyuma yangu,nikageuka kwa kasi, ebo! Nikaona nguo ya rangi ya khaki,aidha gauni au kanzu ikiishia na kufutika machoni kwangu....

Mshtuko uluonipata ukanifanya hata nguvu za miguu ziniishie nikajikuta nikiketi katika mfereji mfupi uliojengwa pembeni ya barabara.

"Ni nini hiki? Ni kweli au ni mawazo yangu tu?" Nikajiuliza,nukatazama huku na huko hali ni shwari,labda niliangalia vibaya bwana nikajizoazoa na kuendelea na safari..

Kiroja kingine tena! Ati nina vivuli viwili,kimoja ni changu na kimoja kimevaa kanzu kama si gauni!(mataa ya barabarani yanawaka hivyo mtu akipita kivuli chake kinaonekana kwa ufasaha kabisa) nikatetemeka kwa woga,nikageuka nyuma ati nacho kikageuka! Nikawa natembea kwa kurudi kinyume nyume,ati nacho kinarudi kinyume nyume!.

Lakini mbona kivuli changu kupo mbele yangu hiki cha nyuma ni cha nani? Na tumeachana umbali wa hatua kama tatu hivi toka kilipo hadi nilipo,nikaona huu sasa utani,nikifa si nife tu ebo! Nikakata shauri kukifuata he! Ati nacho kinageuza kila nikikifuata nacho kinaenda nyuma zaidi,ikabidi nikikimbize sasa..kikapotea.

Nikageuka na kuanza kukimbia kwa taratibu mithiri ya mbio za riadha,nikachoka nikaanza kutembea baada ya mwemdo mrefu kivuli kile kikarudi! Sikusimama nikaendelea kutembea tu.

Hata hivyo nikaanza kuhisi mwili kuchoka sana,miguu inauma na usingizi ni mwingi sana,nikajikalisha juu ya ukingo wa karavati kutafuta pumzi maana ilikuwa ni safari ya masaa mawili zaidi hadi nifike nyumbani...nikaanza kusinzia na hatinaye fahamu zikakomea hapo.


Kelele za watoto wakicheza ndizo zilizonigutusha,nikafumbua macho..afanalek! Nilikuwa nimelala chumbani kwangu..miguu ilikuwa imevimba kiasi na mwili mzima ulikuwa unaniuma...


"Lakini mimi mbona nilikuwa kule barabarani?" Nikajiuliza nisijue kilichotokea,nikaamka na kulibinua bati ninalotumia kama mlango,nikapenyeza kiubavuubavu hadi nje.

Nikawatazama nyusoni niliowakuta nje,wapo kawaida,hawana hata habari,pengine niliokotwa na wasamaria wema! Lakini mbona watu wapo kawaida kama hakuna kitu?...nikashindwa kuvumilia nikaamua kumuuliza mama ni muda gani niliingia kulala!

Akanijibu "we si uliingia kulala saa nne weww? Maswali gani hayo usinisumbue" ni nani aloyenirudisha nyumbani,na kile kivuli ni kiumbe gani? Je ndicho kilichonirudisha nyumbani? Lakini hakijanidhuru, hili ni fumbo niishilo nalo hata sasa kuna wakati natamani kukiona tena kivuli kile kilichovalia kanzu au gauni lililopauka lakini hakitokei tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
kwa kweli story hii, inanihitaji kumtafta mwalimu wangu wa fasihi aliyenifafanulia liwaya ya "joka la mdimu" mpaka nikaelewa, aje anifafanulie na tungo za liwaya hii..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jirani yangu kuna siku alikuwa ananisimulia alikuwa anasafiri na broo wake usiku walikuwa kwenye gari yao. Safari ilivyokuwa inachanganya mbele wakamuona mtu kwa mbali kama anasimamisha gari. Kumuangalia vizuri kumbe ni mwanamke, halafu ni mrembo tu! Dogo akamwambia bro huyu mwanamke atakuwa jini tu haiwezekani usiku huu wote asimame njiani peke yake, tumpite tu.

Brother yake akamwambia usihofu. Akasimamisha gari. Akamwambie ndio mrembo! Yule mwanamke akamwambia naombeni lift nimekwama huu usiku naelekea eneo fulani. Brother yake akamwambia yule mwanamke ingia. Safari inachanja mbuga brother yake akaanza kumwambia yule mwanamke. Inakuaje unatusumbua unasimamisha gari wakati eneo unalotaka kwenda unaouwezo wa kufika?

Yule mwanamke akajibu sielewi unachozungumza. Brother yake akamwambia yule mwanamke, usi' panic! Sisi tuliokupa lift tunajua kwamba wewe ni jini! Ndiyo tunakuuliza kwa nini umetusumbua kusimamisha gari wakati kufika eneo unalotaka uwezo huo unao wewe kama wewe?

Yule mwanamke akawaambia simamisheni gari! Majamaa wakasimamisha. Wakasikia mlango wa siti ya nyuma unafunguliwa. Kugeuka yule mwanamke hawamuoni tena! Brother yake akasema, unatusumbua wakati uwezo wa kufika unao. Wakaendelea na safari.

Nikamuuliza sa mbona huyo jini katumia style ya zamani sana? Jamaa akanijibu, majini ni wapumbavu wapumbavu tu.
Daaa nimecheka broo kauzu huyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimecheka mpk Bia imenipalia!
Huyo jini alikuwa bado mwanafunzi
Haha! Huyo jamaa huwa ananiacha hoi sana! Kuna siku kuna mwanamke alipandisha majini bhana! Wakaja viongozi wa dini kufanya kisomo. Si tulikuwa pembeni tunaangalia picha jinsi linavyokwenda. Yule jini akaanza huyu mwanamke nampenda siwezi kumuacha!

Huyo mshikaji si akanyanyuka bhana akamsogelea huyo mwanamke aliyepandisha majini. Jamaa akaanza; Nyie majini washenzi sana! Kwenu hamna mademu! Unampenda unampenda nani rudi kwenu huko!
 
Sikuwahi shuhudia live uchawi ila niliwahi shuhudia matukio mengi ya kichawi...

Miaka 2007 hadi 9 niliinshi nyumba moja magomeni mikumi karibu na bondeni kule kwa mzee mmoja wanamuita Fungo,

Nikiamka usiku wa manane naenda kukojoa naskia ngoma inachezwa sebuleni kwao waliishi nyumba kubwa mimi chumba cha nje na hiyo ilikua mara nyingi sana kuskia hata ikitokea nikishtuka usingizini naskia wakiimba, kupiga ngoma na kucheza.

Siku nkapanga safari kwenda kusalimia kijijini ikabidi nikubaliane na mzee alale chumbani kwangu maana kulikua na wezi sana miaka hiyo,

Baada ya wiki kurudi nkakuta kapeti limechanwa chanwa sanaaaaa na ni maeneo yale yanayokanyagwa tu, na vipande vimejazana huko chini kibao,
Hata sikuuliza kwa mazingira niliyoyaona nkajua tu ngoma ilihamia gheto kwangu na watakua wanavaa viatu vyenye ncha kali ndio maana wakalichana vile..

Lakini cha ajabu matukio yote hayo sikuwahi kua na hofu hata chembe hata sijui kwanini...

Kuna nyumba tulipanga maeneo ya sinza mapambano, mara nyingi tu mke wangu huona watu wako uchi aidha nje wakichungilia dirishani na wengine wapo chumbani kwetu, na hapo yule macho live, lakini hata anaponiadidhia wala sipati hofu yoyote, hua naona kawaida tu, sijui ni kwanini.

Sent using Jamii Forums mobile app
Msalimie mkeo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiki kisa kilinitokea mimi mwenyewe miaka ya 80, kati ya 86/87. Sikumbuki mwaka sahihi sababu ya umri mdogo niliokuwa nao, ila nilikua najitambua. Tukio hilo lilitokea sehemu ambayo baadaye nilikuja kujua kuwa inaitwa makuburi jijini Dar, baada ya kuwauliza wazee nikiwa na umri wa kutosha kwenye miaka ya 90. Maana ni tukio ambalo hadi leo huwa tunataniana sana tukikutana familia nzima. Nakumbuka ilikuwa kipindi hicho Mzee alikuja Dar kwa ajili ya kusoma UDSM baada ya kuamua kujiendeleza. Sasa akaona ili asome vizuri, ni vema awe pamoja na familia yake. Kwahiyo baada ya kumaliza taratibu za kujisajili chuoni, akaamua kutafuta nyumba. Ndio akapata nyumba nzima huko makuburi. Basi akafuata familia yake, mama, mimi na dada yangu. Basi tukafika jijini Dar, na kuanza maisha mapya. Lakini hatukuchukua raundi, ndani ya mwezi mmoja tu. Ndio likatokea tukio hilo. Siku hiyo ilikuwa ni usiku mnene, sikumbuki ilikuwa ni wa saa ngapi. Ila nilikuwa sijapata usingizi bado. Hata dada angu alikuwa hajalala. Maana tulikuwa tunalala kitanda kimoja(mzungu wa nne). Pia tulikuwa tunalala na binti wa nyumba ya jirani, alimuomba bimkubwa ili atupe kampani maana tulikiwa wadogo kuliko yeye. Pia ni mwenyeji. Mimi kidume niko upande wangu kimya, nasubiria usingizi wakati wao wanapiga tu stori. Hapo tumeshazima taa yetu ya chemli. Nimekaaaa....mara ghafla nikashtuka naona mtu mweupe amesimama pembeni ya kitanda tena usawa wangu!! Nikashtuka, ila sikufanya chochote. Nikawa namtazama tu. Baadae nikamuona anaanza kutembea kukizunguka kitanda. Kapiga raundi moja kisha akakaa juu ya kingo za kitanda upande walikoweka vichwa dada na mwenzie. Mi namuangalia tu! Akapiga raundi ya pili, akakaa tena palepale! Ikabidi nimshtue sista,(nikamwita jina lake) mtu huyo!! Wakashtuka...wakaangaliaa...hawajaona kitu. Akanimaindi"hebu lala huko...usitusumbue!" Mmmh...nikaona hili balaa! Yaan mtu huyu hapa halafu wanasema hawamuoni! Itakuwaje?! Ikabidi nitulie tu...akapiga raundi ya tatu halafu akaja usawa wangu akiwa ukutani akasimama! Nikabaki nashangaa, kitanda kimegota hadi ukutani, huyu anawezaje kutembea bila shida?! Wakati najiuliza nikashangaa kuona ananisogezea mkono wake!! Akisogeza, na mimi nasogea kimyakimya... hadi nikafikia kwenye ukingo wa kitanda, yaani kinachofuata ni kudondoka!! Ujasiri ukanishinda, ikabidi nipige yowee...""baba mtuuuuu!!!" Hapo niko chini tayari!! Sista na mwenzie walivyoskia hivyo ikawa vurugu mechi, na lile giza. Ilikuwa ni mwendo wa kuparamiana tu!!!Dingilai alikurupuka geto kwake na taulo huku kashika panga huku bimkubwa akiwa nyuma yake! Kufika pale kuwasha chemli, akapekuwa hadi uvunguni. Wakaambulia chenga tu, nikawasimulia ilivyokuwa. Ingawa sista nae alidai walivyokurupuka walimuona kabla hajatoeka ingawa simuamini sana. Tangu siku hiyo wote tukawa tunalala chumba kimoja. Na yule binti akakataa kuja kulala. Wiki hiyo hiyo tukarudishwa kwa bibi, dingi akarudi hostel za chuo.
Na kisa kingine nilikutana nacho mwaka ya 2008, ingawa hakikunilenga mimi ila kiliashiria ulozi moja kwa moja. Mimi huwa nilikuwa na tabia ya kupenda kurudi usiku sana nyumbani. Utakuta nakaa home kuanzia asubuh, nafanya shughuli zote. Ila ikifika saa 10 jioni, ndio natoka. Na kurudi ni kuanzia saa 3 hadi 6. Sasa siku hiyo narudi zangu, mida ya saa 4 usiku. Njia ya mkato ina makaburi, naogopa. Njia ndefu kuna kakichaka karefu, kanatisha! Ila huwa napita bila shida. Ila siku hiyo nikajikuta tu naingiwa hofu! Ikabidi nipige moyo konde, maana lazima nirudi home. Basi nikatembea kwa kasi balaa, nikapanga nikikaribia karibu na hicho kichaka nipite kwa kasi ya upepo!! Basi nakaendaaa, nilipokaribia kichaka nywele na mwili vyote vikasisimka. Nikasema leo kazi ipo, nikajikoki...nikatoka nduki la hatari na nakimbia(huwa napenda). Kufika katika ya hicho kichaka nikakuta bonge la kinu limefunikwa!! Hiyo breki na kona niliyokata, Mungu tu ndiyo anajua. Na kipindi hicho nilikuwa niko vizuri kwa mazoezi. Sikugeuka nyuma hadi nyumbani. Niliwaza sana, karibu wiki nzima. Hizi ningekigonga na kubinuka ingekuwaje?! Baada ya mwezi nilimsimulia bimkubwa, alinisema sana! Nikapunguza kutembea usiku. Saa mbili niko home.
 
Mimi nilikuwa siamini hizo mambo lakn kipind cha wife ana ujauzito wa mtt wetu wa kwanza.. nikiwa mchanga kbsa kiimani,siku hio nakumbuka tumelala tukaota ndoto moja mm na wife.. ndoto ilikuwa ni mmama mmoja anasema anataka mtt alieko tumboni ili amtoe kafara,tukashtuka.. baada ya kushtuka tukasikia mipaka inalia nyuma ya nyumba kwa sauti kubwa,nilikuwa nmeshafundishwa kuomba na kukemea.. asee niliomba sana usiku huo kwa ujasiri na nguvu maana wife yeye muda huo alikuwa analalamika tumbo linamuuma na mtt alikuwa anarukaruka hatar tumboni... wakat naendelea kuomba kwa nguvu na ujasiri nkaanza kusikia sauti za paka zinaendelea kusogea mbali na nyumba lakn kitu ambacho kilikuja kunishangaza mpka sasa ni kwamba wakat naendelea kuomba nilianza kusikia vishindo kbsa kwnye bati na nyumba haikuwa na celingboard yaan vile vishindo ni kama mtu akiwa anatembea juu ya bati ikatembea alafu nkasikia hiko kishindo kimetua kama kudondoka nyuma ya chumba changu... nkapata ujasiri wa kukatisha maombi ghafla nkafungua mlango kwenda kuangalia nione hata nyayo.. bt sikuona chochote... Hata siku wife kaumwa na uchungu mida ya jioni mapaka yalilia sana siku hio.. akaenda hosptal akajifungua na alijifungulia pale amana enzi hizo na wakt anajifungua paka alitokea akabeba na kondo lake la nyuma,akatoka salama... tukaendelea kumlea mtt wetu lakn mtt alikuwa anaumwa kila siku mwisho hasa kuharisha na kutapika na tukienda hosptal ugonjwa hauonekani..so mtt alipofika mwaka na miez miwil sku hio hali ya mtt ikiwa dhoofu wazaz wakaomba tupeleke mtt akaugulie huko.. basi nkamwambia wife akapaki akapanda daladala kwenda home.. akiwa kwnye daladala mzee mmoja mwnye mapetepete mengi ya rangirangi na kanzu na kibalaghashia chake akauliza huyu mtt anaonekana anaumwa eeh wife akamjibu ndio.. akamwambia ugonjwa wake sio wa hosptalin bt hakumwelewa alimaanisha nn,kufika home kakaa siku ya kwnza siku ya pili usiku akiwa amelala akaota ndoto wamekuja mmama na kundi lake kavaa kaniki akasema mmalizieni kabiss huyo mtoto afu ndoto ikakatika...kesho yake asbh mie nko mtaani napiga mzgo wife akanipgia simu hali ya mtt imechange na kwl haikupita dk kumi wife akiwa anamnyonyesha mtt akamfia hapohapo... R.I.P katt kangu ka kike first born wangu..


Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana mkuu
 
Nimecheka Kwa nguvu
Haha! Huyo jamaa huwa ananiacha hoi sana! Kuna siku kuna mwanamke alipandisha majini bhana! Wakaja viongozi wa dini kufanya kisomo. Si tulikuwa pembeni tunaangalia picha jinsi linavyokwenda. Yule jini akaanza huyu mwanamke nampenda siwezi kumuacha!

Huyo mshikaji si akanyanyuka bhana akamsogelea huyo mwanamke aliyepandisha majini. Jamaa akaanza; Nyie majini washenzi sana! Kwenu hamna mademu! Unampenda unampenda nani rudi kwenu huko!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom