Chuku chuku
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 873
- 1,360
Ila miji isiyoonekana kwa macho iko mingi sana barani afrika hata ulaya, pengine hawakuchukua idea yao kutoka Gambosh.Huko ndio kuliko wapatia idea Marvel wakatengeneza black panther.
Gambosh=Wakanda. [just saying]
Sent using Jamii Forums mobile app
watu walikuwa wakiamka asubuhi wanakuta hali si hali, na ukikaa kimya anakuja tena. pona yako kuwaambia tu watu kijiwe popobawa kakunaniliu
KubababakeHii ilimtokea Mshiakaji wangu dereva wa lori
Anatoka zake Zambia akavuka Tunduma boda, alipoona yupo Bongo akaenda kuna mahali wanalalaga madereva basi usiku mnene akasikia kama watu wanapita nje akachungulia dirishani akaona kikosi cha WANGA wanawake wako msururu, ile bado anaangalia akamuona mzee mmoja yuko kwa nyuma ndo kama anawa command, basi kufika usawa wa dirisha yule mzee akawa kama kastuka hivi akageuka upande aliko jamaa(jamaa yupo ndani) akaanza kupiga hatua akilifata dirisha, jamaa kuona hivyo akaegesha kama amelala akiskilizia nini kinafuata, Ebana yule mzee alifika akaingiza kichwa kuchungulia ndani bila kufungua dirisha huku mwili wake ukiwa nje na kichwa mpaka usawa wa mabega kaingia ndani, jamaa akakausha mzee akawacheki akaona kama wote wamelala akazepa zake.
Duuh hatari sana....
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Tanga hawafaiii mzeee
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu tanga kusikie hivyo hivyo huko tanga vijijini Kuna vituko ukieleza hapa watu watasema Ni hadithi za kusaidikika.
Sent using Jamii Forums mobile app
Jirani yangu kuna siku alikuwa ananisimulia alikuwa anasafiri na broo wake usiku walikuwa kwenye gari yao. Safari ilivyokuwa inachanganya mbele wakamuona mtu kwa mbali kama anasimamisha gari. Kumuangalia vizuri kumbe ni mwanamke, halafu ni mrembo tu! Dogo akamwambia bro huyu mwanamke atakuwa jini tu haiwezekani usiku huu wote asimame njiani peke yake, tumpite tu.
Brother yake akamwambia usihofu. Akasimamisha gari. Akamwambie ndio mrembo! Yule mwanamke akamwambia naombeni lift nimekwama huu usiku naelekea eneo fulani. Brother yake akamwambia yule mwanamke ingia. Safari inachanja mbuga brother yake akaanza kumwambia yule mwanamke. Inakuaje unatusumbua unasimamisha gari wakati eneo unalotaka kwenda unaouwezo wa kufika?
Yule mwanamke akajibu sielewi unachozungumza. Brother yake akamwambia yule mwanamke, usi' panic! Sisi tuliokupa lift tunajua kwamba wewe ni jini! Ndiyo tunakuuliza kwa nini umetusumbua kusimamisha gari wakati kufika eneo unalotaka uwezo huo unao wewe kama wewe?
Yule mwanamke akawaambia simamisheni gari! Majamaa wakasimamisha. Wakasikia mlango wa siti ya nyuma unafunguliwa. Kugeuka yule mwanamke hawamuoni tena! Brother yake akasema, unatusumbua wakati uwezo wa kufika unao. Wakaendelea na safari.
Nikamuuliza sa mbona huyo jini katumia style ya zamani sana? Jamaa akanijibu, majini ni wapumbavu wapumbavu tu.
kwa kweli story hii, inanihitaji kumtafta mwalimu wangu wa fasihi aliyenifafanulia liwaya ya "joka la mdimu" mpaka nikaelewa, aje anifafanulie na tungo za liwaya hii..Hebu nisimulie hiki kisa changu...
Jumanne 23-08-2019.
Ilikuwa saa nne na nusu usiku nikiwa nimeketi sebuleni,mara gafula mzee akatoka chumbani na kuanza kunitukana matusi ya nguoni...
"Kijana gani wewe kazi kula na kujaza choo,huoni wenzio wanafanya kazi na wanategemewa na wazazi wao...ni bora ningezaa hata mbuzi ningefaidi mchuzi.."
Mara ghafula nashutuka kofi hili hapa sijakaa vizuri ngumi hii hapa,nikasimama imara na kumkazia tu macho...wadogo zangu na mama yangu wakitazama tu pasi na kusema neno.
Nikageuka taratibu na kutoka nje,chozi la uchungu likanitoka ilikuwa ni siku mbili tu toka nifukuzwe shule moja niliyokwenda kuomba ajira ya kujitolea..ati hawawezi kuajiri kiziwi!.
Nilitazama anga jeusi lililosheheni nyota nyingi,mwezi uliotoa nuru angavu nikajiuliza "Mungu upo wapi?".. Nikaingia chumbani na kuvaa viatu.. Nikatoka naenda wapi? Sijui!
Nikaambaa nisijue kama nakanyaga ardhi au ninapaa,napishana na mtu ama kisiki,ilinichukua nusu saa kuuacha mtaa wetu nikaingia mtaa wa pili,huu ulikuwa na watu wachache zaidi na nyumba zilikuwa mbalimbali kiasi.
Nikakatiza pembeni ya makaburi,nikasimama,nikayatazama na kujiuliza " kwanini nisingekuwa nimelala pale? Nipumzike!"...loooh lakini sauti nyingine ikaniambia "una uhakika ukilala pale utapumzika? Nikagutuka nikatazama huku na huko hakuna kiumbe nikaongoza njia kuliacha eneo la makaburi na kuzidi kupotelea mbali zaidi na nyumbani.
Hatimaye nikawasili sehemu pweke,barabara kubwa ya kokoto,kulia na kushoto kukiwa na msitu na vichaka vingi,kiza ni kingi kutupia macho simu yangu ni saa sita na robo usiku!
Ikafika mahali kuna njia panda na upande wa kulia kuna mti mkubwa sana aina ya mbuyu mahali pana pana joto sana bwana,pana joto kali,mapigo ya moyo yakanienda mbio " duuucha dunduncha ducha dunduncha" sasa mapigo niliyasikia hadi masikioni..
Nywele zikanisimama na vipele vya uoga vikanitoka hewa ikawa nzito na uvumilivu ukaniisha na sasa nikatimua mbio hata nilipoliacha eneo lile kwa umbali wa mita mia mbili hivi,na sasa nikaanza kutoka katika makazi ya watu.
Kufika hapa ikanipasa kujiuliza ni wapi naelekea,sikuwa napajua napoelekea kumbukumbu ya misukosuko ya kimaisha na masimango yasiyoisha zikanijia,woga wote ukabiisha donge zito la uchungu,hasira na kukata tamaa likanivaa,machozi yakanitoka,nikashika njia na kuendelea na safari,safari isiyojulikana!
Baada ya mwendo wa dakika ishirini hivi nikaingia katika barabara kubwa ya lami,nikashika uelekeo wa kushoto,ilielekea ufukweni,baada ya masaa mawili hatimaye nikawasili ufukweni,nikazitupia macho hoteli kadhaa zilizotamalaki eneo lile,nikaachana nazo na kushuka mchangani mbali kidogi na mahoteli yale,nikajikalisha kitako na kutafakari nilipotoka,nilupo na ninapoelekea,lakini mbona mbele kyna kiza kizito!
KIZAAZAA!
Hatimaye saa tisa ikawadia,nilichoka,na sasa ilikuwa ni safari ya kurudi,nikajizoa zoa na kushika njia kurudi nyumbani,bahati nzuri barabara hii ilikuwa na taa hivyo ikawa ahueni kwangu.
Baada ya mwendo wa dakika arobaini hivi nikahisi kama kwamba kulikuwa na mtu nyuma yangu,nikageuka kwa kasi, ebo! Nikaona nguo ya rangi ya khaki,aidha gauni au kanzu ikiishia na kufutika machoni kwangu....
Mshtuko uluonipata ukanifanya hata nguvu za miguu ziniishie nikajikuta nikiketi katika mfereji mfupi uliojengwa pembeni ya barabara.
"Ni nini hiki? Ni kweli au ni mawazo yangu tu?" Nikajiuliza,nukatazama huku na huko hali ni shwari,labda niliangalia vibaya bwana nikajizoazoa na kuendelea na safari..
Kiroja kingine tena! Ati nina vivuli viwili,kimoja ni changu na kimoja kimevaa kanzu kama si gauni!(mataa ya barabarani yanawaka hivyo mtu akipita kivuli chake kinaonekana kwa ufasaha kabisa) nikatetemeka kwa woga,nikageuka nyuma ati nacho kikageuka! Nikawa natembea kwa kurudi kinyume nyume,ati nacho kinarudi kinyume nyume!.
Lakini mbona kivuli changu kupo mbele yangu hiki cha nyuma ni cha nani? Na tumeachana umbali wa hatua kama tatu hivi toka kilipo hadi nilipo,nikaona huu sasa utani,nikifa si nife tu ebo! Nikakata shauri kukifuata he! Ati nacho kinageuza kila nikikifuata nacho kinaenda nyuma zaidi,ikabidi nikikimbize sasa..kikapotea.
Nikageuka na kuanza kukimbia kwa taratibu mithiri ya mbio za riadha,nikachoka nikaanza kutembea baada ya mwemdo mrefu kivuli kile kikarudi! Sikusimama nikaendelea kutembea tu.
Hata hivyo nikaanza kuhisi mwili kuchoka sana,miguu inauma na usingizi ni mwingi sana,nikajikalisha juu ya ukingo wa karavati kutafuta pumzi maana ilikuwa ni safari ya masaa mawili zaidi hadi nifike nyumbani...nikaanza kusinzia na hatinaye fahamu zikakomea hapo.
Kelele za watoto wakicheza ndizo zilizonigutusha,nikafumbua macho..afanalek! Nilikuwa nimelala chumbani kwangu..miguu ilikuwa imevimba kiasi na mwili mzima ulikuwa unaniuma...
"Lakini mimi mbona nilikuwa kule barabarani?" Nikajiuliza nisijue kilichotokea,nikaamka na kulibinua bati ninalotumia kama mlango,nikapenyeza kiubavuubavu hadi nje.
Nikawatazama nyusoni niliowakuta nje,wapo kawaida,hawana hata habari,pengine niliokotwa na wasamaria wema! Lakini mbona watu wapo kawaida kama hakuna kitu?...nikashindwa kuvumilia nikaamua kumuuliza mama ni muda gani niliingia kulala!
Akanijibu "we si uliingia kulala saa nne weww? Maswali gani hayo usinisumbue" ni nani aloyenirudisha nyumbani,na kile kivuli ni kiumbe gani? Je ndicho kilichonirudisha nyumbani? Lakini hakijanidhuru, hili ni fumbo niishilo nalo hata sasa kuna wakati natamani kukiona tena kivuli kile kilichovalia kanzu au gauni lililopauka lakini hakitokei tena.
Sent using Jamii Forums mobile app
Daaa nimecheka broo kauzu huyo.Jirani yangu kuna siku alikuwa ananisimulia alikuwa anasafiri na broo wake usiku walikuwa kwenye gari yao. Safari ilivyokuwa inachanganya mbele wakamuona mtu kwa mbali kama anasimamisha gari. Kumuangalia vizuri kumbe ni mwanamke, halafu ni mrembo tu! Dogo akamwambia bro huyu mwanamke atakuwa jini tu haiwezekani usiku huu wote asimame njiani peke yake, tumpite tu.
Brother yake akamwambia usihofu. Akasimamisha gari. Akamwambie ndio mrembo! Yule mwanamke akamwambia naombeni lift nimekwama huu usiku naelekea eneo fulani. Brother yake akamwambia yule mwanamke ingia. Safari inachanja mbuga brother yake akaanza kumwambia yule mwanamke. Inakuaje unatusumbua unasimamisha gari wakati eneo unalotaka kwenda unaouwezo wa kufika?
Yule mwanamke akajibu sielewi unachozungumza. Brother yake akamwambia yule mwanamke, usi' panic! Sisi tuliokupa lift tunajua kwamba wewe ni jini! Ndiyo tunakuuliza kwa nini umetusumbua kusimamisha gari wakati kufika eneo unalotaka uwezo huo unao wewe kama wewe?
Yule mwanamke akawaambia simamisheni gari! Majamaa wakasimamisha. Wakasikia mlango wa siti ya nyuma unafunguliwa. Kugeuka yule mwanamke hawamuoni tena! Brother yake akasema, unatusumbua wakati uwezo wa kufika unao. Wakaendelea na safari.
Nikamuuliza sa mbona huyo jini katumia style ya zamani sana? Jamaa akanijibu, majini ni wapumbavu wapumbavu tu.
Kumbe tupo wengi? Safi sana.Mimi afro ndo style yangu
Haha! Huyo jamaa huwa ananiacha hoi sana! Kuna siku kuna mwanamke alipandisha majini bhana! Wakaja viongozi wa dini kufanya kisomo. Si tulikuwa pembeni tunaangalia picha jinsi linavyokwenda. Yule jini akaanza huyu mwanamke nampenda siwezi kumuacha!Nimecheka mpk Bia imenipalia!
Huyo jini alikuwa bado mwanafunzi
Wakanda Marvel wanasema ni mji wakufikirika uliopo Afrika MasharikiIla miji isiyoonekana kwa macho iko mingi sana barani afrika hata ulaya, pengine hawakuchukua idea yao kutoka Gambosh.
Yeah, ni mji wa kusadikikaWakanda Marvel wanasema ni mji wakufikirika uliopo Afrika Mashariki
Sent using Jamii Forums mobile app
Msalimie mkeoSikuwahi shuhudia live uchawi ila niliwahi shuhudia matukio mengi ya kichawi...
Miaka 2007 hadi 9 niliinshi nyumba moja magomeni mikumi karibu na bondeni kule kwa mzee mmoja wanamuita Fungo,
Nikiamka usiku wa manane naenda kukojoa naskia ngoma inachezwa sebuleni kwao waliishi nyumba kubwa mimi chumba cha nje na hiyo ilikua mara nyingi sana kuskia hata ikitokea nikishtuka usingizini naskia wakiimba, kupiga ngoma na kucheza.
Siku nkapanga safari kwenda kusalimia kijijini ikabidi nikubaliane na mzee alale chumbani kwangu maana kulikua na wezi sana miaka hiyo,
Baada ya wiki kurudi nkakuta kapeti limechanwa chanwa sanaaaaa na ni maeneo yale yanayokanyagwa tu, na vipande vimejazana huko chini kibao,
Hata sikuuliza kwa mazingira niliyoyaona nkajua tu ngoma ilihamia gheto kwangu na watakua wanavaa viatu vyenye ncha kali ndio maana wakalichana vile..
Lakini cha ajabu matukio yote hayo sikuwahi kua na hofu hata chembe hata sijui kwanini...
Kuna nyumba tulipanga maeneo ya sinza mapambano, mara nyingi tu mke wangu huona watu wako uchi aidha nje wakichungilia dirishani na wengine wapo chumbani kwetu, na hapo yule macho live, lakini hata anaponiadidhia wala sipati hofu yoyote, hua naona kawaida tu, sijui ni kwanini.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kulaleki yaani nilale then fala mmoja aje kunichoma na kiginga ch moto kwenye makalio?
Pole sana mkuuMimi nilikuwa siamini hizo mambo lakn kipind cha wife ana ujauzito wa mtt wetu wa kwanza.. nikiwa mchanga kbsa kiimani,siku hio nakumbuka tumelala tukaota ndoto moja mm na wife.. ndoto ilikuwa ni mmama mmoja anasema anataka mtt alieko tumboni ili amtoe kafara,tukashtuka.. baada ya kushtuka tukasikia mipaka inalia nyuma ya nyumba kwa sauti kubwa,nilikuwa nmeshafundishwa kuomba na kukemea.. asee niliomba sana usiku huo kwa ujasiri na nguvu maana wife yeye muda huo alikuwa analalamika tumbo linamuuma na mtt alikuwa anarukaruka hatar tumboni... wakat naendelea kuomba kwa nguvu na ujasiri nkaanza kusikia sauti za paka zinaendelea kusogea mbali na nyumba lakn kitu ambacho kilikuja kunishangaza mpka sasa ni kwamba wakat naendelea kuomba nilianza kusikia vishindo kbsa kwnye bati na nyumba haikuwa na celingboard yaan vile vishindo ni kama mtu akiwa anatembea juu ya bati ikatembea alafu nkasikia hiko kishindo kimetua kama kudondoka nyuma ya chumba changu... nkapata ujasiri wa kukatisha maombi ghafla nkafungua mlango kwenda kuangalia nione hata nyayo.. bt sikuona chochote... Hata siku wife kaumwa na uchungu mida ya jioni mapaka yalilia sana siku hio.. akaenda hosptal akajifungua na alijifungulia pale amana enzi hizo na wakt anajifungua paka alitokea akabeba na kondo lake la nyuma,akatoka salama... tukaendelea kumlea mtt wetu lakn mtt alikuwa anaumwa kila siku mwisho hasa kuharisha na kutapika na tukienda hosptal ugonjwa hauonekani..so mtt alipofika mwaka na miez miwil sku hio hali ya mtt ikiwa dhoofu wazaz wakaomba tupeleke mtt akaugulie huko.. basi nkamwambia wife akapaki akapanda daladala kwenda home.. akiwa kwnye daladala mzee mmoja mwnye mapetepete mengi ya rangirangi na kanzu na kibalaghashia chake akauliza huyu mtt anaonekana anaumwa eeh wife akamjibu ndio.. akamwambia ugonjwa wake sio wa hosptalin bt hakumwelewa alimaanisha nn,kufika home kakaa siku ya kwnza siku ya pili usiku akiwa amelala akaota ndoto wamekuja mmama na kundi lake kavaa kaniki akasema mmalizieni kabiss huyo mtoto afu ndoto ikakatika...kesho yake asbh mie nko mtaani napiga mzgo wife akanipgia simu hali ya mtt imechange na kwl haikupita dk kumi wife akiwa anamnyonyesha mtt akamfia hapohapo... R.I.P katt kangu ka kike first born wangu..
Sent using Jamii Forums mobile app
alama nlobaki nayo mpka leo ya yule dubwana
inshort wengi humu wanasema sjui hakuna uchawi huwa nawaangalia tu but kwa yaliyonikuta nikikuhis hata unatembea na hiriz mfkoni hata kama ndgu yngu hutoniona tena maishan mwakoView attachment 1303100
Sent using Jamii Forums mobile app
Haha! Huyo jamaa huwa ananiacha hoi sana! Kuna siku kuna mwanamke alipandisha majini bhana! Wakaja viongozi wa dini kufanya kisomo. Si tulikuwa pembeni tunaangalia picha jinsi linavyokwenda. Yule jini akaanza huyu mwanamke nampenda siwezi kumuacha!
Huyo mshikaji si akanyanyuka bhana akamsogelea huyo mwanamke aliyepandisha majini. Jamaa akaanza; Nyie majini washenzi sana! Kwenu hamna mademu! Unampenda unampenda nani rudi kwenu huko!
Ni nguvu za giza,hapo zinahusika,Kuna simulizi kuhusu popobawa alikua anafukua mtaro watu usiku wakilala,je hao walikua wanafukuliwaje?Kulaleki yaani nilale then fala mmoja aje kunichoma na kiginga ch moto kwenye makalio?
Sent using Jamii Forums mobile app