Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]mbwa ni snitch alienda kupeleleza
kuna tukio lilitokea mkoa wa Rukwa wilaya na kijiji X.

watu wa kijiji hicho huwa jumapili wanapumzika kazi za shamba wanaenda kanisani kwani kijiji na mashamba yalipo kuna umbali na watu wengine wanalala huko huko kuna nyumba za muda ila jumapili wote wanakuwa kijijini.
basi kuna mama mmoja siku ya jumapili alikuwa anaenda shamba kuchuma mboga za majani, ili ufike shambani kuna msitu unapita. Wakati anakaribia kufika ule msitu akapishana na mbwa akiwa kasi anaelekea njia ya kijijini lakini yeye hakumjali kwani mbwa si kitu cha ajabu kwa kijijini.

akiwa anaendelea na safari yake katikati ya msitu akamuona mtu amekaa kwenye gogo akamsalimia na kuendelea na safari yake, kapiga hatua tatu akasikia yule mtu anamuita jina lake akageuka ili amuaangilie vizuri lakini kila akimuangalia yule mtu sura yake ikawa haileweki kama vile mtu anayejitazama kwenye kioo chenye ukungu.
yule mtu akaanza kumuuliza maswali yule mama:

mtu: huku akimtaja jina, unaenda wap?

mama:shambani.

mtu: kufanya nini?

mama: kutafuta mboga za majani.

mtu: wale samaki aliokuletea D kwa nini hujapika wale.

yule mama alishangaa jinsi alivyomuelezea mambo ya nyumbani kwake lakini akataka kumpuuza ili na safari lakini yule mtu alimwita tena safari hii kwa ukali, yule mama alipogeuka akashangaa baada ya kumuona yule mtu kawa wa ajabu zaidi kuliko mwanzo kwani sasa hata miguu yake utafikiri ni mtu anayeelea angani na sura isiyoeleweka kama ni mwanamke au mwanaume.

yule mtu akamuamuru yule mama kurudi alikotoka haraka huku akimwambia kwamba una bahati sana Leo. yule mama kwa hofu huku akitetemeka akaanza kukimbia kurudi kijijini kufika mwanzo wa msitu akapishana tena na yule mbwa akiwa kasi anarudi msituni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiranga tupe maelezo ya kisayansi hapa
Screenshot_20200109-075236.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahah mkuu hizi zipo sana,ila mara nyingi ni misukule. Unaweza agiza msosi ukitoa mkona na yeye anachota. Yaan ni jino kwa jino hadi mnashiba wote.
Kuna jamaa alitoka Jijini DSM, kwenda kusalimia kwao kijiji x, alipofika akaona aingie mahali apunguze uchovu kwa kupiga pombe ya kienyeji ya kwao huko,basi kulikua kuna wazee pembeni wamekaa na wao wanakula ugimbi, akawasalimia freshi akaagiza na yeye chupa yake, kati ya wale wazee akamwita kijana kwa jina lake maana ni kijana aliekulia kijiji hichohicho akamwomba awanunulie na wao angalau chupa mojamoja, si unajua ukitoka Town,kijiji kinaamini unahela. Dogo akaona wasimzengue yani yeye hajafika hata home kuwatoa wazazi wale wazee wanataka kumtoa upepo mapema, jamaa akawajibu hana kitu,mzee akamuuliza kweli mwanangu then kila mtu akaendelea na hamsini zake, dogo kueka chupa mdomoni hamna pombe akajua labda alijichanganya atakua alishamaliza, akaita chupa ya pili nayo akionja kidogo, akinywa mara ya pili mzigo empty haha haha.. Ilibidi awahi home bila Kuaga

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nina chapter mbili (2), moja ya kwangu ma ya pili ni ya baba yangu,
Nitaanza na yangu mwenyewe..
Mwaka 2016 nikiwa na umri wa kati tu usio na tija kuwa mme wa mtu, ila kutokana na misukumo na vishawishi vya barehe ikanibidi nivute kibinti cha kiislam, kutokana na kuwa nilikuwa mpambanaji wazazi wake waliniamini na kunipa mtoto wao japo sikuwa na kigezo hata cha kuoa wakati ule (20+ yrs only) sasa basi baada kufanya process zote ilibidi niowe kiislam kutokana na kuwa waslam hawana mambo mengi(mimi sio muislam wala sina mpango wa kuwa), yaani wao hata mkiwa watu 10 ndoa inatamadadi na kukwishineyi...sasa wakati ule wa binti kuvundikwa baadhi ya wenyeji, dungu&jamaa walianza kumletea zawadi za hapa na pale, baadae ndoa ilifungwa na maisha ya ndoa yakaanza rasmi, sasa kimbembe kilianza baada ya yeye kutoka kwao tu, yaani binti yule akawa mgumu kutoa papuchi ilihali alinipenda mwanzo na alilia ndoa kwa udi na uvumba sasa nikawa najiuliza huyu vipi, ama ananiectia..basi kwa akili zangu za ujana ujana nikawa na-force game, kisha kibishi namaliza ila alikuwa analia sana kana kwamba alifosiwa kuolewa..
Baada ya zile siku saba za mwanzo baada ya ndoa (honey moon) huko kijijini kwetu, tukawa tumejisogeza maghetto kwangu ili tuyaanze maisha yetu wenyewe, sasa hapo ndipo picha lilianza yaani binti kuanzia asubuhi-saa12 mzima kabisa yaani yupo shwari kimbembe ni ile kigiza cha usoni kikianza kuingia yaani alikuwa mwehu kabisa, sasa nikaanza kujiuliza hii imekaaje ama ndio mke ana act ili asitoe mchezo, basi ikabidi nitoe taarifa ukweni maana hali ifikia pabaya sana,
Sasa wakawa wameniambia kuwa jambo hili linavinasaba vya kishirikina, kwa upande wangu sikuamini hata kidogo, sasa bibi wa mke wangu mzaa mama mkwe alikuwa ni mrokole kindakindaki, basi wakawa wame- organize mama&bibi ili mtoto wao atibiwe hayo maswaibu..basi bana siku hiyo nakumbuka niko zangu ghetto sina hamu hata kidogo na ile ndoa si mama mtu akaja na yule Bibi akiwa na wenzake na mama zake wadogo, mama mkwe na wadogo zake ilibidi wabaki nje kutokana na kulinda itifaki ya kutoingia chumba cha mkwilima wake,
Wakawa wametutaka siye wanandoa tupige magoti ili ombi lianze humo humo ghetto, mwanzoni me nilikuwa na- take easy tu nahisi kama vile movie za kibongo, lakini baada ya ombi kukolea nikamuona wife kaanza kupiga mwano, wakabidi wakomae nae me nipo nacheck tu (ilibidi nifumbue macho[emoji16]) ombi likawa ombi daaah mara mtu chini wapo nae tu, mara wakaanza kuyahoji majini baada ya yule binti kuanza kusema mtuache, mnatuchoma..sasa hapo me siamini tu baada ya kuzungumza nayo yakawa yamesema kuwa pindi binti yule anafundwa ndani siku zile za kuvumdikwa kuna mtu alimpea under wear (chupi) kupitia kwa mdogo wake, yeye pasina kujali akawa kaivaa, na ndipo yalianza maswaibu..me bado hapo sina imani tu na kile kinachoendelea, baadae kabisa baada ya ombi kukolea yule binti akaanza kutema nyama nyama kama stake hivi ila zipo mithiri ya damu iliyoganda, wakachukua mtandio wake wakaanza kumtoa zile nyama mdomoni pia alikuwa anatafuna meno kiasi kwamba unasisimuka kama mtu anae sugua sifuria, hapo sasa ndio nikaanza kupata imani kuwa kweli binti yule ana jambo tena kubwa tu, baada ya ombi kumchek yule binti mdomoni nilishangaa hakuwa na jeraha wala kovu ambalo lilisababisha kutoa nyama zile tena zimejaa kwenye mtandio wake wa kiislam..mzee nilidata mpaka nikakoma na kimbelembele changu cha kuyakimbilia mapenzi,
Baada ya ombi lile tukawa kama temeyaamsha, na siku zilizofuata ndio kikawa kimbembe zaidi ya mwanzo, maana kuna usemi unadai kuwa kama wewe umeombewa na kutokwa na majini basi unatakiwa uishike imani sana sana laasivyo huwa yakitoka 10 yanarudi 20 it means (2x2), sasa sisi tuka- take easy kabisa, yaani majanga yalizidi mpaka kufikia hatua ndoa kuota mbawa ndani ya mwezi mmoja tu(mpaka sasa nipo single, na sina hamu kabisa ya kuwa na mke).
Yaani yule binti alipoteaga, wazazi wake waliuza nyumba ili kumtafuta binti yao kwa wataalamu, walimpata baadaya ya mwaka mmoja (2017) ila waliyumba sana kiuchumi na kuhama mji waliokuwa wanaishi na kwenda kwingine kuanzisha maisha tena ya upangaji, baba mkwe wangu na baba yake mzazi mpaka leo hawasemshani maana ktk jopo lililohusika na hizo inshu pia mke mdogo wa huyu babu wa mke wangu alihusika sana, pia huyu babu hakuwahi kusimama kumtetea mjukuu wake wakati wote alisema kuwa mkewe anasingiziwa huenda ni kutokana na limbwata ama juju alilopewa na huyo mke wake

NB: pia kipindi tunamuuguza mke wangu tuliwahi kwenda kutibiwa kwa mmoja wa bibi zake wa ukoo tukiwa huko, me nyege zikanizidi ikabidi nimuombe show wife maana tulilala kitanda kimoja, alivyogoma kutoa mechi ikabidi nitumie force maana nilikuwa na kama wiki kadhaa pasipo kufanya chochote kwake na isitoshe kwa wakati huu alikuwa keshapona(hapandwi na majini wala hakuwa kichaa), yule bibi alituachia room ambayo ilikuwa ndio kilinge chake, Aiseee nakumbuka wakati na-force kuchojoa chupi nae hayumo kelele zikawa kibao wakati huo ni kama saa11 alfajiri, mara paaap nasikia sauti kwenye angle ya kuta ikisema shiiiiiiiiii, daah nilitoka nje nikiwa na boxer yangu tu hapo nipo kifua wazi nikamfuata yule bibi akaniambia nitulie tu nikiwa ndani maana kilingeni huwa hakuhitaji makelele, sikuomba match tena wala sikusinzia mpaka kunapambazuka kisha nikasepa zangu kurudi mjini..[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah wadau mna mikasa, sema kipururu nacho noma sanaa[emoji38][emoji38][emoji38]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ha haa huyo kweli Mwamba,,yuko ap asee?
Haha! Huyo jamaa huwa ananiacha hoi sana! Kuna siku kuna mwanamke alipandisha majini bhana! Wakaja viongozi wa dini kufanya kisomo. Si tulikuwa pembeni tunaangalia picha jinsi linavyokwenda. Yule jini akaanza huyu mwanamke nampenda siwezi kumuacha!

Huyo mshikaji si akanyanyuka bhana akamsogelea huyo mwanamke aliyepandisha majini. Jamaa akaanza; Nyie majini washenzi sana! Kwenu hamna mademu! Unampenda unampenda nani rudi kwenu huko!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimecheka sana,ameanzisha Uzi gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
Haaaaa 😂 😂 subiri kidogo ntakutag eti jitu linaanzisha uzi ili watu wachangie sasa ukimkosoa linaporomosha shombo za dagaa, sasa kwenye uzi kabaki mwenyewe kama mchawi kachoka kaukimbia na yeye mwenyewe 😂😂😂😂
 
Nina nyuzi nyingi mkuu kama hivi yaani





Beware unaingizwa kwenye bifu la upande mmoja. Huyo chizi wala sijishughulishi kumjibu(eti uzi umedoda ila kutwa yupo mule kuinjoi tamu za numbie)
Nimecheka sana,ameanzisha Uzi gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahahahh savage!!![emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kahawa kidogo [emoji23][emoji23][emoji23]

I remember back in the days in the village when i used to trick boda guys..because our house was close to a cemetery.Once i climbed the bike i would stuff my nostrils with cottonwool without him knowing. Then when we got infront of the cemetery i would scare him and he would run for his life! On this fateful day, i boarded the bike as usual and stuffed my nostrils with cottonwool.when we got to the cemetry i scared him but this time he just stared at me.I danced all the ghost songs i know..but he didnt even move.I even spoke pidgin "oga..you no dey fear ghost!?" nothing happened.He got up and held my shirt "nipatie pesa zangu mjinga ii" I begged the guy to calm down and let me get it for him..i went into the cemetry as he held my shirt and followed me.As i was walking..i jokingly knelt down on a grave and knocked on it "Habari..nsaidie na 200 nipatie hii ghasia iniachilie" i thought this would scare the guy..but nothing! kidogo kidogo a hand stretched out from the grave holding 200/- note "chukua hii na unirudishie ukipata" My brothers and sisters..to date..i still dont know who carried who between me and the bikeman out of that cemetry.ile kitu nakumbuka tu ni nilijipata juu ya pikipiki at a neighbouring town.As for the bikeman sijui alienda wapi..i still have the bike parked at home [emoji23][emoji23].whenever i pass by that place,i always see my one pair of gucci shoe that fell off as i was running [emoji23].It is not that i cannot go and get it oooo...just that i dont like gucci stuff anymore.Infact..i dont like shoes again!! [emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787]
Happy 2020 Fam!!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akitokea mtu anasema uchawi haupo walahi nitamuona ni mjinga wa millennia

Mwaka 2014 huko GEITA ktk mji wa katoro ktk shule inayojulikana kwa jina la Lutozo S/M kuna inshu za kishirikina zilijitokeza bayana pasipo chenga wala nini..ilikuwa hivi majira ya saa2 asubuhi baadhi ya wanafunzi waliokuwa wanaenda toilet walitoka kule kwa kupiga yowe na kudai kuwa kuna miswaki inaongea, jambo lile lilifika ktk uongozi wa shule lakini walipuuza kwa kudhani ni story za kitoto tu, lakini kufikia mida ya saa4 (break) miswaki ile ilikuwa inapiga kelele mithiri ya kwamba kuna gulio vile, baada ya hapo uongozi wa shule pamoja na wanafunzi wote waliongozana hadi choo cha shule, sasa kuna madame mmoja jina lake sefroser (aliwahi kuwa mwalimu wangu wa dalasa nikiwa la 4) alijitia kimbelembele aiseee akashika zile miswaki akazitia ktk moto zikaungua kabisa, kufikia kesho yake tu yule Madame aliaga dunia..R.I.P Madame sefroser.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Effects za uchawi ni zipi, na unajuaje hizi ni effects za uchawi tu, si kitu kingine chochote, ikiwa hata kuu define uchawi huwezi?
Unachekesha sana. Naomba nikuache na imani yako, wewe akili ulishaifunga sehemu moja na hutaki kuchunguza mengine. Haya, hakuna uchawi. Umefurahi sasa!
 
Back
Top Bottom