Mirlz B Matthew
JF-Expert Member
- Oct 10, 2011
- 2,212
- 3,093
kile kipande chote kuanzia ushirombo mpaka nyakanazi kina mambo ya ajabu ajabu sana hasa mchana kipindi cha mvua na usiku mneneNorshad kwa io uyo jini alikutokea kabla ya pale wanapochimba madini (council) au?Hapo Runzewe wasumbwa Wana balaa Sana!....
Ni hatari Sana...Kuna shule ipo strabag pale kwa pembeni....Kila siku usiku Kuna jiwe linatembea na walimu wanafundisha usiku bila wao kujitambua!Dunia Ina mengi hii!kile kipande chote kuanzia ushirombo mpaka nyakanazi kina mambo ya ajabu ajabu sana hasa mchana kipindi cha mvua na usiku mnene
Kushabikia ushirikina ni njaa za ukooo na umaskini wa fkira.
Sent using mijikamimi
DuhMiaka mingi nyuma wakati nipo kanda ya ziwa. Timu yetu ya mtaa ilifanikiwa kuingia nusu fainali ya kombe la wilaya. Kutokana na kuwahofia wapinzani wetu, tukashauriana twende kwa mganga. Tulipofika nakumuelezea shida zetu, akatwambia kamateni yule kuku pale (kulikuwa na kuku wanakula kula pale nje kwa mganga).
Tulikamata kuku jike, mwenye madoa doa kama kanga. Mganga akaongea maneno yake pale, alaf akamchinja. Yule kuku hakutoa damu hata kidogo, mganga akashtuka. Alivyompasua ndani akakuta vitu vyote kuanzia figo, maini, moyo, utumbo n.k vimeoza. Palepale mganga akatwambia nendeni tu mkakamilishe ratiba vijana wangu wenzenu wameshawawahi.
Ile mechi tulipigwa 5-1.
Sent using Jamii Forums mobile app
ngoja tu nimalizie kisa changu kingine,but huwa nikimsikia mtu anasema uchawi hakuna namwangalia na kutikisa kichwa tu.
Nimezaliwa na mama ambae ni mgonjwa wa sicle cell hali iliyokuwa inamfanya mama yangu kuumwa mara kwa mara hasa mifupa na hata kuishiwa damu mara kwa mara naweza kusema mama yangu haikuwahi kupita week bila ya kuumwa au kulazwa hospitali,hali iliyopelekea kuwa anatumia mara kwa mara dawa za valium na hata wakati mwengine kuwa anajichoma mwenyewe sindano za valium ili apunguze maumivu apate usingizi,ilikuwa ni usiku wa saa 8 usiku nimelala na bimkubwa naskia anaugulia maumivu makali mno ya mifupa,nikaanza kutafuta dawa hakuna sindano wala vidonge na nyumba tulikuwa mimi na yeye tu wakati huo simu ni anasa na usafiri huu wa boda boda hakuna na gari ilikuwa saa 4 mwisho, basi kila akiugulia maumivu akili yangu inahangaika mwisho wa siku nikamchukua nikamuweka mgongoni kulikuwa kuna dispensari fulani hvi ipo kigoma ujiji na sisi wakati huo tunakaa bimala kwa wenyeji wa kigoma wanakujua ni umbali wa kama dakika 10 kwa gari,basi nikamuweka mama yangu mgongoni safari ikaanza wakati huo nina umri wa miaka 12 tu,tembea sana kila nikiskia anazidi kuugumia na mm ndo naongeza spidi,basi tukafika sehemu moja inaitwa shine cinema ni ukumbi fulani hivi walikuwa wanaonyesha movies na pembeni kuna shule ya msingi ujiji, baada ya kufika pale ile shule tuliona imegeuka treni watu wanashuka na kupanda wakati huo upande wa pili kwenye ule ukumbi kwa nje tukaona watu wengi mno wapo nje wanapiga kelele mno wanasherehekea wako uchi wa mnyama wanauza vichwa vya watu ulimi na viungo vingne vya binadamu na kulikuwa kunanuka damu kweli kweli cha ajabu ajabu kufika pale nikashikwa na bumbuwazi kiasi cha kanga kulegea bimkubwa akaanguka lakini kwa kusimama sasa alivyofungua macho kuona kilichopo mbele yetu nilishangaa tu amenibeba juu alitoka mbio za ajabu huku akiwa amenibeba mgongoni mpaka ujiji kwenye ile dispensary alivyofika tu akazimia pale pale nakumbuka alikuja kuzinduka siku ya tatu na mtu wa kwanza kuniita alivyoamka tu nilikuwa mimi alinikumbatia na kuanza kulia sana(kisha akanitamkia nimekusamehe leo na siku zote za maisha yako) kauli hii aliirudia akiwa anafariki ndani ya mikono yangu mwaka 2007 kwa kunambia(nakufa mwanangu nakupenda sana na nakufa nikiwa radhi nawe uishi maisha ya kumpendeza mungu na uwapenda nduguzo kama ulivyokuwa unanipenda mama yako)
R.I.P my beloved mom
Sent using Jamii Forums mobile app
Njoo Buza nikupe chumba cha uhani utakaa miezi 6 bureKwanza nianze kwa kuwaomba radhi kwa maelezo marefu ya huu mkasa
Niliandika mara yakwanza sijui nni kikatokea simu ikawa imehome njee kabisa ya aplication cjui nini kilisababisha
Basi bandugu acha namimi niendelee kutoa mikasa ambayo nimekumbana nayo hiii ni post ya 3 nadhani
Nakumbuka kuna nyumaba niliwahi kupanga maeneo ya kigogo jijini Dar, asa wakati naishi pale nikawa nakumbwa na mambo mengi sana ikiwemo mikosi ya hapa na pale homa zisizo na kichwa wala miguu yaani kwakifupi mpaka afya yangu ukazota.
Siku moja alikuja rafiki yangu mmoja hivi kisha nikamueleza matatizo yanayonikumba jamaa akaishia kunipa pole tuu
Basi yule jamaa akaniambia leo nataka kulala hapa gheto kwako kwani cna nauli nikasema poa hatimae giza liliingia ilipofika mida ya saa2 yule yule jamaa alitangulia kulala basi mi nikawa naangalia Tv kwa bimkubwa
Hatimae nilirudi majira ya saa 5 usiku nikamkuta yule jamaa yupo macho ile cjakaa sawa yule jamaa akaniambia kaa chini nikueleze kilichotokea, akaniambia ebhana huyu baba ambae ni ostazi nimemuona anaingia humu ndani yeye na mwanae wa kiume tena waliingilia hapo kwenye kona ila kwakua nimewaona kwenye usingizi niliwatukana kisha wakapotea
Jamaa akaniambia hata hayo matatizo uliyonieleza nahisi nihuyu anaku7bishia aisee ckuamini
Ostazi ambaye kila ikifika jion anaswalisha watoto wake, yaani me nasema hakuna atakae iona pepo mwisho wa Dunia
Basi tulilala me najamaa ingawa yule ostaz hakua na maelewano mazuri na jamaa yangu kwani hata salam akawa anaipokea kinyonge sana kitendo kilichopelekea yule jamaa kukata kabisa kuja pale
Siku zilienda huku nikindelea kuteswa ikifika usiku, na mimi uwezo wa kuhama nikAwa sina kwani mlipa kodi alikua nibimkubwa basi nikaendelea kukomaa palepale
Cku moja nakumbuaka nilikua naangalia Tv ndipo nikamuona jamaa mmoja anaelezea dawa ya mkunazi jinsi ilivyo na uwezo na ktk maelezo yake alisema inauwezo wa kuzuia nguvu za giza na kuondoa mikosi ya hapa na pale
Ikabidi nimvutie waya nijue anauzaje na anapatikana wapi akanipa maelekezo theni nikamuibukia alikua anakaa maeneo ya mbagara kwa Azizi Alli
Hatimae nilifanikiwa kununua ile Dawa nilipo rudi nyumbani nilifuata maelekezo kama alivyoniambia,
Basi nilichanganya kwenye maji ile dawa nyingine nikawa nakunywa nyingine naogea kuondoa mikosi nikachukua nyingine nikamwaga kwenye kona kona mle chumbani kwangu
Hatimae giza liliingia nakumbuka siku hiyo nilala mapema tuu kwani nilikuwa najickia vbaya , asa ilipofika mishale ya saa 7 nikashtuka nikaona mlangoni kunamwanga mkali uliombatana na kishindo nilivyozidi kuamka nikawa naona mtu anakimbia kuelekea Chooni huku kakishikilia kile kifaa kilichokua kinang'aa
Basi baada ya muda fulani nikasikia anarudi kutoka kule chooni na round hii hakua na kile kitu, akafka mpaka pale mlangoni akasimama asa me nikasonya manaake nasikia mchawi na sonyo ni vitu viwili tofauti, aisee alikimbia mpaka ndani kwake
Kumbuka hiyo inaelekea saa8, basi nikatoka nje moja kwa moja nikaelekea chumba cha ndg wa yule ostaz mchawi nkabisha hodi theni jamaa akafungua
Nikamuhadisia, akasema hivyo vitu vpo na sikwamba havipo vipo sana na namjua anae fanya hivi, pia jamaa akaniambia yeye mwenyewe kuna kipindi ilikuwa ikifika jioni kuna kiumbe kinakuja juu ya paa lake na kinaanza kufagia mara michanga inamwagwa juu ya paa lake
Jamaa mwishowe akanishuri niende kwa mama yao ambae anishi kinondoni nikamsemee kwa vtendo anavyonifanyia ila mimi nimamwambia acha tuu kwani nimapito Ya Dunia
Basi yule jamaa akaniamabia nenda kalale kwani usiku ulikua mwingi mnoo nakumbuka ilikua saa9 nikafanya hivyo
Kumbe yale mazungumzo mimi na mdogo wake yule ostazi mchawi aliyasikia hivyo akafanya kila njia akatufarakanisha, siyo siri hali ikawa tofauti kwa jamaa kwa jinsi nilivyo mzoea, mara nikawa nikimueleza kitu yule jamaa anashout tena unakuta ananiambia chukulia kawaida hayo mambo ikaenda yule jamaa kanigeuzia mimi kibao nikawa naonekana mimi ndiyo mchawi pale mtaani
Hali ilienda hivyo hatimaye hata yale madawa niliyoweka kama zindiko akaharibu yakawa hayana nguvu tena hivyo akawa ananitesa balaaa
Akawa anafanya juu chini ili aniue kwani nilishajua siri zake hiyo hali iliendelea mara nikawa naota mindoto ya ajabu ajabu
Bimkubwa naye nikawa namwambia lakini akawa ananiambia yeye hana hela ya kunipa ili nihame kwani biashara zake zilikua haziendi vzuri
Siyo siri wachawi wanaroho za kikatili sana hawana huruma na ukiwa hauna kinga wanakuonea sana..........
Sent using Jamii Forums mobile app
Miaka mingi nyuma wakati nipo kanda ya ziwa. Timu yetu ya mtaa ilifanikiwa kuingia nusu fainali ya kombe la wilaya. Kutokana na kuwahofia wapinzani wetu, tukashauriana twende kwa mganga. Tulipofika nakumuelezea shida zetu, akatwambia kamateni yule kuku pale (kulikuwa na kuku wanakula kula pale nje kwa mganga).
Tulikamata kuku jike, mwenye madoa doa kama kanga. Mganga akaongea maneno yake pale, alaf akamchinja. Yule kuku hakutoa damu hata kidogo, mganga akashtuka. Alivyompasua ndani akakuta vitu vyote kuanzia figo, maini, moyo, utumbo n.k vimeoza. Palepale mganga akatwambia nendeni tu mkakamilishe ratiba vijana wangu wenzenu wameshawawahi.
Ile mechi tulipigwa 5-1.
Sent using Jamii Forums mobile app
Shukuru hujakutana na mikasa nasiyo kwamba tuliomba tukutane nayoDuuu dunia ina mikasa hii
Mbona sijasema kibaya ndugu haya poleShukuru hujakutana na mikasa nasiyo kwamba tuliomba tukutane nayo
Sent using Jamii Forums mobile app
Sijui kama umeelewa jina na lengo la uzi?Kushabikia ushirikina ni njaa za ukooo na umaskini wa fkira.
Sent using mijikamimi
Nikiwa na miaka Tisa ya ndoa yangu sikuwahi dhani wala kujua wife ni mchawi maana alikuwa msomi wa juu sana na mtu wa kanisa sana.siku moja nikiwa nimelala ulivuma upepo mkali mno gafla nikiwa macho nikajikuta nanyanyuliwa juu aisee nilisali sala zote gafla nikarudishwa chini.Kuangalia pembeni yangu alipolala mwenzangu naona mbwa aisee ulikuja kama usingizi hivi sekunde wife akarudi ktk hali yake ya ubinaadamu.Kesho yake nikahama home na ndoa ikafa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kiranga, Nakuuliza,Ulishawahi kufanya tafiti yoyote kuhusiana na existing ya uchawi?
Sent using Jamii Forums mobile app
Mara nyingi Ni michezo ya wanga kukusumbua kusumbua tu.Hii ya kua macho halafu naona nanyuliliwa juu kwa kuvutwa na kitu kisichoonekana imeshanitokea mara mbili sitakaa nisahau, uwa ninasali sala zote mkuu
Ulikutana navyo eneo gani la same secindari?Nlikutana na vibwengo laivu bila chenga...nikiwa same secondary...aisee usiombe ukutane na Hawa jamaa...
Sent using Jamii Forums mobile app