Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

2010 nipo ndani ya fuso, natokea Ifakara kwenda dsm. Kufika Maseyu mida kama saa 8 usiku dereva akapaki, akasema amechoka anapumzika kidogo. Akatuambia saa 10 tumwamshe tuanze safari.

Sijui kama ni uchawi au ni nini, tulipitiwa na usingizi mzito, na wote, tulikuwa watatu tuliota ndoto ya aina moja. TUNAPIGA MECHI. tumejipiga mabao wote, kuangali saa ni dk 20 tu zimepita. Nilichowaeleza wenzangu ndio walichoota. Mwanamke niloyeota namgonga ndio huyo huyo wenzangu walikuwa wakiota wanamgona.

Niliota vipele vya baridi kwa uoga. Tukaondoka kuendelea na safari. Tangu siku hiyo sipandi tena malori ya mzigo yanayosafiri usiku.



Sent from my SM-G570F using Tapatalk
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uchawi ni kweli Upo, Nikiwa Nimeenda Kurudia Shule Baada ya kukosa Nafasi ya kujiunga Form One 1994..Baba yangu Mkubwa..Tumbo moja na Baba Alikuwa anafundisha Shule ya Msingi Nyabhutanga Jimbo La Buchosa wilaya ya Sengerema 1990--1995.. Mzee wangu Alikuwa Anatembeza Bakora kama hana Akili nzuri siku moja Akachapa mwanafunzi wa Darasa la 6 na inasemekana Alikuwa hachapwi na walimu sababu ya Mama yake kuogopwa kwa Uchawi.. sasa baada ya Kwenda kushitaki kwa Mother yake, Saa 2 Usiku mother mtu Alikuja kumuonya Mzee wangu Home Asirudie tena kumchapa Binti yake.. Mzee Akamwambia Asimtishe na Asirudie tena kuja kumletea vitisho..

Siku nyingine tena Miezi kama 3 Baada ya Tukio la mwanzo.. Yule Binti sijui Alikosea nini bhana Mzee Akamcharaza tena Bakora za Kutosha, mother usiku saa 1 Akaibuka home Kwetu Akamfokea sana Mzee wangu na kumuonya tena, Sasa Ba mkubwa Alivyokuwa mbishi sijui nini kilimpa si Akamdaka yule mother Akaanza kumtembezea Bakora za kutosha hadi walimu Jirani wanakuja kuamua Alikuwa Amemvuruga sana.. Hakwenda Polisi wala Hospital Alijiuguza hadi Akapona.. mwisho kwa Ile Fedheha Akahama Kijiji. Lakini mwaka Mmoja Baadae Ba mkubwa Akiwa Anakunywa Pombe kijiji Jirani cha Bukokwa Alishangaa Kumuona Yule mother Akiwa miongoni mwa wahudumu, Akashangaa Sana Ile bado Akiwa hajui La kufanya Akamwambia Afanye Matengenezo ya maisha yake Kisha ghafla kama upepo Akapotea.. Ba mkubwa Akiwa na Pombe kidogo kichwani Alimpuuza Lakini Alikuja Kutusimulia Kesho yake..

Baada ya Mwezi mmoja Ba mkubwa Akiwa Anatoka Kijiji cha Sukuma Akija Nyabhutanga Usiku Kama Saa 6 hivi Akiwa Anaendesha Baiskeli Ghafla Aliona Fuso Linakuja kwa kasi(Na kwa siku hiyo huo muda Hakuna Gari lilikokuja hapo kijijini kwa muda huo) Alijaribu kulikwepa na Kuishia kuanguka na kupoteza Faham. Alikaa Sengerema Hosptl miezi 3 baadae Tukamhamishia Bugando..Baada ya miezi 3 Akiwa Bugando Hospital Alifariki.. Huwa Naumia sana Kila nikitafakari tukio Hilo Maana Nilikuwa Nasomea Hapo kwake na Ndo Alikuwa kila kitu kwangu kwa wakati huo..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
dah nmesoma sana ngoja na mimi ntoe kisa kilichosababisha niape kuwa sitakwenda kwa mganga tena kwenye maisha yangu.

ilikuwa 2002,tunatoka dar tunakwenda mkoa wa kigoma kwa wanojua bara bara enzi hizo wanajua ni jinsi gani kulikuwa na majambazi hasa ndani ya mapori ya Tabora,bahati haikuwa yetu mida ya saa 5 usiku wakati tupo road tukakuta bara bara imewekwa bonge la gogo mzee akataka kujitahid aligeuze ghafla walitokea watu wamebeba bunduki ndo kwa mara yangu ya kwanza kuone mtu kashka bunduki huku kajizungushia mkanda wa risasi mwilini bro wangu ile kuwaona tu akakata moto tuliokuwa hatujazmia tulikuwa watatu 3 mimi mzee na bimkubwa.

Tulichezea sana vitasa mzee alidhalilika mno mwisho wa siku walichukua mpka viatu nakumbuka viatu vyangu vya kitoto vya kuwaka taa,then wakaondoka mpka na gari tulikaa pale mpka saa 11 ndo tukapata msaada tukaenda polisi but hawakuwa na msaada mzee akapiga simu kigoma ikatumwa nauli tukaenda moja kwa moja mpka kwa baba yake(means babu),sasa babu yeye kila alivyokuwa anahadithiwa alikuwa anacheka mno hasa akimuangalia bro na ujanja wake ote et kazimia,upande wa baba yeye alikuwa na hasira mno alichokuwa anataka yeye ni wale watu awashikishe adabu hata kufa wafe basi ilivyofika usiku tukaelekea sehemu fulani inaitwa ujiji kwa mzee fulani alikuwa anaitwa juma njemba.

Nadhani kwa watu wa kigoma wanaweza kuwa wanamjua,akaelezewa kila kitu akasema hicho ni kitu kidogo sana,huku na yeye anacheka kisha akasema kuwa pale kwake kuna mbuzi alimchinja sababu ya sherwhe ya mwanae hvyo itatubidi tumtafutie mbuzi mwengne amreplace ili iwe kama malipo yake baba akakubali,kilichofata akawaita wajukuu zake walete (ubumba) ni udongo fulani hivi wa mfinyanzi kisha akawa anatengeneza kimdoli kidogo cha udongo kama vile vya kitoto toto,baada ya kukitengeneza akaanza kukiandika maneno yake kisha akakisimamisha chini,then akaanza kuongea maneno yake aliongea sana baada kama ya saa 1 akasema mtu yoyote ndani ya hichi chumba haruhusiwi kukimbia wala kupiga kelele kwani kwa kufanya hivyo ndo itakuwa kifo chake.

Basi aliendele kusema maneno yake ghafla yule mdoli pole pole alianza kukua na kuwa mkubwa pole pole,baada kama ya dakika arobaini alikuwa ni mkubwa kama binadamu mwenye mwili mkubwa alikuwa anamkono na kifua kikubwa na mrefu,kwa mara ya pili bro tena akazimia kwa mara ya pili mim mkojo ulishantoka natetemeka kama nmepatwa na dege dege,mwisho yule mdoli akaambiwa shtaka letu kisha akaambiwa nenda hivi vitu vinatakiwa leo leo,theb yule mtu akafungua mlango akatoka mbio alikuwa ni mwanaume lakini yupo uchi na ni mweusi tii kama mkaa mpka macho hakuwa na ichi kiini cheupe ye alikuwa na kiini cha moja kwa moja cha weusi,alivyoondoka tukaanza kumpepea na kumwagia maji bro alivyoshtuka yule mzee akatuambia kazi imeshakwisha kesho mtayapata majibu yenu.


Ilivyofika asubuhi tukapigiwa simu nakumbuka enzi hizo kulikuwa kuna buzz siyo hii tigo na hata simu zilikuwa za mezani,tukaambiwa kuwa kuna gari imepatikana Tabora yenye namba kama tuliyoripoti pamoja na vitu vingine,tukaanza safari na treni mpka tabora kufika kule tukakuta vitu vyetu na vingne vingi tu ila mzee alisema vyote vilikuwa vyetu hela zilikuwa kama 1m lakini zilipatikana 7m polisi hawakuchukua hata cent na hata walivyopewa walikataa kata kata hakikupotea hata kifungo kisha baada ya kuchukua tukaambiwa kuwa hao majambazi waliotuibia walikutwa msituni wakiwa wameuwawa wakasema wanahisi ni wanyama wakali ndo waliwauwa maana walikuwa wanaalama za meno makali milini mwao na kucha.

lakini wakashndwa kuelewa kama ni wanyama ndo waliwashambulia ni wanyama aina gani na kwanini hawakuwapiga hata risasi moja hao wanyama na wakati walikuwa na silaha nzito?Baada ya maelezo mengi mzee akawasha gari mpka kigoma stend ya kwanza mpka kwa yule mganga tulinunua mbuzi na zawadi nyingne nying lakini mzee aligoma hakutaka chochote zaidi ya mbuzi tu,basi tukampka mbuzi wake, akasema imebaki kazi moja tu na kazi yenyewe ni kumrudisha yule kiumbe(mdoli mtu)ili asitudhuru na sisi maana ni wetu hapo mdipo ilipokuwa mtihani maana kuna msharti mengi tulikosea plus kujisahau sasa akawa anatuandama sisi atuue dah kila mmoja nyumbani anaalama ya yule kiumbe yangu ni kungatwa skio na kula kipande nikipata mda ntawamalizia kisa changu but mpka leo mimi kwenda kwa waganga ni big no,but thanks god tulitoka salama


picha ya nilipongatwa kwenye skio ambyo ni alama ambayo sitaweza isahau mpka kifo

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nakumbuka siku moja nimetoka kula chakula usiku, mida ya sa mbili, kuingia chumbani kitandani ile nalala kabla sijafumba macho nilijiona napaa live juu ya kitanda mara tatu.....nkakemea kwa jina la yesu nkaachiwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata mimi hii kitu ilikuwa inanitokea sana, nilikuwa nahisi kama kitanda kinabembea juu kwa juu. Nikawa naipenda sana pasi na kujua "wazee baba" ndo wameingia "ofisini" kutimiza wajibu. Nilikuja kuambiwa baadae sana na bimkubwa kuwa ni wazee baba hao. Ila tangu kipindi hicho ni muda mrefu sana sijaexperience tena hiyo hali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gamboshi ipo kweli usukuman huko ila hizo story zake za kichawi zimetiwa chumvi. Nimesoma na jamaa mmoja mpwapw secondary form four 2004, Emmanuel Holehole alikua katokea Gamboshi. Alinambia Gamboshi kwa kawaida tu hakuna lolote Kama wanavyosema.

Sent using Jamii Forums mobile app
Utakuwa unachanganya kati ya Gamboshi ya jicho la nyama na Gamboshi city ile ya kichawi

Hit direct to the Ntonku
 
Back
Top Bottom