Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
🤣🤣🤣
Mi nauliza tu yule jamaa alieng'atwa sikio kamalizia stori yake ya juma nchemba !
Ameliwa mwli mzima anajiuguzaJerrybanks anazingua
Mkuu toka sept 19 had leo hujamalza tu hzo mishemishenitasimulia na mm changu Tanga ngoja nimalize mishemishe
NipeMe ktk maisha yangu nimeshuhudia mambo mengi sana ya kichawi ingawa mengine nikatka ndoto lakini yalikua na uhalisia
Ila tukio ambalo siwezi kusahau ni ktk hizi nyumaba za kupanga ambapo nilipanga na mmama mmoja hivi wa kiha, basi kuna rafiki yangu yeye alikua na mashetani ya uganga na nilikua nalala naye
Siku moja akaniambia ndg yangu huyu mama jirani yetu mchawi nilimuona kaingia humu na Lengo lake nikutuchezea nikachukulia kawaida
Basi yule jamaa alikuja akaondoka nikabaki Mimi na ndg yangu mmoja asa hapo Yule mama akawa anafanya utawala sasa full kututesa usiku kuna kipindi nikawa namuona kabisa anaingia kupitoa mlango mida ya usiku lakini nikawa nashikwa na bumbuwazi nashindwa kusema
Siku moja nilipoona mambo yamekua si mambo ikabidi niende Kwa dr mmoja hivi akaninipa dawa na kaniambia nenda kadeki ndani na utadeki Kwa muda wa siku 3 kweli Kesho yake asubuhi nikafanya hivyo kablacjaenda kwenye Mishe
Asa nilikuja kushanga ucku nilipo lala mishale ya saa 8 ucku niliskia sauti ya paka alilia mara3 nachakushangaza alitokea mlangoni na mlango nilikua nimefunga akaelekea uvunguni wa kitanda
Mpaka kuna kucha akawa yupo mle ndani na hali ya pale nyumani ikawa imezorota Fulani yaani mtoto wa Yule mama alikua mpole sana na hata mama yake akawa haonekani ovyo na hata nikikutana naye namuona yupo katka Hali ya unyonge na kisasi cha Hali ya juu
Ila nilifuata Yule Dr nakumueleza akaniambia Yule ni adui alivyoingia mle alikuta bahari hivyo akawa hana jinsi na akaniambia nenda kamalizie kudeki hiyo dawa
Ingawa kuna siku wakati nachanganya ile Dawa ili nideki alikuja Yule mtoto wa Yule mama akainyooshea kidodole ndoo ya dawa , ila hapa usiniulize nilimuona vp majibu nitakayokupa huenda hautaamini......
Sent using Jamii Forums mobile app
Ulifanikiwa WATOTO?Nikiwa na miaka Tisa ya ndoa yangu sikuwahi dhani wala kujua wife ni mchawi maana alikuwa msomi wa juu sana na mtu wa kanisa sana.siku moja nikiwa nimelala ulivuma upepo mkali mno gafla nikiwa macho nikajikuta nanyanyuliwa juu aisee nilisali sala zote gafla nikarudishwa chini.Kuangalia pembeni yangu alipolala mwenzangu naona mbwa aisee ulikuja kama usingizi hivi sekunde wife akarudi ktk hali yake ya ubinaadamu.Kesho yake nikahama home na ndoa ikafa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana. Miaka 9 hujagundua duhNikiwa na miaka Tisa ya ndoa yangu sikuwahi dhani wala kujua wife ni mchawi maana alikuwa msomi wa juu sana na mtu wa kanisa sana.siku moja nikiwa nimelala ulivuma upepo mkali mno gafla nikiwa macho nikajikuta nanyanyuliwa juu aisee nilisali sala zote gafla nikarudishwa chini.Kuangalia pembeni yangu alipolala mwenzangu naona mbwa aisee ulikuja kama usingizi hivi sekunde wife akarudi ktk hali yake ya ubinaadamu.Kesho yake nikahama home na ndoa ikafa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kata ya rundugai sehemu gani? Mkoa na kijijiKama uchawi upo kweli naamini upo,
Siku hiyo tunaandika wapiga kula kijiji fulani kinaitwa chokaa,kata ya rundugai , bwanaweee kwenye kupita nyumba kuomba tulilaze lili BVRmachine sio ndio kukutana nguo zimeanikwa zinaning'inia ila kamba haionekani
Dah bro wako yeye kuzimia tu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]dah nmesoma sana ngoja na mimi ntoe kisa kilichosababisha niape kuwa sitakwenda kwa mganga tena kwenye maisha yangu.
ilikuwa 2002,tunatoka dar tunakwenda mkoa wa kigoma kwa wanojua bara bara enzi hizo wanajua ni jinsi gani kulikuwa na majambazi hasa ndani ya mapori ya Tabora,bahati haikuwa yetu mida ya saa 5 usiku wakati tupo road tukakuta bara bara imewekwa bonge la gogo mzee akataka kujitahid aligeuze ghafla walitokea watu wamebeba bunduki ndo kwa mara yangu ya kwanza kuone mtu kashka bunduki huku kajizungushia mkanda wa risasi mwilini bro wangu ile kuwaona tu akakata moto tuliokuwa hatujazmia tulikuwa watatu 3 mimi mzee na bimkubwa.
Tulichezea sana vitasa mzee alidhalilika mno mwisho wa siku walichukua mpka viatu nakumbuka viatu vyangu vya kitoto vya kuwaka taa,then wakaondoka mpka na gari tulikaa pale mpka saa 11 ndo tukapata msaada tukaenda polisi but hawakuwa na msaada mzee akapiga simu kigoma ikatumwa nauli tukaenda moja kwa moja mpka kwa baba yake(means babu),sasa babu yeye kila alivyokuwa anahadithiwa alikuwa anacheka mno hasa akimuangalia bro na ujanja wake ote et kazimia,upande wa baba yeye alikuwa na hasira mno alichokuwa anataka yeye ni wale watu awashikishe adabu hata kufa wafe basi ilivyofika usiku tukaelekea sehemu fulani inaitwa ujiji kwa mzee fulani alikuwa anaitwa juma njemba.
Nadhani kwa watu wa kigoma wanaweza kuwa wanamjua,akaelezewa kila kitu akasema hicho ni kitu kidogo sana,huku na yeye anacheka kisha akasema kuwa pale kwake kuna mbuzi alimchinja sababu ya sherwhe ya mwanae hvyo itatubidi tumtafutie mbuzi mwengne amreplace ili iwe kama malipo yake baba akakubali,kilichofata akawaita wajukuu zake walete (ubumba) ni udongo fulani hivi wa mfinyanzi kisha akawa anatengeneza kimdoli kidogo cha udongo kama vile vya kitoto toto,baada ya kukitengeneza akaanza kukiandika maneno yake kisha akakisimamisha chini,then akaanza kuongea maneno yake aliongea sana baada kama ya saa 1 akasema mtu yoyote ndani ya hichi chumba haruhusiwi kukimbia wala kupiga kelele kwani kwa kufanya hivyo ndo itakuwa kifo chake.
Basi aliendele kusema maneno yake ghafla yule mdoli pole pole alianza kukua na kuwa mkubwa pole pole,baada kama ya dakika arobaini alikuwa ni mkubwa kama binadamu mwenye mwili mkubwa alikuwa anamkono na kifua kikubwa na mrefu,kwa mara ya pili bro tena akazimia kwa mara ya pili mim mkojo ulishantoka natetemeka kama nmepatwa na dege dege,mwisho yule mdoli akaambiwa shtaka letu kisha akaambiwa nenda hivi vitu vinatakiwa leo leo,theb yule mtu akafungua mlango akatoka mbio alikuwa ni mwanaume lakini yupo uchi na ni mweusi tii kama mkaa mpka macho hakuwa na ichi kiini cheupe ye alikuwa na kiini cha moja kwa moja cha weusi,alivyoondoka tukaanza kumpepea na kumwagia maji bro alivyoshtuka yule mzee akatuambia kazi imeshakwisha kesho mtayapata majibu yenu.
Ilivyofika asubuhi tukapigiwa simu nakumbuka enzi hizo kulikuwa kuna buzz siyo hii tigo na hata simu zilikuwa za mezani,tukaambiwa kuwa kuna gari imepatikana Tabora yenye namba kama tuliyoripoti pamoja na vitu vingine,tukaanza safari na treni mpka tabora kufika kule tukakuta vitu vyetu na vingne vingi tu ila mzee alisema vyote vilikuwa vyetu hela zilikuwa kama 1m lakini zilipatikana 7m polisi hawakuchukua hata cent na hata walivyopewa walikataa kata kata hakikupotea hata kifungo kisha baada ya kuchukua tukaambiwa kuwa hao majambazi waliotuibia walikutwa msituni wakiwa wameuwawa wakasema wanahisi ni wanyama wakali ndo waliwauwa maana walikuwa wanaalama za meno makali milini mwao na kucha.
lakini wakashndwa kuelewa kama ni wanyama ndo waliwashambulia ni wanyama aina gani na kwanini hawakuwapiga hata risasi moja hao wanyama na wakati walikuwa na silaha nzito?Baada ya maelezo mengi mzee akawasha gari mpka kigoma stend ya kwanza mpka kwa yule mganga tulinunua mbuzi na zawadi nyingne nying lakini mzee aligoma hakutaka chochote zaidi ya mbuzi tu,basi tukampka mbuzi wake, akasema imebaki kazi moja tu na kazi yenyewe ni kumrudisha yule kiumbe(mdoli mtu)ili asitudhuru na sisi maana ni wetu hapo mdipo ilipokuwa mtihani maana kuna msharti mengi tulikosea plus kujisahau sasa akawa anatuandama sisi atuue dah kila mmoja nyumbani anaalama ya yule kiumbe yangu ni kungatwa skio na kula kipande nikipata mda ntawamalizia kisa changu but mpka leo mimi kwenda kwa waganga ni big no,but thanks god tulitoka salama
picha ya nilipongatwa kwenye skio ambyo ni alama ambayo sitaweza isahau mpka kifo
Sent using Jamii Forums mobile app
ulikuwa speed sana?Mnamo tarehe 04.10.2020 majira ya saa 04:45 Am nikitokea Tunduma kuelekea Vwawa mkoa wa Songwe nilipata ajali mbaya sana ya gari.Chanzo cha ajali hiyo hadi leo sijakifahamu kabisa ila nikiwa kwenye gari kabla ya ajali kutokea usoni nilipigwa na giza nene sana kiasi kwamba nilikuwa sioni chchote mbele yangu,ni ngumu kuamini hili lakini ni tukio ambalo kama na mimi ningekuwa ni mtu mwepesi nafikiri kwa sasa ningekuwa naongea mengine uchawi upo sana Tanzania.
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]Niligombani demu na kijana mwenzangu anaitwa Abdallah K....A...
Jamaa akaniahidi kuwa NITAMUACHA tu huyo demu....
Ikawa kila nikimnanihii SHORTY anawashwa na kuvimba mwili kwa wiki nzima....
Jamaa akawa anamwambia demu kuwa AMEMTENGENEZA VYA KUTOSHA...
Man...nilimuacha Yule mtoto...
Then lijamaa LIKAMUOA MKE WA PILI....
Watu wachawi jamani looh
Vip kwa sasa je mambo ni yale yale? Acha hicho chumbaUchawi upo... Mimi Nina biashara yangu hapa dar mwaka wa 4 napata faida fresh nikajenga kigamboni na duka likakuwa nikawa nahitaji nafasi zaidi... Nikapata chumba nikaongeza store sasa kile chumba kuna mpangaji mwenzangu mtu wa musoma na yeye anakitaka ila mwenye nyumba akanipa Mimi Yule mpangaji alilalamika Sana kwamba nimependelewa Mimi eti nimempa rushwa mwenye nyumba.
Baada ya hapo basi nilipata hasara kutoka ml 40+ mpaka ml 7 msingi woote. Nikafanya dua kwa mashekh ule msingi ukarudi mpaka ml 19 ndani ya mwezi tuu ila baada ya hapo ikawa mwezi huu napata faida mwezi huu hasara mwezi mwengine sipati faida hata 100 mpaka leo hii sina maendeleo yoyote zaidi ya kupata pesa ya Kula tuu na msingi upo vilevile... Nilimuhadithia mwenye nyumba yaliyonikuta na akasema na yeye yamemkuta kama hyo yangu na anataka kumtimua Yule mpangaji maana ni mchawi.
Kimbembe akina kufukuzwa huyu mpangaji anaweza kuuwa mtu asieee.... Uchawa upo jamani Mimi mpaka leo nahangaika ila fiada inayeyukaa nabaki na pesa ya Kula tuu
Sent using Jamii Forums mobile app
Umejuaje Kama nao ni wale wale tu
Lakini maisha yako yameanza kubadilika au yapo vile vile?Nakumbuka niliendaga kwa mganga mmoja hivi ili anisaidie shida niliyokuwa nayo
Basi nilivyofika pale akasema kwanza toa elfu10 hapo mapokezi then uje uonane na mie, nikafanya hivyo
Hatimaye niliruhusiwa kuingia ndani kwa yule mganga kisha akanipa kalatasi na kuniamulu niandike majina yangu mawili
Akaniambia ikiandika ikunje kalatasi kisha niletee nikafanya hivyo, nilipompa ile kalatasi akaichoma na akaniambia unaitwa fulani nikasema ndiyo, hii nikabaki najiuliza? Hiyu jamaa oajuaje jina langu wakati hata kalatasi hajaifungua anyway Acha tuendelee
Akanambia una nyota ya utajiri na ya kupendwa pia inaonyesha huko mbele utakua tajiri hivyo hizi nyota zako zimefifia, acha nikusaidie kusafisha
Basi akanambia nenda kanunue mafuta ya nazi pamoja na wembe kisha ulete nikaenda kununua nikampelekea, nilipofika akanambia vua nguo zako ubaki na boxer, nikafanya hivyo akanichanja kwenye miguu na mikono kisha akaniambia nenda nyumbani kesho uje ila usipeane mikono mtu wala kugusana bega, acha nicheke kwanza kwa vioja nilivyokutana navyo[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
Ebana ile natoka tuu nikakutana na yule mfuasi wake anaingia ndani c nikajisahau nakutaka nimpe mkono bahati nzuri jamaa akanikwepa, Kimbembe nilipofika nyumbani, nakumbuka ilikua majira ya saa moja nikiwa ndani nachukua maji nikaoge ndipo nilisikia sauti ya jamaa niliyekuwa nalala naye akiniita huku anaingia ndani kumbe alikua na rafiki yake aliyekuwa anafanya naye biashara ya mkaa yule jamaa alivyoingia ndani nikashangaa ananilete mkono ili tusalimiane bwana weee nikajikuta nampelekea mkono hiii nikakumbuka masharti niliyopewa najikuta naurudisha mkono haraka[emoji16][emoji16] aisee lile sharti lilinishinda kimtindo. Yote na yote niporudi nilimulezea akanambia najaribu kukuonyesha kuwa mimi siyo hao matapeli, basi alinisaidia kimtindo ingawa kwani alinipa dawa yakuondoa mikosi then akanambia ukipata hela njoo nikusaidie matatizo iliyokuwa nayo nikaachana naye kwa namna hiyo. Hicho ndicho nilichokutana nacho kwa mganga kutoka kigoma.