Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

digba sowey, Duh, mimi nimeshuhudia uchawi wa kutisha kwenye nchi moja inaitwa Tanzania.
Kuna li Chama inaitwa CCM, tangu mwaka 1961 hadi leo 2029 watu wanalala kwenye nyumba Kama mabanda ya nguruwe na kula yao ni taabu lakini wanavumilia tu badala ya kutumia nguvu kuyatoa ma CCM, ama kweli uchawi upo

Sent using Jamii Forums mobile app
CCM Ni chama chankichawi kiroho!

Na vyama pinzani pia Kwa mujibu was wazee was chama,hao wazee ndio wenye chama.na walianzisha wao!!

Zipo dalili za ukombozi hapo mbele tutapata ccm takatifu inayojali maslahi ya watz na mwenyekiti wake atakua mcha mungu aliewekwa na mungu!!
 
dah nmesoma sana ngoja na mimi ntoe kisa kilichosababisha niape kuwa sitakwenda kwa mganga tena kwenye maisha yangu.

ilikuwa 2002,tunatoka dar tunakwenda mkoa wa kigoma kwa wanojua bara bara enzi hizo wanajua ni jinsi gani kulikuwa na majambazi hasa ndani ya mapori ya Tabora,bahati haikuwa yetu mida ya saa 5 usiku wakati tupo road tukakuta bara bara imewekwa bonge la gogo mzee akataka kujitahid aligeuze ghafla walitokea watu wamebeba bunduki ndo kwa mara yangu ya kwanza kuone mtu kashka bunduki huku kajizungushia mkanda wa risasi mwilini bro wangu ile kuwaona tu akakata moto tuliokuwa hatujazmia tulikuwa watatu 3 mimi mzee na bimkubwa.

Tulichezea sana vitasa mzee alidhalilika mno mwisho wa siku walichukua mpka viatu nakumbuka viatu vyangu vya kitoto vya kuwaka taa,then wakaondoka mpka na gari tulikaa pale mpka saa 11 ndo tukapata msaada tukaenda polisi but hawakuwa na msaada mzee akapiga simu kigoma ikatumwa nauli tukaenda moja kwa moja mpka kwa baba yake(means babu),sasa babu yeye kila alivyokuwa anahadithiwa alikuwa anacheka mno hasa akimuangalia bro na ujanja wake ote et kazimia,upande wa baba yeye alikuwa na hasira mno alichokuwa anataka yeye ni wale watu awashikishe adabu hata kufa wafe basi ilivyofika usiku tukaelekea sehemu fulani inaitwa ujiji kwa mzee fulani alikuwa anaitwa juma njemba.

Nadhani kwa watu wa kigoma wanaweza kuwa wanamjua,akaelezewa kila kitu akasema hicho ni kitu kidogo sana,huku na yeye anacheka kisha akasema kuwa pale kwake kuna mbuzi alimchinja sababu ya sherwhe ya mwanae hvyo itatubidi tumtafutie mbuzi mwengne amreplace ili iwe kama malipo yake baba akakubali,kilichofata akawaita wajukuu zake walete (ubumba) ni udongo fulani hivi wa mfinyanzi kisha akawa anatengeneza kimdoli kidogo cha udongo kama vile vya kitoto toto,baada ya kukitengeneza akaanza kukiandika maneno yake kisha akakisimamisha chini,then akaanza kuongea maneno yake aliongea sana baada kama ya saa 1 akasema mtu yoyote ndani ya hichi chumba haruhusiwi kukimbia wala kupiga kelele kwani kwa kufanya hivyo ndo itakuwa kifo chake.

Basi aliendele kusema maneno yake ghafla yule mdoli pole pole alianza kukua na kuwa mkubwa pole pole,baada kama ya dakika arobaini alikuwa ni mkubwa kama binadamu mwenye mwili mkubwa alikuwa anamkono na kifua kikubwa na mrefu,kwa mara ya pili bro tena akazimia kwa mara ya pili mim mkojo ulishantoka natetemeka kama nmepatwa na dege dege,mwisho yule mdoli akaambiwa shtaka letu kisha akaambiwa nenda hivi vitu vinatakiwa leo leo,theb yule mtu akafungua mlango akatoka mbio alikuwa ni mwanaume lakini yupo uchi na ni mweusi tii kama mkaa mpka macho hakuwa na ichi kiini cheupe ye alikuwa na kiini cha moja kwa moja cha weusi,alivyoondoka tukaanza kumpepea na kumwagia maji bro alivyoshtuka yule mzee akatuambia kazi imeshakwisha kesho mtayapata majibu yenu.


Ilivyofika asubuhi tukapigiwa simu nakumbuka enzi hizo kulikuwa kuna buzz siyo hii tigo na hata simu zilikuwa za mezani,tukaambiwa kuwa kuna gari imepatikana Tabora yenye namba kama tuliyoripoti pamoja na vitu vingine,tukaanza safari na treni mpka tabora kufika kule tukakuta vitu vyetu na vingne vingi tu ila mzee alisema vyote vilikuwa vyetu hela zilikuwa kama 1m lakini zilipatikana 7m polisi hawakuchukua hata cent na hata walivyopewa walikataa kata kata hakikupotea hata kifungo kisha baada ya kuchukua tukaambiwa kuwa hao majambazi waliotuibia walikutwa msituni wakiwa wameuwawa wakasema wanahisi ni wanyama wakali ndo waliwauwa maana walikuwa wanaalama za meno makali milini mwao na kucha.

lakini wakashndwa kuelewa kama ni wanyama ndo waliwashambulia ni wanyama aina gani na kwanini hawakuwapiga hata risasi moja hao wanyama na wakati walikuwa na silaha nzito?Baada ya maelezo mengi mzee akawasha gari mpka kigoma stend ya kwanza mpka kwa yule mganga tulinunua mbuzi na zawadi nyingne nying lakini mzee aligoma hakutaka chochote zaidi ya mbuzi tu,basi tukampka mbuzi wake, akasema imebaki kazi moja tu na kazi yenyewe ni kumrudisha yule kiumbe(mdoli mtu)ili asitudhuru na sisi maana ni wetu hapo mdipo ilipokuwa mtihani maana kuna msharti mengi tulikosea plus kujisahau sasa akawa anatuandama sisi atuue dah kila mmoja nyumbani anaalama ya yule kiumbe yangu ni kungatwa skio na kula kipande nikipata mda ntawamalizia kisa changu but mpka leo mimi kwenda kwa waganga ni big no,but thanks god tulitoka salama


picha ya nilipongatwa kwenye skio ambyo ni alama ambayo sitaweza isahau mpka kifo

Sent using Jamii Forums mobile app
Kigoma n balaa huko,tena kunasehem wanaita kibondo haaa uko ndio hatar zaidi
 
Kigoma n balaa huko,tena kunasehem wanaita kibondo haaa uko ndio hatar zaidi
Acha kutisha watu.
Wauza dagaa ndio mnadanganyana kuhusu uchawi.
Hebu muulize tajiri hapo kibondo km ameshawahi kuchezewa na hivyo vibwengo.
Unmaskini husababisha akili kutekwa na yyt mwenye ujanja kidogo.
Ndio maana mnauziwa majivu ya kuni mnaambiwa ni kinga.

Ovyo kabisa
 
Acha kutisha watu.
Wauza dagaa ndio mnadanganyana kuhusu uchawi.
Hebu muulize tajiri hapo kibondo km ameshawahi kuchezewa na hivyo vibwengo.
Unmaskini husababisha akili kutekwa na yyt mwenye ujanja kidogo.
Ndio maana mnauziwa majivu ya kuni mnaambiwa ni kinga.

Ovyo kabisa
Kwan kunasehemu umeitwa au kiranga?,kujifanya kujua kumbe hauna unachojua.
 
CCM Ni chama chankichawi kiroho!

Na vyama pinzani pia Kwa mujibu was wazee was chama,hao wazee ndio wenye chama.na walianzisha wao!!

Zipo dalili za ukombozi hapo mbele tutapata ccm takatifu inayojali maslahi ya watz na mwenyekiti wake atakua mcha mungu aliewekwa na mungu!!
Ccm ni muunganiko wa vyama 13 vya kichawi nchi nzima.
Mwenge ndio zindiko lao na umasikini wetu ndio kafara lao.
Wazee wa Dar e salaam ndio wazee wenyewe wa kamati ya Giza.
Check walimu na polish pamoja na ugumu wa maisha huwaambii kitu kuhusu ccm.
 
Kwan kunasehemu umeitwa au kiranga?,kujifanya kujua kumbe hauna unachojua.
Kiranga maana yake ni nyodo nyingi.
Wanao ogopa uchawi ndio viranga. Waite hao wachawi wamsaidie mbowe kuwa Rais.
Sio kurogana kipumbavu tu.
Ukosa busara ni hasara kubwa kuliko kukosa mali.
We huna vyote.
Manake ni hatari kuliko cancer
 
Miaka ya 1995 - 2000 kuna bwana mmoja alienda kwa mganga mahali fulani wilaya ya Njombe ili apate utajiri.

Masharti aliyopewa pamoja na dawa ni kulala katikati ya reli ya TAZARA usiku. Kwamba akisikia treni inakuja asiondoke aendelee kunuiza anataka utajiri wa kiwango gani.

E bwana ee, jamaa alisikia chuma kinaunguruma kama kilometa 5 kuja uelekeo wake. Sasa shida ikawa upande mmoja sijui ni moyo au ubongo au vyote vikaanza mjadala. Hiki ni kifo hapana huu ni utajiri.

Kukatisha maelezo jamaa aliyoka mbio baada ya kuinua kichwa na kuona kichwa cha treni kinasonga bila mjadala.

Aliamua kurudi kwao kijijini kukomaa na mpini wa jembe.

Hii ni simulizi kutoka kwa mhusika katika mazungumzo ya utajiri wa haraka haraka.

Sent using Jamii Forums mobile app
🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Eti wachawi wa mvua hawapo? Ngoja nikupe msala huu hapa.

Mwaka 1986 nilikuwa kitoto cha darasa la 4, kipindi hicho huko usukumani ndio jeshi la Sungusung ndio liko moto. Kulikuwepo wazee wawili mmoja alikuwa anaitwa Radslaus (walizowea kumwita Silaus) mwingine alikuwa anaitwa Ndonkeye. Hawa wazee wao walikuwa hawapendani, kisa kumbe ilikuwa jinsi walivyokuwa wanazidiana ujuzi wa kuloga.

Hawa wazee vikitokea vipindi mvua ikakosekana katikati ya msimu wa mvua walikuwa wanatamba kwamba wapewe fedha au vyakula ili walete mvua. Mwisho wao ulikuwa mbaya sana.

Siku moja nzengo ikapiga mwano (mbiu) na watu wakakusanyika. Ndonkeye na Silaus wakaletwa. Nakumbuka ilikuwa mida ya saa 9 alasiri hivi. Wakaulizwa mbona mvua hainyeshi. Silaus akasema yeye huwa anajitahidi kuileta ila Ndonkeye huwa analeta upepo mkali mawingu yanapeperushwa.

Ndonkeye naye akaulizwa, yeye akasema ni mtaalam wa kuleta mvua kumzidi hata Silaus. Nzengo ikaona hawa wanawachezea akili. Nzengo ikatengeneza duara kama ya watu 30, wakaambiwa wapite wakiizunguka hiyo round ya watu walio na viboko ili wapigwe, wakapita na kila mtu akatandika kiboko kimoja mgongoni, kisha mzunguko wakaumaliza, yakaandaliwa maji kwenye ndoo yaliyotiwa chunvi, wakamwagiwa, kisha wakapita tena kwenye roundi kutandikwa

Baada ya hapo, Ndonkeye akaamua kusema ukweli kuwa yeye ndie mtaalam wa kuleta mvua na kama hawaamini alete wakati huo huo. Nzengo ikafurahi sana. Akaomba aende atafte dawa polini, nzengo ikampa watu wachache ili wamsindikize na arudi nao akiwa na dawa hiyo. Wakaondoka, walipofika huko polini Ndonkeye akawaambia wamsubiri (hakutaka waone ni dawa ya miti gani) kisha akamaliza na kurudi kwenye kusanyiko

Hicho kipindi nakumbuka kulikuwa na jua kali sana, mazao yalikuwa yameanza kukauka maana ni kami mwezi nakitu kitu mvua hainyeshi.

Ndonkeye akatafuna yale magamba ya miti, akawa anaongea lugha yake ya Kiha akiamrisha mawingu yakusanyike upande wa mashariki kutokea pale kwenye mkutano. Aliongea sana kama nusu saa akiamrisha, kweli yakaanza kukusanyika kwa mbali sana. Aliendelea kuamrisha hayo mawingu yasogee, yakasogea kama nyuzi 90 hivi. Akaamrisha yatande sehemu kubwa kwa lengo ili mvua ikinyesha iweze kunyesha eneo kubwa. Kisha upepo ukaanza kuvuma, akaamrisha upepo utulie, nao ukatulia

Baada ya hapo akawauliza wananzengo kama wako tayari kupokea mvua, wakashangilia kwa kukubali. Akarudia tena kama wanataka mvua ilete salam kwao, wakakubali....ilipiga radi mti mkavu karibu sana na ule mkutano, mti ulisambaa wote mpaka kubakia kisiki kidogo. Wtu wengine walianguka na kuzimia, wengine waklikimbia kusikojulikana, wenye rooho ngumu walibaki. Ilinyesha mvua kubwa sana. Kisha Wajumbe waliobaki walimwambia kesho asubuhi mktano utamuhitaji tena ili aendelee kuleta mvua. Usiku saa 8 ilianza kunyesha mvua mpaka kesho yake saa 10 jioni, nyumba zilianguka, mafuriko makubwa yakatokea na hiyo ndio ilikuwa pona yake Ndonkeye. Ndonkeye na Silaus ni Waha wa huko Kibondo.
Kuna kimbelembele mmoja kanishushua hapo juu sijui n muha wa kibondo,baada ya kusema kibondo n kiboko kwa washirikina
 
Kiranga maana yake ni nyodo nyingi.
Wanao ogopa uchawi ndio viranga. Waite hao wachawi wamsaidie mbowe kuwa Rais.
Sio kurogana kipumbavu tu.
Ukosa busara ni hasara kubwa kuliko kukosa mali.
We huna vyote.
Manake ni hatari kuliko cancer
We ungekuwa na busara ungebishana na asie kuwa na busara?ww ndio huna kitu kabisaaa kwendraaaa
 
🤣🤣 huu uzi umenikumbusha mbali
Nilienda kwa mama mdogo Arusha,
Kuna binti aliaminika ni mchawi sababu mama yake ni mchawi na binti alikua akishuhudia mama yake anataka kumfundisha yeye hataki.

Siku tumelala ndani na huyo binti (kila mtu na kitanda chake) usiku mnene nasikia maji yanamwagika chumbani kama bomba limeachwa wazi huku nje kuna kimbunga kikali mnoooo

AKili ikaja tu ni mama wa yule binti
Nililala bila kutikisika huku nikiomba kimoyo moyo Mungu anilinde 😂😂

Asubuhi tumeamka chumba chote kimejaa maji kama bwawa

Siku hiyo hiyo Beatrice alipewa nauli aende kwao sumbawanga
 
We ungekuwa na busara ungebishana na asie kuwa na busara?ww ndio huna kitu kabisaaa kwendraaaa
Andiko linasema "
Eti wachawi wa mvua hawapo? Ngoja nikupe msala huu hapa.

Mwaka 1986 nilikuwa kitoto cha darasa la 4, kipindi hicho huko usukumani ndio jeshi la Sungusung ndio liko moto. Kulikuwepo wazee wawili mmoja alikuwa anaitwa Radslaus (walizowea kumwita Silaus) mwingine alikuwa anaitwa Ndonkeye. Hawa wazee wao walikuwa hawapendani, kisa kumbe ilikuwa jinsi walivyokuwa wanazidiana ujuzi wa kuloga.

Hawa wazee vikitokea vipindi mvua ikakosekana katikati ya msimu wa mvua walikuwa wanatamba kwamba wapewe fedha au vyakula ili walete mvua. Mwisho wao ulikuwa mbaya sana.

Siku moja nzengo ikapiga mwano (mbiu) na watu wakakusanyika. Ndonkeye na Silaus wakaletwa. Nakumbuka ilikuwa mida ya saa 9 alasiri hivi. Wakaulizwa mbona mvua hainyeshi. Silaus akasema yeye huwa anajitahidi kuileta ila Ndonkeye huwa analeta upepo mkali mawingu yanapeperushwa.

Ndonkeye naye akaulizwa, yeye akasema ni mtaalam wa kuleta mvua kumzidi hata Silaus. Nzengo ikaona hawa wanawachezea akili. Nzengo ikatengeneza duara kama ya watu 30, wakaambiwa wapite wakiizunguka hiyo round ya watu walio na viboko ili wapigwe, wakapita na kila mtu akatandika kiboko kimoja mgongoni, kisha mzunguko wakaumaliza, yakaandaliwa maji kwenye ndoo yaliyotiwa chunvi, wakamwagiwa, kisha wakapita tena kwenye roundi kutandikwa

Baada ya hapo, Ndonkeye akaamua kusema ukweli kuwa yeye ndie mtaalam wa kuleta mvua na kama hawaamini alete wakati huo huo. Nzengo ikafurahi sana. Akaomba aende atafte dawa polini, nzengo ikampa watu wachache ili wamsindikize na arudi nao akiwa na dawa hiyo. Wakaondoka, walipofika huko polini Ndonkeye akawaambia wamsubiri (hakutaka waone ni dawa ya miti gani) kisha akamaliza na kurudi kwenye kusanyiko

Hicho kipindi nakumbuka kulikuwa na jua kali sana, mazao yalikuwa yameanza kukauka maana ni kami mwezi nakitu kitu mvua hainyeshi.

Ndonkeye akatafuna yale magamba ya miti, akawa anaongea lugha yake ya Kiha akiamrisha mawingu yakusanyike upande wa mashariki kutokea pale kwenye mkutano. Aliongea sana kama nusu saa akiamrisha, kweli yakaanza kukusanyika kwa mbali sana. Aliendelea kuamrisha hayo mawingu yasogee, yakasogea kama nyuzi 90 hivi. Akaamrisha yatande sehemu kubwa kwa lengo ili mvua ikinyesha iweze kunyesha eneo kubwa. Kisha upepo ukaanza kuvuma, akaamrisha upepo utulie, nao ukatulia

Baada ya hapo akawauliza wananzengo kama wako tayari kupokea mvua, wakashangilia kwa kukubali. Akarudia tena kama wanataka mvua ilete salam kwao, wakakubali....ilipiga radi mti mkavu karibu sana na ule mkutano, mti ulisambaa wote mpaka kubakia kisiki kidogo. Wtu wengine walianguka na kuzimia, wengine waklikimbia kusikojulikana, wenye rooho ngumu walibaki. Ilinyesha mvua kubwa sana. Kisha Wajumbe waliobaki walimwambia kesho asubuhi mktano utamuhitaji tena ili aendelee kuleta mvua. Usiku saa 8 ilianza kunyesha mvua mpaka kesho yake saa 10 jioni, nyumba zilianguka, mafuriko makubwa yakatokea na hiyo ndio ilikuwa pona yake Ndonkeye. Ndonkeye na Silaus ni Waha wa huko Kibondo.
Wacha kuleta hadithi za kisukuma hapa.
Sungusungu walikuwa wapumbavu flani wanaoneq kila mzee mwenye macho mekundu.
Wasukuma wengi wana imani za kijinga.
Hakuna binaadamu Ana uwezo wa kuleta mvua wala upepo.
Huu upumbavu wenu mmeua wazee wengi wasio na hatia. Mlitakiwa mkamatwe mnyongwe wote.

Mimi ni mkulima na mashamba mengi ya mpunga yanakauka kwa kukosa mvua. Leo kungekuwa na mchawi mmoja tu wa kuweza kuleta mvua Tanzania nzima ingemfahamu.

Nyie kiboko yenu alikuwa magufuli. Tupa ndani miaka 800 .
Nyanoko baghesha.
 
🤣🤣 huu uzi umenikumbusha mbali
Nilienda kwa mama mdogo Arusha,
Kuna binti aliaminika ni mchawi sababu mama yake ni mchawi na binti alikua akishuhudia mama yake anataka kumfundisha yeye hataki.

Siku tumelala ndani na huyo binti (kila mtu na kitanda chake) usiku mnene nasikia maji yanamwagika chumbani kama bomba limeachwa wazi huku nje kuna kimbunga kikali mnoooo

AKili ikaja tu ni mama wa yule binti
Nililala bila kutikisika huku nikiomba kimoyo moyo Mungu anilinde 😂😂

Asubuhi tumeamka chumba chote kimejaa maji kama bwawa

Siku hiyo hiyo Beatrice alipewa nauli aende kwao
Nyie mmejenga nyumba kwenye sehemu inapita maji mtaacha kupata mafuriko?

Acheni imani za kijinga.
Km ni kweli mpeleke huyo binti pale Haidaru au makanya.
Kuna shida kubwa sana ya maji. Tuone huo uchawi wake.
Watanzania wengine ni hasara tu kwa taifa.
Mnamaliza oxygen bure tu.
Bora ya mbuzi .
 
Nyie mmejenga nyumba kwenye sehemu inapita maji mtaacha kupata mafuriko?

Acheni imani za kijinga.
Km ni kweli mpeleke huyo binti pale Haidaru au makanya.
Kuna shida kubwa sana ya maji. Tuone huo uchawi wake.
Watanzania wengine ni hasara tu kwa taifa.
Mnamaliza oxygen bure tu.
Bora ya mbuzi .

Sawa mkuu.
 
Kuna kimbelembele mmoja kanishushua hapo juu sijui n muha wa kibondo,baada ya kusema kibondo n kiboko kwa washirikina
Washirikina wapo kila mahala.
Hapa tumeongelea WACHAWI na wewe na wenzako kudanganya umma kuwa wana uwezo wa kumdhuru mtu.

Hizo ni akili bange. Pigeni kazi acheni ujinga.
We kutokuwa na pesa sio kurogwa. Ni aisha uzembe wako au wakati wa Rizki yako haujafika . Na Mungu amekukadiria rizki unayostahili. Acheni imani za kijinga mtaathirika ubongo.
 
Wakuu habari zenu, ni matumaini yangu kuwa hamjambo.

Leo nataka kuweka ushuhuda wangu kwa niliyoyashuhudia live juu ya nguvu za giza, kwa wasioamini nadhani uzi huu hautakuwa na thamani kwao, kama na wewe unao ushuhuda usisahau kushea nasi.

1. Ushuhuda wangu unaanzia mwaka 1992 nikiwa nafundisha shule X wilaya ya Sengerema, kuna mwalimu nilikuwa nafundisha naye kituo kimoja.

Siku hiyo kuna kamvua kalinyesha sana, baada ya kupungua mwalimu mwenzangu alimuagiza mtoto wake wa kiume aliyekuwa akisoma darasa la kwanza kwenda kuchuma maharage shambani.

Bahati mbaya mtoto akiwa shambani aligongwa/aliumwa na nyoka na kupeleka kifo, tulifanya taratibu za mazishi na kumsitiri mtoto huyo.

Cha kushangaza mwaka 2008 mtoto huyo alionekana akiwa uchi na nywele ndefu sana alikuja moja kwa moja nyumbani na kupitiliza ndani nyumbani kwao, alikuwa ameshakuwa baba mzima, nywele zilikuwa ndefu sana pamoja na mikono iliyofikia usawa wa magoti.

Watu walistaajabu sana lakini hakudumu sana alifariki baada ya kukaa uraiani kwa wiki mbili.

2. Ushuhuda wangu bado unabaki huko huko Sengerema katika kijiji cha Bubandwamhela.

Nikiwa nafundisha shule X, kuna binti kijijini aliyekuwa akisoma darasa la saba aliugua ghafla baada ya kutoka shuleni.

Wazazi wake walipompeleka hospitali daktari aliwaambia mtoto hana ugonjwa, wazazi waliamua kujiongeza na kumpeleka kwa mganga wa jadi.

Cha kushangaza kesho yake shangazi ya binti alikutwa kwa mganga akiwa uchi, huku akiweweseka na akili zimemruka, shangazi mtu alikamatwa na kupelekwa kituo cha polisi lakini kwa kuwa serikali haiamini ushirikina aliachiwa huru, lakini hadi leo hii alishakuwa chizi. Binti yeye alipona kabisa.

3. Kisa cha tatu na mwisho ni hiki kilichotokea Liwale shule ya sekondari X nikiwa na walimu wenzangu ambao tulikuwa tunasoma chuo cha SAUT-Mtwara.

Tulipangiwa field katika wilaya ya Liwale ilikuwa mwaka 2009, mwanachuo mwenzetu akiwa zamu siku hiyo alikumbana na mtoto ambaye kwao iliaminika kuwa bibi yake alikuwa mtaalamu wa mambo ya giza.

Mwanafunzi huyo alichelewa kufika shule, mwalimu alipotaka kumuadhibu aligoma, wakasumbuana sana mwisho wa siku akamuadhibu yakaisha, jioni tukiwa uwanjani tunafanya mazoezi yule mwanachuo mwenzangu alianguka na kupoteza fahamu, ikawa jumla hadi kifo.

Kama na wewe umewahi kukutana/kushuhudia live ushirikina share nasi kisa chako watu tupate ilimu.

Mungu ni mwema siku zote.

Sent using Jamii Forums mobile app
Matukio ya kichawi yaakuandamba kila unapotia mguu...

Angalia usije ukawa una mikoba mahala inakusubiria|

Mimi niliwahi kuona majii na mapepo live kabisa. Nahisi viumbe wengine wazuri niliowahi kuona walikuwa labda ni malaika
 
Matukio ya kichawi yaakuandamba kila unapotia mguu...

Angalia usije ukawa una mikoba mahala inakusubiria|

Mimi niliwahi kuona majii na mapepo live kabisa. Nahisi viumbe wengine wazuri niliowahi kuona walikuwa labda ni malaika
Wewe kudai umeona majini na mapepo huenda ulikuwa bange ya Tabora.
Manake ile sio mchezo .
Bora za mwanza sio kali.

Au kuna mboga flani ya majani sisi wasukuma tunaita "mazzumelo"
Ukiila unaanza kuona viumbe wa ajabu.
 
Wewe kudai umeona majini na mapepo huenda ulikuwa bange ya Tabora.
Manake ile sio mchezo .
Bora za mwanza sio kali.

Au kuna mboga flani ya majani sisi wasukuma tunaita "mazzumelo"
Ukiila unaanza kuona viumbe wa ajabu.
Safi mkuu
 
Endelea kudanganywa.
Nyie ndio mnaambiwa albino analeta utajiri mkaenda kuua wanyonge .

Waafrika tuache imani za kipumbavu.
Tufanye kazi kwa bidii na uaminifu. Iko siku na sisi tutatoka kimaisha.
Vinginevyo tutaua mpk wazazi wetu kwa kudanganywa tutakuwa matajiri.
Ushenzi mtupu.
Sio unavyoamini ww basi waafrika waamini.
Na ndo maana dunia nzima matajiri wachache masikini wa kutosha.
Utajiri upo kwa waaminio tuu sio wasomi.
Na siku yakikukuta ndo utajua why kuna miungu mingine tofauti na hiyo waliyoileta hao jamaa watengeneza silaha zinazotumia na binaadamu kuua watu
 
Back
Top Bottom