Kama una Mtaji Njoo ufungue Gym Mkata Wilaya ya Handeni

Gai da seboga

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2019
Posts
515
Reaction score
1,015
Wasalam mabibi na mababu,

Kama mnavvojua wilaya ya handeni - Mkata kwa sasa ni sehemu inayokuwa kwa kasi sana.

Kuwepo kwa Ofisi za Halmashauri Mkata, Hospital kubwa ya wilaya, Lakini yote kwa yote ni mji uliokuwa na muingiliano na watu tofauti tofauti kama vile watumishi wa umma, wafanya biashara tofaut na hapo mwanzo mji ulikuwa na wenyej tu wenyewe wazigua.

Katika tafiti nilofanya Nimeona kuna watu wengi sana katika Mji huu ambao wanahitaji kufanya mazoezi kwa kupunguza mwili au kuweka mwili Fit lakini hakuna kasehem ata cha dawa cha kufanya mazoezi.

Hivyo kama una hela asee ukifungua gym utapiga hela sana huku mana wateja wapo wengi na mimi nikiwa Miongoni Mwao. Karibuni muwekeze bandugu
 
Hiyo fursa kwako mkuu,ianze na Wewe!
 
Mkata kwenye maji ya shida ata kama una hela ukitoka gym na hiyo mijasho sijui utafanyaje
 
Kijana wacha uwongo, Mkata hiyo ambayo umasikini umetawala, vibanda umiza vya kuangalia soka ni vya makuti, Nyumba za tope 80% katikati ya wilaya, Maji shida mpaka waende kuchota bwawani Dumu moja la lita 20 linauzwa 500/=?
Hicho kiingilio cha Gym unatoa wapi hao wateja zaidi ya watumishi wa umma watano au saba tu?
 
Gym Handeni πŸ€”πŸ€”
 
Mkata kwenye maji ya shida ata kama una hela ukitoka gym na hiyo mijasho sijui utafanyaje
Shida ya maji soon itakuwa historia mana kuna miradi toka mbweni na wami iko asilimia za tamati
 
Una mawazo mgando sn kwahyo unaona kila mtu maskini,! Kwa taarifa yako kuna watumishi zaidi ya 70 idara afya, elimu, Halmashauri had polisi tuko willing na gym ata kiingilio ikiwa laki Tatu kwa mwezi, tumekosa gym kias kwamb mpk tunakuwa na jogging za watumishi. Sasa tu nahitaji gym km una hela tuletee huduma hiyo.
 
Kwamba hawastahil? Hzo ideology zetu za zaman bhn, sasa hv mji una muingiliano wa Wageni wengi
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚kumbe ata wewe una ideology za zamani πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…