Kama una Ndugu au Mpenzi anafanya Biashara ya Magendo ya Mkaa Mlandizi na Kibaha mwambie aache kwani Askari Maliasili wa huko sasa hawatanii

Kama una Ndugu au Mpenzi anafanya Biashara ya Magendo ya Mkaa Mlandizi na Kibaha mwambie aache kwani Askari Maliasili wa huko sasa hawatanii

As lon as hawapotei kwamba watafika vituo vya police na hatimaye mahakamani salama hatuna shida nalo.

Kila Raia na ahukumiwe kwa kosa analofanya kwa mujibu wa sheria zetu.
 
Fujo zinatokea ,na polisi nao waliumizwa,ila kutumiaa risasi za Moto halikua Jambo zuri,sio la kufumbia macho
Police wa Tanzania na Africa wana operate ki analogy...wao kupiga ndiyo hatua yao ya kwanza ya upelelezi.
 
Dakika 30 zilizopita nimetoka Msibani Kumzika Mmoja wao ambaye Utumbo ulitoka Nje na ukarudishiwa kabla ya Kuzikwa.

Kesho tena kama nikipata Nauli na nikijua huko Msibani kuna Wali mzuri wa Nyama na Nazi naweza kwenda Kumzika mwingine huko huko.

Na kama kwa sasa ukiwa Unajiuliza ni kwanini ukiwa barabarani huwaoni tena Wabeba Mkaa / Mikaa katika Pikipiki zao na labda unayajua Majina yao jitahidi utembelee katika Makaburi ya Jirani unaweza ukayakuta huko yakiwa na Maua ya Kimaombolezo kwa juu.

Ikitokea una ama Ndugu yako au Mpenzi wako anayejishughulisha na Biashara hiyo ya Magendo ya Mkaa maeneo ya Mlandizi au Kibaha na kila ukimsihi asiende huko na bado analazimisha kwenda hakikisha akienda umuulize je, ikitokea Akafa huko angependelea azikwe Dar es Salaam au Kijijini Kwao Mkoani?

Askari Maliasili wa Mlandizi na Kibaha ( hasa Mkoa wa Pwani ) ambao Shughuli za Ukataji Miti holela na Biashara ya Magendo ya Mkaa inashamiri Hongereni kwa Kubeti na Roho za Watu na Mochwari wanazohifadhiwa kutokana na Utekelezaji wenu wa Kimedani.

Kinachonishangaza mno GENTAMYCINE ni jinsi Media za Tanzania zilivyo Kimya, hazijui Kunusa Taarifa Nyeti na Muhimu halafu Watu wa Kawaida mno ( tusio na mbele wala nyuma ) kama akina GENTAMYCINE tunazipata na hata Kushiriki katika Maziko au Kutembelea Wahanga ( Majeruhi ) Makwao au Mahospitalini.

Halafu Askari Maliasili wa Siku hizi je, huko Vyuoni Kwenu huwa mnafundishwa sana Somo la Kulenga / Shabaha?

Kwani Mashuhuda wa huko Mlandizi na Kibaha wasema mkiziinua tu Bunduki zenu na mkishusha Mtu Kaondoka mazima Ahera.
mzeee baba kumbe kuna wali mzuri na nyama msibani? hahaaaa nimecheka sana kama mazuri vile
 
Hao watu wametobolewa utumbo. Soma uzi uuelewe uanze kuleta ujuaji. Hakuna mauaji ya risasi yasiyomwaga damu.

Yaani mtu kamwaga utumbo halafu damu isitoke aiseee maajabu ya karne
Jirani yetu Mwamkinga wamemmwaga utumbo wiki lililopita aisee!!
Jamaa hawana huruma kabisa
 
Mkuu hii operation ya kuwaua wauza mkaa mbona wameianza muda tu takribani miezi3 sasa walimuua jirani yetu mmoja almaarufu kunguru jamaa alikuwa mwendesha boza ya mkaa.

Tulipigiwa simu na wasamalia wema kuwa kuna mwendesha pikipiki kapata ajali pande za msoga ila tumefika eneo la tukio pikipiki na mkaa vyote vipo salama ila mwili wa marehemu ulikuwa umepigwa na kitu kizito utosini.
Sasa hawa bodaboda si wasafirishaji tu au ndio wachoma mkaa huko porini?
Nafikiri wangekata mzizi(kiwanda cha kutengeneza mkaa) na si kukata matawi(wasafirishaji).
 
Asante kwa taarifa Genta, hiyo vita ilianza chinichini, rushwa. Wamekula sana rushwa hao, leo wanawaua kama wanyama pori.

Genta ukipata nauli, upate na kahela ka ndizi. Wali nazi na ndizi ndiyo kwenyewe.
Asisahau na kapilipili.
 
Mokaze mimi pia ni mtu wa Mara [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1] tuko mjini tunakula sana. Ugali na kichuri mpaka shughuli maalumu kwa hapa town.
Kasema mwenyewe akipata nauli, akale wali wa msibani [emoji16][emoji16][emoji16]
Kwamba ugali na kichuri? Yawezekana hujawahi taste.
Kichuri si mboga

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Serikali ishushe bei ya gesi ili wakazi wengi wa mijini waweze kumudu gharama za kutumia gesi na hivyo kupunguza matumizi makubwa ya mkaa.
 
Shosti nikujue ili iweje,kanywe chai huko ndo maana una stress
Wewe Auntie, nani kakuambia mimi huwa nakunywa chai?? --
Umeanza matusi??, Wee unanijua mimi??😏😏
 
Back
Top Bottom