Kama una stress pitia hapa, usiache kutupia na wewe maneno yako

HABARI NJEMA KWA WATUMISHI WA UMMA KUHUSU MADARAJA!

SERIKALI imetoa ufafanuzi RASMI kuhusu MADARAJA hii LEO. Kwa kuzingatia hali halisi ya nchi yetu na ukuaji wa uchumi pamoja na kuimarika kwa shilingi dhidi ya DOLA YA MAREKANI, Serikali inapenda kutoa ufafanuzi MADARAJA kama ifutavyo:

1. Daraja la Mkapa - lipo Mto Rufiji kupitia KIBITI.

2. Daraja la Kikwete - Lipo Mto Malagarasi huko Kigoma.

3. Daraja la Mwl Nyerere - lipo Bahari ya Hindi, unavuka kwenda Wilaya mpya ya Kigamboni.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
Watumishi wa Umma mnashauriwa kuwa wastahimilivu mnapovuka madaraja hayo ambayo ni viashiria vya maendeleo ya nchi yetu kwani mengine ni marefu sana!!! [emoji6][emoji6][emoji6][emoji6][emoji13][emoji13][emoji13][emoji13][emoji13][emoji16][emoji16]
 
```Kuna demu wa kizungu nimemuacha sasa anasema eti hawezi ishi bila Mimi..
Sasa nataka nimwambie "pambana na hali yako"....kwa kidhungu wanasemaje vile...!! Msaada tafadhali```
 
[emoji12][emoji12][emoji12][emoji12]

*Ukitaka kuchora tattoo angalia kwanza na umbo lako lipoje coz kuna dada hapa alikua mnene kajichora rose flower sasa hivi kakonda linaonekana kama tembele* [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
dah jmn kumbe kwenda kanisani raha sana

*Jana nimeenda church pasta akasema mgeukie jirani yako mwambie deni langu limelipwa na Yesu*

*ile nageuka tu nakutana na baba mwenye nyumba bas nikaongeza sauti ili asikie vizuri*


sasaivi katoka nje sijui kaenda kuniandikia risiti

[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
HEBU CHEKA UNENEPE!

Binti mmoja wa kitanzania alikuwa anasomea masomo ya kisayansi huko China muda wa miaka 20!
Alipofuzu na akaweza kugundua dawa ya kutozeeka, akawatumia wazazi wake kichupa cha dawa hiyo, wanywe tone moja moja wasizeeke!!
Baada ya miaka 10, akarudi Tanzania. akamkuta mama yake kawa binti, huku kabeba kitoto cha kiume mgongoni. Akafurahi sana kumkuta mama yake kawa binti!
Akamuuliza mama yake "baba yuko wapi"?
Mama akajibu "mwanangu, baba yako alipoona nimekunywa dawa, nimekuwa binti, yeye akanywa kichupa chote! Ndio huyu niliyembeba mgongoni!!.
Binti akazimia pale pale...
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Umetaka kuleta uvunjifu wa amani.
 
Umetaka kuleta uvunjifu wa amani.
Nilikuona mkuu hapo mgahawani ila uliniaibisha sana, maana ulikuwa umeagiza maji, pilipili na papai..
Siku nyingine agiza hata nyanya mbichi vitunguu na karoti ushushie na mirinda nyeusi bhaana [emoji13][emoji13][emoji38]
 
Nilikuona mkuu hapo mgahawani ila uliniaibisha sana, maana ulikuwa umeagiza maji, pilipili na papai..
Siku nyingine agiza hata nyanya mbichi vitunguu na karoti ushushie na mirinda nyeusi bhaana [emoji13][emoji13][emoji38]
Kulikuwa na kipande cha limao pia. [emoji23] [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…