Kama una uwezo jenga nyumba ya nyuma ni muhimu sana

Kama una uwezo jenga nyumba ya nyuma ni muhimu sana

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Rafiki yangu alipata eneo la nusu heka, aliamua kujenga nyumba ya nyuma ya vyumba vitatu na kimoja ni en-suite. Kwa kweli sikumuelewa, ingawa vyumba viwili aliwapa dada na kaka wa kazi na ensuite aliiweka kwaajili ya wageni.

Uchaguzi uliopita baba yake alikua mmoja wa wazee wa chama kimoja. Walizunguka na mgombea wao wa u Rais mikoani. Kwakua Chama si Chama tawala, kila msaada unahitajika katika Chama. Walipofika mkoa anaoishi rafiki yangu mzee alikwenda na wenzake watano kuishi pale kwa siku tatu.

Wakati huo huo mke wake alikua amejifungua na mama mkwe pamoja na mashemeji walikuwepo. Ile nyumba ya nyuma ilimsaidia kwa kiasi kikubwa.

Kama una uwezo nyumba ya nyuma ni muhimu.
 
NYUMBA ZA WAGENI au GUEST HOUSE zilizowekwa maalum kwa ajili ya kupokea wageni.

Tatizo wabongo skuhizi mmezigeuza kua SEX HOUSE kwenda mnapokua mnahitaji KUFANYA ngono.

Mambo ya kulaza wageni ovyo ovyo Nyumbani KWENU mtakuja kuleta MAJANGA Kwenye familia.
 
nyumba ya nyuma ni kuita matatizo. ni bora isiwepo kabisaaaaaa

sure am telling you my friend
Ukishakua na nyumba kubwa au nyumba ya nyuma, Ina vyumba wazi vipo kibao.

Kila mtu atajiskia kuja ovyo ovyo kwako, na bills zote utabeba wewe.

Wengine watakuja na wenza wao Moja kwa moja kuja kutafutia watoto nyumban kwako.

Jamaa ako anatoka kijijini anakuja na mkewe kukusalimia mjini kwa mkupuo wa miez 11.

Wakishamaliza kukusalimia wanarudi kwao na mtoto kabisa
 
Wabongo mnapenda kucomplicate sana maisha jenga nyumba hata kama ni 2 bedroom kama inatosheleza familia yako inatosha kabsa siku familia ikiongezeka unatafuta alternative sio ufanye k2 kisa wageni shiit...
 
Wabongo mnapenda kucomplicate sana maisha jenga nyumba hata kama ni 2 bedroom kama inatosheleza familia yako inatosha kabsa siku familia ikiongezeka unatafuta alternative sio ufanye k2 kisa wageni shiit...
Hata mi nashangaa Sana, yaani unahangaika kujenga nyumba nyingine kwa ajili ya watu wasiojulikana watakuja lini?

Jenga nyumba inayoweza kuwa na vyumba vya wageni Kama viwili hivi Basi, siyo nyumba nzima halafu unasubiri wageni shit!!!
 
Hata mi nashangaa Sana, yaani unahangaika kujenga nyumba nyingine kwa akili ya watu wasiojulikana watakuja lini?

Jenga nyumba inayoweza kuwa na vyumba vya wageni Kama viwili hivi Basi, siyo nyumba nzima halafu unasubiri wageni shit!!!
Tena ukimuweka mgeni nyumba ya pekeyake itamfanya awe comfortable sana ajihisi yuko makazi yake so tegemea wageni wakudumu..
 
Tena ukimuweka mgeni nyumba ya pekeyake itamfanya awe comfortable sana ajihisi yuko makazi yake so tegemea wageni wakudumu..
[emoji23][emoji23][emoji23], watakuwa wanaambizana anaweza kuweka kambi ya mwaka kabisa.

Unaweza kujikuta hata hiyo "nyumba ya nyuma" haitoshi, atakuja mama mkwe na shemeji yako (mdogo wa kike wa mkeo) na mdogo wako wa kiume[emoji1][emoji1], na hawawezi kulala pamoja[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Ukishakua na WAGENI wa Mara kwa Mara Nyumbani kwako unahatarisha usalama mzima wa familia yako.

Hasa hasa suala la maadili,
Mfano:
1. unamkaribisha mgeni anatumia vilevi kupindukia mfano sigara/bangi/pombe afu anashinda mchana kutwa nyumbani kwako na watoto Wako walioko likizo nyumbani.
[emoji117]Unategemea kimaadili wanao watasalimika?

2. Unamkarbisha mgeni wa kiume mwenye tabia ya uzinzi afu anakaa kwako mwezi mchana kutwa anazengea zengea TU Nyumbani kwako na binti zako wadogo.
[emoji117]Unategemea binti zako watasalimika?

3. Unamkarbisha mgeni wa kike mshirikina,
Afu anakaa kwako mwezi, sikU nzima anashinda na mkeo apo Nyumbani.
[emoji117]Hivi sikU ukija kuwekewa malimbwata na tego za kichawi utamlaumu Nani?

4. Unamkarbisha mgeni wa kike Ni mdangaji sugu mjini,
Afu anakaa kwako wiki/mwezi na sikU nzima anashinda na mkeo.
[emoji117]Hivi mkeo akianza kugongwa gongwa ovyo Unategemea utamlaumu Nani?

5. Unamkarbisha mgeni Ni JAMBAZI sugu Uko alikotokea,
Afu anashinda sikU nzima anazengea nyumabni kwako anachora TU ramani,
[emoji117]Hivi sikU ukija pigwa matukio utakuja mlaumu Nani?

Ni mengi Sana,
Ila sio Vema SAna kukaribisha karibishaa wageni hovyo Nyumbani kwako.

Niliwahi kua na iyo nyumba ya uwani, ila yaliyonipata ni mengi sn na siwez kuyaweka yote hapa.

Wageni walikua hawakatiki na familia kimaadili inavurugika kila sikU.

Nowdays,
Nakaa nyumba NDOGO TU ya vyumba 4 kuwatosha wanafamilia wangu Wote, na Sina chumba za ziada Wala Cha dharura.

Nna miti miwili ya kivuli na viti 6 vya plastiki na meza 2 kwa ajili ya kuwapokea wageni nje ya nyumba yangu ila ndani ya uzio.

Wageni Wote wa kulala ntawapeleka GESTI AU LODGE.

Wageni wa kuingia ingia ndani ya Nyumba yangu ni marufuku.

Narudia Tena, NI MARUFUKU[emoji45]
 
Dah!

Way way back awamu ya pili, nyumba tuliyokuwa tunaishi ilikuwa na 'nyumba ya nyuma' kama ulivyoitaja bibie...(eneo naliweka kapuni ila ni maeneo prime kwa Dar)

Sasa tulikuwa tunaishi na cousin bro's fulani, wale jamaa ni kama waliigeuza kile kijumba kuwa danguro, wadada walikuwa wanapishana tu toka 'kupigwa miti'...

Ila kama kawaida, asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu, jamaa sasa hivi wapo six feet under walishatafunwa na miwaya...
 
Rafiki yangu alipata eneo la nusu heka, aliamua kujenga nyumba ya nyuma ya vyumba vitatu na kimoja ni en-suite. Kwa kweli sikumuelewa, ingawa vyumba viwili aliwapa dada na kaka wa kazi na ensuite aliiweka kwaajili ya wageni.

Uchaguzi uliopita baba yake alikua mmoja wa wazee wa chama kimoja. Walizunguka na mgombea wao wa u Rais mikoani. Kwakua Chama si Chama tawala, kila msaada unahitajika katika Chama. Walipofika mkoa anaoishi rafiki yangu mzee alikwenda na wenzake watano kuishi pale kwa siku tatu.

Wakati huo huo mke wake alikua amejifungua na mama mkwe pamoja na mashemeji walikuwepo. Ile nyumba ya nyuma ilimsaidia kwa kiasi kikubwa.

Kama una uwezo nyumba ya nyuma ni muhimu.
Aikaeli anazo tano ktk mikoa mingi ya Tanzania umoja ni nguvu, Shauri yenu sukumaa gang
 
Back
Top Bottom