Kama unakopesheka CRDB kakope umsomeshe mwanao

Kama unakopesheka CRDB kakope umsomeshe mwanao

Carnivora

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2018
Posts
3,650
Reaction score
6,015
Habari za Jumapili ndugu wa JF

Mliowahi misa ya saa 12 punde mtarejea. Na wale wa saa 3 jiandaeni. Na wale wa sala kila siku naimani mmeipata ya alfajiri kwa uwezo wake Mungu Mkuu Aliyejuu. The Merciful, The Compassionate.

Baada ya utangulizi niende kwenye mada. Sote tunafahamu wanafunzi wa kidato cha 6 walifanya mitihani yao miezi kadhaa iliyopita. Wapo waliokwenda JKT pia na wengine tunao mitaani kwetu. Japo matokeo ya hayajatoka bado bali nina imani mmeanza maandalizi ya vijana hao kwenda elimu ya juu kwa kadri matokeo yao yatakavyokuwa.

Linapokuja suala la kufund elimu ya juu wazazi wengi au walezi wamekuwa wakitegemea zaidi bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB) kama plan ya kwanza. Ndugu zangu, hiyo bodi ni jipu. Na inaonekana ina baraka zote za serikali kwa namna inavyowafanya wanufaika wa mikopo hiyo linapokuja suala zima la ulipaji wa madeni. Nitaeleza baadae.

Ndugu yangu, kama unakopesheka na benki za biashara CRDB, NMB, TPB, NBC, n.k wewe nenda huko kaombe mkopo msomeshe mwanao. Tena muusie mwanao aombe vyuo vya serikali ili kupunguza gharama za ada na mambo mengine. Kwa mfano kwa vyuo vingi vya serikali ukikopa mil 3 inatosha kwa mwanao kuanza nayo chuo akamaliza semester zote mbili. Nyingine gharama ndogo ndogo mnajichanga amalize mwaka. Mwaka ukiisha kule CRDB na deni lako la mil 3 limekwisha, unakopa tena mwaka unaofuata. Maisha hivyo hivyo yaendelee. Ingawa wanafunzi hawataki kabisa kusikia suala la kutokuwa na boom, lakini muusie mwanao asijihusishe nalo kabisa. Watu wanalia kwa sasa.

Hao HESLB ni janga, janga kubwa. Kila siku wanalipa mikopo yao lakini deni halipungui. Na wanadai ukistaafu bado una deni eti wanakata pension yako. Mwajiri wako anaweza kuwa anakukata makato ya mkopo kwenye mshahara wako na hapeleki bodi ya mkopo, ukiwaendea HESLB wanasema sio kazi yao kumuwajibisha mwajiri apeleke!! Ni kichekesho. Sasa ni jukumu la nani? Ina maana wao wakae tu ofisini wasubiri maajabu yatokee? Mbona wenzao mifuko ya hifadhi za jamii wana kitengo cha kufatilia makusanyo...why not with HESLB?

Mfano umemaliza chuo unadaiwa mil 10 na bodi. Na ukapata ajira, tuseme una uwezo wa kulipa mil 2 kwa mwaka sababu ya kiwango chako cha mshahara. Mwisho wa mwaka utakuwa unadaiwa mil 8. Wao watakucharge 6% ya mil 8. Ambayo ni 480k. Kwa hiyo deni lako ni mil 8.48. Hivi hesabu hizi wamezipata wapi? Na kwanini? Mbona huko CRDB mtu anakopa mpaka miezi 84 (miaka 7) na riba ni ile ile. Kama ni 9% ni hiyo hiyo miaka yote. Ushajiuliza mwanafunzi wa udaktari aliyesomeshwa kwa miaka 5 na bodi ambae anadaiwa zaidi ya mil 30 hilo deni analimaliza baada ya miaka mingapi? HESLB is a disgrace.

Achana na hiyo 6% ya kila mwaka kwenye outstanding amaount. Kuna penalty ya 10% kwa kuchelewesha kulipa deni katika muda unaotakiwa. Ongezea 1% administration fee. Mkopo wa bodi ni ghali kuliko wa bank yoyote ile hapa Tanzania. Kama una uwezo wa kukopa kusomesha wanao fanya hivyo. Achana kabisa na hao jamaa. Ni wanyonyaji wenye baraka za serikali. Mikopo hiyo inawalenga watoto wa masikini, JPM huwaita wanyonge, lakini ndio anawanyonga kupitia hiyo bodi na sheria aliyosaini mwenyewe mwaka 2016. Akaweka na marejesho ya 15%.....hivi hapo kuna kuwajali wanyonge? kwa mshahara wa TGS D laki saba na ngapi sijui huyo mtu anabaki na Sh ngapi take home? Kijana huyo ndio aoe na asomeshe naye familia yake? They (sirikaali) must be kidding.

Nchi hii umasikini ndio uzalendo? People nowadays hawademand receipt after purchases, it doesn't help them anymore? 1.5T inapotea who cares? Halafu mimi nilipe mkopo wa HESLB, njooni mnikamate kama mnaweza. Silipi hata senti moja.

Msomeshe mwanao mwenyewe. Acha a na hilo dude linaoitwa bodi ya mikopo. Ni janga.
 
Lakini wtznia nikukosa umakini na weledi nakutozoea kusomesha watoto kwa kulipa ada...... kama nimeweza kulipia mtoto angu tangu primary ada ya 2m katika shule nzuri ya Engilish iweje nishindwe ku lipia ada ya laki 8 chuo kikuu kila semester.....tumezoea vitu vya bure ndomaana tunapigwa sana kwa kisingizio cha wanyonge......mtu anachukua kozi asio yitaka kwasababu ya mkopo wakati mkopo ni gari kuliko kujilipia "cheap things are always expensive" wazazi amkeni elimu ni investment sio msaada
 
SIKUBALIANI NA WEWE.

NAWASHAURI VIJANA WAKOPE HESLB TUU KWA SABABU HIZI:

1. KAMA WATAFANIKIWA KUAJIRIWA HAPO BAADAYE WAJUE UCHUNGU WA PESA UKOJE. WATOTO WA SIKU HIZI WAMEKUA KWA SPOON FEEDING NYANJA ZOTE, HAWAJUI MAISHA KABISA KWA HIYO SIKU WAKIPATA AJIRA WAKAANZA KUKATWA AKILI ZITAWAKAA SAWA.

2. SERIKALI HAIJAFANYA ANALYSIS YA ELIMU YENYE TIJA KABISA. VYUO VIMEJAA KOZI NYINGI AMBAZO HAZINA FUTURE MBELENI KABISA. SASA YA NINI KUHARIBU PESA YAKO KUSOMESHA MTOTO WAKATI HUNA UHAKIKA KAMA ATAAJIRIWA?
YA NINI MZAZI UINGIE HASARA? BORA UWAPE HASARA HAO HAO HESLB.

CONCLUSION: KULIKO KUCHUKUA MKOPO NA KUMSOMESHA MWANAO CHUO KIKUU NI BORA UMPE HIO PESA KAMA MTAJI AKISHAMALIZA CHUO ILI AANZE NAYO MAISHA.


 
Umesoma mpaka mwisho.

Ungesoma mpaka mwisho na wewe usingeamua kuwa mbishi tuu[emoji4]
Yaani wajue uchungu wa fedha

Hivi unafikiri vizuri mkuu

Mtoto kujua uchungu wa pesa mpaka akatwe na HESLB

nadhani umeamua tu kubisha au heslb ime kufrustrate
 
Mimi hawa washenzi wameshanikama na sina pa kutokea, nalipa bila kupenda
 
Kingsmann,

Asante kwa mawazo yako. Kozi zote lazima ziwepo. Hata political science lazima iwepo. Ajira ni issue nyingine. Na future sio lazima ajira.

Rudi shule kajifunze maana halisi ye elimu mkuu.
 
mulwanaka,
Mkuu wewe una pesa mkuu. Sisi wenzako wapo ndugu zetu wanashindwa kuhudhurio ya kiukoo kisa hawana elfu 1 ya nauli kuja na kurudi sehemu ya tukio. Naweza kusema hili halikuhusu.

Na nyie mpo wachache sana katika population ya watanzania wengie.
 
ningelijua ningeishia semister ya 5 as if nimedisco mkataba uvunjike kama ni knowledge nimeshapata vyeti ni makaratasi tu nimeviwekea fremu vinaning'inia ukutani kwa sababu nilishajiapia sitokaa niajiriwe
 
Mkuu wewe una pesa mkuu. Sisi wenzako wapo ndugu zetu wanashindwa kuhudhurio ya kiukoo kisa hawana elfu 1 ya nauli kuja na kurudi sehemu ya tukio. Naweza kusema hili halikuhusu.

Na nyie mpo wachache sana katika population ya watanzania wengie.
Kaka nimazoea watanzania zaidi ya 40% tunauwezo wa kusomesha watoto wetu isipo kua tuna dhana potofu kuona kwamba kua masikini/mnyonge ni sifa fulani natumezoea kuomba msaada kwa serikali ambao ni gharama kuliko kujitafutia mwenyewe, tunahitaji new "mind set" ili kuweza hu mfumo wa ubepari/ capitalism...sio rahisi mfanya kazi/mfanya biashara kushindwa ku save laki 8 kwa mwaka ili alipe ada ya mwanae...... " if you think education is expensive try ignorence "...wataalamu wanasema
 
Back
Top Bottom