Kama unatafuta nyumba ya kupanga DSM, kuna vitu vya kuzingatia usivichukulie poa!

wee namba moja NO and YES, nakumbuka nilipanga kihonda manyuki moro kwa mama mmoja mstaafu raha sana...nilikuwa nakaa naye, bill zote tuna share. umeme ukiisha ananiambia mwanangu umeme umeisha ulete hela kama huna tafuta siku mbili tatu ulete, tulikuwa wapangaji wawili tu na geti alikuwa ananiachia wazi..mimi peke yangu nilikuwa na usafiri, narudi usiku najua namna ya kufungua geti then nafunga hakuna wa kutoka wala kuingia tena, maji kama kawaida...mwanangu leta hela uliyonayo najua wewe bachela hutumii sana😛. kodi ikikaribia ananikumbusha kama hukumbuki anza kujipanga kodi..siku ikifika mwanangu huna mbona hujaja kuniambia maisha ndivyo yalivyo utapata utaileta tu. Namkumbuka sana yaani. mwengine nilikuta wapangaji wanne na kausafiri kangu hakuwa na shida hata nikirudi saa 5 geti wamefunga nampigia simu anamka anafungua...ila hawa nilikuwa nawahisha kodi😎...msimu wa mvua nilisafiri nikarudi usiku saa nne duuu..naiona nyumba ila siwezi kuifikia maji yameziba njia...nikarudi kwa mtendaji mazimbu road nikapaki usafiri kwa kulipia..nikaenda kwa miguu..viatu mkononi nikaloana hadi kiunoni...tangu hapo kodi ilipoisha nikajiondokea ila hadi kesho tunaheshimiana sana na mwenye nyumba yule😀😀
 
Yote uliyoanisha ni ya msingi sana
Nilipanga sehem jirani akaninyima penzi halafu akaanza kuweka nyimbo za majigambo namna ye na jamaa yake wanapendana dah ilibidi nihame
Alafu usiombee nyimbo iwe Ile Taarabu 🤣🤣🤣🤣 ya Mzee Yusuph

Yarabii iweee Salaamaa!! Salama Usaliminii
Wasipate Yakusemaa Roho zao ziwaumee
Walopaaangaa Tuachanee Roho zaoo Ziwaumee😝😝😝😝🤣🤣😄

Na Mimi yalinikuta mkuu baada ya Kukosa Penzi la demu mmoja wa Kitwangaa toto lilofundwa nikapigiwa huu utenzi
Nyumba za Kupanga hizi Astaghafirulaaah laana tunlaah!!😆😆😆😆😆
 
hao tuko wengi tunasema dunia njia na hatuwezi kujenga njiani,...🤒🤒
 
Otherwise utajikuta unawahi kurudi kuogopa kufungiwa geti kama mtoto. Zamani nilikua ata saa 8 usiku naweza kutoka sahivi nawahi home saa 4 wasije funga geti. Nishalalamika ila ndio ivo, kila siku ahadi hewa.
Hapo nimekuelewa mkuu
 
Kuna chumba nlipanga aiseee kajukuu ka mwenye nyumba ka kike around 3 yrs kakaweka mazoea ya kunivamia geto kakikuta nakaanga dagaa kanatoka kanamwambia bibi anko anakaanga nyama nataka nyama.basi kiki8va nakapea
Mama mwenye nyumba nyingine akawa na mtindo wa kukaa karibu na mlango wangu nkipika anakuja anasema ana ugali mboga hama nimpee.yaani ni shidaa tupu
 
Kuna tatizo gani kuishi na mwenye nyumba?

Nifafanulie mapungufu hayo ili nami nijifunze kitu.

Halafu kufunga mageti mapema ni kero isiyomithilika, kwa nini asichongeshe funguo za geti kila mpangaji akakaa na nakala yake ili kuwe na uhuru wa mtu kurudi muda anaoutaka?
 
 
Hahaha
 
Huna hiyo nyumba upanga acha kutulisha chai mkuu
 
Atakwambia usalama
 
Kikubwa mwenye nyumba asikar hapo hapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…