Kama unatafuta nyumba ya kupanga DSM, kuna vitu vya kuzingatia usivichukulie poa!

Kama unatafuta nyumba ya kupanga DSM, kuna vitu vya kuzingatia usivichukulie poa!

Mm mama mwenye nyumba ananiibia mabeki 3 zangu sio poa. Anawatafutia KAZI kwingine kisha uko anataka pesa ya nauli kwao ndio anawapeleka.mmoja kashindwa aliko pelekwa ndio kumpigia wife simu na kusema ilivyo kua. Na pia nackia mama mwenye nyumba kasema kua kila nikileta beki 3 atakua anawauza kwa wengine. Nimepata mzuka wa kumaliza kibanda changu ili mwezi ujao nisepe kwangu tu.
All the best
Aisee inakera na kuumiza.
 
Mjenge za kwenu na nyie muweke hayo masharti.
Umefikiria kwa akili fupi, nyumba sio gari ndugu, kuwa utaenda nayo popote.
Kama sehemu ya utafutaji wako ipo permanent utakuwa sawa.
Kumbuka wengine ni wafanyakazi kazi wanaweza kuhamishwa kutoka kituo fulani kwenda kitua kingine au mfanyabiashara akahamisha biashara mkoa mwingine.
 
Nunua kiwanja hata hatua 12 kwa 24.ujenge geto janja,acha utumwa,hizo laki sita utafyatua tofali kibao na kigeto ujanja kiko kama castle house full ujanja,hebu hizo posho unganisha ujenge geto ujanja au cheza mchezo wa kazini.
Unafikiri ukijenga ndo Kero zinaisha?....Bora ukipanga ukipata Kero unahama chap, hata kabla ya kumaliza mkataba. Ukijenga ni kama ndoa ya Katoliki.
1. Umeanza ujenzi fresh, je unaijua matumizi ya kiwanja Cha jirani yako? Wanafunga trubali mkesha daily.
2. Mara jirani anakushitaki umehamisha mpaka, Kila siku mnapelekana Kwa mjumbe. Kutokana na hilo bifu mnajikuta hamuongei Wala kusaidiana Kwa shida Wala Raha.
3 Mara kutokea chizi kafunga njia (unakumbuka issue ya Shukuru Kawambwa?)
4. Mara majirani zako washirikina, Kila asubuhi unakuta vichwa vya kuku na damudamu kwenye kibaraza chako.
5. Unataka ufunge maji jirani anakataa mtu asichimbe kwenye eneo lake. Unatafuta njia mbadala Jirani aliekataa usipitishe maji unakuta kaunga tawi kwenye maji Yako.

Bora tuendelee kupanga, tunakuwa na option nyingi nyingi.

Labda ujenge ushuani ambako Kila kitu planned.
 
Unafikiri ukijenga ndo Kero zinaisha?....Bora ukipanga ukipata Kero unahama chap, hata kabla ya kumaliza mkataba. Ukijenga ni kama ndoa ya Katoliki.
1. Umeanza ujenzi fresh, je unaijua matumizi ya kiwanja Cha jirani yako? Wanafunga trubali mkesha daily.
2. Mara jirani anakushitaki umehamisha mpaka, Kila siku mnapelekana Kwa mjumbe. Kutokana na hilo bifu mnajikuta hamuongei Wala kusaidiana Kwa shida Wala Raha.
3 Mara kutokea chizi kafunga njia (unakumbuka issue ya Shukuru Kawambwa?)
4. Mara majirani zako washirikina, Kila asubuhi unakuta vichwa vya kuku na damudamu kwenye kibaraza chako.
5. Unataka ufunge maji jirani anakataa mtu asichimbe kwenye eneo lake. Unatafuta njia mbadala Jirani aliekataa usipitishe maji unakuta kaunga tawi kwenye maji Yako.

Bora tuendelee kupanga, tunakuwa na option nyingi nyingi.

Labda ujenge ushuani ambako Kila kitu planned.
Wakati Uingereza inaenda kuitawala America walipambana na mengi,kwa taarifa tuu hizi kero za.maisha ndo maisha yenyewe,uwe na Raha katika dunia hii ili iweje,Unaweza ukawa.na majirani wazuri tuu kumbe mke wako kitanda kimoja ndo mwanga mwenyewe anaweza kuwa vizuri kumbe mkweo kila siku anakuwangia,jitahidi sana kuishi maisha yako,hata hao wanaokukera nao pia wanapambana na luku na bili za maji na watoto machixi kila siku. In fact wanga kila Kona wapo hadi Kizmkazi wapo,kulala ikulu kuwaza li nchi lenye wezi kila Kona unafikiri kazi ndogo.
 
Nilikua kwenye nyumba ya kupanga, nzuri tu. Tatizo mwenye nyumba akapandisha bei kwa asilimia zaidi ya 25, bila taarifa mapema.

Nikaona sio shida, nikahama mkataba ulivyoisha. Sasa katika harakati za kutafuta nyumba, kuna vitu nimejifunza na vingine nimeshachelewa nimejikuta najuta tayari niko ndani.

Baadhi yake:

1. Usikae na mwenye nyumba.

Nilipokua zamani nilikua sikai na mwenye nyumba. Anakuja mara chache sana. Ila sahivi nimeyatimba.

Hafu mwenye nyumba ana shughuli kila siku, mazingira yapo ovyo wala sio masafi kwasababu yeye tu ana ndugu zaidi ya 8 na watoto, ukijumlisha mnashare uwanja, aisee.

2. Jitahidi msiwe mna-share bili/matumizi ya maji au umeme.

Iwe na wapangaji wenzako au mwenye nyumba, jitahidi sana ulipie bili mwenyewe.

Ikitokea umebanwa sana bdsi angalau muwe wawili mwisho. Sub-meater hazitasaidia kitu. Mtatoa kila mtu 20,000/= ya umeme kwa mwezi wewe unashinda kazini ukirudi unawasha feni tu, kuna sista duu anachemsha maharage kwa presha cooker.

Lazima mtagombana tu.

3. Hakikisha nyumba imekamilika ujenzi, asikudanganye lipia tu namalizia wiki ili kuweka madirisha sijui.

Unavyoenda kukagua eti nyumba haijakamilika choo au dirisha, akasema lipia namalizia mtego huo.

Ukishalipia tu imeisha. Utakuta jikoni hakuna sink, feni ya sebuleni haweki, na ata maji unaweza kuta akachelewa kuyaingiza.

Jitahidi uende nyumba iliokamilika kila kitu.


4. Kama una gari, angalia upatikanaji wa funguo za geti.

Otherwise utajikuta unawahi kurudi kuogopa kufungiwa geti kama mtoto. Zamani nilikua ata saa 8 usiku naweza kutoka sahivi nawahi home saa 4 wasije funga geti. Nishalalamika ila ndio ivo, kila siku ahadi hewa.

5. Zingatia idadi ya wapangaji wenzako.
Kama unaweza, jitahidi wapangaji muwe wachache. Mkiwa kikosi kuna faida na challenge zake. Faida moja wapo unaweza pata mke hapo hapo. Ila hasara unakuta challenge hadi kwenye kamba za kuanika mfano weekend mkifua wengi kwa pamoja, makelele kila mtu akiweka singeli nk.


6. Uliza kuhusu utaratibu wa bili za maji taka, takataka/usafi na ulinzi shirikishi.

Hii michango haiwagi mikubwa ila nayo ni kero.
Kuna hii ya maji taka kuyatoa kwasababu shimo limejaa, michango ya wale wazoa takataka na ulinxi shirikishi.

7. Zingatia msimu wa mvua kunapitika? Mafuriko na nyumba kuvuja?

Kuna nyumba msimu wa mvua hazifikiki sio kwa gari wala kutembea, pia kuna uwezekano mvua ikinyesha nyumba ikawa inavuja.

8. Kelele/mishemishe za majirani.

Unaweza ukawa umeenda kucheki nyumba ukakuta pako cool, kumbe jioni kuna bar uchwara inapiga music usiku kucha.

Au ukakuta weekend au jioni ni nyumba za ibada wanatumia maspika ww unasema unapumzika wao wakakiwasha.

Edit:

9. Uchumi ukiruhusu tafuta chumba chenye choo ndani.

Kama uchumia na mazingira yanaruhusu, epuka nyumba zenye vyoo vya kushare. Kuna watu ustaarabu mdogo sana .

Kwa sasa nimeyatimba, ila kutaka kuforce kukaa Makongo Juu kumeniponza. Nikimaliza Kodi yangu naamsha.
Aisee ni kweli mkuu, changamoto
 
Kwenye safari ya maisha kupanga chumba/nyumba ni sehemu ya kujitafuta. Uchumi wako ndo unaamua upange Kimara au Mbezi beach. Mbagala au Makongo.

Nakumbuka mara ya kwanza napanga chumba baada ya chuo, wahuni walinikaribisha kitaa kwa kuniibia kila kitu getto. Ulikuwa ubatizo kwa maji ya moto.
 
Jenga ya kwako hata Chumba kimoja hii itaweka huru
Huyu jamaa anakumbusha, vitu vya kuzingatia, unapohitaji kupanga, mfano kwa wafanyakazi, Unaweza kuwa na nyumba hata nne, ila ukapata uhamisho, kwenda kufanyia kazi mji mwingine.
.
.Hivyo, ukalazika kupanga, kuna jamaa kipindi cha ujenzi wa barabara mwendokasi Ubongo kimara, yeye akiwa mkazi wa mbezi, na anafanya biashara kariakoo, na huko mbezi alikua anaishi nyumba yake mwenyewe, gari lakutembelea alikua nayo, ila alilazimika kupanga nyumba magomeni, kutokana hali ilivyokua.
.
KIpindi kile kutoka kariakoo mpaka mbezi, unakata masaa 7 hadi 8 hivyo kupanga hakuna mwisho.
.
 
Back
Top Bottom