Zaidi ya 90% ya vijana wanaokwenda chuo siku hizi wanakwenda kupoteza muda wao na kutengeneza mazingira ya kuwa frustrated siku zijazo.
Siku hizi hata ukimaliza chuo na ufaulu mkubwa unatakiwa uwe na bahati kubwa sana ili uweze kupata ajira.
Badala ya kupoteza muda mwingi na fedha nyingi kwenda chuo ni bora ukaenda Kariakoo ukaanza kufanya biashara yoyote ile unayoweza kufanya na kwa mtaji wowote ule ulionao.
Fanya hata biashara ya kutembeza maji ya kunywa tu na endelea kujijenga katika biashara yako bila kukata tamaa utaniambia baada ya mwaka, miwili au mitatu rafiki zako waliokwenda chuo watakuomba uwarushie mia.
Usipoteze muda na fedha zako kwenda kujitayarishia frustration na kuchelewa kimaisha ukitafuta elimu isiyo na manufaa maishani.
Yatosha tu siku hizi kuwa na fedha za kukidhi mahitaji yako kwani ni fedheha kubwa kuwa na elimu pasipo kuwa na fedha.
Kumbuka kuwa hata hao wanaokwenda chuo mwishowe wanatarajia wataajiriwa na kupata fedha. Kwanini usianze kujiajiri mwenyewe sasa kuliko kusubiri hadi upoteze muda na fedha zako kwanza?
Ukitaka nenda kasome baada ya kuwa na uchumi wa uhakika utafurahia maisha yako zaidi.
Siku hizi hata ukimaliza chuo na ufaulu mkubwa unatakiwa uwe na bahati kubwa sana ili uweze kupata ajira.
Badala ya kupoteza muda mwingi na fedha nyingi kwenda chuo ni bora ukaenda Kariakoo ukaanza kufanya biashara yoyote ile unayoweza kufanya na kwa mtaji wowote ule ulionao.
Fanya hata biashara ya kutembeza maji ya kunywa tu na endelea kujijenga katika biashara yako bila kukata tamaa utaniambia baada ya mwaka, miwili au mitatu rafiki zako waliokwenda chuo watakuomba uwarushie mia.
Usipoteze muda na fedha zako kwenda kujitayarishia frustration na kuchelewa kimaisha ukitafuta elimu isiyo na manufaa maishani.
Yatosha tu siku hizi kuwa na fedha za kukidhi mahitaji yako kwani ni fedheha kubwa kuwa na elimu pasipo kuwa na fedha.
Kumbuka kuwa hata hao wanaokwenda chuo mwishowe wanatarajia wataajiriwa na kupata fedha. Kwanini usianze kujiajiri mwenyewe sasa kuliko kusubiri hadi upoteze muda na fedha zako kwanza?
Ukitaka nenda kasome baada ya kuwa na uchumi wa uhakika utafurahia maisha yako zaidi.