Limbalangule
Senior Member
- Jun 14, 2023
- 131
- 264
Hongera Kwa ujumbe mzurioyah kuwa na huruma basi alfu nina elfu tano hapa badilisha ilo jina nikutumie[emoji23]
Sent using Jamii Forums mobile app
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hongera Kwa ujumbe mzurioyah kuwa na huruma basi alfu nina elfu tano hapa badilisha ilo jina nikutumie[emoji23]
Mkuu sijapenda kulitumia hili jinaoyah kuwa na huruma basi alfu nina elfu tano hapa badilisha ilo jina nikutumie😂
• Haki ya kiuchumi aendelee kubaki nayo mwenyewe, kwa sababu tayari nimeshaona haita nisaidia nitakavyo....(labda angeeleza kuhusu BUSINESS START WITH ZERO CAPITAL) 🤗🤗, kidogo ningemuelewa.Kwanza kabisa, hujui haki ya kiuchumi ya muandishi.
Pili, kufanya kwa vitendo wewe mwenyewe hai guarantee kuweza kufundisha vizuri zaidi.
Kuna watu wana kipaji cha kufanya vizuri, hawawezi kufundisha vizuri.
Na kuna watu wana kioaji cha kufundisha vizuri, lakini hawana kipaji cha kufanya vizuri.
Sasa, utakataa ujuzi wa profesa anayejua kufundisha biashara vizuri kuliko Mangi mwenye duka kwa sababu profesa hana duka?
awapii we tuambie tu hapahapaMkuu sijapenda kulitumia hili jina
Njoo inbox nikwambie sababu
Uko sahihi mkuu!Dhana kuwa mambo hufuata watu ndani ya ukoo ina ukweli wake na mifano yake ipo wazi tu, tukiachana na mfanano wa vinasaba pia hata mazingira huchangia hali hiyo japo kwa ulimwengu wa kiroho watalaam wanasema kuna roho huwa zinatembea ndani ya ukoo fulani.
Ulimwengu wa kitajiri na maskini kuna koo utakuta ni tajiri kutoka Babu mpaka mjuu na kuna koo utakuta ni maskini kuanzia Babu mpaka mjukuu na hapo ndipo kwenye dhana ya urithi wa utajiri na umaskini.
Umewahi kuona ukoo fulani mtu mmoja tu ndio tajiri ila wengine wote ni maskini? Kama ndio Jaribu kufuatilia historia ya huyo mtu lazima katumia nguvu kubwa kuwa hivyo wa pekee na hiyo nguvu ndio inaitwa nguvu ya kujiengua kutoka kwenye ukoo maskini na kujitengenezea ukoo tajiri vivyo hivyo kuna mtu maskini ila wengi kwenye ukoo wake ni matajiri basi huyo yupo anajiengua kutoka ukoo tajiri na kutengeneza ukoo wake maskini.
Sio kazi kubwa kujijua upo kwenye ukoo upi bali angalia tu viashiria kama kwenu hakuna tajiri na historia ya babu zako pia hali ilikuwa hivyo hivyo basi jua una kazi kubwa ya kufanya kuukana ukoo huo na kutengeneza ukoo mpya tajiri (sina maana uukane kuwa wewe sio mwana ukoo la hasha bali uukane umaskini unaotembea kwenye ukoo wenu), Sasa uta ukana vipi?
HAYA NDIO MAMBO YA KUFANYA ILI KUACHANA NA UKOO MASKINI NA KUTENGENEZA UKOO MPYA TAJIRI
1. Kwenye kuoa/kuolewa jitahidi uambatane na mtu ambaye sio maskini wa fikra (anaweza kuwa maskini wa kipato ila asiwe maskini wa fikra yaani akilini awe tajiri ajaye tena kwa vitendo).
2. Usisumbuke kumaliza umaskini wa ukoo wenu hili hutaweza bali nawe utaishia kuwa maskini pia bali anza kuandaa utajiri mpaka utakao wazaa waukute ili waanzie pale ulipoishia wewe.
3. Kubali kulaumiwa na wana ukoo bali usiache kuwa sawa nao maana ukianza kujipata lawama zitakuwa nyingi sana na hasa pale utapokuwa ukikwepa mizigo yao kwa mfano wataanza kutaka usomeshe watoto wao wote, uwajengee nyumba na mengine mengi lakini je kweli ukiwafanyia hivyo utatoboa?
3. Wekeza kwenye mipango ambayo hata ukifa yenyewe haifi bali itaendelea kuishi na hivi ndivyo wafanyavyo matajiri wote ambao wanataka utajiri wao usife pindi wao wakifa.
4. Usikubali kuwa mshirikina ili upate utajiri hapa nawe utakuwa maskini tu kwa sababu kwenye hizo imani za kishirikina kuna laana tupu na kuna ambao wameishia jela na hata utajiri hawajapata, kufikiria utajiri kwa njia ya kishirikina ni matokeo ya uvivu wa kufikiria na kukosa utulivu wa subira.
4. Andaa watoto wako kuwa matajiri pindi wakiwa wadogo na kwenye hili uwe mkali kidogo kwa sababu wanaweza kulemaa wakihisi hata wasipo pambana bado tu watarithi utajiri wako, waandae zaidi kuendeleza mali na sio kurithi mali.
5. Usikate tamaa kizembe ukiona harakati zinakuwa ngumu kwako usianze kujifariji kwa kauli zisizo faa na za kimaskini kama vile.
"Maisha ndio haya haya"
"Maskini pia ni mtu"
"Sisi kwetu ndivyo tulivyo hatuwezi biashara"
Hizo ni kauli za kimaskini na zisizo na ukombozi wowote ule kifikra bali kukukandamiza tu kuwa maskini zaidi.
Makala hii imeandikwa na Mwanasayansi Saul kalivubha.
#fikia ndoto zako.
😊Itasikitisha sana huyo mwandishi(Mwanasayansi Saul kalivubha) kama atakuwa maskini kiuchumi.. 🤒🤒
Asante sana ndugu🤝🤝👏👏
kongole kwa hizi +ve vibes
naunga mkono 100% japo hujaeleza "How?"
Watanzania wengi ni wafitini watu wa kulalamika, watu wenye gubu, muda wa kupambana kutafuta mali wanatumia kuwalaumu wengine kama wakina wajomba baba wadogo, mashangazi makaka na kina Kiranga kisa wanadhani kila kitu kipo mezani wao waambiwe tu nenda pale chukua hizi pesa fanya hichi, hawana uthubutu wa kujiongeza k
Hili linatukwamisha sanaWatanzania wengi ni wafitini watu wa kulalamika, watu wenye gubu, muda wa kupambana kutafuta mali wanatumia kuwalaumu wengine kama wakina wajomba baba wadogo, mashangazi makaka na kina Kiranga kisa wanadhani kila kitu kipo mezani wao waambiwe tu nenda pale chukua hizi pesa fanya hichi, hawana uthubutu wa kujiongeza kabisa.
Kizungu ukoo "clan" ni family ties.. beyond the common grandfatheers name. Mana Leo Kina mushi popote walipo walisema ukoo mzee sio poaMaana ya ukoo ni nini?
Kwasababu kuna watu nakutana nao wana jina langu la ukoo ila siwafahamu....
NondoDhana kuwa mambo hufuata watu ndani ya ukoo ina ukweli wake na mifano yake ipo wazi tu, tukiachana na mfanano wa vinasaba pia hata mazingira huchangia hali hiyo japo kwa ulimwengu wa kiroho watalaam wanasema kuna roho huwa zinatembea ndani ya ukoo fulani.
Ulimwengu wa kitajiri na maskini kuna koo utakuta ni tajiri kutoka Babu mpaka mjuu na kuna koo utakuta ni maskini kuanzia Babu mpaka mjukuu na hapo ndipo kwenye dhana ya urithi wa utajiri na umaskini.
Umewahi kuona ukoo fulani mtu mmoja tu ndio tajiri ila wengine wote ni maskini? Kama ndio Jaribu kufuatilia historia ya huyo mtu lazima katumia nguvu kubwa kuwa hivyo wa pekee na hiyo nguvu ndio inaitwa nguvu ya kujiengua kutoka kwenye ukoo maskini na kujitengenezea ukoo tajiri vivyo hivyo kuna mtu maskini ila wengi kwenye ukoo wake ni matajiri basi huyo yupo anajiengua kutoka ukoo tajiri na kutengeneza ukoo wake maskini.
Sio kazi kubwa kujijua upo kwenye ukoo upi bali angalia tu viashiria kama kwenu hakuna tajiri na historia ya babu zako pia hali ilikuwa hivyo hivyo basi jua una kazi kubwa ya kufanya kuukana ukoo huo na kutengeneza ukoo mpya tajiri (sina maana uukane kuwa wewe sio mwana ukoo la hasha bali uukane umaskini unaotembea kwenye ukoo wenu), Sasa uta ukana vipi?
HAYA NDIO MAMBO YA KUFANYA ILI KUACHANA NA UKOO MASKINI NA KUTENGENEZA UKOO MPYA TAJIRI
1. Kwenye kuoa/kuolewa jitahidi uambatane na mtu ambaye sio maskini wa fikra (anaweza kuwa maskini wa kipato ila asiwe maskini wa fikra yaani akilini awe tajiri ajaye tena kwa vitendo).
2. Usisumbuke kumaliza umaskini wa ukoo wenu hili hutaweza bali nawe utaishia kuwa maskini pia bali anza kuandaa utajiri mpaka utakao wazaa waukute ili waanzie pale ulipoishia wewe.
3. Kubali kulaumiwa na wana ukoo bali usiache kuwa sawa nao maana ukianza kujipata lawama zitakuwa nyingi sana na hasa pale utapokuwa ukikwepa mizigo yao kwa mfano wataanza kutaka usomeshe watoto wao wote, uwajengee nyumba na mengine mengi lakini je kweli ukiwafanyia hivyo utatoboa?
3. Wekeza kwenye mipango ambayo hata ukifa yenyewe haifi bali itaendelea kuishi na hivi ndivyo wafanyavyo matajiri wote ambao wanataka utajiri wao usife pindi wao wakifa.
4. Usikubali kuwa mshirikina ili upate utajiri hapa nawe utakuwa maskini tu kwa sababu kwenye hizo imani za kishirikina kuna laana tupu na kuna ambao wameishia jela na hata utajiri hawajapata, kufikiria utajiri kwa njia ya kishirikina ni matokeo ya uvivu wa kufikiria na kukosa utulivu wa subira.
4. Andaa watoto wako kuwa matajiri pindi wakiwa wadogo na kwenye hili uwe mkali kidogo kwa sababu wanaweza kulemaa wakihisi hata wasipo pambana bado tu watarithi utajiri wako, waandae zaidi kuendeleza mali na sio kurithi mali.
5. Usikate tamaa kizembe ukiona harakati zinakuwa ngumu kwako usianze kujifariji kwa kauli zisizo faa na za kimaskini kama vile.
"Maisha ndio haya haya"
"Maskini pia ni mtu"
"Sisi kwetu ndivyo tulivyo hatuwezi biashara"
Hizo ni kauli za kimaskini na zisizo na ukombozi wowote ule kifikra bali kukukandamiza tu kuwa maskini zaidi.
Makala hii imeandikwa na Mwanasayansi Saul kalivubha.
#fikia ndoto zako.