Pre GE2025 Kama Upinzani unataka mafaniko ya kweli 2025, Iachane na Urais, Ujikite Serikali za Mitaa, Ubunge na Udiwani, Urais labda 2030!

Pre GE2025 Kama Upinzani unataka mafaniko ya kweli 2025, Iachane na Urais, Ujikite Serikali za Mitaa, Ubunge na Udiwani, Urais labda 2030!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wasipochukua 2025 hawana nafasi nyingine kabisa. CCM hawana kipa anaeuzika hata aliyopo bora liende.
Ni wao tu wapinzani goli lipo wazi wafunge au wabutue.
Kwa mfumo uliopo upinzani wanashindaje uchaguzi? tuache kuwaonea upinzani. Yaani kwa tume hii ya uchaguzi, kwa katiba hii, kwa uingiliaji wa dola kwenye chaguzi, kuchafua daftali la wapiga kura, kuingiza kura mapema kabla ya muda wa kupiga kura, kuzuia mawakala wa vyama vingine. Upinzani wanashindaje. Namshangaa hata wakili msomi Paskali anavyoleta hoja yake hapa.
 
Upinzani ulisitawi sana katika, utawala wa j.m.kikwete, na tutaukumbuka sana, ulikua utawala, uliojali demokrasia sana, uhuru, wa kujieleza, pia ulikua uhuru mkubwa sana, sio siku hizi, kesho unatekwa, na kupotezwa, nakukumbuka sana jk.
 
Wanabodi,

Mikutano ya siasa imeruhusiwa, Samia atabadili sheria za uchaguzi, ataruhusu hadi wagombea binafsi, atarekebisha Tume ya Uchaguzi kwa kuunda Tume Huru na Shirikishi, ataleta katiba mpya, lakini bado ni CCM ndio itaendelea kushinda na kutawala Tanzania, kwa kipindi kirefu kijacho and probably milele!, kwasababu Tanzania hatuna any serious and credible opposition to checks out CCM!.

Watu wanamatumaini sana na Chadema, lakini amini usiamini, Chadema kwa hivi ilivyo sasa, chini ya Mbowe, bado ni hakuna kitu pale!, labda ibadilike, kule juu iingie mijitu bold kama Lissu, Heche na Lema Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition?

Nimesema hatuna any serious and credible opposition kwasababu upinzani uliopo nchi ni upinzani myopic, una short sightedness, hauoni mbali!, hauna long distance vision ya unataka kufika wapi, hawana good vision ya kuona mbali kuwa wanataka nini kesho, wanakwenda wapi, watumie njia gani na watafikaje, hivyo kukosa a clear vision of its target, na kukosa clear focus hivyo kushindwa ku focus and eventually end up missing the target. Elections 2015 - Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ... yaani wapinzani Tanzania ni wanatangatanga tuu!.
Ushauri wa bandiko hili umebadilika, iwapo Lissu atachukua uenyekiti wa Chadema, then, akagombea urais, then upinzani una chances ya urais uchaguzi wa 2025.

Ushauri kwa Mbowe, Jumamosi atundike daluga, ampishe Lissu, 2025 Lissu anamsukumia mtu pembeni kama kumsukuma mlevi, yaani anakwenda kuchukua kama vile ameokota dodo chini ya mwembe!.
P.
 
Ushauri wa bandiko hili umebadilika, iwapo Lissu atachukua uenyekiti wa Chadema, then, akagombea urais, then upinzani una chances ya urais uchaguzi wa 2025.

Ushauri kwa Mbowe, Jumamosi atundike daluga, ampishe Lissu, 2025 Lissu anamsukumia mtu pembeni kama kumsukuma mlevi, yaani anakwenda kuchukua kama vile ameokota dodo chini ya mwembe!.
P.
Ahaaaa sawa
 
Huu ni ushauri wa bure kabisa kwa uongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuelekea uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba, 2025 kwamba kwa viashiria vyote vya kitafiti na kiuchambuzi wa sayansi ya siasa na masuala ya kiuchaguzi siioni nafasi yao katika kushinda Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ikiwa walimudu kusimamisha wagombea asilimia 33 tu kote nchini kabla ya kudai kuondolewa ni tafsiri ya kukosekana uongozi imara kuanzia ngazi za chini hadi kanda.

Kwa kazi za maendeleo zilizofanyika na mwenendo huu tunaouona nashawishika kusema Rais aliopo Dkt Samia Suluhu Hassan atashinda tena kwa kishindo.

Sasa kwa kuwa tunahitaji wapinzani wazuri bungeni ni rai yangu chama hiki kielekeze nguvu kwenye udiwani na ubunge angalau waambulie wawakilishi wachache kule kuliko kupoteza muda na Urais halafu wakapigwa pakubwa sana.

Au wanajukwaa mnaonaje???
naunga mkono hoja kama nilivyo shauri。
P
 
Ndiyo mbadilishe mambo kadhaa wa kadhaa muone
Sasa nyie uchaguzi marefa nyie,linesman nyie,ulinzi nyie
Kunakutoboa hapo

Ova
 
Back
Top Bottom