Kama utani Rais Ruto anaondoka Madarakani na kama Arab States, EA inaelekea huko

Kama utani Rais Ruto anaondoka Madarakani na kama Arab States, EA inaelekea huko

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,455
Reaction score
73,145
Hakuna aliyetegemea hali iliyopo Nairobi ingekuwa hivi ilivyo sasa. Nairobi imechafuka na askari wameanza kuonyesha kuchoka mapema kabisa na maandamano yanazidi kushika kasi.

Rais Ruto atashuhudia kama utani akiondoka madarakani maana nguvu ya umma haiwezi kuzuiwa na polisi hata kidogo.

Kama ilivyokuwa mataifa ya kiarabu miaka michache iliyopita ambako vurugu na maandamano yaliambukizana kutoka nchi moja kwenda nyingine, jee hali hiyo yaweza kuambukizwa hapa Afrika mashariki?

Kwamba twaweza kuja sikia Uganda yakotokea au Tanzania (Tanganyika) nako yakifumka? Maana sababu kubwa ni hali ngumu ya maisha na tuhuma za uchaguzi usio haki ambao kwa EAC ni kama gonjwa sugu.

Viongozi wayaangalie matatizo kwa jicho la tatu badala ya kuwaambia watu waende Burundi au wabunge wao wakajadili uganga wa kienyeji maana uchumi sio professional yao.

Mungu ibariki EAC isiingie kwenye machafuko na viongozi walio shindwa kutekeleza majukumu wajitambue na kung'atuka.
 
Hiyo ni nguvu ya Wanachama Wapinzani .

Sio Raia wa Kenya

Ni kama hapa Bongo, Useme wanachadema waandamane wapindue Serikali.

Ruto anajua hayo Maandamano kuanzia Jezi , Bendera, ni nani kazifadhili .

RUTO YUPO, MIAKA YAKE YOTE YA UCHAGUZI MPAKA IICHE.
 
Ndoto zingine muwe mnalala kwanza then muote.......
Usikute nyie ndio mmelala na kuota kuwa jambo hilo haliwezekani.
Jee unataka kuniambia kama maandamano haya yatakuwa hayana ukomo Rais Ruto atakuwa amekaa tuu ikulu na kuendelea kunywa kahawa kwa raha zake kwa vile Chukwu emeka kaota ndoto kuwa hayana madhara?
Kumbuka wamesema kwa hii leo tuu hasara ya kiuchumi ni mamilioni ya dola!
 
Ila nimecheka sana, yaani kuna askari kunya wana mbio walahi...😜😜😜
Kuna mmoja ametoka mbio hadi kiatu kikachomoka mguuni akabaki kukanyaka na soksi tupu, na yenyewe ilikua imetobona kwa mbele ikakunjwa...🤣🤣
Yaani K25 ni watu wabadi sana wameitendea haki news...😂😂
 
Kuna afande mmoja kakimbizwa na raia akaona isiwe tabu akaruka ukuta chubwiii...[emoji12][emoji12]
Hali sio njema huko Kenya. Wenye access na TV stations za Kenya waangalie maana mambo ni live bila chenga
 
Ila nimecheka sana, yaani kuna askari kunya wana mbio walahi...😜😜😜
Kuna mmoja ametoka mbio hadi kiatu kikachomoka mguuni akabaki kukanyaka na soksi tupu, na yenyewe ilikua imetobona kwa mbele ikakunjwa...🤣🤣
Yaani K25 ni watu wabadi sana wameitendea haki news...😂😂
Chanel ipi mkuu
 
Ndoto za mchana, Africa chini ya jangwa la sahara hicho kitu hakipo
Bokina, mali Genea huoini watu wakitolewa madarakani na jeshi . Labda ungesema EA tu sio nchi zote Chini ya jangwa la sahara. UpO USA au
Huko samalia kinawaka sasa miongo., Etheopia nchi ilitaka kywa vipande, hukusikia kaja sio kusoma mitandaoni.
Kujidannganya ni jambo baya sana.
 
Wale wa "weka na picha"mko wapi??
Screenshot_20230320-171113.jpg
 
Kuna mmoja kakimbizwa akaenda kuingia kwenye nyumba ya watu, kisha akavua kombati akabaki na vest na boksa akatoka nje peku akajifanya kichaa....[emoji12][emoji12]
Yaani K24 hawaendi mbinguni aiseeee....[emoji23][emoji23]
Dahhh natamani kuona hii[emoji28]

Sent from my vivo 1906 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom