Kama Yanga watajenga Uwanja hapo Jangwani basi Mo Dewji hastahili kuendelea kuwepo Simba

Kama Yanga watajenga Uwanja hapo Jangwani basi Mo Dewji hastahili kuendelea kuwepo Simba

Simba lunyasi

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2022
Posts
385
Reaction score
840
Jana jioni Nilipita hapo maeneo ya Jangwani nikaona greda zipo kazini, nikajiuliza maswali mbalimbali.

Mojawapo ya maswali yaliyonijia kichwani ni hivi kweli hawa Yanga wapo serious kujenga kiwanja cha kuchezea mpira hapo?

Leo nimesikia Rais wa Yanga kupitia vyombo vya habari ya kuwa ujenzi rasmi utaanza mwezi wa 4 baada ya hili zoezi la sasa la kuandaa eneo la ardhi itakayotumika.

Hapa nimejiuliza maswali mengi, Simba tumekuwa na mwekezaji karibu miaka 10 sasa, ambaye ameenda mbali zaidi na kudai ameshainunua Simba na ni moja ya mali zake.

Huyu mwekezaji wetu aliwahi kuahidi atajenga uwanja wa kuchezea na tukaanza kuchangia fedha kwa ajili ya huo ujenzi. Ila sijui fedha zile walikula wajanja au zilienda kutumika kwenye matumizi mengine.

Point yangu ni kuwa Simba S.C chini ya Mo Dewji ndio walikuwa wa kwanza kuja na hili wazo la kuwa na uwanja wake sasa naona Utopolo ndio wanaenda kutekeleza ilo wazo.

Kwa trend hii tunapoelekea Simba itaachwa na hawa utopolo kwenye kila kitu, hata huko kwenye rank za Caf napo ni suala la muda tu hawa utopolo watakuwa juu yetu.

Endapo ujenzi wa kiwanja utaanza hapo Jangwani basi ndugu Mo Dewji inabidi atuachie timu mapema ili apatikane mwekezaji ambaye ataweza kushindana na kasi ya Yanga maana tunazidi kuachwa na mchawi tunamjua
 
Hizo ni porojo na siasa tu kwa timu za Simba na Yanga haziwezi kuwa na Viwanja kama Azam kwa sababu zile ni timu za Serikali, Sasa vikije ga Viwanja pale kwa Mkapa unataka pageuke kama ule Uwanja wa ndege kule CHATO ?
 
Hizo ni porojo na siasa tu kwa timu za Simba na Yanga haziwezi kuwa na Viwanja kama Azam kwa sababu zile ni timu za Serikali, Sasa vikije ga Viwanja pale kwa Mkapa unataka pageuke kama ule Uwanja wa ndege kule CHATO ?
Unazani Yanga wanatania, mwezi wa nne sio mbali mkuu tuvute subira tuone.
Halafu uwanja wa taifa sio wakuchezea wakati wote, hata serikali imeliona hilo ndio maana baada ya ukarabati kwisha matumizi yake yatakuwa ni kwa baadhi mechi tu na siyo kila siku unachezewa kama ilivyokuwa hapo awali
 
Hizo ni porojo na siasa tu kwa timu za Simba na Yanga haziwezi kuwa na Viwanja kama Azam kwa sababu zile ni timu za Serikali, Sasa vikije ga Viwanja pale kwa Mkapa unataka pageuke kama ule Uwanja wa ndege kule CHATO ?
Weka akiba ya maneno.
 
Na mafuriko yatakalia wapi pale jangwani?
mafuriko yatakuepo vilevile kama ilivyopangwa na bwana Mungu🤸🤸🤸
images (6).jpeg
 
Hastahili kuendelea wakati kanunua timu, hapo hadi aamue yeye mwenyewe
 
mafuriko yatakuepo vilevile kama ilivyopangwa na bwana Mungu[emoji1732][emoji1732][emoji1732]
View attachment 2936677
kwa mtu anayepafamu jangwani vizuri hawezi kujenga uwanja sehemu ya ovyo kama ile Njia tu za kuingila na kutoka jangwani mara nyingi huwa zinafunga had mwendokasi za kimara kuna kipind zinazunguka ilala boma
 
Unazani Yanga wanatania, mwezi wa nne sio mbali mkuu tuvute subira tuone.
Halafu uwanja wa taifa sio wakuchezea wakati wote, hata serikali imeliona hilo ndio maana baada ya ukarabati kwisha matumizi yake yatakuwa ni kwa baadhi mechi tu na siyo kila siku unachezewa kama ilivyokuwa hapo awali
Hata karia alilisema hili uwanja wa taifa utakua ni wa mechi chache
 
Jana jioni Nilipita hapo maeneo ya Jangwani nikaona greda zipo kazini, nikajiuliza maswali mbalimbali.

Mojawapo ya maswali yaliyonijia kichwani ni hivi kweli hawa Yanga wapo serious kujenga kiwanja cha kuchezea mpira hapo?

Leo nimesikia Rais wa Yanga kupitia vyombo vya habari ya kuwa ujenzi rasmi utaanza mwezi wa 4 baada ya hili zoezi la sasa la kuandaa eneo la ardhi itakayotumika.

Hapa nimejiuliza maswali mengi, Simba tumekuwa na mwekezaji karibu miaka 10 sasa, ambaye ameenda mbali zaidi na kudai ameshainunua Simba na ni moja ya mali zake.

Huyu mwekezaji wetu aliwahi kuahidi atajenga uwanja wa kuchezea na tukaanza kuchangia fedha kwa ajili ya huo ujenzi. Ila sijui fedha zile walikula wajanja au zilienda kutumika kwenye matumizi mengine.

Point yangu ni kuwa Simba S.C chini ya Mo Dewji ndio walikuwa wa kwanza kuja na hili wazo la kuwa na uwanja wake sasa naona Utopolo ndio wanaenda kutekeleza ilo wazo.

Kwa trend hii tunapoelekea Simba itaachwa na hawa utopolo kwenye kila kitu, hata huko kwenye rank za Caf napo ni suala la muda tu hawa utopolo watakuwa juu yetu.

Endapo ujenzi wa kiwanja utaanza hapo Jangwani basi ndugu Mo Dewji inabidi atuachie timu mapema ili apatikane mwekezaji ambaye ataweza kushindana na kasi ya Yanga maana tunazidi kuachwa na mchawi tunamjua
kila timu ina mipango yake,sisi yanga tunajenga uwanja simba wana yao
 
Back
Top Bottom