Kamanda Mambosasa: Saruji ipo ya kutosha jijini Dar, wanaopandisha bei ni wahujumu uchumi tutawashughulikia!

Kamanda Mambosasa: Saruji ipo ya kutosha jijini Dar, wanaopandisha bei ni wahujumu uchumi tutawashughulikia!

Polisi na masuala ya cement wapi na wapi??[emoji2955][emoji2955][emoji2955]
Kalewa ile chai aliyokunywa na Mo baada ya utekaji. Cha ajabu hadi leo kashindwa kuwakamata na kuwatia hatiani watekaji wenyewe zaidi ya yule mmoja aliyeandaliwa kuwalaghai wananchi.
 
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP), Lazaro Mambosasa amewataka wafanyabiashara kuuza cement kwa bei iliyowekwa na serikali vingiinevyo watashughulikiwa kisheria.

Mambosasa amesema jiji la Dar es Salaam lina cement ya kutosha hivyo yoyote anayeongeza bei ni muhujumu uchumi.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Huyu polisi ni kichwa nazi.
Hajui hata the slightest principles za uchumi za demand and supply.

Cement ikiadimika solution yake ni kuongeza supply, na bei ina poa yenyewe bila kirungu cha polisi.
Hawa viongozi wa polisi wasifundishwe gwaride tu.
 
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP), Lazaro Mambosasa amewataka wafanyabiashara kuuza cement kwa bei iliyowekwa na serikali vingiinevyo watashughulikiwa kisheria.

Mambosasa amesema jiji la Dar es Salaam lina cement ya kutosha hivyo yoyote anayeongeza bei ni muhujumu uchumi.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Saraji yawa bidhaa ya anasa
 
Sementi ifanyiwe mgawa kama enzi zile za maduka ya kaya ili kila mtu apate
 
Ila ndugu zangu kuna mambo tunayohoji wakati mwingine yanashangaza sana!

Halafu hatuoneshi utayari wa kutaka kujifunza na kufahamu badala yake tunaonesha ujuaji na kama dharau fulani hivi.

Sasa Naomba kuwajibu wale wanaoshangaa polisi kujihusisha na tatizo la kupanda bei holela kwa bidhaa ya cement.

Ni hivi pale ambapo kunakuwa na viashiria vya biashara ya magendo, ulanguzi, utapeli kufanyika, n.k polisi huwa ni jukumu lao kuingilia kati ili kuiondoa hiyo hali sababu ni mojawapo ya aina za wizi zidi ya wananchi.

Ulanguzi, biashara ya magendo, utapeli, Ulaghai n.k hizo zote ni aina za wizi kwa wananchi !

Askari kazi yake ya msingi ni kulinda watu na mali zao.

Mtu akikuuzia cement kwa mfuko mmoja shilingi 16,000 badala ya 14,500 atakuwa amekuibia shilingi 1,500 ? Sasa piga hesabu kama unanunua mifuko mingi itakuwa amekuibia fedha nyingi kiasi gani?

Kutokujua siyo kosa kosa ni kujifanya unajua wakati hujui!

Tuungeni mkono juhudi za serikali katika kuhakikisha !

Hata kama polisi wana mapungufu yao basi wasemeni kwa kosa au udhaifu mahsusi na siyo pale wanapofanya jambo sahihi mnataka kuwabeza itakuwa mnakosea!
 
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP), Lazaro Mambosasa amewataka wafanyabiashara kuuza cement kwa bei iliyowekwa na serikali vingiinevyo watashughulikiwa kisheria.

Mambosasa amesema jiji la Dar es Salaam lina cement ya kutosha hivyo yoyote anayeongeza bei ni muhujumu uchumi.

Chanzo: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Huyu naye kima kweli....sasa yeye anaongea kama nani wakati taasisi zinazohusika na kupanda au kushuka kwa bei ya bidhaa zipo?
Ninavyojua mimi yeye jukumu lake kubwa ni kulinda usalama wa raia na mali zake.
 
That's why i quitted that https://jamii.app/JFUserGuide.n jo.b
Unalazimika kufanya na kuzungumza vitu nonsense hata nje ya maadili ya utumishi wako
 
Hadi police wanatoa tathmininya bei ya cement! Kweli nchi imepatwa
 
Haya ni mambo ya ajabu kabisa. Mtu kazi yake ni ulinzi na usalama wa raia na mali zao lakini anazungumzia bei ya cement. Yupo km wa viwanda na biashara na km waujenzi. Polisi na cement wapi na wapi!
Kajivuruga aliposikia Policy akadhani Polisi. Sasa kumbe katika policy serikali inabidi iangalie kodi na ruzuku katika bidhaa husika. Sasa wao akili zao zipo kubambikia watu utakatishaji. Mitano tena!
 
Back
Top Bottom