Kamanda Muliro: Boniface Jacob na Malisa hawakingwi na Sheria

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema sheria ya watoa taarifa kulindwa, haimaanishi watu kujikite kutoa za uongo, huku wakidai walindwe.

Kamanda Muliro ametoa kauli hiyo leo Aprili 28, 2024 alipotoa elimu kwa umma akijibu kilichoelezwa na Meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob maarufu Boni Yai na mwanaharakati Godlisen Malisa.

Baada ya wawili hao kuachiwa kutoka rumande jana Aprili 27, 2024, walitoa ujumbe kwa Jeshi la Polisi wakieleza watoa taarifa walipaswa kulindwa na si kupambana nao kwa kuwashikilia.

"Tuna sheria ya kuwalinda watoa taarifa. Watoa taarifa si wahalifu ila ni watu wenye nia njema kwenye nchi na kwa jamii na kulisaidia Jeshi la Polisi, wakitumiwa vizuri wanaweza kufanya kazi zao vizuri bila kuingia mgogoro au msuguano," alisema Malisa.

Jacob naye alisema: "Hatutaacha kupigania matukio ya watu kupotea na kutekwa hatutaki kumuonea mtu, tumehojiwa kwa hiyo sitegemei kama Jeshi la Polisi kutuona sisi maadui zao, watuone marafiki namna gani kuhakikisha watu hawapotei na wale wanaopotea wanapatikana."
 
Kumbe Kamanda Muliro huwa anapitia mitandaoni hasa humu JF na kusoma comments zetu! Nilikuwa sijui.

Kwa hiyo kutoa taarifa kwamba Polisi fulani anajihusisha na vitendo viovu vya uhalifu basi wewe mtoa taarifa moja kwa moja unakuwa Mhalifu????
 
Huyu mzee ni wa kusikitikia tu acha utawala upinduke mwingine atasota mitaa na kujilaani mwenyewe maana hakuna raia atakayethubutu hata kumpa taarifa kwake kwamba anachungliwa dirishani. Wenzake waliomtanguliwa walichunga sana ndimi zao. Mambosasa ni mhadhiri wa chuo sasa hivi. Kova ni mjasiriamali na kampuni yake wengine wamepotea seuze huyu.
Mtoa taarifa lazima alindwe hata kama anakutuhumu wewe hiyo ni sheria sio utashi wa taasisi yoyote. Mbona majuzi Boni huyu huyu alitoa taarifa kuhusu mtendaji mmoja huko Mafia na waziri wa ustawi wa jamii alishukuru sana na Rais alimtengua, kwanini hawa law enforcement wanajifanya miungu watu wasiotaka kukosolewa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…