Kamanda Muliro, wewe na watu wote wanajua Polisi wawili uliowasimamisha kazi unawaonea, walichofanya ni utaratibu wa siku nyingi wa traffic polisi!

Kamanda Muliro, wewe na watu wote wanajua Polisi wawili uliowasimamisha kazi unawaonea, walichofanya ni utaratibu wa siku nyingi wa traffic polisi!

Kamanda Jumanne Muliro, tuache unafiki, tuache kuoneana. Unatutangazia kuwasimamisha hawa Polisi wawili walioonekana wakichukua fedha kwa makondakta wa dadadala kwa sababu wamefanya kosa au kwa sababu wameanikwa mitandaoni?

Ina maana hujui kwamba kila siku traffic wanaokuwa barabarani wanafanya hivyo? Leo ndio unajua?
Yaani unataka kutuambia hujui kwamba hata wakuu wao wa vituo, wanapowapeleka barabarani, wakirudi jioni wanawadai mgao wao? Hujui kwamba wasipopeleka mgao hawatawekwa tena barabarani? Unafikiri hela walizokuwa wakichukua ni zao peke yao? Kama hujui hili hufai hata kuwa na nafasi uliyonayo!

Acha kuonea watu kwa kujaribu kuficha aibu. Ni jambo linalojulikana na kila mtu kwamba polisi wakiwa barabarani wanatakiwa kurudi ofisini na mgao wa wakuu wao. Unafikiri wanaupata wapi?

Na sio traffic tu, hata wale askari wanaopangiwa kufanya patrol, iwe usiku au mchana, wakirudi ofisini wanatakiwa wapeleke mgao kwa wakuu wao, la sivyo hawapangwi kwenye detail za patrol. Kupewa ile SMG kwenda Patrol maana yake unapewa jukumu la kurudi na mgao wa afande wako. Hilolinajulikana na kila askari.

Sasa usijikoshe kinafiki kwa kusema jeshi la Polisi limechafuliwa. Jeshi la Polisi ni chafu tu tunajua, na hhuwezi kulisafisha kwa kuwasimamisha hawa wawili. Walichofanya ni jambo la kawaida ndani ya polisi na hata wewe unajua ndivyo ilivyo.

Polisi yeyote alie barabarani anatakiwa apate chochote kutoka daladala, gari za mizigo (kenta) na gari za mchanga. Hakuna gari kenta au ya mchanga itafanya kazi bila kutoa mgao kwa polisi hata siku moja, na hao polisi walio barabarani wakuu wao wanawapangia kabisa fungu la kuwapelekea.

Hata hivyo, Magufuli si aliwaruhusu madereva wawape hela ya ku-brashia viatu? Na Samia si amesema kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake? Sasa unafikiri urefu wa kamba ya polisi ni mshahara peke yake? Umemuuliza Samia alimaanisha nin Polisi kula kwa urefu wa kamba yao?

Hebu warudishe kazini hawa askari wawili. Acha uonevu na kujikomba kwa watu, ni unafiki tu unaofanya hapo. Si ajabu hata wewe mwenyewe Muliro unaletewa magao wako, usitudanganye hapa.
Wew ungetaka aamueje mkuu, yawezekan hayo anajua ila anapaswa kuwaajibsha au kuwajibika maan unachanganya mazoea na sheria
 
Mimi ndio nahalalisha, mimi ndio niliweka huo utaratibu, eboo!
Mbona unatetea rushwa na kudai ni Haki ya Polisi? Hakuna mahala Serikalini Wala Polisi Wameweka uhalali wa hicho unachotetea ndio maana wanaochukua wanajificha.

Pia nilisikia Serikali Ina Mpango wa kuondoa traffic barabarani na kuwa replaced na cameras
 
Kamanda Jumanne Muliro, tuache unafiki, tuache kuoneana. Unatutangazia kuwasimamisha hawa Polisi wawili walioonekana wakichukua fedha kwa makondakta wa dadadala kwa sababu wamefanya kosa au kwa sababu wameanikwa mitandaoni?
Amesema wamekosea kupokea rushwa hadharani
 
Mbona unatetea rushwa na kudai ni Haki ya Polisi? Hakuna mahala Serikalini Wala Polisi Wameweka uhalali wa hicho unachotetea ndio maana wanaochukua wanajificha.

Pia nilisikia Serikali Ina Mpango wa kuondoa traffic barabarani na kuwa replaced na cameras
Mimi nawez kusema tuu uwajibikaji uanzie juu hadi chin utaleta maan san ndan ya governance
 
Kama unanisema mimi, wewe ni mojawapo ya watu walio wepeso kuongea wagumu kuelewa. Sitetei rushwa. Ni sawa kila mtu ajue mumeo awe na mchepuko kwa miaka mingi ila siku unapomfumania ndio anakuomba msamaha kwa kuchepuka. Usingemfumania?

Kwa akili yako unafikiri Muliro haju trafiki barabarani wanapekela mgao kwa wakuu wao vituoni?

Sawa kwa hiyo ulitakaje yani?

Waachwe waendelee na kazi despite pure evidence kuwa wamekula rushwa?

Yaani ulitakaje mkuu?

Sio kila kitu mnakosoa.

Wamekula rushwa watakamatwa, mambo mengine yaendelee.

Again, ulitaka waachiwe waendelee na kazi au ulitakaje?
 
Kama vile ni lazima wale pesa

Sasa ndio hawa au wale wawili pekee?
Yaani hawa waliokamatwa ni za mwizi 40 zimetimia tu, wapo wengi sana huko. Hawa wachukua video ni kwamba wamechoshwa na tabia hii..!!
 
Kamanda Jumanne Muliro, tuache unafiki, tuache kuoneana. Unatutangazia kuwasimamisha hawa Polisi wawili walioonekana wakichukua fedha kwa makondakta wa dadadala kwa sababu wamefanya kosa au kwa sababu wameanikwa mitandaoni?

Ina maana hujui kwamba kila siku traffic wanaokuwa barabarani wanafanya hivyo? Leo ndio unajua?
Yaani unataka kutuambia hujui kwamba hata wakuu wao wa vituo, wanapowapeleka barabarani, wakirudi jioni wanawadai mgao wao? Hujui kwamba wasipopeleka mgao hawatawekwa tena barabarani? Unafikiri hela walizokuwa wakichukua ni zao peke yao? Kama hujui hili hufai hata kuwa na nafasi uliyonayo!

Acha kuonea watu kwa kujaribu kuficha aibu. Ni jambo linalojulikana na kila mtu kwamba polisi wakiwa barabarani wanatakiwa kurudi ofisini na mgao wa wakuu wao. Unafikiri wanaupata wapi?

Na sio traffic tu, hata wale askari wanaopangiwa kufanya patrol, iwe usiku au mchana, wakirudi ofisini wanatakiwa wapeleke mgao kwa wakuu wao, la sivyo hawapangwi kwenye detail za patrol. Kupewa ile SMG kwenda Patrol maana yake unapewa jukumu la kurudi na mgao wa afande wako. Hilolinajulikana na kila askari.

Sasa usijikoshe kinafiki kwa kusema jeshi la Polisi limechafuliwa. Jeshi la Polisi ni chafu tu tunajua, na hhuwezi kulisafisha kwa kuwasimamisha hawa wawili. Walichofanya ni jambo la kawaida ndani ya polisi na hata wewe unajua ndivyo ilivyo.

Polisi yeyote alie barabarani anatakiwa apate chochote kutoka daladala, gari za mizigo (kenta) na gari za mchanga. Hakuna gari kenta au ya mchanga itafanya kazi bila kutoa mgao kwa polisi hata siku moja, na hao polisi walio barabarani wakuu wao wanawapangia kabisa fungu la kuwapelekea.

Hata hivyo, Magufuli si aliwaruhusu madereva wawape hela ya ku-brashia viatu? Na Samia si amesema kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake? Sasa unafikiri urefu wa kamba ya polisi ni mshahara peke yake? Umemuuliza Samia alimaanisha nin Polisi kula kwa urefu wa kamba yao?

Hebu warudishe kazini hawa askari wawili. Acha uonevu na kujikomba kwa watu, ni unafiki tu unaofanya hapo. Si ajabu hata wewe mwenyewe Muliro unaletewa magao wako, usitudanganye hapa.
Sheria ambayo haijaandikwa inasema, we kula rushwa ili mradi usikamatwe kwa picha na video zitakazosambaa kwenye social media.
Kosa lao hapo si kula rushwa, ila ni kunaswa na video zikasambaa basi.
 
Sawa kwa hiyo ulitakaje yani?

Waachwe waendelee na kazi despite pure evidence kuwa wamekula rushwa?

Yaani ulitakaje mkuu?

Sio kila kitu mnakosoa.

Wamekula rushwa watakamatwa, mambo mengine yaendelee.

Again, ulitaka waachiwe waendelee na kazi au ulitakaje?
Ndio. Iwapo unajua trafiki wote wanafanya hivi, na imetokea tu hawa wamepigwa picha, kama kweli una nia njema kwa nini siku zote ukijua hilo umekaa kimya? Kuwafukuza hawa unafanya kosa lao ni kupigwa picha, sio kuchukua fedha, kwa sababu unajua kabisa kila trafiki anachukua fedha na na anapeleka mgao kituoni
 
Hebu warudishe kazini hawa askari wawili.
mbona unamfokea kwani amesha
wataja kuwa ni akina nani?
au ni wa kituo gani?
au wana vyeo gani?
au wamefanya nini zaidi ya kusema wamejihusisha na vitendo visivyo maadili?
 
Sheria ambayo haijaandikwa inasema, we kula rushwa ili mradi usikamatwe kwa picha na video zitakazosambaa kwenye social media.
Kosa lao hapo si kula rushwa, ila ni kunaswa na video zikasambaa basi.
Umenena vema sana Mkuu, kuna watu humu akili matope hawaelewi tunachoongelea hapa
 
mbona unamfokea kwani amesha
wataja kuwa ni akina nani?
au ni wa kituo gani?
au wana vyeo gani?
au wamefanya nini zaidi ya kusema wamejihusisha na vitendo visivyo maadili?
Uko wapi na wewe hufuatilii mambo? Ndio ameshasema wako mahabusu
 
Wew ungetaka aamueje mkuu, yawezekan hayo anajua ila anapaswa kuwaajibsha au kuwajibika maan unachanganya mazoea na sheria
Kama ana nia kweli aanze kula sahani moja na hao makamanda wanaowaambia askari wanaotumwa barabarani waache kudai mgao wao. Kisha kampeni ya kuwaambia madereva wa daladala, kenta, bajaji na gari za mchanga kutotoa rushwa. Pia akomeshe trafiki kulazimisha makosa kwa madereva.

Lakini sasa, kwa mishahara hii ya polisi sio rahisi kukomesha hili. Ndio maana nimesema jeshi la Polisi katika mazingira yao ya kazi halisafishiki
 
Kapokee rushwa na wewe tukunase uone
Mie natoa, sipokei, na imefikia mahali kwa hawa trafiki wala sioni ni rushwa tena, maana natoa bila hata wao kuniambia nina kosa lolote. Akifika tu nasema sema ofisa, hebu shika chai hii halafu nasepa. Sasa hapo nimetoa rushwa? Rushwa ni pale anakambia una kosa ndio unampa hela akuachie. Mie nawapa hela ya kubrashi viatu na kurefusha urefu wa kamba zao, kulingana na maagizo ya Amri jeshi Mkuu wa Tanzania
 
Kamanda Jumanne Muliro, tuache unafiki, tuache kuoneana. Unatutangazia kuwasimamisha hawa Polisi wawili walioonekana wakichukua fedha kwa makondakta wa dadadala kwa sababu wamefanya kosa au kwa sababu wameanikwa mitandaoni?

Ina maana hujui kwamba kila siku traffic wanaokuwa barabarani wanafanya hivyo? Leo ndio unajua?
Yaani unataka kutuambia hujui kwamba hata wakuu wao wa vituo, wanapowapeleka barabarani, wakirudi jioni wanawadai mgao wao? Hujui kwamba wasipopeleka mgao hawatawekwa tena barabarani? Unafikiri hela walizokuwa wakichukua ni zao peke yao? Kama hujui hili hufai hata kuwa na nafasi uliyonayo!

Acha kuonea watu kwa kujaribu kuficha aibu. Ni jambo linalojulikana na kila mtu kwamba polisi wakiwa barabarani wanatakiwa kurudi ofisini na mgao wa wakuu wao. Unafikiri wanaupata wapi?

Na sio traffic tu, hata wale askari wanaopangiwa kufanya patrol, iwe usiku au mchana, wakirudi ofisini wanatakiwa wapeleke mgao kwa wakuu wao, la sivyo hawapangwi kwenye detail za patrol. Kupewa ile SMG kwenda Patrol maana yake unapewa jukumu la kurudi na mgao wa afande wako. Hilolinajulikana na kila askari.

Sasa usijikoshe kinafiki kwa kusema jeshi la Polisi limechafuliwa. Jeshi la Polisi ni chafu tu tunajua, na hhuwezi kulisafisha kwa kuwasimamisha hawa wawili. Walichofanya ni jambo la kawaida ndani ya polisi na hata wewe unajua ndivyo ilivyo.

Polisi yeyote alie barabarani anatakiwa apate chochote kutoka daladala, gari za mizigo (kenta) na gari za mchanga. Hakuna gari kenta au ya mchanga itafanya kazi bila kutoa mgao kwa polisi hata siku moja, na hao polisi walio barabarani wakuu wao wanawapangia kabisa fungu la kuwapelekea.

Hata hivyo, Magufuli si aliwaruhusu madereva wawape hela ya ku-brashia viatu? Na Samia si amesema kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake? Sasa unafikiri urefu wa kamba ya polisi ni mshahara peke yake? Umemuuliza Samia alimaanisha nin Polisi kula kwa urefu wa kamba yao?

Hebu warudishe kazini hawa askari wawili. Acha uonevu na kujikomba kwa watu, ni unafiki tu unaofanya hapo. Si ajabu hata wewe mwenyewe Muliro unaletewa magao wako, usitudanganye hapa.
Inawezekana hatua ndio zimeanza kuchukuliwa labda.

Mi nadhani ili kuamini uungwana wa jeshi letu katika kukabiliana na rushwa kweli hasa za barabarani basi KILA MTU KWA MAHALA ALIPO AVIZIE MATUKIO KAMA HAYA NA KURUSHA HIVYO HIVYO MITANDAONI. Labda rushwa itakoma..
 
Mbona unatetea rushwa na kudai ni Haki ya Polisi? Hakuna mahala Serikalini Wala Polisi Wameweka uhalali wa hicho unachotetea ndio maana wanaochukua wanajificha.

Pia nilisikia Serikali Ina Mpango wa kuondoa traffic barabarani na kuwa replaced na cameras
Ungemlaumu Magufuli basi, aliesema sio vibaya kuwapa askari elfu tano ya kubrashia viatu. Tena hawa askari wapole sana, wanakubali elfu mbili na sio elfu tano aliyoagiza Magufuli.

Unasema wanapokea rushwa, kunakuwaje rushwa wakati anaetoa hela ni konda sio dereva? Umeona hapo dereva akiambiwa amefanya kosa? Maana rushwa ni kutoa hela ili kukwepa kosa. Umeona dereva akitakiwa kulipa faini ndio akatoa rushwa?
 
Back
Top Bottom