Kamati iliyotoa Mapendekezo ya Kamati ya Msajili wa Vyama Kuhusu Katiba Mpya, Kisheria na Kimantiki ni Batili

Kamati iliyotoa Mapendekezo ya Kamati ya Msajili wa Vyama Kuhusu Katiba Mpya, Kisheria na Kimantiki ni Batili

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Kuna mambo katika Taifa hili huwa yanafanyika mpaka unajiuliza, sisi ni Taifa la namna gani?

Mojawapo ya mambo yanayoonekana kutudhalilisha wote kama Taifa ni hili la katiba mpya.

Katiba ni ya wananchi wote, siyo ya wanasiasa na siyo ya vyama vya siasa.

Kinachoitwa kamati ya katiba, hiyo iliyotoa taarifa yake kwa Rais Samia, wajumbe wake na miongozo yake ya kufanya kazi, vimeandaliwa na Mutungi. Mutungi ni msajili wa vyama vya siasa. Ni sheria ipi, ni katiba gani imempa mamlaka msajili wa vyama vya siasa kushughulika na mambo ya katiba mpya? Mutungi ni nani kwenye suala la katiba mpya?

Tume ya Jaji Warioba, kuanzia kuundwa kwake na mchakato wote viliongozwa na sheria iliyotungwa na Bunge, haka kamati kalikoundwa na Mutungi, kameundwa kwa sheria gani?

Msajili wa vyama ashughulike na mambo yanayomhusu. Watanzania tusifanywe wajinga kwa kiwango hiki. Haya ni matumizi mabaya ya easilimali za Taifa.

Tume ya Warioba ilikwishatoa ripoti yake, na ilitamka wazi kuwa WATANZANIA WANATAKA KATIBA MPYA. HATA WALE AMBAO HAWAKUSEMA MOJA KWA MOJA KUWA WANATAKA KATIBA MPYA, MABADILIKO WANAYOYATAKA YANAAMAANISHA UWEPO WA KATIBA MPYA.

Kauli ya Rais Samia kusema kuwa wanaotaka katiba mpya ni watumiaji wa mitandao, watanzania hawataki katiba mpya, nayo ni kauli iliyokosa weledi. Kwani wanaotumia mitandao siyo Watanzania? Rais mwenyewe anatumia twitter, ina maana na yeye siyo Mtanzania?

Kauli na matendo ya viongozi yanaondoa kuaminiana. Tuheshimu maamuzi ya wananchi, hata kama hatuyapendi. Kiongozi mwenye busara na hekima, ni lazima, siku zote uangalie maamuzi ya wananchi, wananchi wanataka nini. Wanachokitaka wananchi, na ambacho walikwishakitolea maamuzi, ni lazima iwe ajenda ya kipaumbele cha kwanza kwa kiongozi yeyote mwenye busara na anayetambua majukumu ya kiongozi.

Hakuna haja ya vijikamati kwenye suala la katiba. Kamati iliyoundwa na Mutungi, msajili wa vyama vya siasa, halafu ikaenda kushughulika na suala la katiba mpya, ni ubatili, kamati yenyewe ni batili na hata maamuzi yake ni batili. Wananchi tunatakiwa kuyapuuza maana wananchi hawakuwahi kumpa Mutungi kazi ya kushughulikia katiba mpya iwe kwa kupitia sheria ya usajili wa vyama vya siasa, au kwa sheria nyingine yoyote ile.

Mod: naomba isomeke

MAPENDEKEZO YA KAMATI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA KUHUSU KATIBA MPYA, KISHERIA NA KIMANTIKI, NI BATILI.
 
Mimi nimekata tamaa maana bunge lenyewe ni la kina babu Tale na covid 19 sasa hata tukiletewa bunge la katiba wabunge wenyewe si ndio hawa kina kibajaji MwanaFa na babu Tale?

Madhara ya kukabidhi nchi vichaa itaendelea kuligharimu Taifa letu kwa miaka mingi ijayo.

Mfano huyu mama ndio angepokea nchi kutoka kwa JK hii kazi ingekuwa rahisi sana, lakini dhambi aliyotufanyia JK kutuletea kichaa damage aliyoacha itatugharimu kwa muda mrefu ujao.

Kwahili mnaomlaumu sana mnamuonea maana yule kichaa yeye alitamka wazi katiba siyo kipaumbele chake, angalau huyu mama anajari utu lakini wa kulaumiwa ni hao wajasiriasiasa kina Zitto Kabwe na wahuni wenzake.
 
Halafu Mama Anasema Watafanya Kazi Miaka 9
Ameanza Kujipigia Campaign Mapema
Rais Samia, kama anataka kufanya kazi yake vizuri, aache kila mara kuufikiria uchaguzi wa 2025. Aliwazuia wenzake wasifikirie uchaguzi wa 2025 ili abakie yeye pekee yake wa kufikiria uchaguzi wa 2025?

Aiweke akili na moyo wake huru, atapata heshima ya kudumu. Aamini kuwa anaweza kuchaguliwa kuwa Rais mwaka 2025, na anaweza asichaguliwe.

Anaweza kuwepo 2025, anaweza pia asiwepo (tunaoamini katika Mungu, tunatambua kuwa maisha yetu yapo mikononi mwa Mungu wakati wote, hatujui siku wala saa ya kuondoka katika Ulimwengu huu). Anatakiwa kufanya yaliyo mema sasa maana ndio wakati alio na uhakika nao.
 
Kuna mambo katika Taifa hili huwa yanafanyika mpaka unajiuliza, sisi ni Taifa la namna gani?

Mojawapo ya mambo yanayoonekana kutudhalilisha wote kama Taifa ni hili la katiba mpya...

Kwani yenyewe ina mwakilisha nani?
 
Mimi nimekata tamaa maana bunge lenyewe ni la kina babu Tale na covid 19 sasa hata tukiletewa bunge la katiba wabunge wenyewe si ndio hawa kina kibajaji MwanaFa na babu Tale...
Ni kweli, ka mwaka 2015, tungempata Rais mwenye hekima na akili japo ya wastani, sahizi tusingekuwa hapa tulipo.

Najua ugumu anaoupata Samia. Anajitahidi kukwepa hili genge la wahuni waliojazwa bungeni na Magufuli lisihusike na katiba mpya.

Tunamwomba aweke wazi hili tatizo la kutokuwa na wabunge wawakilishi wa wananchi ili wananchi waamue ni namna gani Bunge la katiba litengenezwe bila ya kuhusisha hawa wahuni walioteuliwa na Magufuli kuwa wabunge.
 
Rais Samia, kama anataka kufanya kazi yake vizuri, aache kila mara kuufikiria uchaguzi wa 2025. Aliwazuia wenzake wasifikirie uchaguzi wa 2025 ili abakie yeye pekee yake wa kufikiria uchaguzi wa 2025...
Ulichoandika ni kitu ambacho hakipo wala hakiwezekani, otherwise asingekuwepo ccm.

Wengi uwepo wao ccm ni maslahi na si vinginevyo.

Shirikisho la muziki linajiingiza kwenye mgogoro usiokuwa na faida yoyote kwa kumteuwa Stive Nyerere awe msemaji wao kisa tu Stive ana channel ya kumuona mama muda wowote, stive siyo mwanamuziki, nchi ya hovyo sana hii.

Ukiishi kwenye iliyooza kiasi hiki ni ngumu kuamini hizo kamati za kitapeli ndani yake kuna Zitto Kabwe pia.
 
Watanzania wapole sana, tena tunakuwa wapole zaidi tunapozidi kuchokozwa, hii species yetu inatakiwa ipelekwe maabara kuchunguzwa ni ya sampuli gani.
Hata maabara wakipima watakuta upole mkuu
 
Kuna mambo katika Taifa hili huwa yanafanyika mpaka unajiuliza, sisi ni Taifa la namna gani?

Mojawapo ya mambo yanayoonekana kutudhalilisha wote kama Taifa ni hili la katiba mpya...
Katiba Mpya,itapatikana kwa njia rahisi kwa kupiga Kura Za hapana kwa Samia.
Pia tutaondokana na Muungano.
 
Ulichoandika ni kitu ambacho hakipo wala hakiwezekani, otherwise asingekuwepo ccm.

Wengi uwepo wao ccm ni maslahi na si vinginevyo.

Shirikisho la muziki linajiingiza kwenye mgogoro usiokuwa na faida yoyote kwa kumteuwa Stive Nyerere awe msemaji wao kisa tu Stive ana channel ya kumuona mama muda wowote, stive siyo mwanamuziki, nchi ya hovyo sana hii.

Ukiishi kwenye iliyooza kiasi hiki ni ngumu kuamini hizo kamati za kitapeli ndani yake kuna Zitto Kabwe pia.
Zito anafahamika. Agenda kubwa kwake huwa na mapato yake binafsi. Mambo mengine yote huwa yanalenga ajenda yake kuu. Na yeye kuambiwa na Rais kuwa amejihakikishia kazi ya kufanya miaka 9 (ikimaanisha uhakika wa mapato yake binafsi kwa miaka 9, ni mafanikio yake makuu kwa ajenda yake kuu).

Wananchi, tunatakiwa kupuuza maamuzi ya vijikamati hivi ambavyo ni uchochoro wa kupatia pesa kwa watu waliokubali kutumika kama vibaraka wa wasiotaka watanzania wawe na katiba iliyo bora, wanayoitaka, inayoangalia maslahi ya wananchi wote.
 

Katiba Mpya,itapatikana kwa njia rahisi kwa kupiga Kura Za hapana kwa Samia.​

Pia tutaondokana na Muungano.​

Hiyo kura ya Hapana utapigia wapi wakati katiba iliyopo haikupi hiyo nafasi?

Hata ukipata nafasi ya kupiga kura ya hapana, itakuwa na maana gani wakati katiba ya sasa inasema, bila ya kujali Samia amepata kura ngapi, mahera akishamtangaza Samia kuwa ndiye Rais, huruhusiwi kuhoji popote?
 
Back
Top Bottom