Kamati imetumia 'siasa’ suala la Fei Toto

Kamati imetumia 'siasa’ suala la Fei Toto

SIJUI ni lini tutaacha kutumia siasa katika vitu vya msingi. Nawaza sana juu ya hili lakini sijapata majibu.

Ni wiki moja sasa imepita tangu sakata la mchezaji Feisal Salum ‘Fei Toto’ limalizwe kisiasa na kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Fei Toto alivunja mkataba wake na Yanga. Aliandika barua ya kuwafahamisha Yanga kuwa ‘ndoa’ yao imevunjika. Akalipa na fedha za kuvunja huo mkataba.

Yanga wakaenda TFF kulalamika kuwa Fei Toto amevunja mkataba bila kuwashirikisha. Walikuwa na haki ya kushtaki kuhusu sakata hilo. Yawezekana ni kweli Fei Toto alivunja mkataba bila kuwashirikisha Yanga. lakini ukweli ni kwamba aliwafahamisha.

Kwanini Kamati ya TFF haijaamua kesi ya msingi na badala yake wamemlazimisha mchezaji arudi Yanga? Inachekesha sana.

Kwa kifupi ni kwamba mkataba wa Fei na Yanga ulishavunjika. Ndio maana Yanga ililalamika mkataba umevunjwa bila utaratibu. Hii ndio ilipaswa kuwa kesi ya msingi. Lakini badala yake imeamuliwa kesi nyingine kabisa.

Wewe uliona wapi duniani mchezaji analazimishwa arudi kwenye timu yake ya awali baada ya kuvunja mkataba?

Kama ulisoma vizuri mkataba wa Fei Toto na Yanga umeeleza wazi kuwa upande wa mchezaji unaweza kuvunja mkataba muda wowote kwa namna isivyo kawaida kama utafuata utaratibu wa Malipo.

Fei Toto alifanya hivyo. Aliwalipa Yanga fedha ya usajili na mishahara ya miezi mitatu. Hiki ndio kipengele cha wazi katika mkataba wake na Yanga.

Kamati imetumia kipengele gani kumrejesha. Hakuna. Ni siasa tu. Ama wanaogopa kuwa watu watasema kuwa wanaionea Yanga? Ni ajabu na kweli. Kwanini tusiamue vitu vya msingi kwa kufuata utaratibu?

Kama mkataba unasema namna ya kuvunja huwa tunatumia mkataba kufanya hivyo. Hakuna sehemu imeandikwa kuwa tunatumia sheria za FIFA kwa kesi ambayo mkataba wake unazungumza namna ya kufanya.

Mkataba wa Fei na Yanga umesema vyema namna ya kuvunja. Na mchezaji ametumia vipengele hivyo kuvunja mkataba wake na Yanga. Lipa wazi kabisa.

Kwanini TFF haikujadili kesi ya msingi ya mchezaji na Yanga ikaamua tu kumrudisha mchezaji kwenye klabu? Uliwahi kuona wapi jambo kama hili?

Yanga walilalamika kuwa Feisal amevunja mkataba bila kuwashirikisha. Ila ukweli ni kwamba Feisal aliwaandikia barua kuwafahamisha. Walitaka nini zaidi ya hicho wakati mkataba unaeleza wazi ukitaka kuvunja unafanya nini?

Walitaka Fei Toto afanye kitu gani kingine? Ni kichekesho. Kimsingi ni kwamba hadi Yanga na Fei Toto wanakwenda pale TFF mkataba ulishavunjika. Haikupaswa kujadiliwa tena kama Fei ni mchezaji wa Yanga ama la. Ila cha ajabu imejadiliwa hivyo.

Kilichopaswa kujadiliwa ni kama Feisal alikosea popote wakati anavunja mkataba wake huo. Utaratibu unafahamika kuwa ni faini ama adhabu ya kufungiwa. Huu Ndio muafaka wa kisheria. Kwanini hawakutaka kufanya hivyo? Wanajua wenyewe.

Unajua Madhara ya maamuzi haya? Subiri nitakueleza. Kwa namna hali ilivyo sasa Feisal hataki tena kucheza Yanga. Hataki kabisa. Ni kama tu mwanamke aliyeomba talaka kwenye ndoa. Kumlazimisha Feisal arudi Yanga ni kama kumlazimisha mbuzi ale mkate. Ni jambo gumu sana.

Matokeo yake ni kuwa Feisal anaweza kuendelea kucheza Ndondo kwao Zanzibar hadi mwisho wa msimu. Nini kitatokea? Tunapoteza mchezaji Muhimu katika Ligi yetu Pamoja na Taifa Stars.

Sote tunakubaliana kuwa Fei ni mchezaji mahiri zaidi katika nafasi anayocheza hapa nchini. Hana mfanano. Hakuna anayemkaribia hapo.

Hivyo kama Taifa tumeweka rehani kipaji cha mchezaji mkubwa kwa kutumia siasa. Inauma sana.

Source : Mwanaspoti​
Tumechoshwa sasa na haya malalamiko yenu yasiyoisha kuhusu huyo dogo. Mkiona hamjaridhika, kateni rufaa ngazi zinazofuata.

Kulalamika tu pasipo kuchukua hatua madhubuti, haisaidii chochote.
 
Uhuni wake upi kuvunja mkataba au kuangalia maslahi yake ????
Kwani mkataba alisaini na nani? au kwenye mkataba wake kuna saini za pande zipi?

So ukijua ndipo utajua kwamba kama kulikuwa na pande mbili wakati mkataba uliposainiwa hata kwenye kuvunjwa lazima pande mbili zihusishwe ndizo taratibu za mkataba.

Hakatazwi kuvunjwa kwani kwenye mpira mchezaji yoyote mkataba wake unaweza kuvunjwa haijalishi amebakisha miaka mingapi, ila lazima pande mbili zihusihwe na taratibu za usajili zifuatwe.
 
Kwani mkataba alisaini na nani? au kwenye mkataba wake kuna saini za pande zipi?

So ukijua ndipo utajua kwamba kama kulikuwa na pande mbili wakati mkataba uliposainiwa hata kwenye kuvunjwa lazima pande mbili zihusishwe ndizo taratibu za mkataba.

Hakatazwi kuvunjwa kwani kwenye mpira mchezaji yoyote mkataba wake unaweza kuvunjwa haijalishi amebakisha miaka mingapi, ila lazima pande mbili zihusihwe na taratibu za usajili zifuatwe.
Sasa upande wa pili ilikuaje mpaka hakuwahusisha kaka??
 
Nasikia yeye hataki kurudi yanga kapata timu nyingine
Yeye hataki ila mkataba unambana. Sijajua kama unafuatilia mpira, umemuona Mane ,Bayern walikuwa na uwezo wa kucheza rafu kumchukua Mane (sema ulaya kuna taratibu na si uhuni huu wa Fei),ila Mane aliwapa options Liverpool wamuongezee mzigo kwenye mkataba mpya Liverpool wakakataa.

Mane kwa kuwa bado alikuwa na mkataba na Liverpool aliuheshimu mkataba aliousaini, hakugomea mazoezi wala mechi na baada ya mkataba wale kuisha akaondoka FREE. Sasa yy hawezi kuondoka sabau bado anamkataba mwaka na nusu na hataki kufuata taratibu yy na timu inayo mtaka.

Afuate taratibu la sivyo yeye ndiye atakaye umia maana hana sababu ,mshahara mpaka sasa haidai Yanga, TFF kachemka japo ana room ya kukata rufaa CAS.Mwisho wa yote yeye ndiye atakaye umia kwani kwa sasa hawezi cheza timu yoyote na muda si mrefu Yanga wakipeleka malalamiko yao TFF dogo anaweza akala ban na akishamaliza hiyo adhabu atarudi tena kuutumia mkataba wake wa mwaka na nusu.

Sisi tukiongea mnatuambia sababu ni mashabiki wa Yanga nazani juzi ulimsikiliza Rage akimshauri Feitoto arudi Yanga au afuate taratibu za usajili la sivyo yy ndiye ataye umia.
 
Wana simba kwanini mnateseka na suala la fei toto?
Kama mna uchungu sana nendeni CAS
Ukweli mchungu ;
Yanga hana uwezo wa kushinda kesi yoyote ile ikipelekwa CAS kwa kutumia hao wanasheria wake vilaza.

Kesi anazoziweza Yanga ni za hapa Tz kwa kuwatumia wanasiasa kuiwekea vitisho tff.

Kesi ya morisson vigogo wa simba nao wasingeingilia Kati Morisson hapa Tz kwa tff angeshindwa na haki angeenda kuipata CAS .Kwakuwa ili suala la fei limekuwa kama lake binafsi ndo Maana kaminywa kimya kimya.



Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Ukweli mchungu ;
Yanga hana uwezo wa kushinda kesi yoyote ile ikipelekwa CAS kwa kutumia hao wanasheria wake vilaza.

Kesi anazoziweza Yanga ni za hapa Tz kwa kuwatumia wanasiasa kuiwekea vitisho tff.

Kesi ya morisson vigogo wa simba nao wasingeingilia Kati Morisson hapa Tz kwa tff angeshindwa na haki angeenda kuipata CAS .Kwakuwa ili suala la fei limekuwa kama lake binafsi ndo Maana kaminywa kimya kimya.



Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Pole kwa maumivu unayo pitia jikaze utazoea
 
Ukweli mchungu ;
Yanga hana uwezo wa kushinda kesi yoyote ile ikipelekwa CAS kwa kutumia hao wanasheria wake vilaza.

Kesi anazoziweza Yanga ni za hapa Tz kwa kuwatumia wanasiasa kuiwekea vitisho tff.

Kesi ya morisson vigogo wa simba nao wasingeingilia Kati Morisson hapa Tz kwa tff angeshindwa na haki angeenda kuipata CAS .Kwakuwa ili suala la fei limekuwa kama lake binafsi ndo Maana kaminywa kimya kimya.



Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Mbona maneno mengi point zero, kama mna uhakika atashinda uko cas kwanini msiende nae kama mlivyofanya kwa Morrison?
Kama mlimrubuni kuvunja mkataba nini kinawazuia kwenda cas?
 
Kwanini msiende kumlazimisha arudi kambini? Si mmepewa hiyo haki na Kamati kuwa ni mali ya Yanga?
Hakuna mfanyakazi analazimishwa kwa nguvu kurudi kazini. Anabanwa na sheria tu
 
SIJUI ni lini tutaacha kutumia siasa katika vitu vya msingi. Nawaza sana juu ya hili lakini sijapata majibu.

Ni wiki moja sasa imepita tangu sakata la mchezaji Feisal Salum ‘Fei Toto’ limalizwe kisiasa na kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Fei Toto alivunja mkataba wake na Yanga. Aliandika barua ya kuwafahamisha Yanga kuwa ‘ndoa’ yao imevunjika. Akalipa na fedha za kuvunja huo mkataba.

Yanga wakaenda TFF kulalamika kuwa Fei Toto amevunja mkataba bila kuwashirikisha. Walikuwa na haki ya kushtaki kuhusu sakata hilo. Yawezekana ni kweli Fei Toto alivunja mkataba bila kuwashirikisha Yanga. lakini ukweli ni kwamba aliwafahamisha.

Kwanini Kamati ya TFF haijaamua kesi ya msingi na badala yake wamemlazimisha mchezaji arudi Yanga? Inachekesha sana.

Kwa kifupi ni kwamba mkataba wa Fei na Yanga ulishavunjika. Ndio maana Yanga ililalamika mkataba umevunjwa bila utaratibu. Hii ndio ilipaswa kuwa kesi ya msingi. Lakini badala yake imeamuliwa kesi nyingine kabisa.

Wewe uliona wapi duniani mchezaji analazimishwa arudi kwenye timu yake ya awali baada ya kuvunja mkataba?

Kama ulisoma vizuri mkataba wa Fei Toto na Yanga umeeleza wazi kuwa upande wa mchezaji unaweza kuvunja mkataba muda wowote kwa namna isivyo kawaida kama utafuata utaratibu wa Malipo.

Fei Toto alifanya hivyo. Aliwalipa Yanga fedha ya usajili na mishahara ya miezi mitatu. Hiki ndio kipengele cha wazi katika mkataba wake na Yanga.

Kamati imetumia kipengele gani kumrejesha. Hakuna. Ni siasa tu. Ama wanaogopa kuwa watu watasema kuwa wanaionea Yanga? Ni ajabu na kweli. Kwanini tusiamue vitu vya msingi kwa kufuata utaratibu?

Kama mkataba unasema namna ya kuvunja huwa tunatumia mkataba kufanya hivyo. Hakuna sehemu imeandikwa kuwa tunatumia sheria za FIFA kwa kesi ambayo mkataba wake unazungumza namna ya kufanya.

Mkataba wa Fei na Yanga umesema vyema namna ya kuvunja. Na mchezaji ametumia vipengele hivyo kuvunja mkataba wake na Yanga. Lipa wazi kabisa.

Kwanini TFF haikujadili kesi ya msingi ya mchezaji na Yanga ikaamua tu kumrudisha mchezaji kwenye klabu? Uliwahi kuona wapi jambo kama hili?

Yanga walilalamika kuwa Feisal amevunja mkataba bila kuwashirikisha. Ila ukweli ni kwamba Feisal aliwaandikia barua kuwafahamisha. Walitaka nini zaidi ya hicho wakati mkataba unaeleza wazi ukitaka kuvunja unafanya nini?

Walitaka Fei Toto afanye kitu gani kingine? Ni kichekesho. Kimsingi ni kwamba hadi Yanga na Fei Toto wanakwenda pale TFF mkataba ulishavunjika. Haikupaswa kujadiliwa tena kama Fei ni mchezaji wa Yanga ama la. Ila cha ajabu imejadiliwa hivyo.

Kilichopaswa kujadiliwa ni kama Feisal alikosea popote wakati anavunja mkataba wake huo. Utaratibu unafahamika kuwa ni faini ama adhabu ya kufungiwa. Huu Ndio muafaka wa kisheria. Kwanini hawakutaka kufanya hivyo? Wanajua wenyewe.

Unajua Madhara ya maamuzi haya? Subiri nitakueleza. Kwa namna hali ilivyo sasa Feisal hataki tena kucheza Yanga. Hataki kabisa. Ni kama tu mwanamke aliyeomba talaka kwenye ndoa. Kumlazimisha Feisal arudi Yanga ni kama kumlazimisha mbuzi ale mkate. Ni jambo gumu sana.

Matokeo yake ni kuwa Feisal anaweza kuendelea kucheza Ndondo kwao Zanzibar hadi mwisho wa msimu. Nini kitatokea? Tunapoteza mchezaji Muhimu katika Ligi yetu Pamoja na Taifa Stars.

Sote tunakubaliana kuwa Fei ni mchezaji mahiri zaidi katika nafasi anayocheza hapa nchini. Hana mfanano. Hakuna anayemkaribia hapo.

Hivyo kama Taifa tumeweka rehani kipaji cha mchezaji mkubwa kwa kutumia siasa. Inauma sana.

Source : Mwanaspoti​
We ni mwanasiasa? We ndio una shida hujui hata maana ya siasa. Chombo halali kitumie sheria zilizopo mbele ya wanasheria wanaoeleweka leo kirahisi tu limeamuliwa kisiasa. Hivi siasa mnaichukuliaje? kwamba ni jambo la hovyo. Acha ushabiki wa hovyo wacha dogo avune alichopanda. Tatizo la vitoto vya kiswahili vikipata mafanikio kidogo hawajui cha sheria wala taratibu, hawajuikm kuna wakubwa tena. Feitoto ana tabia za kitoto tena za hovyo kabisa.
 
Mkuu City Rider salam kwako.
Kwanza nikiri nimefuatilia hili suala juu juu kutokana na majukumu. Mimi sio mwanasheria ijapo nina ufahamu wa kiasi wa sheria. Leo nilipokuwa napitia makala za gazeti la mwanaspoti nikakutana na hii makala ambayo imenipa maswali mengi kuliko majibu ndipo nikaamua niilete hapa kwenye jukwa ili:-
1. Nipate kwenu wadau ukweli kama kilichoandikwa ndicho kilicho jiri na mwandishi hajatia chumvi
2. Nipate pia ufahamu wa walichopewa Yanga (Mdai) na Fei Toto " statement of Judgement" kinaakisi kilichoandikwa kwenye hili gazeti ama la.

Mkuu City Rider hayo mambo ya CAS tuwaachie wahusika (Yanga, Fei toto na TFF) ila sisi naomba tujikite kwenye hoja tajwa hapo juu.

Ahsante
Uwe na tabia za kuaminika mamlaka halali za nchi siyo kila kitu ujuaji, ubishi ni tabia isiyo na heshima
 
Back
Top Bottom