Kamati kuu CCM yamtosa Hussein Bashe, adaiwa si raia wa Tanzania


Sina hela ya kununua pipi mkuu 🙂 !!!
 
Dark City,

Huyu anajimaliza tena vibaya, hata ulimwengu, Balozi Badora walipiga kelele hivi hivi vitu vilipowekwa hadharani walifayata. CCM hawawezi kukurupuka kiasi hicho, na kama hivyo vyeti ni feki basi wanamfunga.

Wanamfunga wamemkamata navyo?. Kigwangala sasa hivi tumbo joto, anahisi kama uteuzi wake utabatilishwa. Huwezi kumfunga mtu kwa kuwa kuna document zimetolewa gazetini, je kama ni mpango wa wahuni waliomzushia kuzidi kummaliza je. Mtu anaweza kuforge vyeti kuwa hofstede amezaliwa 1958 bila hata ya mimi kufahamu. Hilo halinifanyi mimi kuonekana nimetenda kosa.
 
mkuu nahisi alipost kwa maana ya kisengele nyuma
 
Makamba , ni mshari mkuu wa Kikwete katika siasa za TZ.....SASA NDIO UJUE AINA YA UTAWALA TULIO NAO.
 
Wakuu, Lazima tufahamu kuwa CC na NEC wameliangalia hili jambo kwa umakini hasa ukizingatia nafasi ya bashe UVCCM na mkorogano wa Selelii pale nzega. CC wanaserikali inayowahushisha uhamiaji na kila chombo. Mimi nina amini kuwa hili jambo ni zaidi ya Uraia. Makamba amenukuliwa akisema walipokea vyeti vya kuzaliwa mwaka 2009, lakini akasema uraia ni zaidi ya vyeti. Labda niwape mfano mmoja, hivi kama Bashe amezaliwa TZ lakini kwa namna moja au nyingine ni mweka hazina wa Alshaabab tawi la TZ unadhani CCM wanaweza kusema huyu hapana kwasababu ni Alshabaab, wanajua backlash, ni rahisi kusema si raia[ni mfano tu nisinukuliwe vibaya].
Hili jambo ni pana kuliko tunavyoliona, time will tell
 
Ndo tatizo la kuwa na viongozi waliokwishachoka kufikiria na na faida pia ya kuwa na raia wasiojua kiongozi anatakiwa kufanya nini! Na akifanya kipi kinamwondolea sifa ya kuwa kiongozi
 
Hofstede,
Msimdanganye huyu kijana , CCM wameishamalizana naye wala hana sababu ya kubishana nao magazetini kama anataka tu kuchaguliwa si aende vyama vingine? kila chama kina utaratibu wake. S.M.P2503 katoa ufafanuzi mzuri saana, na si Tanzania tu hata nchi za ulaya wanayo hii ila wao tunapisha kuwa unakuwa raia moja kwa moja kama mama yako ni raia wa nchi hiyo, ila kama baba yako ni raia basi wewe ukifika 18 lazima uombe uraia. Kigezo kuwa mama yake ni mtanzania hakina nguvu kwani sheria zetu zinasema unakuwa mtanzania moja kwa moja kama baba yako ni mtanzania.
 
Wataalamu wa phyisics wanasema there is no work done if there is no distance moved. Kwa mfano hata ukitumia maguvu kiasi gani kusukuma ukuta na usisogee, hakuna workdone yeyote hapo. Na mimi nasema, kujadili kauli za Makamba ni sawa na kusukuma ukuta. Makamba akitamka kitu, the best you can do ni kumshangaa!
 
Kama ni jibu kwa mwalimu aliyeuliza swai hili, basi una max zote!!! SIMPLE AND CLEAR!
 
Halafu wanasema kuna RULE OF LAW Tanzania!! Si walisema wangemkabidhi kwa idara ya uhamiaji; sasa uhamiaji wamesema ni raia kwahiyo suala la kumdeport kama walivyotaka [read Ridhwani] halitowezekana!! Aibu kwa chama cha Kambarage.
 
. Maana kama CCM ni watu wa haki hawawezi kusema mtu aliyepata kura 2000 hakubaliki ila aliyepata kura 1500 ndiye anayekubalika hivyo kupitishwa kuchukua nafasi ya mtu aliyepata kura 14,000!!!!!.

MKUU hii iliniacha hoi nikasema kweli ccm wamekatwa mishipa ya aibu manake hata kama ubabe huu ni kiboko.


Na mambo haya kama nchi yetu itaendelea kuongozwa na hiki chama cha wendawazimu basi TANZANIA itakuwa maskini milele au mpaka kizazi chao kitapo potea.Manake sasa hivi watoto wao wanarithi tabia hii hili kukiendeleza chama kwenye mfumo wa sasa.
 
"1995 citizenship act section 13 inasema ni mpaka aukane ..."

wakuu kuuliza si ujinga mie sio mtaalamu wa sheria na hapa kidogo imenifanya niulize hili nijue.hii sheria ni ya 1995, inaamanisha ilipitishwa 1995? na kama ilipitishwa mwaka huo inamaana ina wa affect watu wa kabla ya 1995 pia au baada ya 1995? na pia kama ilipitishwa 1995 je sheria kabla ya hapo ilikuwa vipi?

swali langu limelenga mwaka wa hio sheria 1995 kama ndio ilipitishwa manake mara nyingi huwa najua mwaka katika sheria yoyote inamaanisha ndio iliposainiwa kuwa sheria kama nimekosa nitapenda kujua leo.wataalam wa sheria naomba msaada wenu.
 

Sounds like upo karibu na aliyeteuliwa kugombea jimbo alilotakiwa kugombea Bashe. Sikiliza mahojiano ya Chiligati na BBC. Yeye hakusema kama baba yake si raia bali amesema kwamba wazazi wake walihamia kitu ambacho Bashe anakipinga kuwa mama yake ni Mzaliwa wa Tabora. Sasa kama wewe ndiyo mama yake Bashe basi tuthibitishie kuwa wewe ni muhamiaji ila kama siyo Bashe ana haki ya kutetea uonevu huu. Yeye anachosema kilichomshitusha si kutoteuliwa ila sababu zilizotolewa kwake ni mpya. Hii witch hunt inaonesha ni jinsi gani CCM ilivyokosa legitimacy ya kuwa chama kinachounda serikali.

Kama Bashe si Raia ashitakiwe mahakamani ambapo ni mahakama huru pekee yenye uwezo wa kuthibitisha uraia wa mtu na si Uhamiaji ambao wao ni enforcer tu wala CCM ambao wao ni wapiga longolongo tu. Hii ni aibu ambayo CCM inapaswa kuchutama, yaani ukivuliwa nguo chutama. Bashe ana haki kikatiba suala la kumdanganya kwani yeye mtoto mdogo, atafute wanasheria wamsaidie. Yeye hapiganii kuteuliwa bali haki yake ya kunyang'anywa uraia kwa misingi ya siasa chafu.
 
..ingekuwa mimi ndiyo Bashe, ningehama tu chama.

..kama ana nia ya kuwawakilisha wana Nzega siyo lazima iwe kupitia CCM.
 
What a shame!!! Shame kwa chama chao, shame kwa kila mmoja wao. Ahhhh TZ bana ni zaidi ya uijuavyo.
 

Si fununu. Ni UKWELI! Bashe alikuwa kambi ya Masauni, na Malisa anabebwa na Ridhiwani! Ndio si-hasa hiyo!

Ametemwa kwa sababu za maslahi binafsi. Kama Malisa angekuwa anagombea Nzega, ni wazi kuwa ANGESHINDA!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…