Kamati Kuu ya CHADEMA, mkiteua wabunge wa Viti Maalumu kuingia Bungeni, mtakuwa mmefanya kosa kubwa sana

Kamati Kuu ya CHADEMA, mkiteua wabunge wa Viti Maalumu kuingia Bungeni, mtakuwa mmefanya kosa kubwa sana

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kwanza nianze kwa kusema kuwa, Katika vitu ambavyo CCM kwa sasa wanatamani vitokee, ni kupata wabunge wa upinzani japo wachache ili kuondoa dhana ya Bunge kuitwa Bunge la CCM-Bunge la chama kimoja.

Kwa sababu hiyo, tarajieni kuona wale wale waliowadhulumu haki zenu wakigeuka wema kwenu na kuanza kuonyesha upendo wa kinafiki kwenu na hata wako wataojidai kuwahurumia ila kamwe msiwaamini na wala msiwasikilize.

Hata hill Bunge likianza mtarajie wabunge hawa hawa wa CCM waliofaidika na matokeo haya, wakaanza kutoa kauli za kukumbuka michango ya wapinzani Bungeni, na hata wanaweza kuja na mapendekezo ya kuwapa mialiko ya kwenda Bungeni kama wageni. Kumbukeni baadhi yao pia nafsi zao zitakuwa zinawasuta na watayatenda haya katika kujaribu kutuliza nafsi zao.

Sio hivyo tu,wanaweza kubadili sheria kuongeza idadi ya wabunge wa kuteuliwa na Raisi, na pia kubadili kanuni/sheria kuongeza wabunge wa vitu maalumu ili nyinyi mpewa nafasi, ila nawambieni kamwe msikubali bali waachieni wao na Bunge lao watimize azima yao na zaidi wakose kisingizio cha kuja kusema wapinzani wanachelewesha/wanakwamisha maendeleo.

Nawaambia angali mapema kabisa kuwa, mkiwa tayari kupeleka wabunge katika Bunge hili, basi pia muwe tayari na masimango: bila huruma ya Raisi au Spika, wengine msingekuwa humu ndani, tumewabeba, hamna shukurani na kauli zingine za aina hiyo pale mtapopishana nao mitazamo ndani ya hilo Bunge.

Pia, iwapo mtapeleka wabunge katika hili Bunge, matapoteza haki na uhalali wa kupinga huu uchaguzi na watatumia uwepo wenu katika hilo Bunge kama hoja ya kujibu tuhuma zozote zinazohusu makandokando ya huu Uchaguzi.

Pia, tambueni hata wao wanaelewa mna wafuasi wengi sana katika nchi hii, hivyo ili kutuliza hasira na machungu ya mashabiki wa upinzani na zaidi chuki inayoweza kujengeka, watataka muwepo Bungeni walau kwa uchache na hapa viongozi wa juu wa vyama vya siasa vya upinzani wanaweza kujikuta katika mtihani wa kukubali ubunge wa kuteuliwa na hata kupewa vyeo serikalini.

Kwahiyo, Kamati Kuu ya CHADEMA, mkikaa myatafari haya yote na mengine ambayo sijayataja hapa kabla ya kufikiri kukubali kuteua wabunge wa vitu maalumu kuingia katika hili Bunge kwani mtakuwa mmefanya kosa kubwa sana la kisiasa kwa kukubali kuwa sehemu ya hili Bunge ambalo uhalali wake ni wa kuhojiwa.

Agenda kuu inapaswa kuwa ni kudai Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi na si kufikiria kuteua wabunge wa vitu maalumu kwenda katika hili Bunge.

Wapinzani, kama kweli mnataka kushika dola, basi lazima muwe tayari ku-sacrifice baadhi ya mambo vinginevyo msahau kuingia Ikulu.

No easy walk to freedom.
 
Kuna mnyukano huko wa hatari kina Matiko, Mdee, Bulaya, Magelesi and the likes wameunda women wing kushinikiza kamati kuu kuwaruhusu wateuliwe na kushiriki bingeni kama viti maalum, vinginevo wakiwahama wasilalamike.
 
Kwanza nianze kwa kusema, Katika vitu ambavyo CCM kwa sasa wanatamani vitokee, ni kupata wabunge wa upinzani japo wachache ili kuondoa dhana ya Bunge kuitwa Bunge la CCM-Bunge la chama kimoja.
Mie nilishapendekeza kwamba CCM na Magufuli need to learn their lesson. Wapinzani wasijishughulishe kabisa na hili BUnge, hata wale wapinzani walioshinda ubunge nilipendekeza wajiuzulu.

Wawaachie CCM Bunge lote kwa 100% Kwanza haitasaidia kitu kuwa na wabunge kidogo BUngeni. Na wala wasikubali kabisa nafasi za kuteuliwa Ubunge na Raisi. Waacheni CCM waone faida ya kuiba ushindi na kukandamiza usawa wa ushindani wa kisiasa. Mtoto akililia wembe mpe. Mwachieni Ndugai ale Bunge lake hadi atapike kwa kukinai.

Kwanza wananchi watawaelewa kwamba hamfanyi siasa kwa ajili ya matumbo yenu bali kwa kuipenda hii nchi. Na pia wabunge wa upinzani wa viti maalum na kuteuliwa watadharauliwa sana na wabunge wa CCM.
 
Walioshinda ubunge kama yule dada wa Nkasi aende bungeni (japo namtilia shaka nyendo zake), viti maalum nao waende bungeni, na wale wanaoona wameonewa kwenye majimbo yao hawakushindwa kihalali waende mahakamani.

Jiwe ni mbabe, na hiki alichofanya kafanya makusudi akitegemea ndio atawapoteza Chadema kabisa, na ndio furaha yake, sasa namna ya ku deal na huyu mtu inahitajika akili ya ziada, sio kukubali defeat kirahisi kwa kugoma, he won't care.

Chadema lazima iendelee kusikika masikioni pa watanzania, zaidi wakiwa bungeni, na ni muhimu waendelee kutoa michango yao kwaajili ya maendeleo ya watanzania, sio kisirani cha mtu mmoja kiwaondoe relini, kwanza mwerevu siku zote hakasirishwi na mpumbavu.

Warudi bungeni wakapiganie Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi, na watumie platform nyingine zote kudai hivyo vitu viwili.

Kama ni kususa, huko kususa kusiishie bungeni tu, maana halisi ya kususa ni pana zaidi ya unavyofikiri; watatakiwa waendelee kususia mpaka uchaguzi mkuu ujao 2025, wasishiriki kama Tume itaendelea kubaki hii iliyopo, sio kususa kwenda bungeni halafu next time washiriki tena uchaguzi, na kwa kufanya hivyo ndio watakuwa wanajifuta wenyewe kwenye ramani ya siasa Tanzania.

Sasa kama wataamua kumsusia fisi butcher wakidhani wanamkomoa, pole zao.
 
Kuna mnyukano huko wa hatari kina matiko, mdee, bulaya, magelesi and the likes wameunda women wing kushinikiza kamati kuu kuwaruhusu wateuliwe na kushiriki bingeni kama viti maalum, vinginevo wakiwahama wasilalamike.
Wahame ila brand ya CHADEMA ililindwe itakuja hata kuuzwa au kuwa re born again na watu wenye akili kubwa na kuleta uhuru. Kumbuka neno CHADEMA kwa ccm na jeshi lote ni kama shetani au pepo kusikia jina la YESU KRISTO likitajwa. Mav* yanagonga.
 
Yaani wewe unawashauri CHADEMA wakubali kuonewa miaka yote. Bora kufutika na kufanya biashara kuliko kuonewa miaka yote na kukubali hali hiyo. Chama cha siasa lengo lake ni kushika dola siku moja. Siyo kuwepo kuwepo tu. Hapo sasa inakuwa NGO.
Walioshinda ubunge kama yule dada wa Nkasi aende bungeni, viti maalum nao waende bungeni, na wale wanaoona wameonewa kwenye majimbo yao hawakushindwa kihalali waende mahakamani..
 
Waende bungeni kwa uchaguzi haramu? CUF walisusa na ikavurugwa, lkn wafuasi halisi wa CUF wakahamia ACT na bado wamepaa zaidi kisiasa.

Binafsi naona ni vema kuwa na msiamamo kwamba uchaguzi huu ulikuwa ni uchafuzi kwahiyo hautambuliki na waliotokana na uchaguzi huu hawatambuliki.
Walioshinda ubunge kama yule dada wa Nkasi aende bungeni, viti maalum nao waende bungeni, na wale wanaoona wameonewa kwenye majimbo yao hawakushindwa kihalali waende mahakamani...
 
Kuna mnyukano huko wa hatari kina matiko, mdee, bulaya, magelesi and the likes wameunda women wing kushinikiza kamati kuu kuwaruhusu wateuliwe na kushiriki bingeni kama viti maalum, vinginevo wakiwahama wasilalamike.
Kina mama wenzie unawatolea unawatungia maneno.
 
Ng'ombe atachijwa alivyolala na msimu huu hakuna kuachia kitu.. Walioshinda waende bungeni na idadi ya viti maalumu itakayopatikana waende bungeni. Ruge Mdee, Matiko ,Bulaya, Mwaifunga, Mwakagenda, Pareso, Aliyegombea Singida mjini na Dodoma mjini wote wateuliwe.
 
Aliyeshinda ubunge aende bungeni kupigania wananchi wake Ila msikubali kupeleka majina ya viti maalum wanaenda kumsimamia Nani bungeni kama sio kutetea maslai yao tu muwe na msimamo Watakao hama wacha wahame Chadema ni taasisi haiwezi anguka na uchaguzi ujao tutaingia kwa tume hiyo hiyo muhamasishe watu kujiandikisha na kupiga kura kwa wingi kura haziwezi kuibiwa
 
Hivi chama si kinapeleka list ya wabunge wa viti maalum tume ya uchaguzi alafu tume ndio watachagua yupi aende bungeni na yupi asiende?

Au mimi ndio sielewi
 
Tumeona mpaka vijijini huko Nkasi, Ukerewe, Tarime, Tunduma, wana sapoti kubwa. Kuchapisha makaratasi ya kura ya CCM ili kupigia majumbani na kupeleka kwenye vituo na kutoruhusu mawakala wa upinzani vituoni siyo bure. CCM walijua wanashindwa kama uchaguzi ungekuwa wa haki. CHADEMA wasiharibu brand yao kwa pesa kidogo za mboga.

Hawakufanya siasa miaka 5 lakini uchaguzi ulipofika, katika miezi 2 wakawapiku CCM. Hiyo yote kwa sababu ya brand ya CHADEMA. Wasiiharibu kabisa.
Wahame ila brand ya CHADEMA ililindwe itakuja hata kuuzwa au kuwa re born again na watu wenye akili kubwa na kuleta uhuru. Kumbuka neno CHADEMA kwa ccm na jeshi lote ni kama shetani au pepo kusikia jina la YESU KRISTO likitajwa. Mav* yanagonga.
 
Kwa kuongezea tu, hawatambuliki - wawe CHADEMA, CCM, ACT ama CUF.
Binafsi naona ni vema kuwa na msiamamo kwamba uchaguzi huu ulikuwa ni uchafuzi kwahiyo hautambuliki na waliotokana na uchaguzi huu hawatambuliki.
 
Back
Top Bottom