Uchaguzi 2020 Kamati Kuu ya CHADEMA yakutana kujadili Uchaguzi Mkuu 2020

Uchaguzi 2020 Kamati Kuu ya CHADEMA yakutana kujadili Uchaguzi Mkuu 2020

CHADEMA

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2013
Posts
490
Reaction score
2,471
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA​

Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) imekutana leo Ijumaa, Juni 26, 2020, Jijini Dar Es Salaam katika kikao chake cha kawaida kwa mujibu wa Katiba ya Chama ya mwaka 2006, toleo la mwaka 2019, ibara ya 7.7.15, ambapo pamoja na masuala mengine, imejadili ajenda zifuatazo;

1. Mchakato wa Uteuzi wa Wagombea wa Urais, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani

2. Taarifa ya Fedha na Bajeti

3. Maandalizi ya Ilani za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 (ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar).

Kikao hicho cha siku moja, kimekutana jijini Dar es Salaam chini ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Taifa Zanzibar, Mhe. Said Issa Mohamed.

Taarifa kuhusu maazimio ya kikao hicho zitatolewa kwa umma kupitia kwa waandishi wa habari wakati muafaka.

Imetolewa leo Ijumaa, Juni 26, 2020 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
Chadema
 
Kamati Kuu ya @chadematzofficial Imekutana Leo tarehe 26 June 2020 Jijini Dar es ( 800 X 640 ).jpg
 
Siku moja tu baada ya Lisu kutumia masaa 4 akiwahutubia watanzania na kuwapa sababu za kwa nini anatangaza nia ya kuwania urais wa Tanzania, huku nyuma Mbowe akaibuka na igizo la kuvamiwa na watu wasiojulikana, kisha kukanyagwa kanyagwa na kuvunjwa mguu wa kulia bila mtoto wake James aliyekuwa ndani kusikia chochote ,badala yake akasikia Joyce Mkuya aliyekuwa umbali wa kilomita
5!!
Lengo la hili igizo ilikuwa ni kufunika habari ya Lisu kuandikwa na vyombo vya habari.

Kana kwamba haitoshi Mbowe baada tu ya kuruhusiwa kutoka hospitali ,huku akichechemea akatangaza nia ya kugombea urais wa Tanzania!
Yani watanzania wakiwa na hamu ya kusikia report kutoka kwa Mbowe mwenyewe kwamba alivamiwaje, ilikuwaje ,badala ya kujibu hizo hoja ,yeye akaja na igizo jingine la kwamba kuna wazee wameenda nyumbani kwake kumshawishi awanie urais wa Tanzania!!.

Hivi Lisu unataka ufanyiwe nini ndiyo ujue kwa sasa hauhitajiki Chadema?
Haya maigizo ya mwenyekiti wako wa chama kufunika utangazaji wako nia hayajakuamsha tu?.

Shituka
 
Jibu unalo zaidi ya miaka 20 wanashiriki chaguzi,wanajua tume ipo huru na inazingatia katiba na sheria za JMT.

Hawakushiriki kwakuwa tume ni huru, bali walishiriki wakitegemea tume itarekebishwa muundo. Ila sasa udhaifu wa tume, umekuwa wazi kwa kiasi ambacho hakivumiliki.
 
Unashauruje

Tudai tume huru ya uchaguzi, hakuna uchaguzi bila kuwa na tume huru uchaguzi. Wapiga kura tunaojitambua hatuko tayari kujitokeza kupiga kura, chini ya tume inayoonyesha kuwa inafuata maelekezo ya chama tawala bila kificho.
 
Tudai tume huru ya uchaguzi, hakuna uchaguzi bila kuwa na tume huru uchaguzi. Wapiga kura tunaojitambua hatuko tayari kujitokeza kupiga kura, chini ya tume inayoonyesha kuwa inafuata maelekezo ya chama tawala bila kificho.
Hivi Mkuu, tume huu inakuaje na hii ya sasa ipoje

ninaomba msaada wa kuelemishwa kwa hili japo kwa uchache
 
Hivi Mkuu, tume huu inakuaje na hii ya sasa ipoje

ninaomba msaada wa kuelemishwa kwa hili japo kwa uchache

Tume huru haiwezi kuchaguliwa na mmoja wa washiriki wa uchaguzi. Tumeona kwa macho yetu tume ikiwa watiifu kwa chama cha mteule wa tume. Hapa tulipofikia hatuna uadilifu tena wa kumuamini kiongozi wa chama kishiriki, kuwa mteuzi wa viongozi wa tume.
 
[emoji3][emoji3][emoji3]uwiii .. ufipa wenzio watakielewa kweli??
Tudai tume huru ya uchaguzi, hakuna uchaguzi bila kuwa na tume huru uchaguzi. Wapiga kura tunaojitambua hatuko tayari kujitokeza kupiga kura, chini ya tume inayoonyesha kuwa inafuata maelekezo ya chama tawala bila kificho.
 
Back
Top Bottom