Kamati ya Bunge yatoa sababu ya kucheleweshwa kwa mradi wa Dege ECo Village wa Kigamboni

Kamati ya Bunge yatoa sababu ya kucheleweshwa kwa mradi wa Dege ECo Village wa Kigamboni

Mkurugenzi mkuu wa NSSF, Godius Kahyayara amesema mradi huo umeshatekelezwa katika awamu mbili

Dar es salaam. Mvutano wa hisa kati ya Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na kampuni ya Azimio, umeelezwa kuwa chanzo cha kuchelewa kwa mradi wa nyumba zaidi 7,000 zilizopo eneo la Dege Beach Kigamboni jijini Dar es salaam.

Hayo yalibainika leo Januari 20, 2018 katika ziara iliyofanywa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) katika eneo la mradi.

Awali Mkurugenzi mkuu wa NSSF, Godius Kahyayara amesema mradi huo umeshatekelezwa katika awamu mbili ambapo nyumba 3,750 zimeshakamilika kati ya nyumba 7,160 za mradi mzima.

Amesema kwa mujibu wa mkataba huo, kampuni ya Azimio iliyotoa ardhi ya hekta 300 inamiliki hisa 55% huku NSSF iliyowekeza zaidi ya Dola 500 ikimiliki hisa asilimia 45.

Amesema mradi huo utakaogharimu dola za 544 za Marekani ulitarajiwa kukamilika mwisho wa mwaka huu lakini haitawezekana kutokana na dosari za mkataba.

Baadhi ya wajumbe wa PAC wamehoji sababu ya Mkurugenzi wa kampuni ya Azimio kutoonekana kila anapotafutwa.

Mbunge wa viti maalum (CCM), Shaly Raymond amesema kuchelewa kwa mradi huo kutapandisha gharama kutoka Dola 544 milioni hadi zaidi ya 700 na kuhoji nani atakayelipa.

"Angalia hiyo meza kuu, mwekezaji hayupo wewe Mkurugenzi umekuja peke yako, wenzako wako wapi?" alihoji Shaly.

Naye mbunge wa viti maalum (CCM), Felister Bura amesema kama Azimio hataki kuonyesha ushirikiano, atafutwe mwekezaji mwingine."Tulipozungumza na mwekezaji huyu alikubali kupunguza hisa zake kwa sababu amewekeza kidogo. Kama anasumbua NSSF waangalie namna ya kupata mwekezaji mwingine,” amesema.

Akijibu hoja za wabunge hao, Profesa Kahyarara amekiri i kucheleweshwa kwa mradi, kwamba bado wanajadiliana na kampuni ya Azimio.

Alimtetea mwekezaji huyo akisema amekuwa na safari nyingi nje ya nchi na kwamba atakuwepo kwenye kikao cha January 26 ambapo mambo yote yatajadiliwa na kutolewa uamuzi.




This was revealed after the Parliamentary Public Accounts Committee (PAC) members yesterday toured the project to inspect its progress.


Dar es Salaam. A dispute over shares between the National Social Security Fund (NSSF) and Tanzania Azimio Construction Co. over the real estate project in Kigamboni has cited as the major cause for delay in implementation of a 7,160-house project at Dege Beach in Kigamboni District.

This was revealed after the Parliamentary Public Accounts Committee (PAC) members yesterday toured the project to inspect its progress.

The contract between the two entities shows that, the Tanzania Azimio Construction Co., which provided 300 hectares for project, owns 55 per cent of the shares while NSSF which has invested over $500 million owns 45 per cent of shares.

However, NSSF director-general Godius Kahyarara revealed that at least 3,750 houses were already constructed as part of the project.

He revealed that the project, whose investment cost was around $544 million, would not have been completed come end of 2018 as it was expected due several inconsistencies.

For her part, Special Seats MP and member of PAC, Ms Shaly Raymond (Kilimanjaro Region) observed that the delay of the project would cause an increasing of investment cost from $500 to $700 million, wondering who would be responsible in footing the difference.

In the same vein, the PAC members wanted to know the reason why the investor was not present during the meeting, this comes after, the director of the Tanzania Azimio Construction Co. did not attend the meeting.

“See! The investor is not here,” adding, “can you tell us where are the other officers?” Ms Raymond questioned NSSF director-general Prof Kahyarara during the meeting.
Hapo penye red palinitia moyo kweli. Nilidhani na mimi ninaweza kuwekeza kwenye miradi mikubwa kiasi hicho na nikawa na share kubwa tu. kumbe ilikuwa ni makosa ya uandishi. Kuweni makini mnapoandika.
 
Pole sana mkuu na hivi tunahamia Dodoma, things will never be the same again!! Biashara gani itafanyika pale tena? Nani atapanga pale na nchi ishahama? Sad!

Ni kweli kabisaaa kila kitu kimeharibika mkuu ila always nyumba za kupanga hazikosi wateja kabisaaa especially karibu na barabara ya Rami
 
Taarifa kumbukizi kuhusu mradi :

11 Dec 2014
Real Madrid Football Player Visit Dege Eco Village in Kigamboni area Dar es Salaam , Tanzania

Mradi huo mkubwa wa kijiji cha kisasa ulioanza mwaka 2013. Hali halisi katika video kama ulivyotembelewa na mwakilishi wa Real Madrid hapo December 2014 na uongozi wa NSSF kuelezea mipango yao kabambe kuvutia wadau mbalimbali kama timu hiyo kubwa ya soka nchini Spain. Mradi huo wenye nyumba elfu saba unatarajiwa kukamilika mwaka 2017.

 
Habari kumbukizi mwaka 2017, mradi wa Dege Beach Eco Village wapigwa mnada

Yono Auction Mart madalali maarufu Tanzania watangaza mnada wa mradi mkubwa baada ya NSSF kuishiwa fedha na hivyo mradi kukwama kuendelea.

Dhima ya mnada huo ni kupata mwekezaji awe wa ndani au nje ya nchi ili kuwezesha mradi huo uweze kukamilika.

Mradi huo una thamani wa USD 350 milioni hivyo anatafutwa mwekezaji kutia kiasi hicho cha fedha ili ukamilishwe kupitia mnada huo.

Kukamilika kwa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutasaidia pia uchochezi wa kiuchumi ktk mradi huo na maeneo ya Kigamboni, Dar-es-Salaam.
 
Habari kumbukizi mwaka 2017, mradi wa Dege Beach Eco Village wapigwa mnada

Yono Auction Mart madalali maarufu Tanzania watangaza mnada wa mradi mkubwa baada ya NSSF kuishiwa fedha na hivyo mradi kukwama kuendelea.

Dhima ya mnada huo ni kupata mwekezaji awe wa ndani au nje ya nchi ili kuwezesha mradi huo uweze kukamilika.

Mradi huo una thamani wa USD 350 milioni hivyo anatafutwa mwekezaji kutia kiasi hicho cha fedha ili ukamilishwe kupitia mnada huo.

Kukamilika kwa ujenzi wa daraja la Kigamboni kutasaidia pia uchochezi wa kiuchumi ktk mradi huo na maeneo ya Kigamboni, Dar-es-Salaam.


Mbona mnashangaa PPP ya ajabu kati ya Jambazi na Serikali ya CCM anapewa ardhi Dege Beach bure kama shamba analipima na kugwa plots mara anakuwa strategic investor na NSSF wao watoe fedha Azimio atoe ardhi kwenye PPP ardhi is a sunken cost huwezi kuipa thamani kubwa kwa vile umiliki ni 66 years kwa estate na 99 year kwa shamba it doesn’t add any value to the project. Hiyo ardhi angepewa NSSF na huyo Mbia wao angetoa fedha kilichofanyika ni Wizi wa mchana.
Daraja la Kigamboni ni mradi bomu kwanza njia ya kutokea kwa upende wa Kigamboni haijakamilika hiyo speed limit ya 30km/ H ni tatizo hakuna mradi pale !
To add salt to the wound go back and review the ppp between Caspian na Wizara ya Mambo ya Ndani kwenye miradi ya majengo ya Police , Oysterbay , Mikocheni na zile nyumba zaidi ya 300 nasikia Jiwe ana tafuta mbinu za kuvunja mkataba nyumba na kituo cha Police vimeshakilika tayari kukizindua hataki anazindua madaraja na kuzindua vibanda walivyojengewa Polisi kule Arusha haya kazi kwenu. Madudu ni mengi ndio maana kuna kasi ya kufungia social media ili watu wavikwe mewani za mbao kama enzi ya Mchongameno ! Wizi uko pale pale hakuna cha kutumbua ilikuwa ni justification ya kuweka watu wake kwenye mfumo but mind you it’s only for ten years baada ya hapo akija mwingine atatumbua wote na kwenda Mahakamani but always ushahidi huwa kama machozi ya Samaki baharini!
 
Back
Top Bottom