Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 15,101
- 56,054
Kuna makosa ya msingi sana kikao kilichoamua kuwapeleka wazee akina Makamba, Kinana na Membe kwenye kamati ya maadili.
1. Wajumbe wa kikao cha maadili wameshatoa hukumu yao.
Katibu mkuu wa CCM ambaye ni mjumbe wa kamati ya maadili ameshasikika tangu zile sauti zilizodukuliwa zilipovuja akitoa hukumu yake, alisikika akibeza yaliyozungumzwa mle huku akiwaita wazungumzaji wale kuwa ni Wapumbavu wa mwaka.
Katika hali kama hii ambapo mshitaki ana maamuzi tayari haki itatendeka vipi?
2. Ushahidi wa kuwashitaki Wazee umebase katika kuingilia faragha zao na udukuzi kinyume cha sheria
Mazungumzo ya Wazee wetu hayakuwa kwa ajili ya public consumption.
Wazee wale faragha zao ziliingiliwa kinyume cha katiba ya nchi na sheria za nchi.
Sidhani kama chama kinachoongoza nchi na kinachotakiwa kulinda na kutetea katiba na sheria za nchi kinaweza kuanza kwenda rogue kudukuadukua au kutegemea udukuzi wa kinyume cha sheria ili kutoa maamuzi dhidi ya wanachama wake.
Ushahidi unaopatikana kwa kuvunja sheria siyo ushahidi at all.
3. Huwezi kumuita Membe bila kumuita pia aliyekuwa akizungumza naye
Kama Membe alitenda kosa, Je huyoaliyekuwa "akiteta" naye kwenye simu hajaitwa kwenye kikao cha maadili? Au Shida yenu ni Membe?
4. Mshitaki kwenye hiyo kamati ya maadili ni nani?
Je ni CCM inashitaki kwaniaba ya Mwenyekiti au Mwenyekiti anashitaki chamani kuvunjiwa heshima?
Kama ni Mwenyekiti mbona Mwenyekiti alitoa kauli mwezi septemba kuwa ameamua kukaa kimya hilo suala asilipeleke kwenye kamati ya maadili, Je mwenyekiti leo kawa kigeugeu? amekuwa na ndimi mbili?
Na kama siye yeye yaani Mwenyekiti kwenda kushitaki kwa kudhani katendewa kosa, ni nani kashitaki? Kwa kuathiriwa vipi huyo aliyeshitaki yeye binafsi hadi ashitaki?
Na kama ni chama ndicho kinashitaki sasa kamati ya chama ya maadili itakwendaje kinyume na chama chenyewe?
5. Hukumu imeshatoka
Kama unasema akina Nape, Makamba mdogo walikosa ila wamesamehewa baada ya Kamati ya maadili kukubaliana na msamaha wa Mwenyekiti.
Ina maana tayari hata wazee waliokuwa wakiongea kwenye simu na hao vijana kamati imeshawaona na Makosa isipokuwa tu "hawajapata msamaha wa Mwenyekiti".
Bashiru alisema, Kusamehewa na Rais Magufuli siyo hoja ya shauri kutofikishwa kwenye kamati ya maadili, lakini Bashiru huyohuyo hakutwambia kuwa Msamaha wa Mwenyekiti sio hoja ya maamuzi ya kikao cha kamati ya maadili, lakini kikao cha maadili kimechukua msamaha wa Mwenyekiti kuwa ni uamuzi wa kikao hicho kwamba sasa vijana wale wasamehewe.
Je ina maana kikao hicho cha maadili kinafanya kazi kwa huruma ya mwenyekiti na hii maana yake maadamu wazee wale hawajapewa msamaha wa mwenyekiti basi hicho kikao kinakwenda kushughulika nao.
Huu ni utaratibu wa ajabu kweli wa utendaji haki ndani ya chama.
HITIMISHO
1. Hili zoezi la kuwaita wazee kwenye kikao cha maadili ni udhalilishaji mwingine kwa hawa wazee.
Yaani kwanza walizushiwa mambo mengi na mwanachama wa CCM aitwaye Musiba walikaa kimya kwa muda mrefu.
Wakajiribu kutafuta haki kupitia baraza la wazee, sauti zao zikadukuliwa, na leo wanadhalilishwa tena kwa kuitwa kwenye kikao cha maadili.
2. Mshitaki hajulikani
Kama ni Mwenyekiti ndiye anayeshitaki kwa kudhani ametendewa mabaya na wale wazee, aseme.
Lakini hata akisema leo ni tofauti na kauli yake ya September ya kuwa aliamua kukaa kimya ili hayo mambo yasiende huko mbali. Sasa je ni nani anashadadia haya mambo, je ni katibu mkuu, au ni nani?
3. Badala ya kuponya hili suala linatibua vidonda, makovu na maumivu
Chama kinahitaji umoja, watu wameumizana kwa namna moja au nyingine, ilihitajika healing process badala ya kutunishiana misuli katika kipindi hiki.
Chama leo kipo hapa sababu kila mwanachama, awaye madarakani au nje ya madaraka amevuja jasho kwa ajili ya chama hiki.
Walioko madarakani leo, wajue miaka mitano iliyopita kuna watu walipambana ili waingie washike usukani katika spirit ya chama.
Fikiria katibu mkuu aliyetumikia chama, akawa amechoka anaomba astaafu, anabembelezwa aendelee, anawaomba jamani niacheni nipumzike, lakini bado tu wanang'ang'ania aendelee kubeba mzigo.
Huyu kweli unaweza kumburuza huko kwenye vikao vya maadili tena kwa kumdukua?
4. This is Kangaroo court
Wanaoshitaki kwa niaba ya Mwenyekiti miongoni mwao ni wajumbe wa kamati ya maadili, yaani washitaki ni haohao na watoa hukumu ni haohao. Hakuna haki hapo, hii ni Kangaroo court.
A party that can for dubious reasons crucify its own comrades who fought and bleed for it is no longer a political party, It is a monster. It can do anything to anybody without bating an eye!
1. Wajumbe wa kikao cha maadili wameshatoa hukumu yao.
Katibu mkuu wa CCM ambaye ni mjumbe wa kamati ya maadili ameshasikika tangu zile sauti zilizodukuliwa zilipovuja akitoa hukumu yake, alisikika akibeza yaliyozungumzwa mle huku akiwaita wazungumzaji wale kuwa ni Wapumbavu wa mwaka.
Katika hali kama hii ambapo mshitaki ana maamuzi tayari haki itatendeka vipi?
2. Ushahidi wa kuwashitaki Wazee umebase katika kuingilia faragha zao na udukuzi kinyume cha sheria
Mazungumzo ya Wazee wetu hayakuwa kwa ajili ya public consumption.
Wazee wale faragha zao ziliingiliwa kinyume cha katiba ya nchi na sheria za nchi.
Sidhani kama chama kinachoongoza nchi na kinachotakiwa kulinda na kutetea katiba na sheria za nchi kinaweza kuanza kwenda rogue kudukuadukua au kutegemea udukuzi wa kinyume cha sheria ili kutoa maamuzi dhidi ya wanachama wake.
Ushahidi unaopatikana kwa kuvunja sheria siyo ushahidi at all.
3. Huwezi kumuita Membe bila kumuita pia aliyekuwa akizungumza naye
Kama Membe alitenda kosa, Je huyoaliyekuwa "akiteta" naye kwenye simu hajaitwa kwenye kikao cha maadili? Au Shida yenu ni Membe?
4. Mshitaki kwenye hiyo kamati ya maadili ni nani?
Je ni CCM inashitaki kwaniaba ya Mwenyekiti au Mwenyekiti anashitaki chamani kuvunjiwa heshima?
Kama ni Mwenyekiti mbona Mwenyekiti alitoa kauli mwezi septemba kuwa ameamua kukaa kimya hilo suala asilipeleke kwenye kamati ya maadili, Je mwenyekiti leo kawa kigeugeu? amekuwa na ndimi mbili?
Na kama siye yeye yaani Mwenyekiti kwenda kushitaki kwa kudhani katendewa kosa, ni nani kashitaki? Kwa kuathiriwa vipi huyo aliyeshitaki yeye binafsi hadi ashitaki?
Na kama ni chama ndicho kinashitaki sasa kamati ya chama ya maadili itakwendaje kinyume na chama chenyewe?
5. Hukumu imeshatoka
Kama unasema akina Nape, Makamba mdogo walikosa ila wamesamehewa baada ya Kamati ya maadili kukubaliana na msamaha wa Mwenyekiti.
Ina maana tayari hata wazee waliokuwa wakiongea kwenye simu na hao vijana kamati imeshawaona na Makosa isipokuwa tu "hawajapata msamaha wa Mwenyekiti".
Bashiru alisema, Kusamehewa na Rais Magufuli siyo hoja ya shauri kutofikishwa kwenye kamati ya maadili, lakini Bashiru huyohuyo hakutwambia kuwa Msamaha wa Mwenyekiti sio hoja ya maamuzi ya kikao cha kamati ya maadili, lakini kikao cha maadili kimechukua msamaha wa Mwenyekiti kuwa ni uamuzi wa kikao hicho kwamba sasa vijana wale wasamehewe.
Je ina maana kikao hicho cha maadili kinafanya kazi kwa huruma ya mwenyekiti na hii maana yake maadamu wazee wale hawajapewa msamaha wa mwenyekiti basi hicho kikao kinakwenda kushughulika nao.
Huu ni utaratibu wa ajabu kweli wa utendaji haki ndani ya chama.
HITIMISHO
1. Hili zoezi la kuwaita wazee kwenye kikao cha maadili ni udhalilishaji mwingine kwa hawa wazee.
Yaani kwanza walizushiwa mambo mengi na mwanachama wa CCM aitwaye Musiba walikaa kimya kwa muda mrefu.
Wakajiribu kutafuta haki kupitia baraza la wazee, sauti zao zikadukuliwa, na leo wanadhalilishwa tena kwa kuitwa kwenye kikao cha maadili.
2. Mshitaki hajulikani
Kama ni Mwenyekiti ndiye anayeshitaki kwa kudhani ametendewa mabaya na wale wazee, aseme.
Lakini hata akisema leo ni tofauti na kauli yake ya September ya kuwa aliamua kukaa kimya ili hayo mambo yasiende huko mbali. Sasa je ni nani anashadadia haya mambo, je ni katibu mkuu, au ni nani?
3. Badala ya kuponya hili suala linatibua vidonda, makovu na maumivu
Chama kinahitaji umoja, watu wameumizana kwa namna moja au nyingine, ilihitajika healing process badala ya kutunishiana misuli katika kipindi hiki.
Chama leo kipo hapa sababu kila mwanachama, awaye madarakani au nje ya madaraka amevuja jasho kwa ajili ya chama hiki.
Walioko madarakani leo, wajue miaka mitano iliyopita kuna watu walipambana ili waingie washike usukani katika spirit ya chama.
Fikiria katibu mkuu aliyetumikia chama, akawa amechoka anaomba astaafu, anabembelezwa aendelee, anawaomba jamani niacheni nipumzike, lakini bado tu wanang'ang'ania aendelee kubeba mzigo.
Huyu kweli unaweza kumburuza huko kwenye vikao vya maadili tena kwa kumdukua?
4. This is Kangaroo court
Wanaoshitaki kwa niaba ya Mwenyekiti miongoni mwao ni wajumbe wa kamati ya maadili, yaani washitaki ni haohao na watoa hukumu ni haohao. Hakuna haki hapo, hii ni Kangaroo court.
A party that can for dubious reasons crucify its own comrades who fought and bleed for it is no longer a political party, It is a monster. It can do anything to anybody without bating an eye!