Kamati ya Maadili ya CCM: Kangaroo court

Kamati ya Maadili ya CCM: Kangaroo court

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Kuna makosa ya msingi sana kikao kilichoamua kuwapeleka wazee akina Makamba, Kinana na Membe kwenye kamati ya maadili.

1. Wajumbe wa kikao cha maadili wameshatoa hukumu yao.

Katibu mkuu wa CCM ambaye ni mjumbe wa kamati ya maadili ameshasikika tangu zile sauti zilizodukuliwa zilipovuja akitoa hukumu yake, alisikika akibeza yaliyozungumzwa mle huku akiwaita wazungumzaji wale kuwa ni Wapumbavu wa mwaka.

Katika hali kama hii ambapo mshitaki ana maamuzi tayari haki itatendeka vipi?

2. Ushahidi wa kuwashitaki Wazee umebase katika kuingilia faragha zao na udukuzi kinyume cha sheria

Mazungumzo ya Wazee wetu hayakuwa kwa ajili ya public consumption.

Wazee wale faragha zao ziliingiliwa kinyume cha katiba ya nchi na sheria za nchi.

Sidhani kama chama kinachoongoza nchi na kinachotakiwa kulinda na kutetea katiba na sheria za nchi kinaweza kuanza kwenda rogue kudukuadukua au kutegemea udukuzi wa kinyume cha sheria ili kutoa maamuzi dhidi ya wanachama wake.

Ushahidi unaopatikana kwa kuvunja sheria siyo ushahidi at all.

3. Huwezi kumuita Membe bila kumuita pia aliyekuwa akizungumza naye

Kama Membe alitenda kosa, Je huyoaliyekuwa "akiteta" naye kwenye simu hajaitwa kwenye kikao cha maadili? Au Shida yenu ni Membe?

4. Mshitaki kwenye hiyo kamati ya maadili ni nani?

Je ni CCM inashitaki kwaniaba ya Mwenyekiti au Mwenyekiti anashitaki chamani kuvunjiwa heshima?

Kama ni Mwenyekiti mbona Mwenyekiti alitoa kauli mwezi septemba kuwa ameamua kukaa kimya hilo suala asilipeleke kwenye kamati ya maadili, Je mwenyekiti leo kawa kigeugeu? amekuwa na ndimi mbili?

Na kama siye yeye yaani Mwenyekiti kwenda kushitaki kwa kudhani katendewa kosa, ni nani kashitaki? Kwa kuathiriwa vipi huyo aliyeshitaki yeye binafsi hadi ashitaki?

Na kama ni chama ndicho kinashitaki sasa kamati ya chama ya maadili itakwendaje kinyume na chama chenyewe?

5. Hukumu imeshatoka

Kama unasema akina Nape, Makamba mdogo walikosa ila wamesamehewa baada ya Kamati ya maadili kukubaliana na msamaha wa Mwenyekiti.

Ina maana tayari hata wazee waliokuwa wakiongea kwenye simu na hao vijana kamati imeshawaona na Makosa isipokuwa tu "hawajapata msamaha wa Mwenyekiti".

Bashiru alisema, Kusamehewa na Rais Magufuli siyo hoja ya shauri kutofikishwa kwenye kamati ya maadili, lakini Bashiru huyohuyo hakutwambia kuwa Msamaha wa Mwenyekiti sio hoja ya maamuzi ya kikao cha kamati ya maadili, lakini kikao cha maadili kimechukua msamaha wa Mwenyekiti kuwa ni uamuzi wa kikao hicho kwamba sasa vijana wale wasamehewe.

Je ina maana kikao hicho cha maadili kinafanya kazi kwa huruma ya mwenyekiti na hii maana yake maadamu wazee wale hawajapewa msamaha wa mwenyekiti basi hicho kikao kinakwenda kushughulika nao.

Huu ni utaratibu wa ajabu kweli wa utendaji haki ndani ya chama.

HITIMISHO
1. Hili zoezi la kuwaita wazee kwenye kikao cha maadili ni udhalilishaji mwingine kwa hawa wazee.

Yaani kwanza walizushiwa mambo mengi na mwanachama wa CCM aitwaye Musiba walikaa kimya kwa muda mrefu.

Wakajiribu kutafuta haki kupitia baraza la wazee, sauti zao zikadukuliwa, na leo wanadhalilishwa tena kwa kuitwa kwenye kikao cha maadili.

2. Mshitaki hajulikani
Kama ni Mwenyekiti ndiye anayeshitaki kwa kudhani ametendewa mabaya na wale wazee, aseme.

Lakini hata akisema leo ni tofauti na kauli yake ya September ya kuwa aliamua kukaa kimya ili hayo mambo yasiende huko mbali. Sasa je ni nani anashadadia haya mambo, je ni katibu mkuu, au ni nani?

3. Badala ya kuponya hili suala linatibua vidonda, makovu na maumivu

Chama kinahitaji umoja, watu wameumizana kwa namna moja au nyingine, ilihitajika healing process badala ya kutunishiana misuli katika kipindi hiki.

Chama leo kipo hapa sababu kila mwanachama, awaye madarakani au nje ya madaraka amevuja jasho kwa ajili ya chama hiki.

Walioko madarakani leo, wajue miaka mitano iliyopita kuna watu walipambana ili waingie washike usukani katika spirit ya chama.

Fikiria katibu mkuu aliyetumikia chama, akawa amechoka anaomba astaafu, anabembelezwa aendelee, anawaomba jamani niacheni nipumzike, lakini bado tu wanang'ang'ania aendelee kubeba mzigo.

Huyu kweli unaweza kumburuza huko kwenye vikao vya maadili tena kwa kumdukua?

4. This is Kangaroo court
Wanaoshitaki kwa niaba ya Mwenyekiti miongoni mwao ni wajumbe wa kamati ya maadili, yaani washitaki ni haohao na watoa hukumu ni haohao. Hakuna haki hapo, hii ni Kangaroo court.

A party that can for dubious reasons crucify its own comrades who fought and bleed for it is no longer a political party, It is a monster. It can do anything to anybody without bating an eye!
 
Wahusika wote uliowataja kwenye màda yako hawajawahi kusema ulichoandika labda pengine wewe ni mtabiri hivyo umetabiri yatakayosemwa
 
Huwa sipendi kujibu hoja za mawazo mfu lakini goja nichangie

Japo wewe sio mwanachama wa CCM ( predictions) bado una maoni yako kwa hiko chama kama ulichokifanya

Sitaki kuingia ndani sana lakini goja nikudokeze tu, kamuulize Bernard Membe namna chombo nyeti kinavyofanya kazi, kama kutakuwa na kosa kisheria kama ulivyobwabwaja humu then atakachokujibu utupe mrejesho, kwa uelewa wangu linapofikia suala la Kiusalama, kuna utaratibu wake wa kuchukua hatua! CCM ni chama kilichopo madarakani, CCM ndio usalama na kwa maana hiyo akiyetukanwa kwenye zile clips ni kiongozi na mkuu wa nchi,hii haina haja kuifafanua sana, nje ya Rais masuala yote ya Kiusalama huweza kushughulikiwa kwa muktadha na mtazamo mpana!

Kinachoangaliwa hapa ni authenticity ya mashtaka hayo, kitendo klichofanywa na watuhumiwa ni cha kiusalama ndio maana wameitwa na chombo hicho, kosa lile ni la uhaini tatizo letu ni siasa tu but hata kama umedai hawakuwa na lengo la ile habari haikuwa for the public consumption, lakini si ukweli unaweza kuthibitisha kuwa walifanya hicho kitendo? Je public consumption tunaiangalia katika dhana ipi? Kama sita wale ama the big three wangeweza ku expose au leak ile taarifa unajua ni kwa watu wangapi ingekuwa consumed?

Chama chochote cha siasa kina utaratibu wake, japo inapofikia kwa umma hata asiye mwanachama huwa mchambuzi mzuri na zaidi hutoa maelekezo kana kwamba anayajua ya ndani mwe; huwezi sema they did so not with the intention of spreading the message to the public, haijalishi na kwa namna gani umefanya kosa kama hilo ukawa defensive kwa nadharia hiyo, ndio maana kuna Cyber crimes but all in all serikali inamkono mrefu na kwa sasa CCM ndio serikali

Tuache chama kiamue kwa wanachama wake

Tusiwe na viherehere vya kuchambua ya ngoswe tumpe mwenyewe!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nime re read nimestaajabu sana kuna mambo mengi umeyaongea kwa mihemko na personal attack imekuongoza kwenye huu uzi, maswali mengi ni utetezi usio na tija, Anyway hivi unakumbuka sakata la Mbunge wa Ubungo Kubenea na Komu? Kwanini waliitwa kwenye kamati?

Je waliowaita source of information haikuwa ile clip? Don't have such doomed kind of arguing, use some evidence to judge,

Tuache mambo ya kinafiki fanya unayoweza mengine kaa kimya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kiranga una mambo upo kama mshipa/ngiri maji/busha. mbele haupo nyuma haupo. unafuata mdundo wa ngoma. shame on you lumumba nzi wa kijani buku 7


Mkubwa umepitiwa au?

Huyu Kawe Alumni kwani ndiye Kiranga?
 
Huwa sipendi kujibu hoja za mawazo mfu lakini goja nichangie

Japo wewe sio mwanachama wa CCM ( predictions) bado una maoni yako kwa hiko chama kama ulichokifanya

Sitaki kuingia ndani sana lakini goja nikudokeze tu, kamuulize Bernard Membe namna chombo nyeti kinavyofanya kazi, kama kutakuwa na kosa kisheria kama ulivyobwabwaja humu then atakachokujibu utupe mrejesho, kwa uelewa wangu linapofikia suala la Kiusalama, kuna utaratibu wake wa kuchukua hatua! CCM ni chama kilichopo madarakani, CCM ndio usalama na kwa maana hiyo akiyetukanwa kwenye zile clips ni kiongozi na mkuu wa nchi,hii haina haja kuifafanua sana, nje ya Rais masuala yote ya Kiusalama huweza kushughulikiwa kwa muktadha na mtazamo mpana!

Kinachoangaliwa hapa ni authenticity ya mashtaka hayo, kitendo klichofanywa na watuhumiwa ni cha kiusalama ndio maana wameitwa na chombo hicho, kosa lile ni la uhaini tatizo letu ni siasa tu but hata kama umedai hawakuwa na lengo la ile habari haikuwa for the public consumption, lakini si ukweli unaweza kuthibitisha kuwa walifanya hicho kitendo? Je public consumption tunaiangalia katika dhana ipi? Kama sita wale ama the big three wangeweza ku expose au leak ile taarifa unajua ni kwa watu wangapi ingekuwa consumed?

Chama chochote cha siasa kina utaratibu wake, japo inapofikia kwa umma hata asiye mwanachama huwa mchambuzi mzuri na zaidi hutoa maelekezo kana kwamba anayajua ya ndani mwe; huwezi sema they did so not with the intention of spreading the message to the public, haijalishi na kwa namna gani umefanya kosa kama hilo ukawa defensive kwa nadharia hiyo, ndio maana kuna Cyber crimes but all in all serikali inamkono mrefu na kwa sasa CCM ndio serikali

Tuache chama kiamue kwa wanachama wake

Tusiwe na viherehere vya kuchambua ya ngoswe tumpe mwenyewe!

Sent using Jamii Forums mobile app

Tusi gn umelisikia wakitamka.

Au kosa si Musiba

Kwann sasa Musiba haongei tena.

Mi dua zangu wajiondoe ktk chama kabla hawajafika kwenye hiyo kamati,

Sitegemei kupata msamiati mpya kabla wakati na baada ya kikao hicho.
 
Tusi gn umelisikia wakitamka.

Au kosa si Musiba

Kwann sasa Musiba haongei tena.

Mi dua zangu wajiondoe ktk chama kabla hawajafika kwenye hiyo kamati,

Sitegemei kupata msamiati mpya kabla wakati na baada ya kikao hicho.

Hawawezi kuondoka

Makandokando mengi na ccm bingwa wa kubamkia sana
 
Mimi nadhani ndio muda muafaka wa Chadema kwenda na Membe kama walivyokua wanataka. Mchukueni tu huku hana nafasi,sa mnamuonea huruma tena,Chadema kuwaelewa kazi sana.

Kana kane ni kamo
 
Cha msingi wahudhurie tu,hiyo ni perception yako,hauwezi kuwa ni utetezi waku discourage kamati ya taifa ya nidhamu ya chama chao.
Kuna makosa ya msingi sana kikao kilichoamua kuwapeleka wazee akina Makamba, Kinana na Membe kwenye kamati ya maadili.

1. Wajumbe wa kikao cha maadili wameshatoa hukumu yao.

Katibu mkuu wa CCM ambaye ni mjumbe wa kamati ya maadili ameshasikika tangu zile sauti zilizodukuliwa zilipovuja akitoa hukumu yake, alisikika akibeza yaliyozungumzwa mle huku akiwaita wazungumzaji wale kuwa ni Wapumbavu wa mwaka.

Katika hali kama hii ambapo mshitaki ana maamuzi tayari haki itatendeka vipi?

2. Ushahidi wa kuwashitaki Wazee umebase katika kuingilia faragha zao na udukuzi kinyume cha sheria

Mazungumzo ya Wazee wetu hayakuwa kwa ajili ya public consumption.

Wazee wale faragha zao ziliingiliwa kinyume cha katiba ya nchi na sheria za nchi.

Sidhani kama chama kinachoongoza nchi na kinachotakiwa kulinda na kutetea katiba na sheria za nchi kinaweza kuanza kwenda rogue kudukuadukua au kutegemea udukuzi wa kinyume cha sheria ili kutoa maamuzi dhidi ya wanachama wake.

Ushahidi unaopatikana kwa kuvunja sheria siyo ushahidi at all.

3. Huwezi kumuita Membe bila kumuita pia aliyekuwa akizungumza naye

Kama Membe alitenda kosa, Je huyoaliyekuwa "akiteta" naye kwenye simu hajaitwa kwenye kikao cha maadili? Au Shida yenu ni Membe?

4. Mshitaki kwenye hiyo kamati ya maadili ni nani?

Je ni CCM inashitaki kwaniaba ya Mwenyekiti au Mwenyekiti anashitaki chamani kuvunjiwa heshima?

Kama ni Mwenyekiti mbona Mwenyekiti alitoa kauli mwezi septemba kuwa ameamua kukaa kimya hilo suala asilipeleke kwenye kamati ya maadili, Je mwenyekiti leo kawa kigeugeu? amekuwa na ndimi mbili?

Na kama siye yeye yaani Mwenyekiti kwenda kushitaki kwa kudhani katendewa kosa, ni nani kashitaki? Kwa kuathiriwa vipi huyo aliyeshitaki yeye binafsi hadi ashitaki?

Na kama ni chama ndicho kinashitaki sasa kamati ya chama ya maadili itakwendaje kinyume na chama chenyewe?

5. Hukumu imeshatoka

Kama unasema akina Nape, Makamba mdogo walikosa ila wamesamehewa baada ya Kamati ya maadili kukubaliana na msamaha wa Mwenyekiti.

Ina maana tayari hata wazee waliokuwa wakiongea kwenye simu na hao vijana kamati imeshawaona na Makosa isipokuwa tu "hawajapata msamaha wa Mwenyekiti".

Bashiru alisema, Kusamehewa na Rais Magufuli siyo hoja ya shauri kutofikishwa kwenye kamati ya maadili, lakini Bashiru huyohuyo hakutwambia kuwa Msamaha wa Mwenyekiti sio hoja ya maamuzi ya kikao cha kamati ya maadili, lakini kikao cha maadili kimechukua msamaha wa Mwenyekiti kuwa ni uamuzi wa kikao hicho kwamba sasa vijana wale wasamehewe.

Je ina maana kikao hicho cha maadili kinafanya kazi kwa huruma ya mwenyekiti na hii maana yake maadamu wazee wale hawajapewa msamaha wa mwenyekiti basi hicho kikao kinakwenda kushughulika nao.

Huu ni utaratibu wa ajabu kweli wa utendaji haki ndani ya chama.

HITIMISHO
1. Hili zoezi la kuwaita wazee kwenye kikao cha maadili ni udhalilishaji mwingine kwa hawa wazee.

Yaani kwanza walizushiwa mambo mengi na mwanachama wa CCM aitwaye Musiba walikaa kimya kwa muda mrefu.

Wakajiribu kutafuta haki kupitia baraza la wazee, sauti zao zikadukuliwa, na leo wanadhalilishwa tena kwa kuitwa kwenye kikao cha maadili.

2. Mshitaki hajulikani
Kama ni Mwenyekiti ndiye anayeshitaki kwa kudhani ametendewa mabaya na wale wazee, aseme.

Lakini hata akisema leo ni tofauti na kauli yake ya September ya kuwa aliamua kukaa kimya ili hayo mambo yasiende huko mbali. Sasa je ni nani anashadadia haya mambo, je ni katibu mkuu, au ni nani?

3. Badala ya kuponya hili suala linatibua vidonda, makovu na maumivu

Chama kinahitaji umoja, watu wameumizana kwa namna moja au nyingine, ilihitajika healing process badala ya kutunishiana misuli katika kipindi hiki.

Chama leo kipo hapa sababu kila mwanachama, awaye madarakani au nje ya madaraka amevuja jasho kwa ajili ya chama hiki.

Walioko madarakani leo, wajue miaka mitano iliyopita kuna watu walipambana ili waingie washike usukani katika spirit ya chama.

Fikiria katibu mkuu aliyetumikia chama, akawa amechoka anaomba astaafu, anabembelezwa aendelee, anawaomba jamani niacheni nipumzike, lakini bado tu wanang'ang'ania aendelee kubeba mzigo.

Huyu kweli unaweza kumburuza huko kwenye vikao vya maadili tena kwa kumdukua?

4. This is Kangaroo court
Wanaoshitaki kwa niaba ya Mwenyekiti miongoni mwao ni wajumbe wa kamati ya maadili, yaani washitaki ni haohao na watoa hukumu ni haohao. Hakuna haki hapo, hii ni Kangaroo court.

A party that can for dubious reasons crucify its own comrades who fought and bleed for it is no longer a political party, It is a monster. It can do anything to anybody without bating an eye!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ccm ni dira ya Nchi

Vyama vya upinzani vinaiga kutoka Ccm

Lazima Ccm ichukue hatua kwa manufaa ya Nchi

Hiyo kamati ya maadili ya ccm naifananisha na ile ya bunge. Lengo hasa la hiyo kamati sio kulinda maadili bali ni kukomoa, kugandamiza na kuwatia uoga wote wasiokubaliana na mwenyekiti. Na hiyo kamati huwa inaundwa na wale watu wa ndio mzee kwa mwenyekiti, ambao wao maamuzi yao ni kuhakikisha wanamfurahisha mwenyekiti kwa kukomoa wasiomsujudia.
 
Well done guy
Huwa sipendi kujibu hoja za mawazo mfu lakini goja nichangie

Japo wewe sio mwanachama wa CCM ( predictions) bado una maoni yako kwa hiko chama kama ulichokifanya

Sitaki kuingia ndani sana lakini goja nikudokeze tu, kamuulize Bernard Membe namna chombo nyeti kinavyofanya kazi, kama kutakuwa na kosa kisheria kama ulivyobwabwaja humu then atakachokujibu utupe mrejesho, kwa uelewa wangu linapofikia suala la Kiusalama, kuna utaratibu wake wa kuchukua hatua! CCM ni chama kilichopo madarakani, CCM ndio usalama na kwa maana hiyo akiyetukanwa kwenye zile clips ni kiongozi na mkuu wa nchi,hii haina haja kuifafanua sana, nje ya Rais masuala yote ya Kiusalama huweza kushughulikiwa kwa muktadha na mtazamo mpana!

Kinachoangaliwa hapa ni authenticity ya mashtaka hayo, kitendo klichofanywa na watuhumiwa ni cha kiusalama ndio maana wameitwa na chombo hicho, kosa lile ni la uhaini tatizo letu ni siasa tu but hata kama umedai hawakuwa na lengo la ile habari haikuwa for the public consumption, lakini si ukweli unaweza kuthibitisha kuwa walifanya hicho kitendo? Je public consumption tunaiangalia katika dhana ipi? Kama sita wale ama the big three wangeweza ku expose au leak ile taarifa unajua ni kwa watu wangapi ingekuwa consumed?

Chama chochote cha siasa kina utaratibu wake, japo inapofikia kwa umma hata asiye mwanachama huwa mchambuzi mzuri na zaidi hutoa maelekezo kana kwamba anayajua ya ndani mwe; huwezi sema they did so not with the intention of spreading the message to the public, haijalishi na kwa namna gani umefanya kosa kama hilo ukawa defensive kwa nadharia hiyo, ndio maana kuna Cyber crimes but all in all serikali inamkono mrefu na kwa sasa CCM ndio serikali

Tuache chama kiamue kwa wanachama wake

Tusiwe na viherehere vya kuchambua ya ngoswe tumpe mwenyewe!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpe Nakoz za kutosha,bwege huyo
Nime re read nimestaajabu sana kuna mambo mengi umeyaongea kwa mihemko na personal attack imekuongoza kwenye huu uzi, maswali mengi ni utetezi usio na tija, Anyway hivi unakumbuka sakata la Mbunge wa Ubungo Kubenea na Komu? Kwanini waliitwa kwenye kamati?

Je waliowaita source of information haikuwa ile clip? Don't have such doomed kind of arguing, use some evidence to judge,

Tuache mambo ya kinafiki fanya unayoweza mengine kaa kimya

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Useless!
Hiyo kamati ya maadili ya ccm naifananisha na ile ya bunge. Lengo hasa la hiyo kamati sio kulinda maadili bali ni kukomoa, kugandamiza na kuwatia uoga wote wasiokubaliana na mwenyekiti. Na hiyo kamati huwa inaundwa na wale watu wa ndio mzee kwa mwenyekiti, ambao wao maamuzi yao ni kuhakikisha wanamfurahisha mwenyekiti kwa kukomoa wasiomsujudia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom