Kamati ya Mambo ya Nje ya Umoja wa Ulaya (EU) wataka kujua msaada wa Euro Mil. 27 za COVID-19 kwa Tanzania uliahidiwa kwa vigezo gani?

Kamati ya Mambo ya Nje ya Umoja wa Ulaya (EU) wataka kujua msaada wa Euro Mil. 27 za COVID-19 kwa Tanzania uliahidiwa kwa vigezo gani?

Hapo kwa dadayako jiandae na wewe kuolewa
Nyie Lisu kawaambia andamaneni ili hata wazungu watuone basi. Mkaishia kucoment kwenye social media huku mkila ugali maharage kwa shemeji zenu.

Umeona wenzenu wa Bob Wine kule Uganda? Umeona wanajibebisha kwa Amsterdam?
 
Hivi una akili sawa sawa kweli?

Yani EU wanateseka kwa ajili ya TZ?

Mataga akili zenu mnaziweka kwenye makalio ama
Niwe mataga au nisiwe mataga havihusiani na nilichokiandika Mkuu.
Tatizo lako hujui hata **** Utajiri wa ulaya umetoka Afrika na bado Wanaitegemea Sana Afrika katika kuendeleza uchumi wao.

Hivyo Basi naomba tu utambue yakuwa Taifa lolote Afrika lenye kiongozi shupavu na imara anaetanguliza masilahi ya taifa lake na kuwabania ulaji mamboleo hao jamaa wa ulaya lazima waliogope na watafute namna ya kulivunjavunja.

Tanzania kwa Sasa ipo chini ya kiongozi shupavu hivyo wanateseka Sana namna ya kuingia na kutimiza malengo yao ya upigaji na unyonyaji wa rasilimali.
 
Sio tanzania. Wanatetea binadamu. Leo Tanzania ikibaki na mawe hakuna atakayehangaika nayo.
 
Umesoma nilichoandika?Unajua kusoma kwa uelewa?Masharti ya EU ya kutumia fedha zao ni unatakiwa kupima watu na utoe takwimu hata kama ugonjwa haupo.Maana yake serekali walipaswa kupima watu na kutoa takwimu kwamba hakuna maambukizi.Yaani unapima kwa mfano watu elfu moja kisha unasema kuwa wenye Corona ni sifuri.Tanzania ilifanya haya?Halafu umejua vipi kuwa Corona hamna bila ya kufanya vipimo?Unaelewa kuwa njia pekee na official na inayotambuliwa na EU pamoja na WHO ya kujua kama Corona ipo au laa ni kwa kufanya vipimo?
Vipimo vyenyewe vilikuwa feki!

Usiamini kila uhuni wa wazungu!
 
Inabidi kwanza tuache ulafi wa hela zao ndio wataacha kutufuatilia, kwani situliambiwa na kiongozi wako sisi ni dona kantrii..??
Kwani kuna mtu kawarazimisha?
Wakati wanaleta hiyo pesa waliiwekea hayo masharti wanayodai masi.tukaridhia au walikaa kimya na badae kuleta ujinga wao?

Kama mtu anaweza kukupa pesa kwa mkopo au kukusaidia kisha unapotaka kumuingilia mkeo chumbani anakuja kukukoromea huo utakua ujinga mkubwa,
Walizoea kufanya hivyo huko nyuma sasa wanadhani bado tupo katika umasikini zaidi.
Wanapsswa kujiheshimu.
 
"NAPE RAIS MAHUFULI NI MSHAMBA SANA" KINANA.
.
Tumewakabidhi nchi watu washamba sana. ZZK.

"OYA WASKAJI E KICHAA KAPEWA RUNGU".NEY

acha tuisome namba.

RIP KAMBARAGE NYERERE.
MKAPA NDIO KASABABISHA YOTE.
 
Hahahahahahah........bwashe una mizaha mingi sana. The good thing you are composed, hunaga kejeli. Umewaacha kwa mbali wenzio wa Lumumba including Bw. Bashiru Ally pamoja na pH yake.
Hahahaaaa.......siasa siyo uadui bwashee!
 
Acheni longolongo rudisheni pesa za watu....
 
Sijui, ila wanapima na Cheti wanatoa, kuna wageni kibao pamoja na Muzungu, wanapima kila siku, ...
Masharti ya fedha za EU ni kwamba serekali inapaswa kutangaza publicly(kwa umma ) kwa kutumia njia ambazo ni official kama vile radio,magazeti,tv,e.t.c kuwa kwa siku wamepima watu wangapi,wangapi wamekutwa na Corona na ni wangapi hawajakutwa na Corona.Serekali ya Magufuli iliyafanya haya?Na siyo kupima tu wageni,ila ni wananchi wote
 
Hivi una akili sawa sawa kweli?

Yani EU wanateseka kwa ajili ya TZ?

Mataga akili zenu mnaziweka kwenye makalio ama
Ndiyo EU Wanateseka kwa ajili ya Tanzania! Kama unaelewa kingereza vizuri na umesikiliza mjadala wao kuhusu Tanzania, kuna mchangiaji analialia na kusema walituiita tujadiliane nao - tukakataa! Wakatuita tena tuyamalize nao tukakataa! Na tulifukuza wawakilishi wao! Huoni hapo kwamba sisi mpaka sasa tumeshika mpini na wao makali!
 
Yote yalifutwa baada ya matokeo ya vipimo vya maabara.

Tukaonekana hatujawahi kuwa na corona. Hivyo mengine tulifanya kwa maigizo yetu.

Mzee Mgaya anasemaje?
 
Amani iwe nanyi tena wadau!!

Nimetoka kutazama mjadala mzito unaoihusu Tanzania katika Kamati ya Mambo ya Nje Bunge la EU.

Napenda tu kusema yafuatayo

1. Tanzania tuna hali mbaya sana. Wajumbe wa kamati hii wameijadili vibaya sana Tanzania na wengine kupendekeza hatua kali zaidi zichukuliwe juu ya Tanzania ikiwemo kuondoa kabisa misaada yote ya kifedha kwa Tanzania

2. Mwenyekiti wa Kamati ametoa maelekezo umoja wa Ulaya sasa iuangalie Tanzania kwa jicho makini zaidi na kufuatilia kwa makini zaidi juu ya Tanzania na hali ya kutisha ya Haki kukandamizwa kwa Haki za binadamu na utawala Bora kunakoendelea Tanzania

3. Wamehoji hadi kwanini walitoa hela za ku support harakati za Covid na wamembana afisa wao kuwa walitumia vigezo gani kutoa hela hizo wakati Tanzania haifuati maelekezo ya WHO na wametangaza kuwa wako covid free

4. Wamemuamuru afisa wao anayejishughulisha na Tanzania kutoa maelezo ya uhakika juu na kwa nini walitoa hela kwa Tanzania na kwanini hawajafuatilia hizo hela zimetumika kwenye nini?

5. Wamesema sasa waangalie kwa namna gani watatoa msaada wao na hela zao kwa vyama vya siasa vinavyotetea demokrasia na watetezi wa Haki za binadamu waliopo Tanzania na sio kutoa tena hela kwa Serikali.


Sasa kama EU wametoa maelekezo haya sijui ICC watasemaje 😂😂😂😂

Naomba waliopo kwenye list ya ICC wajiandae tu.
Comment yoyote iliyotolewa na EU kuhusu mwenendo wa uchaguzi utatumika kama reference kwenye kesi za ICC. Na hichi ndio kitu kikubwa tulikuwa tunasibiri.
 
Bunge la Ulaya kwa kauli moja limeazimia kuifutia Tanzania misaada na mikopo yote ambayo imeomba kwenye Umoja wa Ulaya (EU) na mashirika yake.

Moja ya misaada mikubwa ambayo Tanzania imefutiwa ni ule wa £626M (sawa na TZS Trilioni 1.6) ambazo tumekuwa tukipewa kila mwaka tangu 2014 kwa ajili ya kuimarisha demokrasia, utawala bora, kujenga miundombinu na kusambaza nishati ya umeme vijijini.

EU imefikia uamuzi huo kutokana na madai ya Ukiukwaji wa demokrasia kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Oktoba mwaka huu. Pia vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu vinavyodaiwa kufanywa na vyombo vya dola na madai ya serikali kushindwa kudhibiti matukio ya ugaidi kusini mwa Tanzania.

Mwenyekiti wa Kamati ya mambo ya nje wa bunge la Ulaya (Chairman of the European Parliament Foreign Affairs Committee), David McAllister amesema pamoja na kuinyima Tanzania msaada huo wa TZS Trilioni 1.6 pia EU inafikiria kuiwekea Tanzania vikwazo vya kiuchumi (Economic sanctions) ikiwa ni pamoja na kuizuia Tanzania kufanya biashara na nchi yoyote ya Ulaya.

McAllister amesema vikwazo hivyo vikiwekwa havitaondolewa mpaka pale serikali ya Tanzania "itakapojicommit" kwa maandishi kuheshimu demokrasia, kuruhusu ushindani wenye usawa wa vyama vya siasa na kulinda haki za binadamu. Mjadala wa kuiwekea Tanzania vikwazo vya kiuchumi bado unaendelea
 
Wazungu wanapaswa kuelewa kuwa Tanzania tulipambana na Corona na tukaishinda hivyo msaada tuliopewa na EU ulikuwa ni halali yetu.

Nani asiyejua hatua mbalimbali zilizochukuliwa na serikali kupambana na Corona ikiwemo social distancing, kuvaa barakoa, kuweka sehemu za jamii kunawa mikono, kufanyia kazi nyumbani, shule na vyuo kufungwa nk nk.

Wazungu watafute sababu nyingine za kutubania misaada lakini hili la Covid 19 wanatuonea bure.

Maendeleo hayana vyama!
Peleka huu utetezi wako Yuropa hahahahahaaaa. Mnaacha watu wanakufa halafu mnatoka mbele mnasema Corona ilikimbia! Pumbavu
 
Wazungu wanapaswa kuelewa kuwa Tanzania tulipambana na Corona na tukaishinda hivyo msaada tuliopewa na EU ulikuwa ni halali yetu.

Nani asiyejua hatua mbalimbali zilizochukuliwa na serikali kupambana na Corona ikiwemo social distancing, kuvaa barakoa, kuweka sehemu za jamii kunawa mikono, kufanyia kazi nyumbani, shule na vyuo kufungwa nk nk.

Wazungu watafute sababu nyingine za kutubania misaada lakini hili la Covid 19 wanatuonea bure.

Maendeleo hayana vyama!
Msaada unauomba na aliyekupa alikuwa anasababu ya kukupa...Kama wao waliutoa bila sababu then is up to them...Wahangaike na hali zao...Hawa wanatapatapa kwakua wanaiona Tanzania ikitoa darasa kwa Africa na hotuba ya mwelekeo wa nchi ya Mh. Rais imewatisha maana soon watakosa jinsi ya kupiga propaganda kwakua aliyeitoa ana record ya kutimiza kila nukta ya neno alilolitamka...Shame to them...Africa is gone friends too little too late the train has vanished into the space...
 
Back
Top Bottom