Kamishna Camillus Wambura ateuliwa kuwa IGP Mpya. Sirro apewa Ubalozi Zimbabwe, Kingai ateuliwa kuwa DCI

Kamishna Camillus Wambura ateuliwa kuwa IGP Mpya. Sirro apewa Ubalozi Zimbabwe, Kingai ateuliwa kuwa DCI

Kuna mwanafalsafa aliwahi sema

"free things are never served with respect, learn to hustle"

Leo hii Sirro anakua balozi same as Polepole tena Zimbabwe huku akina Hoyce Temu wakipewa balozi nchi nzito nzito huko Ulaya.
Sirro kwa ukati;li ule hawezi kupelekwa nchi za Mabeberu wakamkubali. Itakuwa yuko blacklisted ....... ndiyo maana wanapelekwa nchi Rafiki za Tanzania kama Zimbabwe, Namibia .... huko kwingine labda Cuba, China, North Korea au Venezuela.
 
Kuna chizi The Sunk Cost Fallacy hajaja kutia neno.
 
Naona Sirro anakwenda +263 kama Adadi Rajab wakati ule wa JK. Wambura simjui lakini kuhusu Kingai, mama amejishushia credit.
ulitaka apangwe nani?!
jifunze adabu na heshima kwa Rais.
Rais huwa hapangiwi wala hateui mtu ili kukufurahisha wewe na kikundi chako.
 
Siro umri umeenda anaendelea kustaafu kwa neema,

Jililie wewe na ukoo wako
Sina ukoo wa kuulilia,
Baba yangu alikua mkurugenzi NMC enzi hizo na baadae katibu mkuu wizarani... my mom alikua RDD kwahiyo sina shida ya kumlilia mtu.
 
Kumbe kuwa barozi lazima uwe askari au wasiojulikana?
Basi itakuwa hata kale kajamaa kigeugeu(Haraka haraka) kalikopelekwa ubarozi wa Malawi katakuwa ka afwande[emoji1787]
Huenda ikawa hivyo! Hata mataifa yaliyoendelea kama sikosei mabarozi wao ni watu wasiojulikana!
 
Kama yupi anbaye hakustaafishwa kama yeye?
Wewe ni mgeni kwenye kupata taarifa za wakuu wa majeshi yetu? Ok ngoja nikutajie hawa wa karibuni kama retired IGP Mahita, retired IGP Mwema. Nimekusadia au bado kijana?
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amefanya mabadiliko katika Jeshi la Polisi.

Aliyekuwa IGP Simon Sirro ateulikuwa kuwa balozi nchi Zimbambwe.

Wakati huo huo amefanya mabadiliko ya Makamanda wengine kama inavyoonesha hapa chini
[emoji116][emoji116]

View attachment 2297191View attachment 2297189

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 20 Julai, 2022 amefanya uteuzi kama ifuatavyo:-

Amempandisha cheo Kamishna wa Polisi Camillus Mongoso Wambura, aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kuwa Inspekta Jenerali na Mkuu wa Jeshi la Polisi.

Amemteua aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Simon Nyakoro Sirro kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe.

Amempangia kituo Balozi Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zambia.

Amemteua Dkt. Suleiman Haji Suleiman kuwa Balozi. Dkt. Suleiman ni Afisa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Uteuzi huu umeanza tarehe 19 Julai, 2022 na uapisho utafanyika leo tarehe 20 Julai, 2022 saa 05:00 Asubuhi Ikulu, Chamwino Dodoma.

Wakati huo huo, Mhe. Rais amewateua wafuatao kushika nyadhifa mbalimbali kwenye Jeshi la Polisi: -

Amemteua Kamishna wa Polisi (CP) Liberati Sabas Materu kuwa Kamishna wa Fedha na Logistiki. Anachukua nafasi ya (CP) Hamad Khamis Hamad.

Amemteua Kamishna wa Polisi (CP) Hamad Khamis Hamad kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar. Anachukua nafasi ya Kamishna wa Polisi Awadhi Juma Haji.

Amemteua Kamishna wa Polisi (CP) Awadhi Juma Haji kuwa Mkurugenzi wa Operesheni Makao Makuu;

Amempandisha Cheo Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Faustine Constantine Shilogile kuwa Kamishna wa Polisi Jamii. Anachukua nafasi ya CP Mussa Ali Mussa ambaye atapangiwa majukumu mengine.

Amempandisha Cheo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ramadhan Hamisi Kingai na kumteua kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).

PIA, SOMA: Rais Samia, asema kuna mabadiliko makubwa zaidi yanafuata, ameanza na Jeshi la Polisi
Unaletaje Uzi bila picha aise!
 
Kwani mbaya wenu si alishakufa?
Wazalendo wa kweli wa nchi hii, mbaya wetu ni ccm! Sasa uniambie hapa hiyo ccm imekufa lini ili nichinje jogoo na kulila na wanangu?

Maana ukombozi wa kweli hatimaye utakuwa umepatikana.
 
Sina ukoo wa kuulilia,
Baba yangu alikua mkurugenzi NMC enzi hizo na baadae katibu mkuu wizarani... my mom alikua RDD kwahiyo sina shida ya kumlilia mtu.
Ungekua huna shida usingekua unalialia humu
 
Wambura anastahili na nafasi hiyo ya uIGP imetendewa haki. Aliye mchangua Wambura na waliomfanyia vetting ndio huyo huyo na hao hao ndio waliofanya kwa Kingai. Pongezi kwa Mh Rais SSH kila siku ziendavyo kazi ya nchi unaimudu kutoka kiwango kimoja kwenda kingine cha juu.
 
Aliwasulubu CDM wasio na silaha, kisha kawashinda wenye silaha kwenye mpaka na Msumbiji, hiyo ni akili au matope?
Wote aliwasurubu! Kule msumbiji aliwakomesha na machadema nao akawakomesha!

Unaonaje lakini huu uteuzi wa kingai? Haya ni matokeo ya maridhiano kati ya mbowe na hangya
 
Wazalendo wa kweli wa nchi hii, mbaya wetu ni ccm! Sasa uniambie hapa hiyo ccm imekufa lini ili nichinje jogoo na kulila na wanangu?

Maana ukombozi wa kweli hatimaye utakuwa umepatikana.
Kwani wewe siyo bavicha?

Maana kwa mujibu wa bavicha mbaya wao alishakufa na sasa wanapumua
 
Polepole malawi huyu Siro zimbabwe yaani kama ni mimi nakataa uteuzi kutoka IGP wa nchi mpaka unaenda kufanya kazi Zimbabwe, Anyway nampongeza mama ameupiga mwingi sana,
 
Back
Top Bottom