Kampeni chafu zaanza UVCCM

Kampeni chafu zaanza UVCCM

Mkuu nimeamini ikiwa na mihela uwe karibu na viongozi na kutoa toa viposho hata kama 5000 kwa kila mjumbe basi utalindwa balaa.Hata ukitaka kugombea ujumbe wa NEC hutumii nguvu nyingi kama wengine.

Sumaye wakati fulani aliwahi kuwaambia wananchi sehemu fulani kuwa "ukitaka kufanikiwa kwa lolote fanya biashara na CCM", Hata kuuza mirungi, gongo etc!
 
Huyo ametoa pesa kwa niaba ya akina Jeetu Patel ili mambo yao yasiende vibaya mahakamani. Rushwa hiyo jamani. Jamani hicho ni Chama Cha Matajiri (CCM) , msishangae.
 
Kwa wasiomjua TANIL ndio huyu, katika KULIKONI na THISDAY, tutafakari hatima ya CCM kuelekea 2010.

Mshirika wa mtuhumiwa ufisadi
amwaga mamilioni kwa CCM

MWANDISHI WETU
Dodoma

TANIL Somaiya, mshirika wa kibiashara wa mtuhumiwa wa rushwa ya rada aliyekimbilia nje ya nchi, Shailesh Vithlani, amechanga zaidi ya milioni 400/- kugharimia uchaguzi ujao wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM).

Somaiya alikabidhi vifaa kadhaa vyenye thamani ya mamilioni ya shilingi ili vitumike kwenye uchaguzi huo wa kuwapata viongozi wa kitaifa wa umoja huo.

Vifaa hivyo vya uchaguzi vyenye thamani ya milioni 400/- vilikabidhiwa kwa CCM mjini Dodoma jana wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho tawala cha CCM (NEC).

Taarifa za uhakika kutoka Dodoma zinaeleza kuwa mfanyabiashara huyo, Somaiya, alikabidhi msaada huo makao makuu ya CCM yaliyopo mji unaotarajiwa kuwa makao makuu ya nchi, Dodoma.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekuwa ikichunguza bohari moja la kutunza bidhaa zisizolipiwa ushuru/kodi linalomilikiwa na kampuni moja iliyo chini ya kundi la kampuni za Shivacom za Dar es Salaam kwa tuhuma za kukwepa kodi. Kampuni hiyo ni mali ya Somaiya.

Somaiya pia anamiliki kampuni ya Incar (Tanzania)Limited, ambayo ndiyo inatajwa kumiliki bohari kati ya mabohari 22 ya kutunzia bidhaa zisizolipiwa ushuru/kodi yaliyofungwa na TRA hivi karibuni.

Incar (T) Limited, kampuni ambayo ni ajenti wa magari yanayotengenezwa Italia ya IVECO, pia iliwahi kufuma zabuni ya mabilioni ya shilingi ya kuliuzia magari ya kijeshi Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Wote wawili, Somaiya na Vithlani, wamewahi kuhojiwa chini ya kiapo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu jijini Dar es Salaam, kuhusu tuhuma za kuhusika kwao katika kashfa ya rushwa ya rada.

Wafanyabiashara hao walikiri kwamba walikuwa na hati ya kiapo ya kuwaruhusu kufanya mambo kwa niaba ya kampuni ya Envers Trading Corporation, inayodaiwa kupokea mabilioni kama rushwa ya rada.

Kulingana na uchunguzi, Envers Trading Corporation, ililipwa na kampuni nyingine ya Red Diamond Trading, dola za Marekani milioni 12 (karibu bilioni 15/-).

Red Diamond Trading ilianzishwa katika visiwa vya Uingereza vya Virgin mwaka 1998 na kampuni nyingine inayohusishwa na kampuni ya Uingereza ya kutengeneza silaha ya BAE Systems, ambayo ndiyo iliyoiuzia Tanzania rada kwa bei ya kuruka enzi za utawala wa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa mwaka 2002.

Alipobanwa na makachero wa Kiingereza, Somaiya alikiri kuwa alipewa haki ya kisheria kupitia hati ya kiapo iliyomruhusu kuiwakilisha kampuni ya Envers Trading Corporation kwa kipindi cha miezi 11.

Lakini, alisisitiza kwamba hakuwa na mambo mengine aliyoshiriki katika kampuni hiyo na kwamba hakujua kabisa uhalisi wa kampuni hiyo wala mahali zilipo ofisi zake.

Nyaraka rasmi kutoka Mahakama ya Kisutu zinaonyesha kachero wa Uingereza, Sajini Steve Rosenthal akiwabana kwa maswali Vithlani na Somaiya mwaka 2006 na kukiri kuhusika kwao.

Wakati wa mahojiano hayo, Somaiya alikiri kwamba yeye pamoja na mwenzake Vithlani aliyemweleza kuwa “rafiki yangu mkubwa” walikuwa wamiliki wa kampuni ya Jijini Dar es Salaam, Merlin International company.

“Shailesh Vithlani ni rafiki yangu mkubwa sana. Yeye pia ni mkurugenzi wa Merlin International. Sijui kama yeye ni mmiliki pia wa Envers Trading … nilihamishia kwake haki ya kisheria ya kuiwakilisha Envers Trading. Sijui kama yeye ndiye mmiliki wa kampuni hiyo,” nyaraka za mahakama zinaonyesha ndivyo alivyosema Somaiya.

Kwa upande wake, Vithlani aliiambia mahakama chini ya kiapo kwamba alikuwa akiendesha kampuni ya Merlin International kama kampuni ya ushauri kwa kushirikiana na “wamiliki wengine … mmojawapo akiwa Tanil Somaiya.”

Vithlani ameshafunguliwa mashitaka katika Mahakama ya Kisutu kwa kusema uongo chini ya kiapo na kuwadanganya maofisa wa upelelezi huku wapelelezi wakidai kuwa aliwadanganya kuwa yeye hakuwa mmiliki wa Envers Trading na kuhusu kupokea dola 390,000 kama rushwa ya rada. Inadaiwa kuwa kwa ujumla alilipwa dola milioni 12 kama rushwa.

Mfanyabiashara huyo aliyetorokea nje ya nchi, alifunguliwa mashtaka bila yeye kuwapo mahakamani na bado anatafutwa pamoja na kutolewa hati ya kimataifa ya kukamatwa kwake popote atakapopatikana duniani.

Uchunguzi umeonyesha kwamba, Somaiya aliifahamisha Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru) kupitia kwa mawakili wake kwamba alikoma kuwa mmiliki na mkurugenzi wa Merlin International Januari 8, 2007.

Hata hivyo, pamoja na kutolewa taarifa ya kukomeshwa uhusiano na Vithlani, Somaiya alikuwa mfanyabiashara mshirika wa Vithlani wakati wa kutendeka kosa la rushwa ya rada.

Haieleweki kama uongozi wa nchi bado unamchukulia Somaiya kama mtuhumiwa katika uchunguzi unaoendelea kuhusu rushwa ya rada.

Source: KULIKONI Na.484, Jumatatu Novemba 10, 2008
Ex-partner of radar fugitive donates 400m/- to CCM



TANIL Somaiya, a former business partner of radar fugitive Shailesh Vithlani, has donated more than 400m/- towards the upcoming national election of the Chama Cha Mapinduzi’s youth wing (CCM-VIJANA).

Somaiya presented various election materials to be used in the VIJANA national leadership polls worth hundreds of millions of shillings.

The election materials, worth an estimated 400m/-, were handed over to CCM in Dodoma yesterday, where the ruling party held its national executive committee (NEC) meeting.

According to reports from Dodoma, the businessman presented his donation at the CCM headquarters in the designated capital.

The Tanzania Revenue Authority (TRA) has been investigating a customs bonded warehouse owned by one of the companies under the Shivacom Group in Dar es Salaam on allegations of tax fraud.

The company linked to Somaiya, Incar (Tanzania) Limited, was among a total of 22 bonded warehouses recently shut down indefinitely by TRA.

Incar (T) Ltd, the local agent of the Italian-made IVECO vehicles, had previously won a hugely controversial tender to supply hundreds of military trucks and buses to the Tanzania People’s Defence Forces (TPDF).

Somaiya and Vithlani have both been questioned under oath at the Kisutu Resident Magistrate’s Court in Dar es Salaam over their alleged connections with the radar corruption scandal.

Both businessmen admitted that they had power of attorney - a legal instrument used to delegate legal authority to them - to act on behalf of Envers Trading Corporation, a company alleged to have received illegal kickbacks for the radar transaction.

According to investigators, Envers Trading Corp. was paid $12m (approx. 15bn/-) by Red Diamond Trading, another shadowy company set up in the British Virgin Islands in 1998 by a firm linked to Britain’s BAE Systems, manufacturers of the overpriced air traffic control system sold to former President Benjamin Mkapa’s government in 2002.

When subjected to questioning by British detectives, Somaiya admitted that he was given power of attorney over Envers Trading Corp. for a period of 11 months.

But he insisted that he had no other involvement with the company, and was not even aware of the company’s official location.

Official documents from the Kisutu resident magistrate’s court in Dar es Salaam show that the courtroom grilling of both Vithlani and Somaiya was conducted in 2006 by assistant detective sergeant Steve Rosenthal of Britain’s Ministry of Defence Police and another investigator from the UK’s Serious Fraud Office (SFO), Carl Brown.

The two were interrogated under oath before Kisutu Resident Magistrate Katarina Revocati on two separate occasions - July 25 and July 28, 2006.

At the time of the interrogation, Somaiya admitted he was a co-owner of the city-based Merlin International company with Vithlani, whom he described as his ’’very good friend.’’

’’Shailesh Vithlani is a very good friend of mine. He is also a director of Merlin International. I don’t know if he is the owner of Envers Trading ... I transferred to him the power of attorney. I don’t know whether he is the owner,’’ the court documents quote Somaiya as saying during questioning.

On his part, Vithlani told the court in his sworn testimony that he was running Merlin International as a consultancy firm with ’’other owners ... one (of them) is Tanil Somaiya.’’

Vithlani has since been charged at the Kisutu court with committing perjury and making false statements to an investigating officer, with prosecutors alleging that he lied about not being the owner of Envers Trading and about receiving a $390,000 commission for the radar deal while he was actually paid $12m.

The fugitive businessman was charged in absentia and remains at large, despite an international arrest warrant issued for him.

According to THISDAY investigations, Somaiya informed the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) through his lawyers that he ceased being a shareholder and director of Merlin International on January 8, 2007.

However, despite reportedly severing all his business ties with Vithlani, Somaiya was business a partner with the wanted fugitive at the time the radar deal was concluded. It remains uncertain whether or not authorities consider him a formal suspect in the ongoing radar investigation.

SOURCE: Thisday No. 814, Monday 10, November, 2008

ThisDay

Picha inayoonekana imepigwa na Mpiga Picha wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Amour Nassor.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya SHIVACOM GROUP iliyodhamini utengenezajia wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu wa umoja wa vijana wa CCM ndugu TANIL SOMAIYA, akimkabidhi baazi ya vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni 400 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete Makamo Makuu ya CCM Dodoma.
 

Attachments

  • Tanil.jpg
    Tanil.jpg
    169 KB · Views: 188
400m. Halafu huyu mtathubutu kumwambia kitu? Mtu akikufadhili kwa kiwango hiki unakuwa huna ubavu wa kusema chochote, hata akisema chochote lazima ukenue meno hata kama inakuuma vipi! haya na tuone. Kina Fisadi Shah wengine hao!

Kwani Jeetu alichanga kiasi gani wakati wa kampeni za CCM/JK 2005? Sasa hivi yuko wapi? JK ni zaidi ya tunavyomfahamu!
 
Kinachofurahisha ni Mzee Pius kuchekelea na Nchimbi kukaba Penati,hachezi mbali na za hivi
 
Nimeipenda hiyo Picha,

Pale kuna moja viongozi wakubwa wote wa chama na serikali hii mpya na ya zamani

1.Rostam
2.kigoda
3.mama meghji
4.Msekwa
5.Waziri kiongozi
..............................

Jamiiforums lini tuakwachangie CHADEMA au CCM?
 
Sasa tukisema kwamba CCM maanake ni chama cha mafisadi si tunakuwa tumesema kweli tupu?, Tena fisadi anajigamba kwa nguvu zote kwamba ni ukereketwa ndo....

Yaani mtakumbatiaje pesa za mafisadi kama nyie si mafisadi? Tena mna washadadia eti wanajitangaza?

ILA YANA MWISHO HAYA, TENA MWISHO WAKE U KARIBU SANA!
 
Kwa wasiomjua TANIL ndio huyu, katika KULIKONI na THISDAY, tutafakari hatima ya CCM kuelekea 2010.



Source: KULIKONI Na.484, Jumatatu Novemba 10, 2008

SOURCE: Thisday No. 814, Monday 10, November, 2008

ThisDay

Picha inayoonekana imepigwa na Mpiga Picha wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Amour Nassor.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya SHIVACOM GROUP iliyodhamini utengenezajia wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu wa umoja wa vijana wa CCM ndugu TANIL SOMAIYA, akimkabidhi baazi ya vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni 400 Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete Makamo Makuu ya CCM Dodoma.




Naona vigogo wote wamejazana na mkuu mwenyewe anapokea furushi!Halafu akijulikana amechota mahali mkuu ataunda tume ya mwaka mzima kumchunguza!!!!!
 
Huyu anatafuta nini kufutiwa kodi?
Tulisha ambiwa hawalipi kodi hawa jamaa ndo kulipa fadhira nini?
Ameacha kuchangia maendeleo huko vijijini kwa kutoa madawati yeye anafadhili ufisadi.
Anajitengenezea jina..

Hili jina ni kama la yule Mfanyabiashara wa Goldberg scandal kule Kenya ambaye amefungwa au ni yeye?

Achangie maendeleo ili iweje? Salama yake ni CCM kuendelea kutawala vinginevyo ni ???
 
Kweli hawa wahindi wamewashika pabaya viongozi wetu wa chama.
Ukitaka usibughudhiwe katika biashara yako njia pekee ni kujikomba komba kwa akina Makamba kama hivi utaona hata siku moja TRA hawaji kukubughi unakuwa mtu wao.
Hata wale wenye malori au mabus ya wafadhili wa CCM hayapigwi pigwi mkono barabarani Trafic akisimamisha labda kama haitaki kazi yake.
 
Hili jina ni kama la yule Mfanyabiashara wa Goldberg scandal kule Kenya ambaye amefungwa au ni yeye?

Achangie maendeleo ili iweje? Salama yake ni CCM kuendelea kutawala vinginevyo ni ???

Mkuu hii inathibitisha ule usemi usemao.
"Nimewaweka mfukoni au kiganjani viongozi wote wa nchi hii"
Utasikia nenda kashitaki popote pale......ukienda kushitaki utatendewa haki kweli? kama mnavyo ona jamaa wamepokea fuko la mihela hiyo huku wakicheka teh! teh! teh!..
Hivi mababu zetu wa enzi hizo walio kuwa wakiuza ardhi kwa kioo au chuba ya mvinyo na hawa viongozi wetu wanatofauti gani??????
 
Lakini Tajiri Soros mbona amewahi kutumia dola millioni 20 kusaidia Democrats huko USA, hasa kwenye uchaguzi dhidi ya Bush kwenye term ya pili?

Hapa sidhani kama tatizo ni kutolewa kwa hela, au kwa CCM kupokea hizo hela, labda tatizo ni mtoaji anataka nini au amewahi kutaka nini au amewahi kupewa nini na watawala wetu, kama yanafahamika yawekwe wazi hapa otherwise tusiwakatishe tamaa wananchi wenye nia ya kutoa misaada kusaidia vyama vyetu vya siasa.

Kutoa misaada kwa vyama vyetu vya siasa sio kuvunja sheria ya jamhuri yetu, au?
 
Lakini Tajiri Soros mbona amewahi kutumia dola millioni 20 kusaidia Democrats huko USA, hasa kwenye uchaguzi dhidi ya Bush kwenye term ya pili?

Hapa sidhani kama tatizo ni kutolewa kwa hela, au kwa CCM kupokea hizo hela, labda tatizo ni mtoaji anataka nini au amewahi kutaka nini au amewahi kupewa nini na watawala wetu, kama yanafahamika yawekwe wazi hapa otherwise tusiwakatishe tamaa wananchi wenye nia ya kutoa misaada kusaidia vyama vyetu vya siasa.

Kutoa misaada kwa vyama vyetu vya siasa sio kuvunja sheria ya jamhuri yetu, au?

Ni kweli si kuvunja sheria, lakini kuna sheria yoyote inayo-guide michango/zawadi za wafanyabiashara, raia wengine wa Tanzania au wasio raia kwa vyama? CCM wanajua 'status quo' iliyopo inawa-favour wao kupokea michango na fedha kutoka kwa wafanyabiashra, raia na wasio raia ili waendelee kuwa madarakani. Kikwete alizungumzia muda mrefu kupeleka muswaada bungeni ili itungwe sheria ya kufuatilia hii michango na zawadi kwa vyama vya siasa lakini mpaka sasa ni kimya. Kwa maoni yangu suala hili ni mojawapo linalofanya uwanja wa siasa Tanzania usiwe 'fair ground to all players'
 
Ni kweli si kuvunja sheria, lakini kuna sheria yoyote inayo-guide michango/zawadi za wafanyabiashara, raia wengine wa Tanzania au wasio raia kwa vyama? CCM wanajua 'status quo' iliyopo inawa-favour wao kupokea michango na fedha kutoka kwa wafanyabiashra, raia na wasio raia ili waendelee kuwa madarakani. Kikwete alizungumzia muda mrefu kupeleka muswaada bungeni ili itungwe sheria ya kufuatilia hii michango na zawadi kwa vyama vya siasa lakini mpaka sasa ni kimya. Kwa maoni yangu suala hili ni mojawapo linalofanya uwanja wa siasa Tanzania usiwe 'fair ground to all players'

Tanzania hatuna sheria inayo-guide misaada ya wananchi kwa vyama vyetu vya siasa, sasa sina uhakika kama ni vyema kuanza kushambulia CCM au chama chochote cha siasa nchini kikipokea msaada, maana ninajua kuna wakati Mrema, alipokea msaada flani wa kusaidia umeme kutoka nje mpaka leo sielewi aliishia wapi, na vyama vyetu vingi vya siasa vimekua vikipata misaada toka nje na ndani, ingawa sio wakati wote hizo habari husemwa to the public kama CCM,

Sasa ninafahamu kuwa ni kawaida ya siasa kwamba the incumbent hupata misaada mingi zaidi kuliko the challenger, unless you are Obama, sasa in the absence of sheria ya kuzuia wananchi kusaidia vyama vyetu vya siasa, tunalaumu huu msaada kwa mantiki ipi hasa?
 
This is an embarrasment kwa kweli.CCM inaongozwa na genge la wahuni maana huu ni uhuni wa kupindukia.Yaani mtu anachangia CCM 400M leo tukisikia kafanya ufisadi kweli atakamatwa huyu?
 
Tanzania hatuna sheria inayo-guide misaada ya wananchi kwa vyama vyetu vya siasa, sasa sina uhakika kama ni vyema kuanza kushambulia CCM au chama chochote cha siasa nchini kikipokea msaada, maana ninajua kuna wakati Mrema, alipokea msaada flani wa kusaidia umeme kutoka nje mpaka leo sielewi aliishia wapi, na vyama vyetu vingi vya siasa vimekua vikipata misaada toka nje na ndani, ingawa sio wakati wote hizo habari husemwa to the public kama CCM,

Sasa ninafahamu kuwa ni kawaida ya siasa kwamba the incumbent hupata misaada mingi zaidi kuliko the challenger, unless you are Obama, sasa in the absence of sheria ya kuzuia wananchi kusaidia vyama vyetu vya siasa, tunalaumu huu msaada kwa mantiki ipi hasa?

Mantiki ya mchango wangu si kulaumu msaada, bali kuelezea unfairness ya uwanja wa kisiasa ulivyo na kwa CCM wakijua hilo hawajataka kuweka fair ground. Pili tunajua kutokana na maelezo ya viongozi waliopita CCM/serikalini kuwa ili mfanyabiashara mambo yako yakuendee vizuri inabidi uwapigie magoti hawa waheshimiwa wa CCM ....kama tunayoona kwenye hili na hiyo statement haijawahi kukanushwa na yoyote ndani ya CCM. Mind you also CCM ndio wanaouchukua ruzuku kubwa kuliko vyama vyote, wana wanachama wengi kuliko vyama vyote, wana vitega uchumu lukuki nchi nzima na bado kuandaa mikutano yao inabidi kuwaabudia wafanyabiashara. This says alot of the party itself na watu wanaokiongoza na kwa nini Tanzania ipo hapa ilipo.
 
This is an embarrasment kwa kweli.CCM inaongozwa na genge la wahuni maana huu ni uhuni wa kupindukia.Yaani mtu anachangia CCM 400M leo tukisikia kafanya ufisadi kweli atakamatwa huyu?

Kumbe so far hatujasikia? Mimi nilifikiri tumesikia tayari, au?
 
Mantiki ya mchango wangu si kulaumu msaada, bali kuelezea unfairness ya uwanja wa kisiasa ulivyo na kwa CCM wakijua hilo hawajataka kuweka fair ground. Pili tunajua kutokana na maelezo ya viongozi waliopita CCM/serikalini kuwa ili mfanyabiashara mambo yako yakuendee vizuri inabidi uwapigie magoti hawa waheshimiwa wa CCM ....kama tunayoona kwenye hili na hiyo statement haijawahi kukanushwa na yoyote ndani ya CCM.

Mkuu unless kuna zaidi ya haya ya kuhisi na kusikia, hata siku moja hakujawahi kuwa na fairness kwenye siasa za dunia between the incumbent na the challenger, nafikiri hiyo ni kwa siasa za dunia nzima inapokuja kwenye uchaguzi,

Sasa unasema kwamba biashara za Mwenyekiti wa sasa wa
Chadema zinanyooka wka sababu anawapigia magoti viongozi wa CCM, au? Mbunge wa Chadema Ndesamburo, naye anawapigia magoti CCM au?

I mean kwa maneno ya kusikia na kuhisi, yes kuna hoja ya kulaumu huu msaada, lakini kwa mjadala wa kisomi na kutraka kuisaidia jamii yetu ninashindwa kuona hoja ya msingi against hii misaada kwa vyma vyetu vya siasa.
 
Back
Top Bottom