Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
Leo kampeni zinaendelea na mwenyekiti na mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi, John Magufuli yupo Nzega mkoani Tabora akinadi sera na ahadi ya nini atafanya katika kipindi chake cha pili endapo atachaguliwa.
Kuwa nami kukujuza kitachojiri kutoka wilayani Nzega.
=======
7:50 Mchana: Wananchi wameshajaa na zinatoka salamu za utangulizi kutoka wilaya na mkoa.
Kigwangala: Umenipa heshma kuwa waziri wa kwanza kutoka wilaya ya Nzega tangu nchi ya uhuru tena ninaetokea katika familia dhalili kabisa ya Kinyonge. Watu wengi hukuzungumzia kama kiongozi mchapakazi, mambo magumu magumu umeyafanya, hawakuzungumzii soft part, umegusa maisha yangu. Umekuwa kiongozi mwenye huruma, mwenye kujali maisha ya watu wa chini.
Kwa kuwa tumeliamsha tutazunguka kukutafutia kuhakikisha unashinda kwa zaidi ya asilimia 95.
Bashe: Mheshimiwa Rais, sisi wananchi wa Nzega tulishafanya maamuzi na jana nilivyosikia kwamba unapita, tumepata taarifa jana saa saba tukasema lazima uwasalimie wananchi wote wa Nzega na hali leo ni wewe kupita kwa salamu tu, hakukua na maandalizi ya mkutano na nyomi ndio umeiona.
Sisi wananchi wa Nzega tumejipanga kuhakikisha tunakuchagua kwa zaidi ya asilimia 90 kwa sababu kuna mambo umetufanyia kwa kipindi cha miaka 5.
Polepole: Miaka miwili iliyopita alikwenda kwa ndugu zenu mkoa wa Manyara ambapo wanachimba madini ya Tanzanite ambako hayapatikani pengine kokote duniani. Kwa takwimu za mwaka 2015, Tanzanite iliyokuwa ikizalishwa ni kiloram 300 kwa mwaka mmoja yaani gunia tatu za mahindi zilizojaa.
Akamuelekeza mkuu wa JKT, piga ukuta kuzunguka mgodi wote zaidi ya kilomita 24. Mimi nilikuwa mmojawapo ya watu walioshangaa sana kwa sababu duniani hatujawahi kuzungusha ukuta mgodi.
Watani wa jadi wakatubeza sana, wakasema wapi wamezungusha ukuta mgodi, tukafikiria mimi huwa naamini kwamba imani ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayo ni bayana ya mambo usiyoyaona. Kwenye chama chetu tunamuamini ndugu John Magufuli.
Baada ya muda mchache ukuta ukakamilika, nilienda 2019 nikauliza Tanzanite kiasi gani imezalishwa na mwaka huu nimepita. Takwimu za mwezi wa sita mwaka huu tanzanite iliyochimbwa ni zaidi ya kilogram 4,000 kutoka kilogram 300 kwa mwaka mzima.
Magufuli: Tumenunua ndege 11 kwa mpigo mpya, sisi ni masikini? Wapo watakaosema ndege za nini? Nyinyi mnapanda ndege? Wale wamepungukiwa kwelikweli. Kwa sababu ukishakuwa na ndege ndio itakayoleta madawa, watalii wakija hapa wataletwa na ndege ndio maana makusanyo ya fedha zilizopatikana kwenye utalii zimetoka bilioni na ushee mpaka 2.6 ni kwa sababu watalii wanaletwa na ndege. Ndege ni matunda ya kunesha nyinyi ni matajiri.
Hatukununua ndege tu, tumeanza kujenga reli ya umeme, vinavyopatikana ulaya tunavileta Tanzania, tumejenga mpaka Morogoro tunaendelea mpaka Dodoma Makutupora.
Tumeshatangaza juzi kuanza kujenga kutoka Mwanza mpaka Isaka, fedha zipo na tukimaliza, tunaanza Isaka mpaka Makutupora kwa fedha zetu.
Matusi ninayotukanwa mimi ninayafurahia kwa sababu hili ni jibu zuri kwa sadaka ya watanzania na ndio maana nimekuwa niwaomba muendelee kuniombea kwa sababu wale tuliowanyima nafasi ya kuiibia hii Tanzania hawatafurahia.
Mimi matusi niyapate lakini nyinyi mpate maendeleo ya kweli. Mimi nipo kwa niaba ya watanzania wote ndio maana ninawaomba kwa upendo mkubwa sana mturudishe tena katika miaka mitano myaone maajabu yale tutakayoyafanya.
Nitashangaa kama yote haya mazuri tuliyoyafanya katika awamu ya tano, shukrani yake iwe kunyimwa kura.
Kuwa nami kukujuza kitachojiri kutoka wilayani Nzega.
=======
7:50 Mchana: Wananchi wameshajaa na zinatoka salamu za utangulizi kutoka wilaya na mkoa.
Kigwangala: Umenipa heshma kuwa waziri wa kwanza kutoka wilaya ya Nzega tangu nchi ya uhuru tena ninaetokea katika familia dhalili kabisa ya Kinyonge. Watu wengi hukuzungumzia kama kiongozi mchapakazi, mambo magumu magumu umeyafanya, hawakuzungumzii soft part, umegusa maisha yangu. Umekuwa kiongozi mwenye huruma, mwenye kujali maisha ya watu wa chini.
Kwa kuwa tumeliamsha tutazunguka kukutafutia kuhakikisha unashinda kwa zaidi ya asilimia 95.
Bashe: Mheshimiwa Rais, sisi wananchi wa Nzega tulishafanya maamuzi na jana nilivyosikia kwamba unapita, tumepata taarifa jana saa saba tukasema lazima uwasalimie wananchi wote wa Nzega na hali leo ni wewe kupita kwa salamu tu, hakukua na maandalizi ya mkutano na nyomi ndio umeiona.
Sisi wananchi wa Nzega tumejipanga kuhakikisha tunakuchagua kwa zaidi ya asilimia 90 kwa sababu kuna mambo umetufanyia kwa kipindi cha miaka 5.
Polepole: Miaka miwili iliyopita alikwenda kwa ndugu zenu mkoa wa Manyara ambapo wanachimba madini ya Tanzanite ambako hayapatikani pengine kokote duniani. Kwa takwimu za mwaka 2015, Tanzanite iliyokuwa ikizalishwa ni kiloram 300 kwa mwaka mmoja yaani gunia tatu za mahindi zilizojaa.
Akamuelekeza mkuu wa JKT, piga ukuta kuzunguka mgodi wote zaidi ya kilomita 24. Mimi nilikuwa mmojawapo ya watu walioshangaa sana kwa sababu duniani hatujawahi kuzungusha ukuta mgodi.
Watani wa jadi wakatubeza sana, wakasema wapi wamezungusha ukuta mgodi, tukafikiria mimi huwa naamini kwamba imani ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayo ni bayana ya mambo usiyoyaona. Kwenye chama chetu tunamuamini ndugu John Magufuli.
Baada ya muda mchache ukuta ukakamilika, nilienda 2019 nikauliza Tanzanite kiasi gani imezalishwa na mwaka huu nimepita. Takwimu za mwezi wa sita mwaka huu tanzanite iliyochimbwa ni zaidi ya kilogram 4,000 kutoka kilogram 300 kwa mwaka mzima.
Magufuli: Tumenunua ndege 11 kwa mpigo mpya, sisi ni masikini? Wapo watakaosema ndege za nini? Nyinyi mnapanda ndege? Wale wamepungukiwa kwelikweli. Kwa sababu ukishakuwa na ndege ndio itakayoleta madawa, watalii wakija hapa wataletwa na ndege ndio maana makusanyo ya fedha zilizopatikana kwenye utalii zimetoka bilioni na ushee mpaka 2.6 ni kwa sababu watalii wanaletwa na ndege. Ndege ni matunda ya kunesha nyinyi ni matajiri.
Hatukununua ndege tu, tumeanza kujenga reli ya umeme, vinavyopatikana ulaya tunavileta Tanzania, tumejenga mpaka Morogoro tunaendelea mpaka Dodoma Makutupora.
Tumeshatangaza juzi kuanza kujenga kutoka Mwanza mpaka Isaka, fedha zipo na tukimaliza, tunaanza Isaka mpaka Makutupora kwa fedha zetu.
Matusi ninayotukanwa mimi ninayafurahia kwa sababu hili ni jibu zuri kwa sadaka ya watanzania na ndio maana nimekuwa niwaomba muendelee kuniombea kwa sababu wale tuliowanyima nafasi ya kuiibia hii Tanzania hawatafurahia.
Mimi matusi niyapate lakini nyinyi mpate maendeleo ya kweli. Mimi nipo kwa niaba ya watanzania wote ndio maana ninawaomba kwa upendo mkubwa sana mturudishe tena katika miaka mitano myaone maajabu yale tutakayoyafanya.
Nitashangaa kama yote haya mazuri tuliyoyafanya katika awamu ya tano, shukrani yake iwe kunyimwa kura.