Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 2,428
- 3,937
Moja ya matukio makubwa yaliyowahi kutokea Tanzania ambayo vizazi vijavyo vitarudi na kuvitafakari itakuwa ni kampeni za uchaguzi wa Urais wa 2020 wa mgombea kupitia CHADEMA, Tundu Lissu.
Ni kampeni iliyokuwa umegubikwa na sintofahamu nyingi, ni uchaguzi ambao ulikuwa na mchanganyiko wa matumaini na kukata tamaa. Ni kampeni ambayo wachache sana walikuwa na ujasiri mkubwa kulinda uhuru mdogo wa kujieleza uliokuwa umebaki miongoni mwa Watanzania wengi huku wengi wakiamua, labda bila kupenda, kukaa kimya au wengine hata 'kuunga mkono juhudi' waziwazi au kwa kificho.
Huku 'theme song' ya kampeni hiyo ukiwa ni wimbo sahihi kabisa katika nyakati zile wa 'One Love' ya Bob Marley, Watanzania walikuwa katika ile wanaita 'at the crossroads'.
Nikimnukuhu mwandishi Charles Dickens, "....ulikuwa ni msimu wa mwanga, ulikuwa ni msimu wa giza nene....". Kampeni zile zilikuwa ni moja ya dozi za mwisho mwisho katika jitihada za kuokoa uhai wa Mama Tanzania.
Ni kampeni iliyokuwa umegubikwa na sintofahamu nyingi, ni uchaguzi ambao ulikuwa na mchanganyiko wa matumaini na kukata tamaa. Ni kampeni ambayo wachache sana walikuwa na ujasiri mkubwa kulinda uhuru mdogo wa kujieleza uliokuwa umebaki miongoni mwa Watanzania wengi huku wengi wakiamua, labda bila kupenda, kukaa kimya au wengine hata 'kuunga mkono juhudi' waziwazi au kwa kificho.
Huku 'theme song' ya kampeni hiyo ukiwa ni wimbo sahihi kabisa katika nyakati zile wa 'One Love' ya Bob Marley, Watanzania walikuwa katika ile wanaita 'at the crossroads'.
Nikimnukuhu mwandishi Charles Dickens, "....ulikuwa ni msimu wa mwanga, ulikuwa ni msimu wa giza nene....". Kampeni zile zilikuwa ni moja ya dozi za mwisho mwisho katika jitihada za kuokoa uhai wa Mama Tanzania.