Tetesi: Kampuni ya Azam kuanza usafirishaji wa Abiria kwa njia ya Mabasi hivi karibuni

Inasemekana na treni ya mwendokasi yetu ameuziwa na mama yetu muuzaji wa Mali za Tanganyika.Hii awamu azam ananeemeka sana
Hajauziwa bali kaambiwa kama anaweza kununua treni zake naye aingize njiani. Si yeye tu hata wewe ukiweza.
 
Za Azam tv hizo boss kwa ajili ya matangazo , anaongeza
 
Mwambie aliyekwambia aache uongo. Nenda page ya azam tv huko Facebook na baadhi social networks utaona. Hizo ni kwaajili ya broadcasting ndugu. Gari nzima hiyo ina seat kama 6 hivi.
 
Sisi wenye vimekumweku barabarani tutakoma jamani
 
Uwe na hakika na unachosema hayo ni magar ya kubeba wafanya kazi huoni yamechakaa Kawaida kabsa???
 

Hayo ni magari ya kurushia matangazo OB Van (Outside Broadcasting)

Hayo magari ya kurusha matangazo ya Azam
Huenda mengine yataenda nchi jirani
ambapo kuna uuzwaj na urushaj wa matangazo mfano Kenya, Rwanda n.k

Anayo baadhi mpaka sasa hivyo kaongeza kutokana na uongezekaji wa matangazo ndani ya nchi na nje ya nchi mfano Kenya na Uganda, pia michuano ya CHAN imechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza hizo OB van kwa ajili ya kurushia matangazo kumbuka ni nchi 3 zinaunganika.

Angalia structure ya hizo bus
Gari zina generator nyuma lina studio ndani halafu zimeandikwa Azam tv zitabebaje abiria si angeandika Azam transport.
 
hao wenyewe wanamfikia mzee bakhresa kwa pesa ? Kama ameweza kuliteka soko la majini atashindwa la now nchi kavu
Kwa trust ni mipango aliyo nayo azam co. Akiweka basi barabarani wengine watakuwa wanasubiri basi zake zijae kwanza ndio nao wapakie
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…